Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Unapatkana wap?
Hongera Dada!! Nitakutafuta hasa kwa ajili ya sun protection
Mi nipo hapa chalinze, pwani, ila hua naenda sana dar. Ni sh ngapi kwa bei ya k/koo?
gari ni gamet! na lini mnaweza kunitumia? na nitauziwa kwa bei hiyo hiyo au?
gari ni gamet! na lini mnaweza kunitumia? na nitauziwa kwa bei hiyo hiyo au?
Samahani kwa kuuliza, vipeperushi mnavyo vya kutosha au agent anafanya ubunifu?
Zainab usije tu ukawa unaacha mahandaki kwenye upande mmoja wa Tanzania kwa kusomba udongo........:lol:
Hamna agent upande wa Kinondoni na Msasani?
Kwa sasa upo Sinza kwa Remy pale Loliondo uliza Mwajuma wa Loya, atakupatia. Kariakoo unapatikana Saloon ya Bi Saira mtaa wa Nyamwezi na Twiga.
Lakini tunajitahidi kupata mawakala kila sehemu, na ikiwa utalipia gharama za usafiri tutakuletea popote ulipo.
Piga simu 0769302206
Naupataje mwanza???naweza kuchanganya na liwa maana huu nnaotumia now nilikuwa nachanganya na liwa ni wa kimasai
Huu wetu tunashauri usichanganye na kitu mwanzoni, kwa majaribio yetu unafanya kazi vizuri kuliko liwa na tofauti sana na ule wa kimasai.
Jaribu hivi hivi kisha utatueleza.
Mwanza tunategemea utakuwepo huko baada ya siku mbili au tatu. Tutakujulisha wapi pakuupata.