Kwa wanaume ambao mlikuwa na kazi lakini sasa hamna na wake zenu ndio wanaoendesha familia mliwezaje kutoboa?

Kwa wanaume ambao mlikuwa na kazi lakini sasa hamna na wake zenu ndio wanaoendesha familia mliwezaje kutoboa?

Ushauri wako nauzingatia sema watoto watabaki wanapata tabu
Watoto ni wenu na mwanamke wako hawezi kuwa na tatizo na watoto hao sababu anajimudu! Atawalea vizuri tu wala usiwe na hofu.

Ana tatizo na wewe unaekula hela yake tu kama mtoto mdogo bila kujali kuwa wakati una kazi uliweza simamia majukumu yako vizuri tu. Yani anaumia wewe kutumia hela yake tu hilo ndio analomaindisha.
 
Kama kuna kitu cha thamani hapo nyumbani uza halafu pesa yote peleka sadaka kwenye kanisa la ufufuo na uzima kwa mzee wetu Gwajiboy halafu baada ya wiki uje hapa utoe ushuda jinsi ulivyofurumushwa home na my wife wako.
Dah, hunitakii mema ww
 
Point, pesa ndio rafiki number moja kwa mwanaume, kosa hiyo pesa then sikilizia huyo mke aliyekuwa anajinasibu kukupenda vile atakuwa anakufanyia.

Tujitahidi kuzitafuta lakini tuombe Mungu tusipigike maana kuwa bankrupt ni zaidi ya kupata ugonjwa.
Yaani napitia kipindi kigumu sn
 
Son, vita haitaisha km utaendelea na lifestyle yako ya sasa ya kukaa nyumbani bila kujishughulisha....

Ushauri
_______

1.Pesa ipo, nyingi , kila sehemu ...unblock your mindset
2. Ajira sio kila kitu, kwa sasa hazipo kabisa, chache zilizopo zinahitaji connection ya hali ya juu sana, probability ya wewe kuzipata kwa haraka ni 0.
3.sijui mkoa uliopo, lakini km upo Daresalaam hama mara moja, fursa zimejifunga kwa 99% hapo..... jaribu Mbeya, Iringa , Mwanza Arusha...au sehemu yoyote wasiokujua" fanya shughuli yoyote ndogo ya kukuingizia kipato kuweza kuishi huku macho yakiwa yanaendelea ku-search fursa kubwa.

Hitimisho
_________
Wanawake ni viumbe visivyotabirika, kwa sasa ameanza kukuona km takataka kwani you don't provide anything to the family...ukiendelea kubaki hapo bila kujishughulisha na shughuli ya maana ya kuleta at least chakula nyumbani .....(kuna bomu kubwa linakuja ) pin those few words on brackets .
Nitaufanyia kazi ushauri ndugu yangu
 
kwa moja chumbani akija sebleni anachukuwa remote na kuweka kipindi anachotaka yeye na anapiga bit ole wake mtu abadilishe.





[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]and yet unajihesabu ni kidume.

So umeuza uanaume wako kwa kuhofia Ukizengua tu..UNAACHWA [emoji23][emoji23][emoji23]
Sa kosa langu kukaa sebleni ndugu, kwa hiyo ulitaka akija anikute chooni
 
Hii statement ya kuwaambia watu watafute pesa imekuwa too much humu jamvini. Kwani nani hatafuti pesa hadi aambiwe kuwa tafuta pesa? Muache huu uhuni.
Kiukweli waache uhuni, huku mikoani kila mtu anachakarika labda huko Dar.
 
Kwahiyo unataka kusema visa vitaongezeka zaidi ya hapa as long as sina mkwanja, ila jua hii sio chai ni kweli nayapitia, tena kuna siku alirudi usiku sana alidai kuwa alikuwa kwenye kikao cha harusi lkn hakuniaga kama alikwenda kwenye kikao cha harusi,

Alirudi mida mibaya ikanibidi nimsubirie kumfungulia mlango, yy sio mnywaji wa pombe lkn niliskia harufu ya pombe kutoka kinywa chake, nilipojaribu kuhoji hakunijbu alijitupa tu kitandani na kwanza kukoroma

Sent from my HUAWEI LUA-U22 using JamiiForums mobile app
Si muda mrefu utaletewa zawafi ya VVU endelea kumpenda tu.
 
Pole mtoa mada.
Wengi walioachishwa kazi huwa wanapitia changamoto kama zako toka kwa wake zao.

Kwenye maelezo yako ya awali inaonyesha ulipoachishwa kazi mkeo alianza kwa kukusaidia - (Hapo alifanya vizuri na hicho ndio kilikuwa ni kipimo tosha kuwa umeoa mke au galasa - (Maisha ya Ndoa lazima yapitie vipindi vya Shida na Raha)

Kwa tabia anazokuonyesha sasa ni dhahiri alikuvumilia kwa lengo la kukuona unachacharika kutafuta kazi. Kitendo cha wewe kukosa kazi ndicho kilichomchosha. Kumbuka asili ya mwanamke wao wamezoea kupokea sio kutoa. Wanawake galasa ndio wapo hivyo hata kama kazi na kipato alichonacho kilitokana na mchango wako.

Suluhisho ni wewe kuvumilia hizo kero kwa muda na kupambana kutafuta shughuli ya kukuingizia kipato.

Sumu kubwa kwa mkeo ni pale atapofikia wakati wa kukuonyesha wazi kuwa anachepuka na mtu mwingine.

Wanaume wakipitia changamoto za hivi halafu wakija kupata kazi, Ndoa zao huwa zitakufa Maana kumbukumbu mbaya huwa hazitoki kichwani na kupelekea mahusiano yenu kufikia tamati.
 
Tafuta majiko 2, eneo lenye mkusanyiko wa watu, kijiwe cha boda boda au junction yeyote uchome mishikaki na mahindi,

Unaweza kuanza na kimoja kwanza then unafatia kingine,
Elfu kumi kumi hizi kama faida kwa siku ni kitu cha kawaida,
Kwa mwezi laki 3 na zaidi inatosha kabisa kurudisha heshima hapo kwako.


Kama unaogopa dharau kwa majirani endelea kubaki hapo home kama beki tatu.
Nashukuru kwa ushauri
 
Ushauri wako nauzingatia sema watoto watabaki wanapata tabu
Tabu ipi wakati huna mchango?
Tafuta gheto wala usimuage kaa huko fanya mishe zako, kama atakuja kukutafuta nenda kamsalimie kisha rudi gheto kwako jitegemee, tafuta vyako, kula vyako, vaa vyako mbona unakuwa bwege!
Mwanamke hamjazaliwa tumbo moja mwache na mambo yake awe huru wewe katafute pesa kwa ajili ya watoto wako kwenda shule.
Nyie wanaume msoo na michepuko mnakuwaga mafala sana, mnapelekeshwa atakuletea bwana ndani ndio uisome namba.
 
Na hela ya kununulia kifurushi cha internet ili huweze kuingia jamii forum si amekununulia yeye, acha majungu kumsemea mbovu mke wako anayekulisha na kukuvisha, inaonekana umekaa kindezi ndezi sana, mtoto wakiume pambana acha ubwege.
Hela ya bando hawezi kunipa yy huwa sometimes najishughulisha hapa na pale lkn nachopata ni kidogo kulinganisha na chake na ndio hela ya bando napatia huko
 
Watoto ni wenu na mwanamke wako hawezi kuwa na tatizo na watoto hao sababu anajimudu! Atawalea vizuri tu wala usiwe na hofu.

Ana tatizo na wewe unaekula hela yake tu kama mtoto mdogo bila kujali kuwa wakati una kazi uliweza simamia majukumu yako vizuri tu. Yani anaumia wewe kutumia hela yake tu hilo ndio analomaindisha.
Kama nilivyosema hatuna bek3 na yy anashinda job ana ni treat as if me ndio bek3 wake
 
Back
Top Bottom