Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

Wakuu huu uzi umepoa sana sikuizi no update, no information about ongoing and unreleased projects, what's the problem?

Au bando kupanda ndo sababu ??
 
Wakuu huu uzi umepoa sana sikuizi no update, no information about ongoing and unreleased projects, what's the problem?

Au bando kupanda ndo sababu ??
[emoji23][emoji23][emoji23] sema huenda ubize ila updates zipo za kutosha tumetoka kutazama The King's Affection Episode ya 16 hapa huku narukia Idol The Coup maana mimi ni fanboy sana
 
mwanzoni nilikua naangalia drama za wakorea kwa kununua CD zilizotafsiriwa kwa kiswahili, baada ya kuifahamu JF hususani thread hii mwishoni mwaka 2015 ndipo nilipoanza kuifahamu kiundani zaidi sanaa ya wakorea.
  1. nilianza kupakua drama mwenyewe kupitia msaada wa members niliowakuta
  2. nikaanza kufuatilia drama zinazoendelea , mwanzoni sikuwa nafahamu chochote juu ya hili (nilijua drama zote hutolewa completed)
  3. nikawafahamu na wasanii kwa kufuatilia profiles zao,
  4. nikazifahamu modern drama kiundani na historical kiundani.
kilichofuata kimebaki kuwa ni historia isiyofutika, kuna siku nilipatwa na uraibu wa kufuta kila comment niliyoiandika humu na nakumbuka nilianza page no 34 mpaka page no 100 au 200 (nimeshasahau), nilifikiri kufuta kwangu comments inaweza kuwa njia moja wapo ya kuufuta huu uraibu wa kuishi humu muda mrefu (nilitaka nionekane kijana), aigoooo kumbe nilikuwa najipumbaza,

kila niliyemkuta alikuwa anakimbia kama mbio za baiskeli (wengine wanarudi, baadae wanakimbia zaidi)
maisha yangu ya kuangalia wakorea yaliendelea na kuendelea bila ya kujali wengineo,
pakutoa mawazo sikuwa mvivu kutoa mawazo yangu,
pakutoa msaada sikuwa mvivu kutoa msaada iwe ndani ya thread au nje (msaada si lazima wa mali au fedha),
pakuzingua, kukera, kutukana, kudhihaki nilifanya hivyo (leo naomba radhi kwa kila niliyemkosea)
yote nilifanya kwa lengo moja tu la kuikuza hii familia inayotuunganisha bila ya kujali itikadi zetu.
========================

mwishoni mwa mwezi oktoba 2020 nikiwa home nimetulia na kicomputer changu nafuatilia taarifa mbali mbali zinazohusu zaidi taifa letu hususani zanzibar (tulikuwa kwenye uchaguzi bila ya internet imara) nilipatwa na janga la kuungua kwa computer yangu, lilikuwa ni pigo kubwa sana kwa sababu ndio kifaa ninachokitegemea majukumu yangu (sipendi kabisa kutumia simu) , hali ilipotulia baada ya vurumai za uchaguzi nilikwenda kwa fundi lakini aliniambia hii mashine itabidi uivalishe motherbord nyengine.

kuungua kwa computer ndio sababu kuu ilionifanya niache kuapload drama kule telegram (wala hapakuwepo na sababu nyengine) na hata ule ujumbe niliandika kwa kutumia computer ya rafiki anayeishi mbali nami (sikutaka kuwakimbia wale watu bila ya taarifa).

baadae nikanunua computer nyengine lakini sikurudi tena telegram japokuwa nilitamani kufanya hivyo (kipindi kile Nifah hakuwa akionekana sana humu JF niliona hata ugumu kumshitua aniunge tena).

Tarehe kama ile ya mwezi Oktoba 2021 nimepatwa na janga linalofanana kabisa na lile lililotokezea mwaka 2020 hatimaye nikabaki najiuliza
hili jambo limetokezea kibahati mbaya au ni majaaliwa?

Mimi nimeichagua sababu ya pili (majaaliwa), pengine ni ujumbe maalumu unaonitaka nibadili mfumo wangu wa maisha
teh teh teh.

Nikaianza rasmi safari ya kuangalia korean drama kwa kutumia simu(tablet), nakumbuka nilikuwa naangalia jirisan drama (nilifika episode 3) na kings affection drama (nilifika episode 6).

ilipofika tarehe 1 November, bila ya kushinikizwa na mtu niliamua kubadili muelekeo wangu wa maisha kwa kuanzia hapa kwa wakorea. Haijawahi kutokezea maishani mwangu tokea niifahamu thread hii kupumzika japo wiki moja bila ya kuangalia korean drama lakini leo nimetimiza mwezi mmoja bila ya kufanya hivyo.
Namshukuru Maulana kwa hilo.

kwa jambo ulilokwishalizoea kulifanya kwa miaka 8 si rahisi hata kidogo kuliacha lakini yote yamewezekana kwa sababu ya kuweka kwangu dhamira iliojaa umadhubuti ndani yake (japokuwa nakutana na dhoruba za mvua, upepo na kiangazi).

Dae nauanza mwezi wa pili hapo kesho, nitakapouvuka mwezi huu wa December sijui nijipongeze kwa jambo gani kubwa nililo na uwezo nalo kulitenda.
sijui nikaogelee kwenye mkondo wa Nungwi (nilisikia watu wembamba hawazami).

Mac Alpho , mimi nipo kimya kwa sababu hiyo sijui wenzangu.
Nategemea ukimya huu utaendelea kutoka kwangu,
kwa hilo naomba unisamehe.
============

huu wimbo haumuhusu yeyote yule



ANYEOng

Wakati naandika ile comment sikutaka kumlenga mtu moja kwa moja, ila kiuhalisia nilimaanisha wewe mkuu kwasababu umekuwa mzito sana kuonekana humu ilihali kule kwenye jukwaa la MAN UTD nakuona sana, kwahiyo nikawa najiuliza kulikoni?


Natumia kuwa umeamua kupumzika tu, ila swala la kuuacha huu ulimwengu moja kwa moja sidhani, anyway pamoja na yote uliyosema unapopata update zozote usisite kututembelea huku.
 
mwanzoni nilikua naangalia drama za wakorea kwa kununua CD zilizotafsiriwa kwa kiswahili, baada ya kuifahamu JF hususani thread hii mwishoni mwaka 2015 ndipo nilipoanza kuifahamu kiundani zaidi sanaa ya wakorea.
  1. nilianza kupakua drama mwenyewe kupitia msaada wa members niliowakuta
  2. nikaanza kufuatilia drama zinazoendelea , mwanzoni sikuwa nafahamu chochote juu ya hili (nilijua drama zote hutolewa completed)
  3. nikawafahamu na wasanii kwa kufuatilia profiles zao,
  4. nikazifahamu modern drama kiundani na historical kiundani.
kilichofuata kimebaki kuwa ni historia isiyofutika, kuna siku nilipatwa na uraibu wa kufuta kila comment niliyoiandika humu na nakumbuka nilianza page no 34 mpaka page no 100 au 200 (nimeshasahau), nilifikiri kufuta kwangu comments inaweza kuwa njia moja wapo ya kuufuta huu uraibu wa kuishi humu muda mrefu (nilitaka nionekane kijana), aigoooo kumbe nilikuwa najipumbaza,

kila niliyemkuta alikuwa anakimbia kama mbio za baiskeli (wengine wanarudi, baadae wanakimbia zaidi)
maisha yangu ya kuangalia wakorea yaliendelea na kuendelea bila ya kujali wengineo,
pakutoa mawazo sikuwa mvivu kutoa mawazo yangu,
pakutoa msaada sikuwa mvivu kutoa msaada iwe ndani ya thread au nje (msaada si lazima wa mali au fedha),
pakuzingua, kukera, kutukana, kudhihaki nilifanya hivyo (leo naomba radhi kwa kila niliyemkosea)
yote nilifanya kwa lengo moja tu la kuikuza hii familia inayotuunganisha bila ya kujali itikadi zetu.
========================

mwishoni mwa mwezi oktoba 2020 nikiwa home nimetulia na kicomputer changu nafuatilia taarifa mbali mbali zinazohusu zaidi taifa letu hususani zanzibar (tulikuwa kwenye uchaguzi bila ya internet imara) nilipatwa na janga la kuungua kwa computer yangu, lilikuwa ni pigo kubwa sana kwa sababu ndio kifaa ninachokitegemea majukumu yangu (sipendi kabisa kutumia simu) , hali ilipotulia baada ya vurumai za uchaguzi nilikwenda kwa fundi lakini aliniambia hii mashine itabidi uivalishe motherbord nyengine.

kuungua kwa computer ndio sababu kuu ilionifanya niache kuapload drama kule telegram (wala hapakuwepo na sababu nyengine) na hata ule ujumbe niliandika kwa kutumia computer ya rafiki anayeishi mbali nami (sikutaka kuwakimbia wale watu bila ya taarifa).

baadae nikanunua computer nyengine lakini sikurudi tena telegram japokuwa nilitamani kufanya hivyo (kipindi kile Nifah hakuwa akionekana sana humu JF niliona hata ugumu kumshitua aniunge tena).

Tarehe kama ile ya mwezi Oktoba 2021 nimepatwa na janga linalofanana kabisa na lile lililotokezea mwaka 2020 hatimaye nikabaki najiuliza
hili jambo limetokezea kibahati mbaya au ni majaaliwa?

Mimi nimeichagua sababu ya pili (majaaliwa), pengine ni ujumbe maalumu unaonitaka nibadili mfumo wangu wa maisha
teh teh teh.

Nikaianza rasmi safari ya kuangalia korean drama kwa kutumia simu(tablet), nakumbuka nilikuwa naangalia jirisan drama (nilifika episode 3) na kings affection drama (nilifika episode 6).

ilipofika tarehe 1 November, bila ya kushinikizwa na mtu niliamua kubadili muelekeo wangu wa maisha kwa kuanzia hapa kwa wakorea. Haijawahi kutokezea maishani mwangu tokea niifahamu thread hii kupumzika japo wiki moja bila ya kuangalia korean drama lakini leo nimetimiza mwezi mmoja bila ya kufanya hivyo.
Namshukuru Maulana kwa hilo.

kwa jambo ulilokwishalizoea kulifanya kwa miaka 8 si rahisi hata kidogo kuliacha lakini yote yamewezekana kwa sababu ya kuweka kwangu dhamira iliojaa umadhubuti ndani yake (japokuwa nakutana na dhoruba za mvua, upepo na kiangazi).

Dae nauanza mwezi wa pili hapo kesho, nitakapouvuka mwezi huu wa December sijui nijipongeze kwa jambo gani kubwa nililo na uwezo nalo kulitenda.
sijui nikaogelee kwenye mkondo wa Nungwi (nilisikia watu wembamba hawazami).

Mac Alpho , mimi nipo kimya kwa sababu hiyo sijui wenzangu.
Nategemea ukimya huu utaendelea kutoka kwangu,
kwa hilo naomba unisamehe.
============

huu wimbo haumuhusu yeyote yule



ANYEOng
Utarudi tu. Samahani lakini kama komenti yangu ni ya kukatisha tamaa.... mimi kuna wakati huwa napitisha hata mwaka bila kufuatilia wakorea ingawa lengo langu Mimi huwa ni kupumzika tu kulingana na mambo nayokuwa nayo kwa wakati huo. Cha kureplace kdrama sijaona bado maana wengine pombe hatunywi, hatuendi klabu, hatuna ma- baby kwa hiyo starehe yangu pekee ni hi na usingizi[emoji1787][emoji1787][emoji1787] naombeni niachweee nitaangalia kdrama hadi nitakapoona mwenyewe moyo wangu hautaki ila si kwa kujilazimisha kuacha
 
Utarudi tu. Samahani lakini kama komenti yangu ni ya kukatisha tamaa.... mimi kuna wakati huwa napitisha hata mwaka bila kufuatilia wakorea ingawa lengo langu Mimi huwa ni kupumzika tu kulingana na mambo nayokuwa nayo kwa wakati huo. Cha kureplace kdrama sijaona bado maana wengine pombe hatunywi, hatuendi klabu, hatuna ma- baby kwa hiyo starehe yangu pekee ni hi na usingizi[emoji1787][emoji1787][emoji1787] naombeni niachweee nitaangalia kdrama hadi nitakapoona mwenyewe moyo wangu hautaki ila si kwa kujilazimisha kuacha
Yeah ni kweli kama baada ya kazi huna burudani nyingine kama pombe n.k basi drama ndio mahala pake.Ila dah Wakorea sio watu wazuri aisee[emoji23][emoji23]
 
Utarudi tu. Samahani lakini kama komenti yangu ni ya kukatisha tamaa.... mimi kuna wakati huwa napitisha hata mwaka bila kufuatilia wakorea ingawa lengo langu Mimi huwa ni kupumzika tu kulingana na mambo nayokuwa nayo kwa wakati huo. Cha kureplace kdrama sijaona bado maana wengine pombe hatunywi, hatuendi klabu, hatuna ma- baby kwa hiyo starehe yangu pekee ni hi na usingizi[emoji1787][emoji1787][emoji1787] naombeni niachweee nitaangalia kdrama hadi nitakapoona mwenyewe moyo wangu hautaki ila si kwa kujilazimisha kuacha
Khantwe nimefurahi kusikia hauna baby so nakuomba niwe baby wako nikuliwaze na nikufariji kipindi Cha uzuni na karaha nafikiri ukinipa moyo wako kwangu nitakusaidia kwa namna fulani kupunguza ugonjwa wa Korean drama
 
Chimera naikubali Sana ila yule dada alikuwa adopt huko marekani nimevutiwa nae Sana anajua kuigiza kingine zaidi ni pisi Kali ile mbaya
Unavyonambia Kam ni shoga yangu Yule kwamba naweza kukuunganisha[emoji23]

Naitizama kivivu story yake imeanza kama mouse au Awaken, Ila ntaendelea nayo tu. Nimemaliza ep ya pili
 
Back
Top Bottom