Kwa wanaoamini hakuna Mungu, njooni hapa

Mkuu,

Kuna mchungaji mmoja wa Marekani, Mmarekani mweusi, alitaabishwa sana na mafundisho kwamba mababu zake wa Afrika ambao walikufa kabla ya kumjua Yesu Kristo, kwa sababu Yesu hakujulikana kwao, watachomwa moto milele.

Yule mchungaji alihoji sana hoja hii, akisema inawezekana vipi Mungu mwenye upendo wote akawanyima Waafrika neema ya kumjua Yesu, halafu akawachoma moto wa milele kwa sababu kawanyima neema ya kumjua Yesu.

Sakata jili linaonesha ujinga wa hoja ya kwamba watu wote ambao hawajamkubali Yesu watachomwa moto wa milele.

Kisa hiki kilitengenezewa sinema inaitwa "Come Sunday".

Starring Chiwetel Ejiofor (yule slave wa "12 Years A Slave"). Yule jamaa huwa hakosei kila movie yake nimependa. Sasa hivi amekuwa katika movie nyinginge "Rob Peace" nayo kali sana.

Kama hujaiangalia itafute, kama unafuatilia hoja hizi hii movie inafikirisha sana. Based on true events.


View: https://youtu.be/pVQFWvm_fbU?si=hkhS0BvqQvoiQUuK
 
Wewe haujaumbwa na mungu science ndio imekuuumba hakuna mungu kama yupo thibitisha uwepo
Uislamu umeeleza mambo mengi kuhusu mungu mmoja asiye zaa wala kuziliwa wala kufanana au kuendana na mtu ama jambo ama mambo fulani, na umefundisha vipi tunasadikisha uwepo wake, tunasadikisha uwepo wake kwa jinsi uendeshaji wa dunia unavyo kwenda, mfano usiku mchana, tunaamini kwamba uendeshaji huu si alinacha si alinacha sababu unaonekana huu uendesha, na tunasadikisha kama mungu huyu angekuwa na mshirika basi utaratibu huu usikuwa endelevu, pili ni namna jua linapotoka mashariki na kuzama magharibi tunaamini pia uendeshaji si alinacha sababu tunauona haya ni machache kati ya mengi sana kuhusu mungu huyu wa kweli.
 
Stories tu za kudanganya watu kwa manufaa au SABABU za watu
 
Hayo sio kujifunza kirahisi kama wapendavyo vitabu vyao alifu lela ulela, ni ya kuunda uzi mzito, lakini najua bado watapinga
 
Kwa wanaoamini hakuna mungu, ukiwachunguza kwa makini hawa watu ndiyo ujifanya wao ni majiniazi, kumbe ni wapumbavu wa mwisho katika hii dunia,
Kwanza Atheists hatuamini hakuna Mungu.

Tunajua hakuna Mungu. Hatuamini kwenye kuamini. Hatuna imani ya aina yeyote ile.

Wewe ndio mpumbavu wa mwisho kudai kuna Mungu ilhali huwezi kuthibitisha uwepo wake.
Mpaka hapa ushabugi.

Atheists hatuamini kwenye kuamini. Hatuna imani ya aina yeyote ile.
Hatuamini simu anatengeneza mzungu. Simu haziaminiwi.

Simu zinajulikana kwamba hutengenezwa.

Una elewa kiswahili wewe?
ila jinsi mungu alivyoumba kila kitu kwa ustadi wa hali ya juu wanasema ni nature, ushuuzi!
Hakuna Mungu aliyeumba chochote kile.

Mungu hajawahi kuwepo, hayupo na hatakaa awepo.

Huyo Mungu mmemtunga vichwani mwenu tu, Na wala huwezi kuthibitisha uwepo wake.
 
Hapa nimekuelewa vizuri sana ulichoandika ila na mimi kidogo nina hoja, je ingetokea umezaliwa kwenye jamii ambazo hazina mafundisho ya Imani za dini Ibrahim mfano ulizaliwa na kukuzwa na Imani kama budha, Tao, hindu n.k

Je ni kweli kabisa ungeamini katika Mungu wa Ibrahim si kwamba umezaliwa katika dini hizo na kukulia katika hayo mafundisho na kujikuta ukiwa na Imani hiyo?
 
Stories tu za kudanganya watu kwa manufaa au SABABU za watu
Naam,

Cha kushangaza ni kwamba, huko zamani zama za giza, watu wengi hawakujua hata kusoma, vitabu vya dini walikuwa wanasomewa, mambo mengi walikuwa hawajui, elimu ilikuwa ngumu sana kuipata, hawa watu wa zamani naweza kuwasamehe kirahisi kabisa kudanganywa.

Watu wa leo wanajua kusoma, elimu iko nje nje, hata kama hujui kusoma unaweza kusikiliza vitabu ya audio, kuna elimu kubwa sana hata Youtube tu ukijua kuitafuta.

Hata hapa JF watu tunaelimishana sana.

Lakini, bado watu wanachagua kubaki kwenye ujinga.

Unamuonesha mtu kabisa hii ni logical fallacy, lakini anaing'ang'ania tu kiimani.
 
Ukomo wa kufikiri umemuumba mungu kwani nje ya upeo wako vitu vyote vimefanyika kwa miujiza.Hebu fikiri katika mazingira yako endapo mtauguza mgonjwa hospitali,madktari wakishindwa watampa rufaa.Uchumi ukiruhusu mtampeleka na usiporuhusu mtamwachia mungu.Masikini mungu wake yuko karibu na tajiri mungu wake yuko mbali.Swali ni:huyu ni mungu au ukomo wa kufikiri?
 
Nature is chaotic, so the perfection of man and other living things alone proves beyond reasonable doubt that there is God ( The designer). Kamwe " nature" haiwezi tengeneza ktu perfect, ndio mana milima , bahari, mabonde, nk haviwez kufanana . I rest my case
# No malice to anybody
 
Uzuri uislamu umeeleza mambo mengi kwa kina kuliko dini yeyote duniani, tukiwa watafuta maalifa hatuna mipaka lakini kwenye maalifa pia kuna pumba nyingi, na ndio maana uislamu ni dini inayowataka watu kutafakari kabla ya kuchukua hatua, nikijibu hoja moja moja kuzaliwa katika imani tofauti hakualalishi wewe kukimbia maalifa mengine na maarifa unapo yapata inakupasa kupima na kuchuja kwa undani kabisa kuliko kuacha kutoa haki yako fulani ambayo ulistahiki kutoa, na kuanguka kwenye upotofu na natumaini kwa kadri ya uwelewa wangu ulivyo aijalishi nimelelewa katika imani gani, natumaini kwamba ninge chuja mambo kwa ufasaha mpaka kupata usahihi.
 
hao kweli ni wapumbavu sana.
Wewe ni mpumbavu zaidi ya hao.
Nilidhani umekuja na ushaidi wa uthibitisho wa uwepo wa Mungu.
Kumbe blabla tu.
 
Katika upimaji wa hayo maarifa,unatumia maarifa gani?
 
Logical non sequitur.

Unaunganisha vitu viwili tofauti visivyo na uhusiano wowote ule kuunda hitimisho potofu.

Ulimwengu kuwepo sio uthibitisho wa uwepo wa Mungu.

Kwanza thibitisha uwepo wa huyo Mungu, Kabla ya kusema Mungu huyo ndio chanzo cha ulimwengu.

Huyo Mungu mmemtunga vichwani mwenu tu. Ndio maana hamuwezi kuthibitisha uwepo wake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…