Kwa uzalishaji na masoko ya biashara za madini, njoo hapa uliza chochote

Kwa uzalishaji na masoko ya biashara za madini, njoo hapa uliza chochote

Mimi ninataka kuifanya hii kazi unanishauri nianzie atua gani kabla sijaanza na pakununulia na kujua haya ni madini gani na bei ya kuuza na changamoto zake japo madini yapo mengi sana unisaidie zinazopatikana kwa wingi zsidi hapa kwetu?
ongera sana kwakupenda hii biashara
kifupi mm nilianza biashara hii kwa kupata hasara sana na nilikua sijui bali nilifata hobi yangu ya kupenda hii biashara.nilianza biashara waka2009 na nilikua na jamaa yangu ambae niliamini anajua kumbe na yeye alikua hajui .hivyo nilinunu mawe kwa bei juu na kupata hasara

mara nyingine nilipewa fake na kupeleka sokoni na kupata hasara ., lakini mara zote nilikua sikati tamaa niliamini ipo siku nitaijui hii biashara ... nakumbuka niliwai kununu madini ambayo ni ya kiwango cha chini na nikapeleka dar es salaam ila sikuweza kuuza na nilirudi nayo home kipindi hicho nilikua naishi songea .... ila sikukata tamaa nikatoka nikaend amsumbiji nikaanza kuchimba na ila tulipata madini na tulivamiwa na askli wakatupiga na kutunyanganya madni ....mm niliwaacha wenzangu na kurudi home

nilipo rudi nilianza upya kutafuta mtaji nikata pesa kidogo nikaenda sumbwawanga nilipofika nilitafuta watu nikawambia natafuta madini wakanipa jamaa ambaye alijifanya anayajua mawe na atanileteeea baade alitoroka na pesa yangu ikabidi nirudi home nilipofika nikapiga kazi tena lakin nikapata kama mil2 then nikaenda kongo kufata madini yanayo itwa tomalin nilifanikiwa kumuona jamaa ila sikufanikiwa kupata ya quality nzur mudahuu nilikua tayari naya jua mawe then nikarudi home


baada ya hapo
nikaanza kufahamu kuwa biashra ya mawe sio rahisi inaitaji kujitoa nakujua kuwa biashara hii inaitaji kuwa serious sana kuliko biashra nyingine maana unadeal na vitu usivyo vijua kama vipo ala ndio nikaanza kuchimba kwa kuwapa watu pesa na kuchimbisha nakuona faida


nimekueleza haya yote ujue
(1) ina matapeli
(2) sio rahisi kama wengi wanavyo zania
(3)hutakiwi kuta tamaa
(4)nikazi kama kazi zingine yaani inaitaji kujua unachokifanya

jinsi ya kufanya kama unataka kufanya biashara hii
kunanjia mbili
1. uwe broker
2.mchimbaji
3.super deals

broker
huyu niyule anae nunua madini kutoka kwa wachimbaji wadhabu wanaitwa digaras.hapa unaitaji sana kuwa na pesa na pili unaitaji kuwa vifaa vya kuangalia mawe unayo nunu maana unaweza kupewa chupa au fake mawe . unatakiwa kuyafahamu mawe in details na jiwe linakuwa lina thamni gani mfn jiwe zuri linakua halina babo,cloud ,shape nzuri,no crack , pili inatakiwa ulipie leseni nadhani kwa sasa ni 250,000/=
na maweyenye than i ni yale yenye hardness kubwa kama ruby ,diamond ,sapphaya ,ya nayo bakia hayana thamani mani ya kawaida .... hubroker pia unauzuri wake maana wachimbaji wengi hawajui dhamn halisi ya bei
hii kwa kuanzia sikushaulio ufanye hii kuwa broker

uchimbaji
uchimbajio unaugumu wake ila au hitaji pesa zaidi ya pesa kidogo ya kuwapa wanao chimba na chakula .uchimbaj nimgumu kwakua unakaa polini kwa muda mrefu hadi unapo kuta njia au vein ya madini .... Kwa watu mlio zoea town hapa inakua ngumu sana wengi wanashindwa kukaa polini wanashindwa kuishi bina net work wanashindwa kuishi kwenye ugumu wa kula ugali na maharage .... hapa kwenye uchimbaji lazima ufate caption ndizo zinakupeleka kwenye gem mawe mazuri so inawenza kuchukua hata miezi 3 au zaidi na pia unaweza kukosa..kwa sasa kuna geologist wa kukodi unaweza kumkodi na akakuelekeza jinsi ya kuchimba na kupata kwa haraka

super deals
hawa niwele wanao nunu kutoka kwa blokers ..hawa kwa ruby wapo sana waphilipino . na wananunu kulingana na ubora nilio kueleza hapo mwanzo .pia wapo wanao kujaribu kujua kama unachokiuuza unakijua hii inaitaji mtaji mkubwa maana hawa ndio wanao uza nje ya nchi .unaweza umkauza hadio kwanza upate mteja kutoka nje na mara nyingi wanakuwa wannunua kwa kontena

mwisho
hakuna pesa rahis wangu inaitaji kujituma na kukubali kitu kilichpopo moyoni kwako
jaribu kama ukipata hasara usikate temaa komaaa
 
Madini ya dhahabu naomba kujua soko lake nje ya nchi na jinsi yakujua bei yake kwenye soko la dunia.? Na inahitaji mtaji kias gan ili niweze kuuza nje ya nchi
 
Je kwa mwanzo wa biashara naweza kuanza na kiasi gani hasa kwa upande wa tanzanite na je bei kwa gram ni shilingi ngapi?
biashara ya madini kwanza lazima uyajue ,,,, narudia razima uyajue so ninakushauli mtafute mtu anaye yajua au geologist kama unaitaji nitakutumia kwenye in box then ndio uwaze kununu pili angalia unataka kuwa bloker au mchimbaji then ingia kazini
 
Madini ya dhahabu naomba kujua soko lake nje ya nchi na jinsi yakujua bei yake kwenye soko la dunia.? Na inahitaji mtaji kias gan ili niweze kuuza nje ya nchi
bei ya dhahabu inajulikana duniani ingia stoke exchange ya england na au USA utaona pili unatakiwa kuwa super dealer so unatakiwa kuwa na leseni ya super dealer
 
bei ya dhahabu inajulikana duniani ingia stoke exchange ya england na au USA utaona pili unatakiwa kuwa super dealer so unatakiwa kuwa na leseni ya super dealer
Asante mkuu ! na inahitaji mtaji kias gan au dhahabu kias gan ili kuwa super dealer??
 
super dealer ananunua kutoka kwa broker .... so kama unataka kufanya biashara ya dhahabu kwa urahisi nakushauli uwe mchimbaji unaemiliki vitaru ... nirahisi sana unachotakiwa unakwenda sehemu ambayo kuna dhababu unakata leseni kwa 900000 then unaadha kuchimba kwa kuweka watu ili kujua unatakiwa kuwa na geologist

hapa unatakiwa kuwa na
1.digger
2.vifaaa vya kulipulia
3.nguvu kazi
4.compressor
5.vifaa vya kusafisha dhahabu
,eg chemical , maji,pump,na propotinal force

kama unataka kupata faida kwenye dhahabu anza hvyo utafanikiwa
 
Naomba ushauri tafadhali. Nimewahi kuchimba mawe kijijini kwetu na tukapata captions. Hatukuwahi jua ni za madini gani, though niliposearch online na kulinganisha, zilifanana na aquamarine. Je, Kuna maabara zozote zinazopima madini ya vito na kukueleza aina ya mawe uliyonayo? Roughly, gharama za kumchukua mtaalamu wa kuelekeza uchimbaji, usafiri, malazi na chakula vikiwa juu yangu.
 
Naomba ushauri tafadhali. Nimewahi kuchimba mawe kijijini kwetu na tukapata captions. Hatukuwahi jua ni za madini gani, though niliposearch online na kulinganisha, zilifanana na aquamarine. Je, Kuna maabara zozote zinazopima madini ya vito na kukueleza aina ya mawe uliyonayo? Roughly, gharama za kumchukua mtaalamu wa kuelekeza uchimbaji, usafiri, malazi na chakula vikiwa juu yangu.
kama unataka kujua mawe usi pate shida neda TMJ hapo wakuambia ni ainagani ya madini ukisha jua unamkodi geologist ambae takuwambia jinsi ya kuchimba na upate madini safi mapema bila kukosea na kupata faida
 
Habari. Nimepigiwa simu na jamaa angu mmoja geologist.... Kaniambia kwamba wanaotaka kupata WASTE zitokanazo na processes kwenye kampuni madini waanzishe vikundi ili wawe wanapewa huo uchafu. Sasa swali langu ni kwamba....
1. Huo uchafu una madini kweli?
2. Security ya wanakikundi
kupata mgao bila
kudhulumiana
 
Madini ya graphite soko lake liko na yanapatikanaje nikwa ajili battery za magari kweli nauliza
 
Habari. Nimepigiwa simu na jamaa angu mmoja geologist.... Kaniambia kwamba wanaotaka kupata WASTE zitokanazo na processes kwenye kampuni madini waanzishe vikundi ili wawe wanapewa huo uchafu. Sasa swali langu ni kwamba....
1. Huo uchafu una madini kweli?
2. Security ya wanakikundi
kupata mgao bila
kudhulumiana
hiyo ni habari njema na nibahati au frusa usio takiwa kuiacha ni kwamba nimabaki ya dhababu baada ya kuchujwa na inakua na dhababu 70% .... kikundi nibora kuanzisha vikundi mnavyo ona nafanana na mnaaamini ana hiyo ni pesa ya bure .pili kwa sasa hawatumii chemical nying ...mgawo ni jinsi mnavyo ona wenyeywe inafaa
 
Madini ya graphite soko lake liko na yanapatikanaje nikwa ajili battery za magari kweli nauliza
inatumika kwa battery ,lubricant ,pencil , gun poweder ,na electrolyte soko pima anagalia kwenye viwanda hvyo vitu nilivyo kutajia utapata soko tu
 
hiyo ni habari njema na nibahati au frusa usio takiwa kuiacha ni kwamba nimabaki ya dhababu baada ya kuchujwa na inakua na dhababu 70% .... kikundi nibora kuanzisha vikundi mnavyo ona nafanana na mnaaamini ana hiyo ni pesa ya bure .pili kwa sasa hawatumii chemical nying ...mgawo ni jinsi mnavyo ona wenyeywe inafaa
Hapana mkuu naona hapa hujaelewa ,
Hii kitu iko hivi, waste inayotoka mgodini ni mawe ambayo hutokana na upanulizi wa mwamba madini (ore) sasa mawe yaliyo karibu na mwamba madini lazima yawe na kiasi flani cha madini hapa waweza pata au kukosa hakuna uhalisia wa madini yaliyomo maana inategemea na mtu aliyekua anafanya panulizi alikuwa makini namna gani kuulinda mwamba madini asiuingilie. Hapa hakuna kemikali yeyote inayotumika mbali ni vilipuzi tu, kama utahitaji kuelimishwa zaidi kuhusu uchimbaji mdogo au mkubwa karibu mie nimezaliwa machimboni hivyo nimechimba vyakutosha na nimebahatika kufanya kazi mgodi mkubwa wa dhahabu tanzania hivyo nina weledi mkubwa Katka nyanja hii. Nakuhisi utegemee hata siku moja mchanga dhahabu kumwagwa hiyo haipo na haitokuwepo.
 
Hapana mkuu naona hapa hujaelewa ,
Hii kitu iko hivi, waste inayotoka mgodini ni mawe ambayo hutokana na upanulizi wa mwamba madini (ore) sasa mawe yaliyo karibu na mwamba madini lazima yawe na kiasi flani cha madini hapa waweza pata au kukosa hakuna uhalisia wa madini yaliyomo maana inategemea na mtu aliyekua anafanya panulizi alikuwa makini namna gani kuulinda mwamba madini asiuingilie. Hapa hakuna kemikali yeyote inayotumika mbali ni vilipuzi tu, kama utahitaji kuelimishwa zaidi kuhusu uchimbaji mdogo au mkubwa karibu mie nimezaliwa machimboni hivyo nimechimba vyakutosha na nimebahatika kufanya kazi mgodi mkubwa wa dhahabu tanzania hivyo nina weledi mkubwa Katka nyanja hii. Nakuhisi utegemee hata siku moja mchanga dhahabu kumwagwa hiyo haipo na haitokuwepo.
nashukuru na nimekuelewa ila wewe ujanielewa pia mm sijasomea ila kama umesoma vzr utaona nilivyo pitia hadi sana naendelea vzr kwenye hii industry nimepitia mengi sna .... nilichosema hi kwamba kuna residue(mabaki ) ambayo yakua nadhahabu hapa ..... hayo unayo yasema sehemu nyimgine yanaitwa magwangala mm ninavitaru ila natoa dhahabu na nimeona niwaelimishe watu wanao penda kufanya hii biashara ..wasipitie maba kama nilio pitia mm .Wewe kama una penda unawenza kuongezea pale unapoona inafanaa.... ila huwa nawatumia geologist na kuwalipa pale ninapoanza mgodi mpya
 
super dealer ananunua kutoka kwa broker .... so kama unataka kufanya biashara ya dhahabu kwa urahisi nakushauli uwe mchimbaji unaemiliki vitaru ... nirahisi sana unachotakiwa unakwenda sehemu ambayo kuna dhababu unakata leseni kwa 900000 then unaadha kuchimba kwa kuweka watu ili kujua unatakiwa kuwa na geologist

hapa unatakiwa kuwa na
1.digger
2.vifaaa vya kulipulia
3.nguvu kazi
4.compressor
5.vifaa vya kusafisha dhahabu
,eg chemical , maji,pump,na propotinal force

kama unataka kupata faida kwenye dhahabu anza hvyo utafanikiwa
Vyote hvyo nmeshafanya na huwa nanunua dhahabu zangu mwenyewe na kuuza kwa ma broker wakubwa kwa huku kwetu wenyewe wanapeleka dar au Dubai sasa nngependa kujua ukoo wanako uza wenyewe kuna faida gan na n kunahitaj mtaj kias gan ?? Sababu hawaa ma broker au ma superdealer wetu huku hawasemi ukwel !?
 
Naomba kujua soko la dhahabu kwa gram kwa hapa dar es salaam imefikia kiasi gani?

Je duka/maduka yanaouza scales za kupimia dhahabu yanapatikana wapi kwa dar es salaam?

Je wanunuzi wa dhahabu wa uhakika nje ya hawa wahindi wa kisutu nk wanapatikana wapi? Manake bei ya porini unaweza kuta sokoni dar haitofautiani au ipo chini ya kiwango ulichonunulia porini!
 
Nina madini ya graphite ktk form mbili ulya unga na mawe. Serious buyer plz contact through Private msg.
Karibuni sana.
Ni zaidi ya tani 200 zipo site
 
Nataka kufahamu madini ya Rubi.. upatikanaji wake na bei kwa ujumla
 
Mkuu Nina Ruby ya Longido kama kilo 2 na ushee na opal kidogo pamoja na mawe tofautitofauti ya kuchongwa ni Pm unitafutie mteja maana hali tete.
 
Back
Top Bottom