Kwa wanaoamini hakuna Mungu, njooni hapa

Kwa wanaoamini hakuna Mungu, njooni hapa

Sababu hakuna binadamu anaweza kufanya hivyo, na mungu ni mkuu mwenye uwezo wote bila mipaka
Umefanya logical fallacy ya non sequitur.

Inawezekana hakuna binadamu anayeweza jufanya hivyo.

Lakini hilo halimaanishi ikiwa hakuna binadamu anayeweza kufanya hivyo, ni lazima kafanya Mungu.

Hujathibitisha Mungu yupo.
 
Vitabu nimesoma na Ndo maana Ninao uwezo wa Kujenga hoja Kwa sababu asiye na Elimu hawezi kujenga hoja..

Hoja zangu hata Moja Hujajibu
Hoja zako natumaini nimezijibu kwa kile nimewezeshwa na mungu na nazani kama liko jambo linakupa ukakasi naweza pia kukujibu
 
Ndio wanavyokiwa Hawa wakizidiwa hoja
Hakuna hoja ambayo mmezidi, uzuri wa kueleza jambo yatakiwa upate watu wakutafakari, tumewaeleza na tutawaeleza kila siku na kwa kadri mungu anapotubaliki, tunatumaini kuelewa kwenu kuliko vile mnakumbatia.
 
Umepewa uhuru wa kufanya unachotaka katika ukomo wa ubinadamu wako

Sijapewa uhuru huo, hii ni kauli ya kiimani.
Kila kitu kilichopo ndani ya uwezo wa kibinadamu umepewa uhuru wa kufanya kiwe kizuru au kibaya

Nimepewa na nani? Mungu? Huyu huyu Mungu ambaye hujaweza kuthibitisha yupo?

Hayo unayo Sema wewe sijui urudi nyuma miaka ya 1980 hayo yapo nje ya uwezo wa ubinadamu wako

Nnai kaamua yapo nje ya uwezo wangu? N akama kuna mwingine anaamua mwanzo na mwisho w auhuru wangu, je, ni kweli nina uhuru?

Huo ulimwengu wenye mazuri tupu Kwa Sasa upo ila sio Kwa binadamu ni Kwa malaika ulimwengu wa malaika una mazuri matupu labda kama na wewe unataka uwe malaika

Huu ulimwengu wa malaika huwezi kuthibitisha upo. Ukibisha, thibitisha upo.
Wewe binadamu hapa sio mwisho hapa unapita tu na hapa upo katika mtihani ukifaulu utaenda katika ulimwengu wenye mazuri tupu na ukifeli Jahanamu inakusuburi

Hata kama haya yangekuwa kweli, kwa nini Mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote atupitishe kwenye mapito yenye mabaya wakati aliweza kutupitisha kwenye mapito yasiyoweza kuwa na mabaya?

Kituo chako Cha kwanza
Ulianza maisha katika tumbo la mama yako yalikuwa maisha ya Raha sana Hadi siku uliyotolewa katika hayo maisha ukawa unalia maana mwili wako ulitambua kabisa kuwa Sasa unaingia katika tabu

Bado hujajibu kwa nini Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote karuhusu viumbe wake anaowapenda waishi kwenye dunia yenye tabu na mabaya mengi?

Kituo chako Cha pili
Ni hapa Duniani hapa Duniani ndio umepewa uhuru wa kufanya unachotaka na kuchagua unataka kuishi maisha gani Baada ya maisha haya ya Duniani

Si kweli, sijapewa uhuru wa kufanya ninachotaka. Nataka an endless source of energy, sina uhuru wa kuwa nayo.

Kituo chako Cha tatu
Ni kaburini utaka ukisubiri siku ya hukumu ifike

Hujathibitisha kwamba baada ya kufa kuna siku ya hukumu, hii ni kauli ya imani tu.

Kituo chako Cha nne
Ni peponi au motoni
Na huko ni maisha ya milele hakutokuwa na kufa tena iwe upo peponi au motoni utaishi milele

Hujaweza kuthibitisha kuwa huko peponi au motoni kupo, hizo ni kauli za imani tu.

Usiweke kauli za imani tu, thibitisha unachoandika.
 
Back
Top Bottom