Kwa wazazi na walezi: Mada maalum ya watoto

Kwa wazazi na walezi: Mada maalum ya watoto

Mmh sijawahi kusikia hii kitu anaweza kuwa na kasoro huyo..ulemavu wa korodani
Wapo wa design hiyo na huwa wanakua wazima tu. Anaweza akakua hivyo hivyo had utu uzima. Au inawezekana baada ya muda nyingine ikatokea pia
 
Nimesoma kwa kusikitika sana taarifa ya leo kwenye magazeti kuwa ongezeko la wazazi wa kike kuwanyima watoto wao maziwa ya mama yaani kutokunyonyesha watoto waliowazaa
Kuna haja kubwa ya kuwapa elimu wazazi watatajiwa manufaa na faida kubwa ya kumnyonyesha mwanzo kuanzia magonjwa mpaka afya ya akili na makuzi bora
Wazazi wa kileo wengi ni mabinti waliobeba mimba bila kutaka au bila maandalizi ya kutosha...! Wengi bado wanautaka ujana na hivyo kuona kama kwamba kumnyonyesha mtoto ni kupoteza shepu ya matiti
Maziwa ya mama yana faida nyingi kuliko hasara tofauti na maziwa ya kutengeneza na yale ya wanyama pia
Kwahiyo Kama mzazi unayenyonyesha nawe unayetarajia kupata mtoto/watoto karibuni kamwe mtu asikughilibu kwa maneno matamu ya kisasa ukaacha kumpa mwanao lishe bora itokayo kwenye titi lako
 
Wadau wanajukwaa... Nauliza hivi, kuna manesi au baadhi ya watu wanawazuia wamama wasiwaogeshe watoto wao siku ya kuzaliwa au siku chache baada ya kuzaliwa, bali wawa sponge walau kwa siku 3 hivi.

Hivi kwa joto lililopo Dar inawezekana kweli? Nini logic ya hili? Wataalamu wa afya tunaomba ufafanuzi
 
Wadau wanajukwaa... Nauliza hivi, kuna manesi au baadhi ya watu wanawazuia wamama wasiwaogeshe watoto wao siku ya kuzaliwa au siku chache baada ya kuzaliwa, bali wawa sponge walau kwa siku 3 hivi.

Hivi kwa joto lililopo Dar inawezekana kweli? Nini logic ya hili? Wataalamu wa afya tunaomba ufafanuzi
Nafikiri kwa uelewa Wangu ni kumwepusha mtoto na magonjwa ya kifua kama nimonia....
 
Wala huhitaji kugombana na mtu kama mtoto yuko salama nitakuja na post yake!nywele za watoto hutumiwa na washirikina kwenda kufanya yao kwa wengine ila huelekezwa ni nywele za aina gani na za mtoto wa aina gani zinafaa !!!cha muhimu ni kumkabidhi mtoto mbele za mikono ya Mungu bila kusahau ibada zaka na matoleo
Vile vile unaweza ukachagua siku moja ya ibada ya imani yako ukamtolea Mungu sadaka maalum kwa ajili ya mtoto
Hili jambo niliwahi ambiwa na mzazi wangu kuwa tulikutolea sadaka ndo maana unasema unabahati. Kiukweli nw naanza kuelewa.
 
Mmmh, kumuogesha mtoto ni suala la usafi. Je nimonia inakujaje?

Evelyn Salt, Lizzy, gfsonwin kuja huku.
charminglady sio kweli kwamba kumuogesha tu mtoto kunaweza kumsababishia magonjwa ya kifua. Wangu wa kwanza alioga the next day maana alizaliwa usiku na wa pili alioga siku ya tatu nilivyorudi tu nyumbani na hamna kati yao ambae amewahi kuumwa kifua. Nadhani ni imani tu kama vile wengine wanavyolazimisha watoto wagubikwe manguo kibao wakati hali ya hewa hairuhusu.

Kitu cha kuzingatia ni temp. ya maji ili mtoto asiwe unconfortable, kuhakikisha amekaushwa vizuri na kumvalisha nguo kiasi kuendana na hali ya hewa.
 
charminglady sio kweli kwamba kumuogesha tu mtoto kunaweza kumsababishia magonjwa ya kifua. Wangu wa kwanza alioga the next day maana alizaliwa usiku na wa pili alioga siku ya tatu nilivyorudi tu nyumbani na hamna kati yao ambae amewahi kuumwa kifua. Nadhani ni imani tu kama vile wengine wanavyolazimisha watoto wagubikwe manguo kibao wakati hali ya hewa hairuhusu.

Kitu cha kuzingatia ni temp. ya maji ili mtoto asiwe unconfortable, kuhakikisha amekaushwa vizuri na kumvalisha nguo kiasi kuendana na hali ya hewa.

Maadam nakusoma hapo ujue sijaelewa.....wa kwanza na wa pili lol haya mamito........ni kweli hata mie wangu nilimwogesha baada ya siku 3 niliporudi home lakini inaogopesha jinsi mdogo unakuwa unaogopa kumwangusha au kumkwarua na kitu
 
Maadam nakusoma hapo ujue sijaelewa.....wa kwanza na wa pili lol haya mamito........ni kweli hata mie wangu nilimwogesha baada ya siku 3 niliporudi home lakini inaogopesha jinsi mdogo unakuwa unaogopa kumwangusha au kumkwarua na kitu

Kuwa mzito yaani kutokufanya haraka wakati wakumwogesha kipindi hicho anakuwa anapulizwa na upepo basi inapelekea kupata shida kifua ndio maana wanaona washauri hivyo
Nafikiri kwa uhakika si kumwogesha kwa maana halisi ya kumwogesha kwakuwa bado kako so tiny na hakana uchafu wowote wa kivile
Labda tukubaliane tu kuwa ni kukamwagia maji ya vuguvugu na kukafutafuta
 
Kuhusu Kumuogesha mtoto :Ni muhimu kumwogesha kila siku uogeshaji unategemea umri na wakati ,kwa mtoto mchanga siku tatu hadi tano za mwanzo..... jitahidi mfunike vizuri kwenye taulo kavu uwe na vitambaa vidogo dogo ambavyo utavitumia kumfuta tandika taulo safi miguuni pako na hakikisha chumba kiwe na joto la kutosha funga madirisha na milango,uwe umetayarisha maji vuguvugu tumia utaratibu wa kumfuta kwa kitambaa laini usoni huku ukijitahidi kusupport kichwa chake mkaushe,mfute kichwani mkaushe awe mkavu ,mfunue taulo mfute pia kwa maji vuguvuvu ukiwa makini sehemu zilizo na mikunjo mkaushe mfunike malizia miguuni na pia mkaushe vizuri na kumfunika.Ni vizuri ukatumia sabuni zisizo kali na umpake mafuta ya nazi uliyoyaandaa nyumbani maji ya kuoga mtoto jitahidi uchemshe kama ya kunywa mapema na uache yapoe au uwe na yaliyochemshwa na kupoa kwa ajili ya kuzimulia,kiwiko cha mkono kitumike kupima uvuguvugu wa maji mtoto anapoongezeka uzito unaweza ukaandaa mahali maalumu mezani mahali ambapo vifaa vya mtoto vya kuogea vitatunzwa kumbuka kumsafisha pua na masikio kwa kutumia pamba maalumu a pia kumvalisha nguo kavu na zilizonyooshwa kuuwa vijidudu.
 
Kuhusu kupata watoto wenye mahitaji maalumu:Katika mpango wa Mungu wa kupata watoto wakati mngine familia hupokea watoto wenye ulemavu wa ngozi,wasiiona,wenye ulemavu wa viungo nk mara nyingi hili jambo huleta maswali,maumivu,hofu ,kukataaa na hata kukata tamaa ukweli unabaki kuwa ndiye mtoto tuliyempokea na ni muhimu muhudumu aliyetoa huduma atoe taarifa mapema ili wazazi wafahamu na waendelee kukubaliana na hali hiyo, ulemavu mngine huchukua muda kujulikana ni vizuri wazazi baada ya kujifungua tujitahidi kuwachunguza watoto wetu wakati wa kuwaogesha ,kuwavalisha na kuwa nao ili kuweza kufahamu miili ya watoto wetu kuna vitu vingine vikipata uangalizi wa daktari mapema vinarekebishika na yale ambayo hayawezekane tunapata nafasi ya kuwaona wataalamu mapema na hakika watatuelekeza namna nzuri ya kuwapokea kuwapenda na kuwatunza watoto wenye hali hizo na kuendelea kumshukuru Mungu kwa zawadi ya watoto anazotupatia
 
Mtoto wa wangu ananisumbua tangia juzi ameanza kulia yaan analia mpaka anageuza macho, nimempeleka hospital wamemchekI wanasema hana tatizo lolote, kiukwelI napata wakat mgumu sana hasa mama ake. Yaani siku nzima analia anaweza kuacha kulia mda flan tuu na hataki umlaZe kitandani, anataka abebwe mikononi mda wote.
Ni mtoto ambae ametimiza mwezi mmoja tuu, naombeni mnisaidie wenye uzoefu na hali hii.
 
Pole sana mama mtoto muangalie mtoto anashiba vizuri?anakula nini?joto je unamsaidiaje kupata hewa ya kutosha?
 
Kuhusu kupata watoto wenye mahitaji maalumu:Katika mpango wa Mungu wa kupata watoto wakati mngine familia hupokea watoto wenye ulemavu wa ngozi,wasiiona,wenye ulemavu wa viungo nk mara nyingi hili jambo huleta maswali,maumivu,hofu ,kukataaa na hata kukata tamaa ukweli unabaki kuwa ndiye mtoto tuliyempokea na ni muhimu muhudumu aliyetoa huduma atoe taarifa mapema ili wazazi wafahamu na waendelee kukubaliana na hali hiyo, ulemavu mngine huchukua muda kujulikana ni vizuri wazazi baada ya kujifungua tujitahidi kuwachunguza watoto wetu wakati wa kuwaogesha ,kuwavalisha na kuwa nao ili kuweza kufahamu miili ya watoto wetu kuna vitu vingine vikipata uangalizi wa daktari mapema vinarekebishika na yale ambayo hayawezekane tunapata nafasi ya kuwaona wataalamu mapema na hakika watatuelekeza namna nzuri ya kuwapokea kuwapenda na kuwatunza watoto wenye hali hizo na kuendelea kumshukuru Mungu kwa zawadi ya watoto anazotupatia
Umegusia engo moja muhimu sana lakini kuna wazazi huzaa watoto wasio na tatizo kabisa lakini mzazi akaja kumsababishia mtoto ulemavu au tatizo lingine lolote
Kwa mfano haishauriwi kabisa kumzaba mtoto vibao vya masikioni unaweza kumletea ulemavu wa kutosikia au kumlaza mtoto upande mmoja muda wote huleta tatizo la chogo au kichwa bapa au kilichobonyea upande
 
Mtoto wa wangu ananisumbua tangia juzi ameanza kulia yaan analia mpaka anageuza macho, nimempeleka hospital wamemchekI wanasema hana tatizo lolote, kiukwelI napata wakat mgumu sana hasa mama ake. Yaani siku nzima analia anaweza kuacha kulia mda flan tuu na hataki umlaZe kitandani, anataka abebwe mikononi mda wote.
Ni mtoto ambae ametimiza mwezi mmoja tuu, naombeni mnisaidie wenye uzoefu na hali hii.
Kwa ushauri wangu binafsi jaribu tiba ya kitunguu saumu...kiponde kisha mpake kwenye nyayo viganjani tumboni na kwenye paji la uso
 
Anapata choo vizuri?akila unamtoa gesi vizuri chunguza kwa makini na fanya marekebisho kwa kuhakikisha anashiba angalia kama nawe unakula vya kutosha ili utoe maziwa ya kutosha ashibe mtoe gesi na mpunguzie nguo pia maombi kwa mtoto ni muhimu muombee
 
Back
Top Bottom