Kwa waliosikiliza mwanzo mwisho utekaji aliofanyiwa Sativa kwenye Jambo TV ni episode gani imekuumiza kuliko zingine zote kwenye simulizi yake?

Uki analyse vizuri utaona hilo genge linapewa amri toka juu maana lenyewe halikuwa sure jamaa kakosa nini ila pia inaweza kuwa mamlaka ya mkoa hasa rejea swali aliloulizwa we una duka kariakoo?
Ndiyo hivyo tena,serikali na mifumo mingi ya nchi mbalimbali
Wana vikundi wanavyotumia kuteka...

Ova
 
Kassim Hanga alikuwa na mke "Mzungu" na walibahatika kupata mtoto mmoja wa kike anayeishi Uingereza kwa Sasa.
 
Kwahiyo wewe ulitaka Moshi iwe jamhuri? Kati ya Nyerere na mawazo yako hayo nani mkabila na mkanda? Ni vipi kama kila jimbo/lingetaka kuwa jamhuri tungekua na Nchi kweli?

..hakujawahi kuwa na madai ya Moshi kuwa jamhuri. Hizo zilikuwa propaganda za kikabila za wakati fulani hapa Tanzania.
 
Ukisoma kitabu cha Ludovick Mwijage kiitwacho " The dark side of Nyerere's legacy " utaona hayo mambo yote hata hiyo iitwayo karakana ya mateso kwa mateka ya Oysterbay ilikuwepo tangu enzi za Julius ikiitwa "gestapo"

Uwepo wa detention camp za siri ambapo wakosoaji wa sera mbovu za ujamaa walifungiwa "incommunicado" bila kupelekwa mahakamani wala kujua makosa yao kwa miaka na miaka.

Ludovick Mwijage aliandika ilifika kipindi alifanikiwa kuliona jua baada ya mwaka mmoja maana walifungia katika chumba kidogo tena kisicho na dirisha la kueleweka hivyo hata hawakujua sasa ni usiku na sasa ni mchana.

Kwa Kenya , Daniel Arap Moi nae hakuwa nyuma wakosoaji wake waliteswa Nyayo house huku akiwaweka katika kina cha maji kinachowafikia kifuani halafu unaambiwa ulale usiku hapo bahati nzuri Mwai Kibaki alipoishinda KANU ambayo ilijisimika madarakani tangu Kenya ipate uhuru kama CCM aliunda tume ya maridhiano huku wale wahanga wa mateso ya Nyayo house wakilipwa fidia sambamba na wale wa Kamiti na Manyani na Nyayo house ikafunguliwa na kuwa jengo la makumbusho ya kitaifa.

Utofauti wa Moi na Nyerere ulikuwa mdogo sana ,Nyerere alikuwa msosi sana ila hakuweza kushindana kwa hoja kisomi kama ambavyo Ludovick aliamini kwa elimu aliyokuwa nayo Nyerere hakupaswa kuwahenyesha wale waliopinga sera zake za ujamaa kwa mtutu wa bunduki bali hoja kwa hoja mezani.

Hivyo ukichunguza vizuri utaamini muundo wa kurecruit vyombo vya dola ndio ule ule tangu enzi zile na amri na maelekezo ni yaleyale.


Wengi walipotea sana zama zile sababu nchi ilikuwa gizani ila walau sasa tunaona nguvu ya mitandao inahabarisha matukio kama haya.
 
Uki analyse vizuri utaona hilo genge linapewa amri toka juu maana lenyewe halikuwa sure jamaa kakosa nini ila pia inaweza kuwa mamlaka ya mkoa hasa rejea swali aliloulizwa we una duka kariakoo?

..Sativa alishikiliwa ktk vituo viwili vya jeshi la Polisi.

..Lazima waliomteka ni watu wa serikali.

..Serikali inapaswa kuwajibika. Waziri wa Mambo ya ndani, Igp, na Ma-Rpc wa maeneo alikoshikiliwa Sativa, wawajibike.

..Pia waliomteka, na kujaribu kumuua Sativa, wafikishwe MAHAKAMANI.
 
Siku moja nikawekwa sero ,kwa ujinga wa mtu mmoja hivi wa karibu , huko nyuma yupo na wapambe nduguze maana pesa ipo ,

Mle sero kuna hali ya hewa sio nzuri, ila lipo bench la zege , nikaa pale kwenye bench washikaji wengine wamejilaza chini, roho wa Mungu akaniambia omba ,pale kwenye benchi nilipokaa na baadhi ya washikaji nikainamisha kichwa huku nimefumba macho, ilikuja ghafla sala moja tu ,

Mungu nipo mikononi mwako wewe wajua maisha yangu tangu natoka tumboni mwa mama yangu , then nikafumbua macho .

Ndugu zangu ile hali ya hewa mbaya sikuikia tena , nikabaki nimetoa macho huku nikiangali na kusikia story mbali mbali za washikaji , Mle ni chuo wakuu .

Haikupita mda nimejiegesha kwenye bench usinginzi ukanichukua ,kumbe nipo usingizini ndugu na jamaa wamefika pale kituoni na kwa kuwa nilikua nimeingizwa mda mchache so jina langu ilikua washikaji walikua hawajalijua vizuri , kila wakiita mie kimia kumbe nipo kwenye usingizi.

Badae sana nazinduka nakutana na sauti , aliekua ananiita ni mpelelezi wa kesi yangu ambayo kimsingi sikua na kosa , nikaitika nikatolewa kwenda hojiwa ila wakati huo mpelelezi yupo na jaziba sana kisa nimeitwa mara nyingi ila sikuitika, (nami nili mjibu nilipumzika) akanijibu so unataka pumzika tena?) Nikamwambia ikikupendeza afande.

Uzuri mwanasheria wangu , ndugu na jamaa walisha kamilisha taratibu za dhamana .

Kile kituo nawashukuru askari wawili hivi walikua waungwana sana kwangu , na kweli sio askari wote ni matatizo wengine wanajua nini wanatakiwa kufanya kwa mtuhumiwa , nilitoka kwa dhamana na mambo badae yaliisha
 

Kuwakosoa, kuwaambia na kuwashauri ni tofauti na kugombana. Usifanye kama ben saa 8 na kabendera. Hutashinda, kwa maana ikitokea kuna watu walikuwa wanakuwinda wataitumia vibaya jamhuri kukupiga.
 
Nyuma ya mzee mwenye kibaraghashia, mwenye shati jeupe, yuko katikati ya polisi wamekaa nae kulia na kushoto.

Sasa unajua kosa lake ? Alikwenda kukaa nyumba ya Kambona wakati Kambona kakimbia.

Kassim Hanga alipotumbuliwa alijiondokea bila bifu, akasimama Egypt akafikia kwa balozi, halafu akaenda Guinea, halafu akiwa njiani kurudi nyumbani akasimama Uingereza, nyumbani kwa Kambona. Kambona anasema akamwita Hanga chumbani kwake, akamwambia unarudi Tanzania, watakukula kichwa. Hanga hakuwa convinced. Kambona akawaita Wazanzibari wawili nyumbani kwake akawaambia hebu ongeeni na huyu mtu, anaenda kuwambwa msalabani huko kwa Nyerere. Hanga akawaambia, jamani mimi nimeondoka sina ugomvi na Nyerere. Haya. Alipofika airport Kiwalani Jet Lumo, akaja rafiki yake mwingine na mke wake, wakamwambia umerudi huku ? Nyerere anatafuta kichwa chako kwenye sinia.

Hanga akaenda kufikia nyumbani kwa Kambona, Msasani, two doors down the block kutoka kwa Nyerere. Kesho yake magazeti yakaandika Hanga kaingia nchini. Gestapo wa Nyerere wakaja kumkwida. Akaenda mahabusu, baada ya siku chache akaletwa Mnazi Mmoja kwenye mkutano wa Nyerere. Toka siku ile mpaka leo anaejua alipo Hanga ni Mungu, shetani na Nyerere.



Ingekuwa Nyerere alikuwa under pressure ya Karume, na kwamba Karume ndio mbaya, basi Nyerere asingemleta Waziri Hanga uwanjani Mnazi Mmoja yeye mwenyewe binafsi Nyerere kumtukana Hanga.

Huwezi kum sanitize Julius Nyerere. Nyerere hasafishiki, alikuwa na yeye ni primitive, ignorant third world despot, masikini ya Mungu.

Baada ya kuwa wakubwa na kupata elimu ya juu inayofundisha kujifunza kwa kutafiti, wengine tulishajiosha majini na maruhani ya ule utoporo wa mwalimu wa siasa wa primary school, ambae nae, tuseme ukweli, alikuwa hazimo, you and I know that.... masikini ya Mungu. Mwalimu wa primary aliyetufundisha hizi historia alikuwa hana uwezo wa kuchambua ule uharo wa propaganda za chama kimoja cha enzi zile, hajui chochote.
 
Basi nami kusema ukweli nilisoma historia zilizotoholewa, nakubali nili-'brain woshiwa'.
 
Episode 3.. Mpige chuma

..hao jamaa wakihojiwa vizuri watataja alipo Ben Saanane, Azory Gwanda, na wengine.

..Na Sativa ametoa clue zote za kuwafikia na kuwatambua kuanzia kwa madalali waliotaka kumpangisha nyumba.
 
Wasipowapata itakuwa confirmatory test ya state kuwatesa watu foot print zinaanzia kwa madalali.
 
Somo ni kwamba kutukana viongozi wa nchi mwisho wake uwa sio mzuri.

..anayetukana viongozi wa nchi anapaswa kushtakiwa na kuhukumiwa kifungo.

..Na viongozi isiwe chama tawala peke yao, hata miongoni mwa wapinzani kuna viongozi.

..lakini pia hivi viongozi wetu wanajisikiaje wanapopewa taarifa kwamba mwananchi aliyewatukana ameuliwa?
 
Lord Acton, “Power tends to corrupt and absolute power corrupts absolutely”.
 
Kikubwa kama anawafahamu walomfanyia hivyo achukue hatua stahiki pia ajirekebishe kwenye yale mabaya ambayo yalimpelekea madhila maana bado uhai anao
Bado anatumbua zile 35 zikiisha anapiga tukio jingine aingiziwe walau 100/200 mjini mipango
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…