Unavoidable Servant
JF-Expert Member
- Oct 13, 2021
- 1,728
- 4,545
Yani kama kocha wa Simba Gomez? [emoji1][emoji1]Jamaa hana ujanja usimcheke! Yani huwa tunaita kuishiwa mbinu! Jamaa ameishiwa mbinu kwa hakika hajui hata akitoka aelekee wapi. Labda tungemshauri katika hayo mambo.
Soma vizuri Uzi wng nimekwambia nimejaribu issues nyingi tu hadi za umachinga lkn zimejamba, embu fikiria kutoka kutunza kumbukumbu hadi kuwa machinga na huku kitaa unakuta watu wapo kwenye hizo mishe kitambo tu halafu we wakuja uje utoboe kirahisi tu wanakuangali ..Mkuu kuna uzembe umeufanya lazima ukubali. Tangu magu atumbue ni miaka 5 sasa imekuwaje umeshindwa kujifunza ujuzi wowote au gata biashara ? Mkeo amekuvumilua sna kusema ukweli.
Chukulia wewe kuna ndugu yako wa kiume kaja kukaa kwako miaka 5 hana ishu ya maana anayoifanya je ungemvumilia ?
Ulitumia uamuzi wa busara sana kujifungulia kijiwe kimya kimya!Mkuu mm niliamua kujiendeleza kielimu (self-sponsored) kwa ngazi ya Masters, Sasa nikayumba kiuchumi japo mke alikua na kazi. Nikaamua kufungua genge kisirisiri (maana mke wangu amejaa mdomo wa kubwabwaja&kukatisha tamaa). Nilipambana shule, kazi na Biashara mpaka Mei 2021 nikawa nimemaliza Masters huku mke hakui kilichoendelea.
**Kutafuta pesa hakuna aibu.
Kama wamepanga na yeye Mwanaume ndiyo aliingia Mkataba na mwenye Nyumba,basi hana budi kuvunja huo Mkataba! Usikubali kunyanyasika kisa Mwanamke wako ana pesa! Na kuna muda mwingine Wanawake wanaonyanyasa Waume zao mara nyingi inakuwaga Kama payback,wanalipiza Mume aliyokua anafanya akiwa njema!!Utafukuza nyumba ikiwa yako! Kama wamepangisha je!?
Eeh mzee baba sasa mkimpondea bila kumpa line kwamba apambane vipi inakuwa haijakaa sawa! Kama hata unachakalika uko mahali unamwita kama anaweza fika bana hapa tunabeba boksi toka shimoni mpaka msimbazi kule tuunge unge kwa day haikosekani 15-20 mbona safi!Yani kama kocha wa Simba Gomez? [emoji1][emoji1]
Wewe umefuata huo ushauri? Kwa nini unataka mwenzio aanze ulozi, hujui ataongeza tatizo la 3.Mimi sasa nakupa solution ya kudumu hakuna mtu mwingine atakusaidia msaada huu ninaokupa.
Naamini wewe ni mwislamu, sasa tafuta sheikh mwenye mke zaidi ya mmoja na hana kazi yoyote hapa mjini lakini wake zake wametulia tuli, wala hagongewi na wanaishi kwa amani.
Mueleze hii shida yako huyo ndio atakupa msaada wa kweli, atakupa siri kwa nini yeye hana kitu na ana mke zaidi ya mmoja na wote ni wazuri na hawamsumbui.
Hii dunia ione hivihivi watu wengi hawawezi kukwambia ukweli hii duniani wanafanyaje mpaka mambo yananyooka.
Fanya nilichokwambia utakuja kunishukuru in future days.
Unapoambiwa muishi nao kwa akili tumia akili yoyote itakayoleta majibu chanya.Kwamba akamfunge mkewe kiakili au sio? [emoji23][emoji23][emoji23] mambo ya kipemba hayo dah!
Mwanamke sio payback mwanamke hata ukimnunulia iphone kila ikitoka na kumlisha KfC mwaka mzima siku nguvu ya kumfanyia hivyo ikiwa haipo anaanza dharau automatically! Yupo kwa ajili ya kulishwa na kupewa raha tu yeye ila sio yeye akupe wewe!Kama wamepanga na yeye Mwanaume ndiyo aliingia Mkataba na mwenye Nyumba,basi hana budi kuvunja huo Mkataba! Usikubali kunyanyasika kisa Mwanamke wako ana pesa! Na kuna muda mwingine Wanawake wanaonyanyasa Waume zao mara nyingi inakuwaga Kama payback,wanalipiza Mume aliyokua anafanya akiwa njema!!
Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
Sawa sawa chifuUnapoambiwa muishi nao kwa akili tumia akili yoyote itakayoleta majibu chanya.
Mungu ametupa akili kuzitumia ni hiyari yako.
Wale tulioko mtaani tunakuelewa vizuri sana! Game ngumu sana aisee yani ni nyokest! Ugumu unakuwa mara mbili kama ulishawahi kupatia hela kwenye kiyoyozi na kiti cha kuzunguruka!Soma vizuri Uzi wng nimekwambia nimejaribu issues nyingi tu hadi za umachinga lkn zimejamba, embu fikiria kutoka kutunza kumbukumbu hadi kuwa machinga na huku kitaa unakuta watu wapo kwenye hizo mishe kitambo tu halafu we wakuja uje utoboe kirahisi tu wanakuangali ..
So skukaa kindezi lkn kitaa kiskie tu ndugu yangu hali sio nzuri sn
Nn tenaAiseee!!
Wengine tunaishi mjini kwa hesabu kubwa sana na kwa kutumia akili nyingi, kwa mwaka naweza kupata ela mara 4 tu na tunakwenda nazo kwa mzunguko wa mwaka mzima.Eeh mzee baba sasa mkimpondea bila kumpa line kwamba apambane vipi inakuwa haijakaa sawa! Kama hata unachakalika uko mahali unamwita kama anaweza fika bana hapa tunabeba boksi toka shimoni mpaka msimbazi kule tuunge unge kwa day haikosekani 15-20 mbona safi!
Ila sio mnapondea oh tafta hela mara hama hapo aende wapi? Akalale chini ya Kijazi interchange ama?
Kaka kuna kitu watu hawakielewi mpaka labda kiwakute, watu wanaomwambia mtoa mada kwanini amekaa miaka mitano bila kupata kazi kuna kitu hawaelewi, kwanza watu tuko tofauti, kitendo cha kupoteza kazi nitakavyokipokea mimi ni tofauti na utakavyokipokea wewe. Kuna mtu akipoteza kazi anaingia kwenye depression moja kwa moja, mtu kama huyu kuja kupata kazi nyingine anahitaji msaada wa kisaikolojia na kiroho kwanza ili arudi kwenye utimamu wake wa akili ndio ataweza kuwa "functional".Atleast umejaribu kuvaa viatu vya mtoa mada kwa mifano halisi kabisa!
Too bad ku maintain mahusiano kibongo bongo bila mwanaume kuwa sole provider ni ngumu sana yani namuonea huruma bro wako kujiopolea slay queen maana kipigo chake kitakuwa cha mbwa koko! Mwanamke ambaye hawezi zalisha hata sh.100 huwa wazuri sana kwenye kulalamika na kuzalisha stress! Cha msingi kaka yako unajua yupo so weak so msimuache akiwa hana ramani msaidieni tu.
Vivyo hivyo kwa mtu wako kama mnafanya maisha sio mbaya kama utampa connection nae awe vyema ili wote muweze kufurahia maisha!
Boda boda ni sawa ila labda apate ya mkatabaWengine tunaishi mjini kwa hesabu kubwa sana na kwa kutumia akili nyingi, kwa mwaka naweza kupata ela mara 4 tu na tunakwenda nazo kwa mzunguko wa mwaka mzima.
Kazi rahisi mjini ndio hizo bodaboda na wanapata sana hela, mademu wa mtaani kina Mwajuma mchokonowe siku hizi hawa bodaboda ndio wanawala sana, wana mzunguko wa hela ndogondogo za kila siku.
We Dada mungu akubariki na abariki ndoa yako, it seems u have got a heart, be blecdTrue, huu ni ukweli mchungu sana ila ni dawa. Hata hivyo wanawake tukumbuke tuna kaka zetu pia, unachomfanyia mtoto wa watu fikiria akifanyiwa hivyo wa kwenu, Labda kama haujali kuhusu wengine.
Mimi binafsi kaka yangu enzi za ujana alikataa kazi ya serikali akakimbilia NGO's. Kama ujuavyo kule mikataba mingi ni 3-5 years, ikiisha msoto wa kutafuta kazi uko pale pale kama hamjawin project nyingine, Kumekuwa na changamoto kwenye ndoa yao hasa jamaa anapokuwa hana kazi, na sio kwamba mke ana kazi, no hana ni mama wa nyumbani 24/7 na si mtu anayeweza kufanya kazi au biashara yoyote (sisi kama familia tulishajaribu kupush hili limeshindikana kabisa) as for me kuna kipindi i was willing hata kumpa mtaji, mama pia alikubali tuchange mtaji tumpe alitujibu anataka mtaji wa kufungua boutique!!!!! Yaani haujawahi miliki hata kiosk gafla unataka boutique! na pia hatuna mtaji wa kumpa kufungua boutique labda tungejipiga pia sana zingepatikana 4-5M aanze na biashara ya kawaida akakataa. (okay nisimuongelee sana maana sisi ni mawifi nisijeambiwa namchukia)
Back to their life, Hata mumewe akiwa na kazi maisha yao yote hawajawahi kusave hata 200k kwa mwezi sababu ya matumizi ya hovyo hovyo waliyonayo, yakiwakuta mzigo unarudi kwetu (mimi na mama) Hayo manyanyaso hadi marafiki wa bro wanampigia mama kumwambia kwanini umemuacha mtoto wako ananyanyaswa hivi na mkewe? Ohh huwa nafanya kila linalowezekana kwa uwezo wangu huyu kaka apate kazi au deals maana ndio namna pekee wanaweza kusurvive na angalau wakawa na amani. To my brother alioa slay queen form two failure anavuna alichopanda and he is too weak kumsimamia mkewe hana anachoweza kumwambia mkewe akasikilizwa.
Back to me, nimejifunza kuwa kama kweli unawapenda ndugu zako na kuwajali, ni habari mbaya sana kusikia wananyanyasika in the name of NDOA, bora mtu asiwe na ndoa kuliko kunyanyasika kwenye ndoa, Nimejipanga kuhakikisha nitamsaidia huyu "mtoto wa mtu" Kama yakimkuta (ambayo siyaombei), nitamsaidia tu kuongea na watu kumconnect kwa huyu na huyu, deal hili na lile, hata hivyo kujipanga mapema kusimamisha "chetu kikubwa" ukiachana na hivi vidogo vidogo vilivyopo.
I once saw my mama crying alivyoambiwa habari za mwanae, it was a bad feeling kwangu na inanitesa hadi leo hii. Mwenyezi Mungu awasimamie wanaume na awape mkate wao wa kila siku, tena hawa wanaume zetu wa kiafrica hawa, kipato kwao kimefanywa kama vazi, kama hawana wanaonwa uchi kabisa. Guys its sad.
Mleta mada pambana, ikishindikana akapambanie huko mbele ya safari, ukiondoka usipofanikiwa kurudi kwa habari ya watoto utakuja kuwaeleza na wataelewa hata wasiooelewa dhamira yako iko clean. Jitahidini kwa kadri muwezavyo kulinda afya ya akili zenu.
Sababu limeshatokea mimi nakushauri vumilia endelea kupambana.Kichwa cha habari kinahusika, kama mnavyojua ktk maisha kuna kupanda na kushuka Leo unacho kesho huna ndio kanuni ya maisha ilivyo.
Suala la ajira limekuwa Changamoto sn kwa dunia ya leo kwa jinsia zote mbele yaani wake kwa waume lkn inakuwa maradufu kwa upande wa kiume kwakuwa utamaduni wetu hasa wa kiafrika imezoeleka kwamba wanaume ndio watafutaji na ndio watunza familia.
Back to the topics, kufuatia sera mbovu za uchumi za mwenda zake watu wengi nikiwemo mie turifurushwa makazini na kupelekea ajira kuwa changamoto sasa basi mke wng ndio alichukua jukumu la kuendesha familia ili siku zisonge.
Sio kwamba Mimi nilibaki tu hom kumsubili wife alete hapana nilikuwa naingia kitaa na mm Ku hustle ili nisikae kindezi na kuonekana mpenda kitonga, lkn kama mnavyojua kitaani sio kwa mchezomchezo kitaa kigumu kinyama,
Kila deal unalojaribu linabuma, ingia kwenye umachinga na kitambulisho changu cha elfu20 napo hamna kitu, basi maisha yakawa ni tyt ile mbaya japo mtoto wa kiume nikawa najipa moyo kwamba 1day nitatoboa tu na life litakuwa normal.
Sasa turudi kwa upande wa mke wng at first my wife wangu alikuwa ndio comfort wng akinipa moyo kwamba yupo pamoja nami na ataweza kuhandle changamoto ninazopitia, kiukweli na Mimi ni shahidi wife ali play part yake kwa kiwango fulani, maji nilikuwa nawekewa bafuni, boksa nanunuliwa, mbususu nilikuwa naichakata kila ninapohitaji, na vitu vingine vingi siwezi kuweka vyote hapa ambavyo mtoto wa kiume alistahili kupata kutoka kwa mwanamke.
Sasa wajuba naona mambo yamebadilika sio kama zamani my wife wangu ame change to the extent nahisi atakuwa amenichoka na kuniona takataka mbele ya jamii,
Kwanza ile heshima kama mume ndani ya nyumba siioni tena, maji sikumbuki Mara ya mwisho kuweka ilikuwa lini, akirudi kutoka kazini ananikuta nipo sebleni nimeshika remote, kwanza hanisalimii atapitiliza moja kwa moja chumbani akija sebleni anachukuwa remote na kuweka kipindi anachotaka yeye na anapiga bit ole wake mtu abadilishe.
Kipindi chenyewe haangalii anenda zake jikoni huko tena ataanza kufoka mbona glass haijaoshwa, kijiko kipo chini, dirisha hujafunga, chakula mbona kimebaki kidogo mtoto wa kike anafoka na uso umemvimba utasema nyoka aina ya koboko amemeza simbilisi.
Kwakuwa hatuna house girl kazi zote nafanya mie ikiwemo kufua nguo zake, hadi za ndani nafua mie, kuna wkt nikifua nakuta vitone kwenye chupi najiuliza nn hiki lkn napotezea tu yy ndio kashika mpini mm sina vyangu, mbususu sipewi na nikipewa kwa masharti mpaka yy siku hiyo ajiskie, asipo jiskia miezi inaweza kukatika na usipewe harafu nikitaka kuchepuka nashindwa sijui kaniroga huyu.
Kwa kweli mambo ni mengi na visa ni vingi ukurasa huu hauwezi kutosha kuelezea, vijembe vimekuwa ndio wimbo wa Taifa siku akiwa nyumbani ,akiwa jikoni huko mm nipo sebleni anaongea na mwenzie kwenye simu, ........ningekuwa na uwezo ningemuoa mimi, mara utaskia lipolipo tu kama ling'ombe bora ng'ombe unapata maziwa na nyama, hujakaa vizuri utaskia yaani we na mista wako couple yenu nimeikubali sn huku wakicheka kicheko chao cha umbea,
Swali kwa wanaume wenzangu je mlitumia njia gani kwanza kuwa handle wanawake wa aina hii na mliwezaje kuhandle situation hii na baadae kuja kutoboa na heshima ikarudi kama zamani, angalizo kumpenda bado nampenda kwani tuna watoto na sitaki familia yangu isambaratike,
Nakaribisha ushauri mzuri tu mbaya baki nao.