Kwa tunaosafiri na mabasi, ni vitu gani huvizingatia kabla ya kufanya maamuzi ya kusafiri na basi husika

Kwa tunaosafiri na mabasi, ni vitu gani huvizingatia kabla ya kufanya maamuzi ya kusafiri na basi husika

Dah, hapo mzee nitacheki vigezo vingine ila nishapanda gari nikakuta kunguni man. Aisee.

Pia kuna magari yana reputation nzuri sana ata yakiwa namba za mbali sio mbaya.

Mfano, kipindi Stend ya Mabasi Dar bado ipo Ubungo bwana nilitaka kwenda Moro. Nafika pale nakuta Abood ndio anatoka ameshajaa. Wakasema linakuja jingine. Ila pembeni kuna BM. Zaidi ya nusu seat zina watu na nikaambiwa zingine zimeshachukuliwa zimebaki seat nane tu waamshe, wengine wapo nje wanasubiri dere aondoe.

Nikaona kupanda Abood inayotegemewa kuja ndani ya dakika 5 jau. Nikakata BM

Oya, ziliondoka Abood 3 mi nipo hapo nasubiria hao watu waliosema nane aisee.
Nimepita hapa Shekilango muda huu naona Abood inapakia.
Nikacheka,comment Yako.
 
Back
Top Bottom