Pole sana,huo ndo msalaba wako una budi kuubeba, pambana kupata kazi na kuomba Mungu akupatie riziki ya kila siku,kama we ni Mkristu usipite bila kutokusali sala ya Baba yetu...Huu ni ukweli mtupu hakika napita kwenye tanuri
Hata mm mwanzoni hali ilikuwa nzuri tu wife hakuwa na shida ila naona sasa mzigo umemuelemea na anataka kuutua ila kwa visaBinafsi niliwahi kupitia hiyo hali namuheshimu sana wife maana hakuwahi kuonyesha tofauti au kunidharau, alikua anamtumia hado bi mkubwa hela za matumizi kijijini na anamwambia kwamba mimi ndio nimempa atume, familia yangu haikuwahi kujua kwamba sina kazi maana wife aliendelea kuwasapoti, baada ya muda alichukua mkopo ofisini kwao akanipatia nikaanza biashara na mpaka sasa tumesimama
Jambo ambalo nilijifunza, baada ya mimi kusimama, ninajitahidi kufanya mahitaji yote kwenye familia ili wife apate kusave hela, maana kipindi nimekwamba wife alikua na akiba ya kutosha kwa sababu huko nyuma nilikua nafanya kila kitu hivyo nae akawa mjanja akaweka akiba ya hela ambayo ilitusaidia sana kipindi cha mpito
Nauzingatia ushauri wako mwambaAma hujui maana na mamlaka ya kuwa "mume" au hujui namna ya kuitumia mamlaka hiyo. Natamani ufanye study tour uje huku mtaani nikuoneshe mwanaume mwezetu mmoja hivi(jirani yangu na ni rafiki yangu pia) jinsi ambavyo yupo consistent na mamlaka yake licha ya kwamba ana changomoto kubwa sana ya kifedha kwa takribani mwaka sasa(mimi mwenyewe namdai). Lakini anasimama kwenye nafasi yake kama mume kana kwamba ana mihela Bill Gates akasome. Panapostahili kuonya anaonya na kukemea tena kwa mamlaka. Mahali pa kupongeza anapongeza safi kabisa. Panapohitaji kukemea anakemea kwa ukali hatari. Rafiki,umemuuzia mkeo mamlaka yako pasipo kujua na kwa bahati mbaya na yeye anajidanganya eti kwa vile anaprovide mahitaji ya kimwili kwenye familia basi ndio kashapata tiketi ya kupindua meza na kuitwaa mamlaka ya kuwa "kichwa cha familia".Kwa faida yako na wana JF kwa ujumla niwadokeze tu kwamba hakuna mwanamke anayefit kuwa kichwa wa familia haijalishi ni tajiri au ana hadhi au cheo gani kwenye jamii.Kuwa "kichwa cha familia" sio mchezo mchezo.Ni zaidi ya vyeo vyote katika dunia hii unavyovifahamu na usivyovijua pia. Kama unabisha muulize aliyetuumba atakupasha habari kiundani zaidi.
Sasa niende wp ndugu sio rahisi tu kusema ondoka hapo na hujui pa kuelekea,Kama inawezekana wewe ondoka hapo nenda mbali kaanze upya na ndio utafanya hata hizo kazi unazodai huwezifanyia around home. Mungu akikusaidia ukatoboa rudi atakupigia magoti huyo,kuendelea kukaa hapo unazidi kuharibu. Kama unapitia hayo kweli Mungu wa Israeli na skutanglie Ila nassitiza ondoka hapo.
Sio chai ni kweli tupu I'm in hellHata mimi nimehisi hii ni chai lakini nicomment hivyo hivyo kuongezea sukari
Usiseme hivyo mwambaMwambie akapambane zaidi we utafua hivyo vitone au madoa ya mabao ili akupatie mtaji ujichanganye kitaa huwezi kufanikiwa kwa kukaa sebleni anza ata kuuza matunda ya kukataa kwenye parcel town au bar flan acha na mambo ya kuona noma mkeo atafumuliwa marinda kwa kutafuta pesa ya kuwalishaView attachment 1973007
Kuna mambo ulipaswa kuyajua kabla hujaingia ndoani.Sio chai ni kweli tupu I'm in hell
Yaani msalaba uko begani na ninakaribia kwenda chiniPole sana,huo ndo msalaba wako una budi kuubeba, pambana kupata kazi na kuomba Mungu akupatie riziki ya kila siku,kama we ni Mkristu usipite bila kutokusali sala ya Baba yetu...
Sent from my TECNO B1g using JamiiForums mobile app
Nashukuru kwa ushauriMwanamke mkilingana kipato anakudharau kiaina bila wewe kugundua, kama huna kabisa ndio atakukalia kichwa ni na kuvunjilia mbali ile amri ya Mungu kuwa mwanaume ni kichwa cha nyumba. Pole ndugu yangu, ukombozi wako ni kutafuta kazi yoyote ili mradi mkono uende kinywani.
Kama yapiKuna mambo ulipaswa kuyajua kabla hujaingia ndoani.
Mfano,Kujua kwa nini uliumbwa "mwanaume"Kama yapi
Inategemea na unavyojiweka. Maisha ni mwandiko unaandika wengine wanakusoma.Mwanamke mkilingana kipato anakudharau kiaina bila wewe kugundua, kama huna kabisa ndio atakukalia kichwa ni na kuvunjilia mbali ile amri ya Mungu kuwa mwanaume ni kichwa cha nyumba. Pole ndugu yangu, ukombozi wako ni kutafuta kazi yoyote ili mradi mkono uende kinywani.
watatesekaje wakati we upo tu hapo umkalisha pu****u na mama yao anawalisha vizuri tu hawateseki we sepa zako ili mkeo apate nafasi ya kuwalea bila kuwa na kinyongo na uwepo wa mtu kama wewe usiye na maamuziTuna watoto na ukisema nisepe watoto watateseka, kuna kipindi nilifikiria kusepa lkn lilipokuja suala la watoto ikabidi niwe mpole. Napitia kipindi kigumu sn
Sent from my HUAWEI LUA-U22 using JamiiForums mobile app
Pole mkuu.. "Ukitaka kuchepuka hauwezi", hajakuloga mkuu, ni vile tu kwasasa huna nguvu za kiume aka mpunga.. Jambo la kheri ni kwamba muda ni suluhisho la kudumu, jipe muda kidogo mambo yatakaa sawa!Kichwa cha habari kinahusika, kama mnavyojua ktk maisha kuna kupanda na kushuka Leo unacho kesho huna ndio kanuni ya maisha ilivyo.
Suala la ajira limekuwa Changamoto sn kwa dunia ya leo kwa jinsia zote mbele yaani wake kwa waume lkn inakuwa maradufu kwa upande wa kiume kwakuwa utamaduni wetu hasa wa kiafrika imezoeleka kwamba wanaume ndio watafutaji na ndio watunza familia.
Back to the topics, kufuatia sera mbovu za uchumi za mwenda zake watu wengi nikiwemo mie turifurushwa makazini na kupelekea ajira kuwa changamoto sasa basi mke wng ndio alichukua jukumu la kuendesha familia ili siku zisonge.
Sio kwamba Mimi nilibaki tu hom kumsubili wife alete hapana nilikuwa naingia kitaa na mm Ku hustle ili nisikae kindezi na kuonekana mpenda kitonga, lkn kama mnavyojua kitaani sio kwa mchezomchezo kitaa kigumu kinyama,
Kila deal unalojaribu linabuma, ingia kwenye umachinga na kitambulisho changu cha elfu20 napo hamna kitu, basi maisha yakawa ni tyt ile mbaya japo mtoto wa kiume nikawa najipa moyo kwamba 1day nitatoboa tu na life litakuwa normal.
Sasa turudi kwa upande wa mke wng at first my wife wangu alikuwa ndio comfort wng akinipa moyo kwamba yupo pamoja nami na ataweza kuhandle changamoto ninazopitia, kiukweli na Mimi ni shahidi wife ali play part yake kwa kiwango fulani, maji nilikuwa nawekewa bafuni, boksa nanunuliwa, mbususu nilikuwa naichakata kila ninapohitaji, na vitu vingine vingi siwezi kuweka vyote hapa ambavyo mtoto wa kiume alistahili kupata kutoka kwa mwanamke.
Sasa wajuba naona mambo yamebadilika sio kama zamani my wife wangu ame change to the extent nahisi atakuwa amenichoka na kuniona takataka mbele ya jamii,
Kwanza ile heshima kama mume ndani ya nyumba siioni tena, maji sikumbuki Mara ya mwisho kuweka ilikuwa lini, akirudi kutoka kazini ananikuta nipo sebleni nimeshika remote, kwanza hanisalimii atapitiliza moja kwa moja chumbani akija sebleni anachukuwa remote na kuweka kipindi anachotaka yeye na anapiga bit ole wake mtu abadilishe.
Kipindi chenyewe haangalii anenda zake jikoni huko tena ataanza kufoka mbona glass haijaoshwa, kijiko kipo chini, dirisha hujafunga, chakula mbona kimebaki kidogo mtoto wa kike anafoka na uso umemvimba utasema nyoka aina ya koboko amemeza simbilisi.
Kwakuwa hatuna house girl kazi zote nafanya mie ikiwemo kufua nguo zake, hadi za ndani nafua mie, kuna wkt nikifua nakuta vitone kwenye chupi najiuliza nn hiki lkn napotezea tu yy ndio kashika mpini mm sina vyangu, mbususu sipewi na nikipewa kwa masharti mpaka yy siku hiyo ajiskie, asipo jiskia miezi inaweza kukatika na usipewe harafu nikitaka kuchepuka nashindwa sijui kaniroga huyu.
Kwa kweli mambo ni mengi na visa ni vingi ukurasa huu hauwezi kutosha kuelezea, vijembe vimekuwa ndio wimbo wa Taifa siku akiwa nyumbani ,akiwa jikoni huko mm nipo sebleni anaongea na mwenzie kwenye simu, ........ningekuwa na uwezo ningemuoa mimi, mara utaskia lipolipo tu kama ling'ombe bora ng'ombe unapata maziwa na nyama, hujakaa vizuri utaskia yaani we na mista wako couple yenu nimeikubali sn huku wakicheka kicheko chao cha umbea,
Swali kwa wanaume wenzangu je mlitumia njia gani kwanza kuwa handle wanawake wa aina hii na mliwezaje kuhandle situation hii na baadae kuja kutoboa na heshima ikarudi kama zamani, angalizo kumpenda bado nampenda kwani tuna watoto na sitaki familia yangu isambaratike,
Nakaribisha ushauri mzuri tu mbaya baki nao.
Kwanini unamsema? Me numemuelewa kuwa baada ya kuachishwa kazi akaendelea kupambana kadiri ya uwezo wake, lkn mambo bado hayajakaa sawa.. Sijaona kama amekaa tu na kumbweteka "mbweta"πππwatatesekaje wakati we upo tu hapo umkalisha pu****u na mama yao anawalisha vizuri tu hawateseki we sepa zako ili mkeo apate nafasi ya kuwalea bila kuwa na kinyongo na uwepo wa mtu kama wewe usiye na maamuzi
Kuna mambo umeyachukulia juu juu.Nimecheka hapo ulipoeleza kwamba unakuta vitone kwenye nguo zake za ndani unapofua(nisamehe kwa kucheka)!Nimewaza mbali na mengi.
Hata hivyo,kwa sababu umeamua kuvumilia,ni vema ukatafuta kazi yako ya kujiajiri.Mimi ningeweza;
1-Udobi.Nina uwezo mkubwa wa kufua na kunyoosha nguo aina kwa aina.Hebu na weye jaribu.
2-Ufundi/urekebishaji/Ushonaji wa viatu.Utundu wa kushona(marekebisho)viatu nilijifunza tangu darasa la kwanza.Haiihitaji mtaji mkubwa.Nyuzi,sindano na vigozi vya kuunganishia palipoharibika au kuchanika.
3-Kusafisha na kung'arisha viatu.Kama upo katika mji mkubwa,usione soo!Hizi ni shughuli tumeanza kuzifanya tangu utotoni.Unasafisha raba,viatu vya ngozi na "ku-brush" vingae kwa kiwi.
NB:Hizo ni shughuli zisizohitaji mtaji mkubwa.Jaribu upate mahitaji yako ya kawaida.Kama ulizoea "ubossboss" unakwama.