Kwa wenye Uzoefu na Biashara ya Vituo vya Mafuta [Fuel Stations]

Kwa wenye Uzoefu na Biashara ya Vituo vya Mafuta [Fuel Stations]

0719357919
Fundi Canopy na Matenk. Ukiwa serious mtafute huyo fundi atakusaidia ni Mzuri na mwaminifu. Matenk usipopata fundi mzuri yakawa na vilinkage yatakupa hasara sana kuvuja mafuta na hutaona kwa kuwa yatakuwa yamefukiwa. Sasa kwa kuwa Fedha bado ya kuunga unga Anza kutengeneza matenk huku ukijenga Ofisi mdogo mdogo maana Ofisi haiitaji Fedha nyingi kwa wakati mmoja
 
Mkuu, kuna kitu unakijua zaidi ya ulichoandika, ongezea ongea maneno
najua coz ni biashara nimejihusisha nayo illegal na legal so najua kwa kiasi changu some of my relatives wanamiliki hii biashara so kwa muda niliofanya kazi zangu za mafuta pamoja na kufanya kazi ktika ofisi za ndugu zangu nimejifunza kiasi
Mimi napenda kushauri kiuchumi+ ukwel ni sekta nzuri kuwekeza lakin inahitaji uzoefu,umakini+ nidhamu bila kusahau ubunifu wafanya biashara wengi tu sio mmoja wanaingia na mitaji full na wanashindwa kuindeleza so kwa huu mtaji wa ndugu yetu si mbaya wala si mdogo unaweza ujafanya kitu kizuri lakin tu kimkakati ukikaza sana
 
Mil 50 haitoshi na benk hawezi kukupa ela ya kujenga kituo kwa dhamana ya lodge maana kituo size unayotaka roughly lazima uwekeze mil 300 mpaka 350 hapo bila mafuta. Mfumo wa mafuta peke yake yaani canopy, matenk, pump tatu ,stand by generator, VFD system na zege la canopy kwa haraka lazima vile mil 200. Majengo ya iyo filling station na vibali lazima vikule mil 150 to mil 200. Pambana
kaka umeandika kidaftari zaidi hio pesa kwa mutu mwenye nia anafanya kazi ingawa itamchukua muda
 
kaka umeandika kidaftari zaidi hio pesa kwa mutu mwenye nia anafanya kazi ingawa itamchukua muda
Mie nimejenga, BOQ ya injinia ilikuwa mil 350 ila ujenzi imefika mpk mil 500. Ila changu kikubwa kina majengo mengi, Kuna mgahawa, supermarket, ATMashine room mbili, Gym and fitness, car wash, car service na barbershop. Na nimetumia miaka miwili pesa imelala ila kimeanza kufanya kazi, return naona ndani ya miaka mitatu nitakuwa bilionea
 
Kwanza kuna aina mbili ya vituo vya mafuta Filling station na service station. Filling station unapaswa kuwa na eneo lisilopungu 600sq.m. wakati service station unapswa kuwa na eneo lisilopungua 1,150sq.m

KAma ni filling station basi unatakiwa kujenga jengo la ofisi, changing room, toilet. Ambapo kama vifaa vya ujenzi sio ghali hiyo fedha onatosha na kubakia.

Unapaswa kujenga canopy pamoja na kumwaga zege eneo lote la kuingilia kituoni pamoja eneo la canopy zege lisilopungua 9inches.

Matank ya mafuta kama ulivyoshauriwa hapo juu walau 30,000 each. Mafuta hayapaswi kuisha kwemye tank.

Vibali na mtaji wa mafuta.

Mtaji wa Mafuta unaweza kuingia mkataba na wauzaji wakubwa wakakuletea on credit au ukachukua mkopp bank. Hii itawezekana kama utakuwa na hati ya eneo la hiyo station.

Basically ni mradi mzuri sanasana kama utapata sehemu strategic. Kama utataka ufanyie feasibility study tukupe ni actual costs tuwasiliane inbox
 
I have some experience ktk hio biashara nimefanya ktk petrol station kwa muda nimepata kufahamu biashara hii .
1. kitu cha kwanza sikushauri utengeneze storage tank ndogo kwa sababu tofauti tofauti umesema unaanza biashara kwa gari ya kukodi ni sawa unatakiwa uangalie namna ambavo utaongeza tija zaidi kwa mfano kama utakodi kipisi kufanyia delivery mind vipisi Vingi ni approximately 22000ltr sasa in case ukaagiza 10000ltrs za PMS na 5000 kulingana na storage facilities kibiashara unatakiwa uagize litre 1500 tu sasa hio space unayotaka kuicha huoni kama itakuongezea gharama za usafiri ?
2.ukijenga storage tanks za 10000 Ltrs kwa PMS(petrol) na 5000ltr kwa ajili ya PMS bado itafikia wakati itabidi uongeze ili kupunguza gharama na kuchukua faida zile za ghafla kulingana na trend ya biashara
Shukrani kwa ushauri wako Mkuu, nitazingatia.

Na vipi ishu ya faida, naweza kurejesha gharama zangu baada ya miaka mingapi wastani?

Kuna kituo kimoja nimekiona Dodoma, jamaa wanauza mafuta kwa gharama ya chini kiasi cha kama shilingi 50 - 78 pungufu ya vituo vingine kwa lita moja.

Inawezekana hao jamaa wanaagiza wenyewe nje ya Nchi?
 
Kwanza kuna aina mbili ya vituo vya mafuta Filling station na service station. Filling station unapaswa kuwa na eneo lisilopungu 600sq.m. wakati service station unapswa kuwa na eneo lisilopungua 1,150sq.m

KAma ni filling station basi unatakiwa kujenga jengo la ofisi, changing room, toilet. Ambapo kama vifaa vya ujenzi sio ghali hiyo fedha onatosha na kubakia.

Unapaswa kujenga canopy pamoja na kumwaga zege eneo lote la kuingilia kituoni pamoja eneo la canopy zege lisilopungua 9inches.

Matank ya mafuta kama ulivyoshauriwa hapo juu walau 30,000 each. Mafuta hayapaswi kuisha kwemye tank.

Vibali na mtaji wa mafuta.

Mtaji wa Mafuta unaweza kuingia mkataba na wauzaji wakubwa wakakuletea on credit au ukachukua mkopp bank. Hii itawezekana kama utakuwa na hati ya eneo la hiyo station.

Basically ni mradi mzuri sanasana kama utapata sehemu strategic. Kama utataka ufanyie feasibility study tukupe ni actual costs tuwasiliane inbox
Shukrani Chief

Eneo ninalo la kutosha, ekari 5 ni approximately mita za mraba 24,000 kwahiyo linatosha kabisa.

Hofu yangu ilikuwa kwenye huo mtaji na namna hiyo biashara kama ni practical au inaweza kunipotezea hela yangu.

Kama kuna supplies wanaweza kunikopesha mzigo then nikarejesha hela baada ya mauzo kumbe naweza kufanikisha lengo
 
Shukrani kwa ushauri wako Mkuu, nitazingatia.

Na vipi ishu ya faida, naweza kurejesha gharama zangu baada ya miaka mingapi wastani?

Kuna kituo kimoja nimekiona Dodoma, jamaa wanauza mafuta kwa gharama ya chini kiasi cha kama shilingi 50 - 78 pungufu ya vituo vingine kwa lita moja.

Inawezekana hao jamaa wanaagiza wenyewe nje ya Nchi?
Sio GBP hao?
 
Mie nimejenga, BOQ ya injinia ilikuwa mil 350 ila ujenzi imefika mpk mil 500. Ila changu kikubwa kina majengo mengi, Kuna mgahawa, supermarket, ATMashine room mbili, Gym and fitness, car wash, car service na barbershop. Na nimetumia miaka miwili pesa imelala ila kimeanza kufanya kazi, return naona ndani ya miaka mitatu nitakuwa bilionea
Huenda uliamua kujenga kwa kutumia mafundi wazoefu wa mtaani (Local Fundis).

Njia ya Force account imeonekana ina okoa gharama sana kuliko kutumia Mkandarasi
 
Mimi kwa ushauri wangu tafuta fundi mzuri akufanyie construction cost quotation ya filling yenye canopy ndogo ya pump mbili storage tanks mbili 25000Ltr ya PMS na 25000 au 22000Ltrs za AGO then suka effective storage tanks zako hakikisha haina leakage tafuta pump za kichina mbili kwa budget yako ukiwa mjanja 50 mil inaweza ikafilisha even 45% ya mradi wako kuukamilisha utahitaji mtaji mwingine kwa sababu kuna gharama nyingi nyingi zinazochukua muda mfano kupata some license mambo ya ajira kiushauri umebuni mradi mzuri sana lakin kulingana na muda na technology kama unataka uwekeze ktk nishati basi jitahidi kufanya proper investment na strategy mpya ili uwe salama sokoni hongera sana kaka
Mimi mwenyewe nipo kwenye construction industry kwa miaka kadhaa sasa, nadhani kuna haja ya kupata mafundi wenye uzoefu na aina hii ya miradi then tuta share knowledge.

Hapo pia nikipata watu wenye uzoefu na hii biashara hope naweza kujifunza mengi na pengine nikaondoa wazo la uoga wa hii biashara
 
Mil 50 haitoshi na benk hawezi kukupa ela ya kujenga kituo kwa dhamana ya lodge maana kituo size unayotaka roughly lazima uwekeze mil 300 mpaka 350 hapo bila mafuta. Mfumo wa mafuta peke yake yaani canopy, matenk, pump tatu ,stand by generator, VFD system na zege la canopy kwa haraka lazima vile mil 200. Majengo ya iyo filling station na vibali lazima vikule mil 150 to mil 200. Pambana
Kwamba hiyo 50M siwezi kujenga hizo items chache muhimu hata kama nikitumia mafundi yaani Force Account?
 
0719357919
Fundi Canopy na Matenk. Ukiwa serious mtafute huyo fundi atakusaidia ni Mzuri na mwaminifu. Matenk usipopata fundi mzuri yakawa na vilinkage yatakupa hasara sana kuvuja mafuta na hutaona kwa kuwa yatakuwa yamefukiwa. Sasa kwa kuwa Fedha bado ya kuunga unga Anza kutengeneza matenk huku ukijenga Ofisi mdogo mdogo maana Ofisi haiitaji Fedha nyingi kwa wakati mmoja
Asante kwa mchango wako Mkuu.

Nitafanya mawasiliano na Mdau.

Hata kama itanilazimu kujenga kwa miaka 2 lakini nimeshatia nia lazima niikamilishe hii project
 
kaka umeandika kidaftari zaidi hio pesa kwa mutu mwenye nia anafanya kazi ingawa itamchukua muda
Mkuu amenitisha sana kwa gharama hizo, Ina maana nitahitaji zaidi ya miaka 2 hadi 3 kuianza hadi kuikamilisha project yangu 🙆
 
Back
Top Bottom