Kwa tunaosafiri na mabasi, ni vitu gani huvizingatia kabla ya kufanya maamuzi ya kusafiri na basi husika

Kwa tunaosafiri na mabasi, ni vitu gani huvizingatia kabla ya kufanya maamuzi ya kusafiri na basi husika

ndani ya chuma kwanza kuna kuku, bata, mbuzi. abiria bidhaa zetu tunanunua ni mahind ya kuchemsha mayai ya kuchemsha, makande abiria 50 ila chuma ina 60 mafund kama wa3 hivi mda wote spana mkononi maji begani, suka kavaa kikapelo upande au pama tv moja, chuma injini ya scania plate no AAB, oya inamwaga moto mwendo wa ngiri mkia juu honi kama vinanda ukishuka stend mwekenduu inabidi ukaoge kwanza MSAFIRI KAFIRI.
syo majinja
 
Mwendo wa Buffalo...
Whatever is Excellent...

Sio Basi yenye kujikongoja kama ajuza.
 
Kumbe!
Kwa nini LATRA wanaruhusu uhuni kama huo?!
Watu wengi watz wanamuachia Mungu..kukomaa kufuatilia hawawezi.
Mimi Sauli walimfanyia ndugu yangu huo uhuni,,ni last month tu hapo

Niliwapeleka LATRA na polisi walienda kuwakamata wakajificha.

Walirudisha nauli.



Wanachofanya wanakatisha tiketi
Halafu siku ya siku bus halitokei,
Wanawatafutia gari lolote limechoka wanawapandisha.
Na kwa ubovu wa gari lao,nadhani Wana gari moja tu!nalo linakuwepo kwa manati trip 1 barabarani,kumi garage.

Unakuta mtu amebahatika kusafiri siku ambayo lipo barabarani,anaamini ndo iko hivyo, kumbe!


Na hata likiwepo,wanagonganisha abiria kibao seat moja.
Hii tabia ni ya muda mrefu...last yr nilipanda nikashuhudia watu wanagombaniana seat moja.


Imani hata ofisini zao washafunga kabisa nadhani
Mwaka huu mwezi wa 3 nilienda nitume mzigo,nikaambiwa zilishafungiwa..ofisi walifunga.
Gari jazipo..zilikuwa zinakamatwa kila siku.
 
Muda muda muda.... Kuna basi ukipanda ikifika muda ni linang'oa hata kama lina abiria 10 utalikimbiza na pikipiki unaliona hili hapa na dereva hasimami utaenda kupandia tena mailimoja.

Maana watanzania wengi wazembe sana.

Mara nyingi gari inayojali muda hata kwenye mengine linakuwa limejitosheleza. Usmart n.k
 
Back
Top Bottom