Kwa waliomaliza form 4, kama una roho ndogo usiende kusoma special schools (shule za vipaji maalumu)

Kwa waliomaliza form 4, kama una roho ndogo usiende kusoma special schools (shule za vipaji maalumu)

Advance unaenda unafundishwa na mtu lakini mwisho wa siku unakuja kumzidi kila kitu..

Kuna mwanangu alinipiga msasa Mechanics topics zote lakini akaja kuishia kupata three ya mwishoni..iliniuma sana hii.

Kwahiyo vijana wasiogope
 
Imagine natoka kibaha nakuja kupiga kipindi mchikichini kwa mudi physics (rip) ticha

Nilipiga division 4 o level lkn leo mimi ndo yule ambae matangazo yote ya mpira kutoka azam tv hayaendi hewani bila mimi kuhusika kwa asilimia 95%.

Sent from Tesla device phone
Safi kabisa

Sent from my SM-J410F using JamiiForums mobile app
 
Nina washkaji zangu wakali wa mathematics mwaka huo waliondoka na C ,hata ndegeulaya alipiga C ,ule mtihani wa mwaka 2013 ulikuwa wa laana aisee , Tanzania nzima A za advance mathematics zilikuwa 12

Sent from my Infinix X652C using JamiiForums mobile app
Poleni sanaaa, Form IV ya 2012 na Form VI ya 2013 zilikumbwa na dhoruba kali kama Covid 19!

Sent from my SM-A025F using JamiiForums mobile app
 
Umenikumbusha kijana mmoja anaitwa Rajabu ndegeulaya.

Tuna report advance Azania yeye alipitisha tangazo la kuwa anafundisha tuition Kwa WANACHUKUA PHYSICS, CHEMISTRY NA PURE MATHEMATICS.

WATU walizani ni form six kumbe ni form five alishamaliza topic zote mpaka za six basi ikabidi tuendelee kupiga mapindi kwa Ndegeulaya.
Vijana wa siku hizi!!! "Eti pure mathematics"..... ni Advanced mathematics. Hakuna somo la mathematics A level katika combinations za PCM, PGM na EGM linaloitwa pure mathematics. Hiyo pure maths ni hesabu tu katika Advanced maths. NB: mimi nimesoma PCM miaka kadhaa ya nyuma.
 
Wengi waliopiga One form six miaka ya 2010 kurudi nyuma wana maisha safi... wengi wapo vitengo vizuri wanakula mema ya nchi. Darasa nililomaliza nalo chuo kwa kozi niliyokuwa ninasoma nadhani zaidi ya 35% wako TRA. Tulikuwa kama 40 tu kwenye kozi yetu. Hawa vijana wa sasa wanafanya vizuri sana kitaaluma kwenye CSEE na ACSEE ila watakumbana na changamoto kubwa sana hata kupata sehemu ya field. Huko tuendako watu watakuwa na ONE kali za f4 na f6 huku wakiwa hawana kazi au wanafanya kazi za kuzuia tu msiba. Maendeleo huja na changamoto.
 
Elimu ya kidato cha tano na Sita ni ya kupoteza muda tu. Binafsi nimeipitia kwa sababu sikuwa na taarifa sahihi za kujitosheleza.
Kwa masomo ya arts ni kupoteza muda Ila sayansi hasa PCM siyo level ya kuiruka.
Muhimu sana mbele ya safari huko elimu ya juu. Pia katika maisha ya kawaida ya fundi sanifu au mhandisi.
 
Yaani mi nilikua nikishapata pilot test natupa mavifaa Yao Huko yaani hapo practical imeisha.....

Mwaka wetu kemia practical ya titration tulifanya mpaka jasho likatoka, ngoma haibadiliki Wala Nini... Mpaka jamaa mmoja akaropoka 'huu ni ujinga' watu wakacheka, msimamizi anauliza Nini watu wakamwambia mbona hii practical Kila mtu inamgomea, wakamtafuta teacher wa kemia kaja kujaribu ikamshinda... Kumbe Hawa kenge walileta chemical sijui za wapi bana, ikabidi msimamizi aandike ripoti kuhusu Hilo swala tukaambiwa tuachane na Hilo swali... Wajinga sijui kama walitupa marks zetu
[emoji1787][emoji1787][emoji1787], daaah!! Hatari sanaa

Sent from my SM-A025F using JamiiForums mobile app
 
Haiwezekani siku ya pure ndiosiku ya bam.hapo umetupiga fix🤣🤣🤣🤣🪑💺
Kuna dogo Alisoma ilboru nadhani alimaliza 2011 kama sikosei ana asili ya kiarabu/mhindi alifanya hizo Pepa zote 4 sijui kwa kusimamiwa mwenyewe au vipi, ikitokea bahati mtu alipita hapo huu mwaka atakuja kuelezea... Alikua anasoma pcbm
 
.
Nakuelewa sana mkuu...nakumbuka siku ya kwanza nafika shule fulan, nikawauliza washkaji waalimu wataanza kufundisha lini? Jamaa walinicheka mbayaaa. Wakaniambia dogo unasubiri walimu??! Umeshafeli. Wakati huo jamaa wanagonga maswali ya topics za form 6...
.
Kwenda tu hiyo shule manake sio mnyonge lakini wazee kuna watu wana akili. Kukupa picha ndogo tu, kwa mwaka wetu walitoka Tanzania One wanne!
.
Kuna jamaa muda mwingi alikuwa anashinda msikitini anawapiga watoto ilim ila ukikutana nae ukampa yale matango ya NECTA yaliyojibiwa, jamaa anakwambia sheikh haya nayajua yote.
.
Ila nasikitika kwamba those guys wanaishia kuishi very normal life mbeleni na wengine wanakuwa even frustrated na maisha. Hii ni kwasababu mazingira yetu hayana creative industries qmbazo zinaweza ku-absorb potential waliyonayo.
 
Wanafunzi pia hawapendi kufundishwa wanaona kama wanapotezewa muda tu... Tulikua na mwalimu wa chemistry jamaa alikua anafundisha shule mbili za private huku kaajiriwa serikali

Jamaa ukiacha practical sidhani kama aliwahi hata kutufundisha, alikua mtu wa vyombo alikua anakuja class tunapiga nae story tu za mademu[emoji2][emoji2]
.
Hehee umenikumbusha teacher wa pure Maths, jamaa
anafundisha anafika mahali anacheck notes zake then anaanza kuruka kurasa. Anaruka weeee halafu anasema sehemu hii na hii mtajisomea wenyewe.
.
Anaua zaidi anaposema hii ndio raha ya kufundisha vipaji maalumu, hata usipowafundisha wameshaelewa.
 
Kuna dogo nyuma yetu alikua anasoma pcbm.... Yaani physics, chemistry, biology na pure mathematics.... Na bam juu nikawa namwambia ikifika necta utakataliwa kufanya mtihani wa pure mathematics maana hawawezi ruhusu usome masomo manne, aisee sijui ilikuaje nilikuja sikia aliruhusiwa kufanya mitihani yote

Wataalam hapa watatusaidia
Au alikuwa mtu wa system?

Sent from my SM-A025F using JamiiForums mobile app
 
Yaani mi nilikua nikishapata pilot test natupa mavifaa Yao Huko yaani hapo practical imeisha.....

Mwaka wetu kemia practical ya titration tulifanya mpaka jasho likatoka, ngoma haibadiliki Wala Nini... Mpaka jamaa mmoja akaropoka 'huu ni ujinga' watu wakacheka, msimamizi anauliza Nini watu wakamwambia mbona hii practical Kila mtu inamgomea, wakamtafuta teacher wa kemia kaja kujaribu ikamshinda... Kumbe Hawa kenge walileta chemical sijui za wapi bana, ikabidi msimamizi aandike ripoti kuhusu Hilo swala tukaambiwa tuachane na Hilo swali... Wajinga sijui kama walitupa marks zetu
.
Mkuu, ulikuwa Mzumbe nn? Hii case na mi ilinikuta.
 
Hizi shule(mzumbe,pugu,kisimiri,ilboru,kibaha and the likes) japokua siku izi nyingi zimepoteza sifa zake aisee kama una moyo mwepesi usiende huko unaweza kupata depression au pressure ukashindwa kusoma

Miaka Hio mwisho wa miaka ya 2000 niliripoti Moja ya shule tajwa hapo combination ya pcm... Kipindi hicho special school wamejaa watoto wa dar kutoka (kibaha, Azania, pugu) aisee Hawa madogo wana sifa kishenzi.... Mtu anakuja kuripoti form 5 ameshamaliza topic zote za form 5 anakaribia kumaliza za form 6

Sasa si matozi tulivyomaliza form 4 vitabu tukatupa Kule mpaka siku ya kuripoti hujawahi kupiga pindi lolote... Unakutana na vitoto vimesoma sijui mchikichini huko aisee wamefuta topic zote, aisee nilipata presha sana mpaka kuzoea ile Hali.... Nakuta madogo wanapiga integration kama hawana akili, ukikaa bwenini wanaulizana kwa nguvu reaction za organic. Chemistry huko....

Dah yaani mwezi wa kwanza form 5 watu wanasolve necta review nikasema hapa nimeyatimba... Aisee ile presha ya ku catch up nilipata shida Sana sio Siri... Ukiwa na roho nyepesi unaweza kukata tamaa Moja kwa Moja

Kuna dogo tumeingia form 5 alikua anaitwa T.O (Tanzania one) alitukimbiza wote form 4 aisee huyu Jamaa mpaka Leo hua namuogopa. Hua namwambia hata hii kazi ya u engineer unayofanya unastahili kua somewhere else una potential kubwa sana, picha linaanza tumeingia form 5 hapo.... Sasa form 6 walikua wanafanya fitness tests (hii anatokea mwanafunzi mmoja au wawili wanatunga mtihani alafu wengine wanafanya japo sio lazima)

Ujinga wa hii mitihani wanafunzi wanajua kukomoana yaani maswali yote unakuta ya kibabe... Kuzungusha 0 huku ni kawaida tu ndo maana wengi walikua hawataki huu ujinga, dogo bana tunafika form 5 kaskia form 6 wanafanya fitness test ya physics dogo akazamia akapiga Pepa... Matokeo yanatoka form 6 karibu wote wamefeli dogo kawakimbiza.... Wote wanaulizana hili jina nani mbona hatumjui... Kuja kuulizia wakaja kugundua ni dogo wa form 5 aisee jamaa walimind kinoma akapigwa marufuku kabisa kusogeza pua kwenye fitness tests za form 6

Huyu dogo tulipofika form 6 sidhani kama aliwahi kukaa akasoma, jamaa alikua anakaa zake class watu wamepanga foleni na maswali Yao yaliowashinda dogo anapiga yote tu hajali kama ni ya physics, chemistry, pure au bam ye anasolve tu. Alikuja kua Tanzania one tena form 6 jamaa walimtangaza hesabu paper 1 na 2 zote alipiga 100%.

Huku kama una roho ndogo sio pa kwenda mi nusura panishinde nilitaka nirudishe mpira kwa kipa(kuhamia private)
Acha kuwatisha vijana, hakuna cha ajabu huko
 
Organic chemistry shikamoo, Kuna dogo aisee alimeza organic yaani akawa kama kichaa anatembea anaongea mwenyewe maswala ya chemical reactions tu[emoji2]
.
Mwaka wetu kuna mwamba alichanganyikiwa na Pipo Confuse Brain (PCB). Tuko class tunapiga msuli tunashangaa jamaa anaanza kujimwagia maji ya kunywa kichwani. Kumuuliza oya mwana vp, akaanza kujibu vitu havieleweki. Huku na kule akaanza fujo, wana wakamtia kamba chap.
.
Oya mazee, ule mziki wa BS ni noma miaka laki 8.
 
Back
Top Bottom