Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

Ila wewe bwana wenzio kitonga cha asubuhi kimetugomea ila ndio huachi kukitaja ili tuumie roho au..?

Katoto hakajali hisia zetu[emoji1787][emoji1787]
Yan kile cha mb 300 kinavyosumbua, natamanig nibamize simu
 
Hiyo ni drama gani? Nimependa ulivyoelezea kifupi inaonesha ni kali
 
Variety show.

Bros on Foot

Humu wana challenges mbali mbali ila ikifika kwenye kupika nimeona kuna tofauti ya mapishi ya wanawake wa kikorea na akina oppas and ahjussi.

akina ahjussi wanapika kisafi yaani kuonja mara chache tena kwa kijiko tofauti,kuja kwa akina ahjumma ,ahjumooon hawa wamama ni shida wanaonja kwa mdomo kwenye mwiko huo huo na kuurudisha jikoni
 
[emoji3][emoji3][emoji3] hadi wazee wa taste mmeikubali, ina upekee gani kwani mbona mimi naona kawaida tu. Naona vibe lilelile la What's wrong with secretary Kim, business proposal and the like...
Hii ina utofauti sana tena secretary kim inaweza pigwa chini kwa uzuri
 
Hatimae nimeikamilisha drama ya The Merchant Gaekju.
Kwangu mimi Jang Hyuk ni gwiji. Amelionesha hilo si tu kwenye drama bali hata kwenye Single film hakuna alocheza mbovu.

Hii drama kuna mafunzo 2 makuu nimepata
1. Watu ni nguvu, ukiwa na support kubwa ya watu, wanaweza kukupa kitu moja kati ya viwili 2 au vyote; utajir ama nguvu ambayo automatically nguvu hiyo yaweza kufanya ulete mabadiliko ya kisera, kimfumo, na hata kisheria. Chun Bong Sum( Jang hyuk) aliweza kupambana na mfumo ukiritimba ulokuwepo katika sekta ya biashara na aliweza kuwa na support ya zaidi ya watu 200k kwa miaka hiyo ni idadi kubwa mno. Kama sensa ya kwanza ilofanyika Nchini kwetu huku ambako tunapenda mambo ya ..... tulikuwa milion 12. Waza Joseon walikuwa wangapi? Maana Korea, Japan sasa kuna kampeni za kuhamasisha watu wazaliane. Tena Japan hali ndio mbaya kabisa maana kuna siku nilikuwa naangalia Makala ya EAST 101 ya Al Jazeera hii ni documentary kuhusiana na Nchi za Asia Mashariki. Wajapan walikuwa wanahojiwa karibia kila mtu yuko busy na mambo ya maendeleo kwahiyo muda wa kufanya mapenzi hawana. Anyway unaweza kuona kiasi gani Bw. CHUN BONG SUM alivyokuwa na Power na aliweza kubadili hali yote.

2. Nimejifunza pia maono uliyonayo ni kitu unachofaa kukishika kwq moyo wako wote, akili na roho yako yote. Haijalishi ni vikwaZo gani utakutana navyo badala yake changamoto hiyo zigeuze kuwa fursa au kuwa darasa. Kwnaj hukumbuki kuwa Risk si threat peke yake ni opportunity pia. Chun Bong Sum alipitia Mazito lakini hakuweza kukata tamaa.
Sasa kituo kifuatacho ndio bado nawaza, maana historical drama za vijana wa siku hizi zinaboa, wanaurembo mwingi mno. Ndio maana naangalia drama kurudi miaka ya nyuma. Kama ni drama mpya basi wawe wamecheza magwiji.
 
[emoji3][emoji3][emoji3] hadi wazee wa taste mmeikubali, ina upekee gani kwani mbona mimi naona kawaida tu. Naona vibe lilelile la What's wrong with secretary Kim, business proposal and the like...
Eti "wazee wa taste" 😂
 

Mimi dating show zimeniteka hata silali nikilala naziota [emoji26]

Nimetoka kuichek love catcher in bali, humu wengi wanafanana na celebrities ingawa wakaka sio wakal sanaaa
 
Basi io celebrity ilikua inanitia uvivu kutazama ep 1 nimeitaza karib siku tatu tofauti leo nimefanikiwa kufika mwisho wa ep 1

Now am hooked, kujua kumbe kuna kastori behind and na take some notes ya kua influencer[emoji1488]

Nimejikuta napiga ep 3 chap chap hapa inanipa mawazo nifike niendelee.
 
Huko nimezipumzisha kwa muda nipo na hizi wanazohangaika kukamilisha mission kuna hii the backpacker chef ni mwendo wa kupika tu. Watu wanne wanapewa mission kali kali za kupikia wateja mbali mbali mfano wanajeshi,wacheza soka,wale ahjummas wanaozama baharini etc unakuta wanapika msosi hadi wa watu 400 kwa masaa manne tu
Mimi dating show zimeniteka hata silali nikilala naziota [emoji26]

Nimetoka kuichek love catcher in bali, humu wengi wanafanana na celebrities ingawa wakaka sio wakal sanaaa
 
Kule nkiri niliiona hio na nyingine the fabulous inahusu masuala ya mitindo daah sijaipenda kuna jamaa kaigiza kwenye bora debora (true to love)kama mmiliki wa mgahawa na mume wa shosti wa bora,humu kwenye fabulous kaigiza kama designer shoga anavojirendemsha sasa hadi huruma.
 
Celebrity ni nzuri kati ya favourite character wangu ni Oh Min Hye(Jun Hyo Seong) llicha ya hateful character yake.

Baada ya kujua alikuwa ni K-Pop Idol hapo nyuma nikafall zaidi
 

Eeh hiyo hatari ntaitafuta

Hivi ile ya seun gi mpya ambayo watafanyia dubai sijui ishaanza? Nimeisahau jina sijui travela au nin
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…