Kwa uchafu wa mama ntilie wa Tanzania, Bibi na Bwana Afya wako likizo?

Kwa uchafu wa mama ntilie wa Tanzania, Bibi na Bwana Afya wako likizo?

Unaweza kua na njaa ikaisha ghafla
Kuna mmoja yupo pale sgd mjini kati kibanda cha torobali ya blue nlikua napita mtoto wake kama miaka miwili anakunya pembeni daaah hatariiii Sana

Ndan ameweka benchi watu wanakula
Halafu mvua zinanyesha

Watu wa afya wanakula viyoyoz
Wanamatumbo kubwaaa kama viroba hawata kwenda kwenye eneo la tukio

Kipindu pindu kikija ndiyo wanajifajya wapo busy
 
Hivi hawa Bibi na Bwana afya wapo?
Migahawa ya Tanzania ni michafu sana na hao wapishi wenyewe ni wachafu mno.
Hatukatai haki za watoto lakini kwa nini mtu mwenye mtoto mdogo asiejiweza aruhusiwe kufanya biashara ya chakula?
Mtoto mdogo anakunya, mama ntilie anamtawaza muda huohuo keshaenda kupakua chakula tena hajanawa na sabuni hapo ikitokea magonjwa ya milipuko inakuaje kwa mfano.
Vitu vingine tungeni sheria ndogo ndogo zinazoambatana na adhabu, piteni mara kwa mara kukagua usafi mkikuta dosari waandikieni faini hiyo itasaidia kuboresha huduma,
Bibi afya na Bwana afya nadhani ni kundi la watu wasio na kazi ndio maana ni walevi sana , hata kukagua mazingira ya makazi usafi wake ukoje hakuna unakuta mapori kwenye makazi ya watu, pita piga faini uone kama hawatofanya usafi huko majumbani.
Angalau chips ni salama kiasi ila usiwekewe kachumbari wala chachandu wala zile nyanya za chupa. Nyanya ya chupa unakuta pale juu pamejaa inzi na nyanya yenyewe imetiwa maji. Maji gani wameweka? Maji hayo ni salama? Tomato ikishatiwa maji usalama wake ukoje? Life span ya uhifadhi inakuwa imevurugwa.[emoji125][emoji125]
 
Nadhan wapo manispaa au ofisi za watendaj kata. Hawa walipaswa kuwa na daftari la kila mtoa huduma ya chakula.na kupita kukagua. Kisutu pale jioni kunawekwa mameza nje.vyakula vinatoka ndan.wala hujui vinaandaliwa vipi.napoelekea kula kula nje itakua ngumu sana
Mtanzania anachojal ni kutengeneza faida sio wewe unakula nini,
Tena ingekua chanzo kikubwa cha mapato.
Kwanza nashangaa kwanin wasitunge by law.kila.mpika chakula sharti ashone uniform nyeupe na kofia.hilo nalo mpaka waziri aje?
 
Naskia Wengine wanapikia maji waliyotawazia ili kuongeza soko
Hayo ndio usiseme
Nenda feri pale uone unavogombaniwa.sasa iman zimekua haba,watu tunalishwa uchafu sana. Mfano feri ukienda usipomwangalia vizuri sahan iliyotoka kuliwa anaisuuza maji machafu kabisa yan anatoa tu kile chakula kilichobaki anaanza kukupakulia wewe.ukimfokea kussuza sahan anasusa.labda ndio masharti yao
 
Hayo ndio usiseme
Nenda feri pale uone unavogombaniwa.sasa iman zimekua haba,watu tunalishwa uchafu sana. Mfano feri ukienda usipomwangalia vizuri sahan iliyotoka kuliwa anaisuuza maji machafu kabisa yan anatoa tu kile chakula kilichobaki anaanza kukupakulia wewe.ukimfokea kussuza sahan anasusa.labda ndio masharti yao
Ndio zao hizo wamezidi uchafuu sana
Me bora nishinde njaa kuliko nile pachafu
 
halafu cha ajabu chakula chao kama wali wanafunikia nailon ili iwive wakati nailon kemikali yake inaingia kwenye wali kwa ajili ya lile joto na husababisha cancer kwa walaji ndio maana cancer imekuwa nyingi, mabibi afya wapo mabwana afya wapo wao wanakimbilia hoteli kubwa ili kukagua wapate rushwa
Aisee hili ni balaa, kweli chakula bora kiandae mwenyewe nyumbani. Mijitu mingine mingine inakera sana sijui shida ndio elimu ama nini. Yaani mifuko ya plastic mtu anafunikia wali, wengine wanatumia kuchemshia ugali. Aisee watanzania tuamke, kamwe hatuwezi kujenga taifa letu kama hatuna afya njema
 
Kuna mmoja yupo pale sgd mjini kati kibanda cha torobali ya blue nlikua napita mtoto wake kama miaka miwili anakunya pembeni daaah hatariiii Sana

Ndan ameweka benchi watu wanakula
Halafu mvua zinanyesha

Watu wa afya wanakula viyoyoz
Wanamatumbo kubwaaa kama viroba hawata kwenda kwenye eneo la tukio

Kipindu pindu kikija ndiyo wanajifajya wapo busy
Bora ungeend kwa mama claree.
 
Aisee hili ni balaa, kweli chakula bora kiandae mwenyewe nyumbani. Mijitu mingine mingine inakera sana sijui shida ndio elimu ama nini. Yaani mifuko ya plastic mtu anafunikia wali, wengine wanatumia kuchemshia ugali. Aisee watanzania tuamke, kamwe hatuwezi kujenga taifa letu kama hatuna afya njema
Huwa ugal ukishakatwa unatiwa ndan ya nailon unawekwa kwenye sufuria ya moto.yan kama tupo Goma
 
Hakuna chakula hapo ni takataka tupu,ugali wanatia hamira mboga ndio zile ya hovyo yani ni uchafu mtupu kuanzia chakula hadi wapishii.
Aisee kuna kipindi wakati nipo mbeya huko maeneo ya Airport ya zamani mtaa wa maendeleo ilikuwa kila nikienda kula ugali tumbo lilikuwa ninajaa gas balaa yaani unaweza kujaza taili la trekta walah, yaani nilikuwa siwezi kukaa dakika 3 bila kujamba.

Ikafika kipindi jamaa yangu mmoja kumbe naye alikuwa na lile tatizo wakati mimi nilikuwa nauchuna tu sikuwahi kumwambia, sasa yule jamaa akaniambia bro tumbo linanisumbua sana, nikamuuliza vipi linauma? Akasema hapana haliumi hata kidogo ila huwa linajaa upepo sana. Nilivyosikia neno upepo aisee nilicheka.

Basi nikamwambia jamaa labda hivyo vyakula tunavyokula, jamaa akasema hata mimi nahisi hivyo maana nasikia huwa wanatia hamira, aisee hapo hapo namimi nikaanza kupata ufahamu.

Finally tulichukua geto tukawa tunapika wenyewe. Tatizo likawa limeishia hapo
 
Ni kweli wanatakiwa kusimamiwa usafi ila kuwakazia kabisa kama ilivyokuwa enzi za JK ninapinga kwa nguvu zote. Hawa kina mama karibu wote wana mizigo mizito mno wanabeba kwa maana ya familia. Wengi hawana waume na wale wenye waume utakuta hawana msaada na ni walevi. Kingine ni kwamba wateja wa Mama Ntilie wengi wao ni watu waliopigika.... mtu ana buku halafu anataka ashibe. Mleta mada nadhani wewe jali usafi wako binafsi na familia yako.. mama ntilie waachie wao wenyewe.
 
Hivi hawa Bibi na Bwana afya wapo?
Migahawa ya Tanzania ni michafu sana na hao wapishi wenyewe ni wachafu mno.
Hatukatai haki za watoto lakini kwa nini mtu mwenye mtoto mdogo asiejiweza aruhusiwe kufanya biashara ya chakula?
Mtoto mdogo anakunya, mama ntilie anamtawaza muda huohuo keshaenda kupakua chakula tena hajanawa na sabuni hapo ikitokea magonjwa ya milipuko inakuaje kwa mfano.
Vitu vingine tungeni sheria ndogo ndogo zinazoambatana na adhabu, piteni mara kwa mara kukagua usafi mkikuta dosari waandikieni faini hiyo itasaidia kuboresha huduma,
Bibi afya na Bwana afya nadhani ni kundi la watu wasio na kazi ndio maana ni walevi sana , hata kukagua mazingira ya makazi usafi wake ukoje hakuna unakuta mapori kwenye makazi ya watu, pita piga faini uone kama hawatofanya usafi huko majumbani.
Hapa naona unachanganya mambo. Kichwa cha habari umezungumzia Mama Ntilie, lakini ulivyoanza utangulizi umehamia kwenye migahawa na umezungumzia uchafu wa wapishi kwa ujumla bila kusema ni wachafu kwa vigezo gani.

Kabla hata hujafafanua kuhusu uchafu umerukia kwenye tabia ya kuwa na watoto wadogo kwenye maandalizi ya vyakula na kuijadili kiujumla wake kama vile kila kwenye Mama lishe kunakuwa na watoto kama sifa moja wapo ya maeneo hayo. Binafsi naamini kuna jambo umekutana nalo mahali na halijakufurahisha kuhusu Afya ya jamii. Lakini kuifanya hali hiyo kuwa ni ya kila mahali ni makosa makubwa sana.

Jifunze namna nzuri ya kuwasilisha hoja ili isaidie katika kuboresha Afya ya jamii yetu. Kuanza kulaumu kundi fulani la wataalamu kwa sababu ya jambo moja uliloliona kwa siku moja na sehemu moja ni kuwavunjia heshima na kuwakatisha tamaa ya kazi hasa kutokana na mazingira magumu yenye changamoto nyingi katika utekelezaji wa majukumu ya kazi za siku kwa siku.

Mama/Baba lishe ni maeneo yasiyo rasmi kwa ajili ya maandalizi na kutolea huduma za vyakula. Maeneo haya yameshamiri katika maeneo mengi yenye mikusanyiko mikubwa ya watu kutokana na changamoto za kiuchumi katika jamii yetu. Kutokana na idadi kubwa ya wtu kutomudu gharama za vyakula kwenye maeneo rasmi (Migahawa na Hoteli), Mama/Baba lishe imekuwa ndio kimbilio la walio wengi. Serikali imekuwa ikitoa miongozo mbalimbali ya namna ya kudhibiti ubora wa vyakula na usafi katika maeneo hayo na imekuwa ikisimamiwa kikamilifu ili kulinda Afya ya Jamii. Hata hivyo kwenye wengi kuna mengi, baadhi ya nyakati mambo yanaweza kuwa tofauti kutokana na tabia za watu wa eneo husika. Huu ndio msingi wa uwepo wa Sheria na Miongozo kwa kuwa inajulikana kuwa binadamu tumeumbiwa upungufu. Kwa hiyo inapotokea hali kama hiyo, Sheria inapaswa kuchukua mkondo wake na sio kuwakosea wengine heshima.
 
Wali wanapoupalia wwnaweka lailoni juu kisha wanaweka sinia la moto wa mkaa.

Imagine moto unayeyusha lile lailoni kisha watu wanakula malailoni [emoji24] sijui madhara ya magonjwa wanayaju?!
 
Back
Top Bottom