Kwa Yanayoendelea Jeshi la Polisi, “Tume ya Haki Jinai” Ilikuwa ni Matumizi Mabaya ya Fedha Zetu

Kwa Yanayoendelea Jeshi la Polisi, “Tume ya Haki Jinai” Ilikuwa ni Matumizi Mabaya ya Fedha Zetu

Ni wazi pesa za wananchi zimetumika kwenye Tume hii ya Mh Jaji Mkuu mstaafu Othman Chande hivyo wananchi tungetamani kuona matokeo chanya ya utekelezaji. Wakuu wa Mikoa na Wilaya, Makamanda wa Polisi Mikoa na Wilaya na Taasisi zote zinapaswa kuzingatia maelekezo ya Rais ambaye ni Mkuu wa Nchi kuhusu utekelezaji wa mikakati na mbinu iliyoibuliwa kwenye mipango hii.

Lakini kwa masuala haya yaliyotokea ndani ya Jeshi la polisi kwa mwaka 2023/ 24, ni kama vile Jeshi la Polisi linamkwamisha Rais Samia kwa makusudi.

Mifano michache hii hapa:-
1. Kutekwa kwa kijana Sativa na kutupwa mbuga ya Katavi
View attachment 3073811
2. Kushikiliwa kwa kijana Kombo wa Tanga kwa siku 29 bila mashtaka
View attachment 3073810
3. Kubakwa na kulawitiwa kwa binti wa Yombo na wanajeshi 5. Halafu RPC Mallya badala ya kupeleka Mahakamani yeye anadai binti alikuwa anajiuza
View attachment 3073806

Kama Rais Samia hatochukua mabadiliko dhidi ya Jeshi la Polisi basi ametumia fedha za walipa kodi vibaya.
Ripoti ya Tume ya Haki Jinai ni changa la macho tu. Hakuna chochote tunachokiona.

Kimsingi hata kama Katiba Mpya itachelewa basi kiundwe chombo cha kuikagua/ kuihukumu Polisi na TAKUKURU. Maana hivi vimebakia kuwa ni vyombo vya maafisa kujitajirisha kutoka kwa watuhumiwa.

Wakati wa awamu ya JKN kulikuwa na kitu kinaitwa Permanent Commission of Inquiry. Ambapo raia alikuwa anaweza peleka issue yake na hatua stahiki zikachukuliwa
 
Hizo tume ni miradi ya mafisadi kutumia pesa ya umma hovyo,hazina tofauti na zile za PM Majaliwa.
Jeshi la police Tanzania ni genge la majizi na majambazi.
 
Kajisemea lissu tatizo ni.mfumo na sio polisi. Hata akienda malaika itabidi ageuke shetani na kufuata chain of command na SOPs.
Wakati mama anaingia na falsafa zake na uteuzi wake wa kamanda wambura nilijua kutakuwa na major reforms in the police force..yawezekana bajeti labda ndogo ya kuwezesha reforms
Na Camilius Wambura alikuja na masifa mengi kama Ex RCO wa Dar na kisha DCI. Kumbe ni mweupe tu
 
Ni wazi pesa za wananchi zimetumika kwenye Tume hii ya Mh Jaji Mkuu mstaafu Othman Chande hivyo wananchi tungetamani kuona matokeo chanya ya utekelezaji. Wakuu wa Mikoa na Wilaya, Makamanda wa Polisi Mikoa na Wilaya na Taasisi zote zinapaswa kuzingatia maelekezo ya Rais ambaye ni Mkuu wa Nchi kuhusu utekelezaji wa mikakati na mbinu iliyoibuliwa kwenye mipango hii.

Lakini kwa masuala haya yaliyotokea ndani ya Jeshi la polisi kwa mwaka 2023/ 24, ni kama vile Jeshi la Polisi linamkwamisha Rais Samia kwa makusudi.

Mifano michache hii hapa:-
1. Kutekwa kwa kijana Sativa na kutupwa mbuga ya Katavi
View attachment 3073811
2. Kushikiliwa kwa kijana Kombo wa Tanga kwa siku 29 bila mashtaka
View attachment 3073810
3. Kubakwa na kulawitiwa kwa binti wa Yombo na wanajeshi 5. Halafu RPC Mallya badala ya kupeleka Mahakamani yeye anadai binti alikuwa anajiuza
View attachment 3073806

Kama Rais Samia hatochukua mabadiliko dhidi ya Jeshi la Polisi basi ametumia fedha za walipa kodi vibaya.
Kama mpaka sasa kuna mtu bado ana amini tuna jeshi la polisi na mpa pole sana …. Hawa ni mawakala wa kijani wwnye njaa na chuki iliyo ota mizizi
 
Jeshi la polisi linatakiwa kufumuliwa hasa ngazi ya SACP kwenda vyeo vya CP wastaafishwe wote.

Hii itasaidia kurejesha usimamizi wa nidhamu na utendaji wa walio chini yao kuzingatia kanuni na GPO ya polisi wanapotumwa askari kwenda kukamata watuhumiwa.
 

19 Agosti 2024

Temeke Dar es Salaam , Tanzania

KUTOWEKA VIONGOZI WA CHADEMA MKOA WA WILAYA DSM KATIKA MAZINGIRA YA KUTATANISHA CHADEMA WATOA TAMKO


View: https://m.youtube.com/watch?v=nfBNEaVqMBE

Benito Mwapinga mwenyekiti wa CHADEMA wilaya ya Temeke akiongoa na waandishi wa habari kisha kubainisha viongozi Deusdedith Soka na wenzake walipigiwa simu tarehe 18 Agosti 2024 kutoka kituo cha polisi Changombe kuwa ....


Benito Mwapinga mwenyekiti wa wilaya Temeke anabainisha wamefuatilia lakini jeshi la polisi halitoi ushirikiano .....
 

Kuwajibika kwa dola juu ya utendaji wa Polisi, Inawezekana kwa kuchukua hatua sahihi​

HISTORIA: Januari 22, 1977​

Mwinyi Alivyojiuzulu Uwaziri kwa Mauaji ya Kanda ya Ziwa​

Last updated Jan 1, 2021
0
Share
mwinyi.png

TUNAMALIZA mwaka mpya kwa kuwakumbusha utamaduni ambao husukumwa na maadili ambayo wakubwa serikalini wanaokumbwa na kashfa nzito hulazimika kujiuzulu nyadhifa zao, lakini katika zama hizi maadili haya yametoweka na badala yake wakiharibu husubiri kutumbuliwa.

Hata hivyo, si sahihi kabisa kusema kwamba zamani utamaduni wa kujiuzulu kwa wakubwa haukuwapo. Ulikuwapo tangu katika utawala wa Awamu ya Kwanza wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere.

Kwa mfano; Januari 22, 1977 aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani katika Serikali ya Muungano, Ali Hassan Mwinyi, alijiuzulu mara moja baada ya kuibuka kwa ripoti za mauaji ya kikatili ya raia katika mikoa ya kanda ya ziwa yaliyofanywa na maofisa usalama chini ya wizara yake.

Baadaye Ali Hassan Mwinyi akiwa rais alikuwa kiongozi pekee aliyelifukuza baraza lake lote la mawaziri mapema mwaka wa 1990 baada ya manung’guniko mengi kutoka kwa wananchi kutokana na utendaji mbovu wa majukumu yao. Rais Mwinyi aliwaita Ikulu mawaziri wake wote na kuwaambia anataka wote waandike barua hapo hapo za kujiuzulu nyadhifa zao.

Akasimama Joseph Warioba aliyekuwa waziri mkuu na kuuliza: “Hata mimi?” Mwinyi akamjibu: “Naam, hata wewe, kwani Katiba yetu inasema waziri mkuu ni waziri pia.”

Akiwa waziri wa mambo ya ndani, Mwinyi aliwahi kuandika barua ya kujiuzulu ikithibitisha jinsi kiongozi huyo alivyo juu kwa viwango vya utiifu na uadilifu.

Katika barua hiyo ambayo ilisambazwa kwenye vyombo vya habari kwa sasa, inaonyesha jinsi Mwinyi alivyojiuzulu kwa unyenyekevu hiyo Januari 22, 1977 wadhifa wa Waziri wa Mambo ya Ndani.

Kiongozi huyo ambaye mwaka 1985 alikuja kukwea tena ngazi ya uongozi na kuwa Rais wa awamu ya pili wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, katika barua aliyomwandikia Rais wake, Mwalimu Julius Nyerere, alieleza jinsi alivyoguswa na mauaji ya watu wasio na hatia walioshukiwa kuwa wachawi katika mikoa ya Shinyanga na Mwanza mwaka 1975.

Kwa maneno yake Mwinyi alisema: “Kisiasa nakiri kuwa nahusika, siwezi kukwepa kwa sababu dhamana yangu ya uwaziri inaambatana na wajibu unaonitaka nijue yanayotendeka wizarani na pia niweze kudhibiti na kuhakikisha mwenendo mwema wa Jeshi la Polisi.”

Mwinyi alijikuta katika matatizo hayo baada ya Jeshi la Polisi kuendesha operesheni ya kusaka wauaji wa wachawi katika mikoa ya Mwanza na Shinyanga, na alikiri kwamba:

“…vyombo vinavyohusika na utekelezaji, polisi ikiwemo, vilivuka mipaka ya wajibu wao na vikajipa madaraka ya kuogelea katika vitendo viovu vya kishenzi, kinyama na kikatili hata baadhi ya watu waliokamatwa kwa kushukiwa tu kwamba wanahusika, wakafa na wengine wakapata vilema vya kudumu.”

Ingawa Mwinyi aliweka bayana kwa mkuu wa nchi Mwalimu Nyerere, kwamba kijinai asingehusika kwani hakushiriki wala kushauri, kuagiza wala kuelekeza mambo hayo yafanywe hivyo, aliandika barua isiyo na kinyongo kabisa na yenye unyenyekevu mkubwa kwa Rais Nyerere.

Kwa unyeyekevu mkubwa, Mwinyi alisema: “Kwa hiyo, Mwalimu, nakuomba mambo matatu. Kwanza naomba radhi mimi nafsi yangu na pia naomba radhi kwa niaba ya askari wote walio wema. Pili, naomba vilevile uelewe sehemu yangu katika kosa hili. Tatu, kwa fedheha hili, naomba unikubalie kujiuzulu.”

Kwa barua hiyo ya Mwinyi ambayo gazeti hili limeamua kunukuu baadhi ya maneno kama ulivyosoma hapo juu kwa nia ya kuamsha uadilifu unaofanana na kiongozi huyo wa awamu ya pili, ni fursa nzuri sasa kwa viongozi wote wa umma kuiga mfano huo ambao humpunguzia rais majukumu ya kutumbua iwapo kuna matatizo mazito yametokea katika ofisi unayoisimamia.

Mzee Mwinyi kwa maudhui ya barua yake ya mwaka 1977 haikuwa jambo la ajabu kuja kuwa Rais wa Tanzania miaka minane baadaye, huku akionekana kama kiongozi aliyeshinda vishawishi na kila aina ya hila kwenye uongozi wake.

Kupatikana kwa barua hiyo ya Mwinyi ya kujiuzulu na kuwekwa hadharani iliweka mizania mpya kabisa ya uadilifu katika uwajibikaji wa viongozi wa umma wanapoingia matatani na kutakiwa kujiuzulu.

Miongoni mwa viongozi wakuu waliowahi kujiuzulu katika miaka ya hivi karibuni ni pamoja na aliyekuwa Waziri Mkuu wa kwanza wa Serikali ya Awamu ya Nne, Edward Lowassa, pamoja na mawaziri wawili waliowahi kusimamia Wizara ya Nishati na Madini kwa nyakati tofauti za utawala wa awamu hiyo, Dk. Ibrahim Msabaha na Nazir Karamagi.

Viongozi hao, ingawa barua zao za kujiuzulu kwa Rais Jakaya Kikwete hazijapata kuwekwa hadharani, lakini kwa kauli na maelezo yao bungeni wakati wanatangaza kujiuzulu walionyesha kuwa walionewa tu kufikishwa katika hatua hiyo.

Kwa mfano, Lowassa alisema wazi “ameonewa na kudhalilishwa sana kisa ni uwaziri mkuu” kuhusiana na suala la mkataba tata wa kuzalisha umeme wa dharura ambao ulitolewa kwa kampuni ya Richmond.

Baada ya Lowassa na wenzake wawili kujiuzulu kulizuka mpasuko mkubwa miongoni mwa wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), vita ikapiganwa kuonyesha kwamba kujiuzulu kwa viongozi hao ulikuwa ni uonevu.

Mivutano hiyo ya wabunge ndiyo ilifanya hata Halmashauri Kuu ya CCM kuunda kamati ya wazee watatu wa busara ikiongozwa na Ali Hassan Mwinyi na wajumbe ni Spika wa zamani wa Bunge la Afrika Mashariki, Abdulrahman Kinana na Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara), Pius Msekwa, kusaka suluhu ya uhasama huo.

Wakati kamati hiyo ikiendelea na kazi ya kusaka suluhu ya uhasama huo, suala la Richmond ambalo ni chimbuko la kujiuzulu kwa viongozi hao watatu, likazidi kuwa tete kila kukicha, zaidi likijitokeza katika makundi ya wapinga ufisadi na wale wanaotajwa kuutetea
 
Toka maktaba: Mwaka 1990

Rais Ali Hassan Mwinyi aitisha kikao cha baraza la mawaziri na kuwaambia mawaziri wajiuzulu Mwaka 1990

1724113151622.png

Ally Hassan Mwinyi pekee alijaribu, alivunja Baraza la Mawaziri la Muungano mwaka 1990 alipoona kuna shida mahala​

  • mwaka 1990 magazeti yote ya Tanzania yalikuwa na vichwa vya habari vilivyohusu kujiuzulu kwa baraza la mawaziri jana yake yaani tarehe 12.

    Taarifa hizo zilisema kuwa katika kikao cha baraza la mawaziri kilichoongozwa na Rais mzee Ally Hassan Mwinyi aliwaambia mawaziri wote wakiongozwa na waziri mkuu na makamu wa kwanza wa Rais, Joseph Sinde Warioba kwamba, wajiuzulu na warudi makwao na wampishe atengeneze baraza jingine la mawaziri.

    Taarifa hizo zileendelea kutaarifu kuwa Rais Mwinyi alisema kuwa shughuli zote za baraza la mawaziri zingekuwa chini ya makatibu wakuu wa wizara.

    Baraza hilo pamoja na mzee Warioba lilikuwa na waziri wa Fedha Cleopa Msuya, waziri wa serikali za mitaa Paul Bomani rip, waziri wa mambo ya Nje Benjamin Mkapa rip, na mzee Rashid Mfaume Kawawa rip ambae alikuwa waziri asie na wizara maalum.

    Wengine ni mzee Al Noor Kassum rip ambae alikuwa waziri wa madini na nishati, Jackson Makweta rip waziri ofisi ya Rais(Ulinzi) na mzee Muhidin Kimario rip ambae alikuwa waziri wa mambo ya Ndani.

    Hawa mawaziri ni baadhi ya mawaziri wa serikali hiyo ambayo iliundwa mawaziri 26 na manaibu waziri 14.

    Kama kawaida mawaziri waliwasili Ikulu siku hiyo kwa mkutano wa baraza la mawaziri ambao ungechukua hadi masaa matatu.

    Kwa mshangao wao kikao hicho kilichukua dakika tatu tu pale Rais Mwinyi alipotamka kwamba anataka mawaziri hao wote wajiuzulu na warudi makwao.

    Waziri wa mambo ya nje, mzee Mkapa(RIP) alichanganyikiwa na kumwambia Rais kuwa alikuwa tayari ana "engagement" za mikutano Ulaya na akaambiwa "Cancel it".

    Wakati hayo yote yakifanyika mwenyekiti wa CCM hayati baba wa taifa, Mwalimu Nyerere alikuwa angani akielekea Rome nchini Italia.

    Mwalimu pamoja na kuongea sana na siasa thabiti, moja ya udhaifu wake ulikuwa ni kutowachukulia hatua mawaziri ambao walikuwa wanamuangusha kwenye idara ya kuwajibika na ufisadi.

    Kuna kipindi hayati Mwalimu aliwahi kutembezwa maeneo ya Msasani na Mikocheni na kuonyeshwa nyumba za baadhi ya mawaziri wake na alifahamu walipata kiasi gani cha mshahara kulinganisha na majumba aloyaona lakini alibakia kushangaa.

    Hivyo mzee Mwinyi akiwa anaelewa hayo alimfuata hayati Mwalimu uwanja wa ndege kabla hajatimkia Rome na kuhakikisha ameondoka kabla ya kurudi Ikulu na kuchukua maamuzi hayo magumu.

    Hayati Nyerere alipofika Rome na kupokelewa na vijana wa pale wakampasha habari za Dar-es-Salaam na akashangaa kweli, ila kimoyomoyo alishukuru kuona angalau Mwinyi ameweza.

    Baadae, Rais Mwinyi akiongea na vyombo vya habari alitoa sababu za msingi za kuwataka mawaziri wake wote wajiuzulu na akasema kuwa ni vitendo vya rushwa na kutowajibika kwa mawaziri kulikokithiri khasa katika wizara zao.

    Alitoa mifano ya wachuuzi kuombwa kitu kidogo pale walipotaka haki zao na hata wastaafu hali ilikuwa ni hiyohiyo, na hata kuambiwa "njoo kesho, njoo kesho".

    Msemo wa njoo kesho ulikuja kupata maarufu baadae pale ulipotumika kukemea vitendo vya rushwa na ufisadi na hata kutungwa wimbo wa FAGIO LA CHUMA KUWAKUMBA WALE WASOWAJIBIKA.

    Huku kukiwa na shauku ya kutaka kufahamu baraza jipya la mawaziri laja, wananchi walianza kuvumisha kuwa kutakuwa baraza jipya kabisa lenye sura mpya, lakini wakikatishwa tamaa pale mzee Joseph Sinde Warioba alipotangazwa ndiye waziri mkuu anaeendelea.

    Si kwamba Mzee Warioba nae alikuwa ni fisadi au mla rushwa lakini wananchi walitegemea Rais Mwinyi angebadilisha kila kitu na kuanza upya "once for all" au "the beginning of new chapter".

    Hivyohivyo kwa baraza la mawaziri mawaziri saba walipoteza nafasi zao Al Noor Kassum, Aaron Chiduo, Muhidin Kimario, Damian Lubuva, Chrisant Kissanji, Arcado Ntagazwa na mama Getrude Mongela.

    Mzee Mwinyi akatolea mfano wa yeye mwenyewe akiwa waziri wa mambo ya ndani ilibidi ajiuzulu pale yalipotokea mauaji yasiyoeleweka kule Shinyanga ambapo polisi walihusika na mauaji yale.

    Lakini uamuzi wa mzee Mwinyi kuwataka mawaziri wake wajiuzulu haukutoka bure bali kuliktokana na uchunguzi wa kina uliofanywa na kamati kuu ta CCM au CC kama inavyojulikana na kamati hiyo chini ya mwenyekiti Mwalimu ilibaini taasisi na wizara zipatazo 12 ndizo zilikuwa na shida.

    Wizara ya sheria, mambo ya ndani, wizara ya afya na wizara ya ardhi zilisemwa kuwa hali ya rushwa na ufisadi ilikuwa imefikia kiwango cha juu.

    Mwalimu akaamuru wahusika wote ambao ni mawaziri wafike kwenye kikao cha kamati kuu lakini uamuzi huo ukapigwa chenga na mawaziri khasa mzee Kimario wakaamua kujiuzulu kuliko kwenda kwa CC kujibu masuali ya Mwalimu na wajumbe.

    Ila tatizo kama kawaida likajirudia na mzee Mwinyi akawarudisha mawaziri wake waandamizi kama Mkapa, Msuya, na wengine akawabadili wizara.

    Ila kukaja sura mpya kama mzee Nalaila Kiula ( kukawa na kichwa cha habari kilochosema "Nalaila Kiula aula"), mazee Jakaya Mrisho Kikwete akawa waziri wa nishati, madini na maji, Charles Kabeho (elimu).

    Akijitetea raisi Mwinyi akasema hakutaka kubadili baraza zima kwa sababu ilibakia miezi minne kabla ya kuvunja bunge kwa ajili ya maandalizi ya uchuguzi mkuu.

    Hata hivyo raia Mwinyi aliagiza kuwepo uwajibikaji, kuondoshwa kwa vitendo vya rushwa, kupunguza safari za nje na semina zisizoeleweka.

    Kuhusu balozi zetu nje, akaagiza kuwepo balozi na msaidizi wake mmoja tu na kila mwezi atakuwa akifanya mikutano na wananchi.

    Wananchi wenye shida mbalimbali za ardhi, mikopo, mafao na kesi kucheleweshwa zote raisi Mwinyi alikuwa akizishughulikia mwenywe na wasaidizi wake pale CCM Lumumba.

    Hata kule Zanzibar raisi Idris Abdul Wakil nae alifanya hayo na kukutana na wananchi kusikiliza shida zao na aliwaita polis, maofisa wa wizara na CCM kujibu masuali kadhaa.

    Ninachotaka kusema ni kwamba matatizo ya nchi yetu hayakuanza leo na wala hayataisha leo.

    Tunahitaji viongozi wetu kujituma na kufanya maamuzi khasa ya kuokomboa nchi yetu kiuchumi.

    Raisi aweza kufanya mabadiliko ya hapa na pale katika baraza lake la mawaziri lakini tatizo lipo kwenye mfumo wote na khasa kule chini ambako mkurugenzi wa maendeleo au afisa mtoza ushuru ana uwezo wa kukwapua fedha za umma na kujilimbikizia mali bila kugundulika mapema.

    Serikali itengeneze mifumo sahihi iliyo na ufanisi na uelevu wa kubaini wizi na matumizi mabaya ya fedha za walipa kodi
 
TOKA MAKTABA:

Waziri Siyovelwa ajiuzulu
alikuwa Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Rais yenye dhamana ya Idara ya Usalama wa Taifa.

Kashfa ya mauaji, utesaji yafanya Peter Siyovelwa ambaye alikuwa Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Rais yenye dhamana ya Idara ya Usalama wa Taifa.

Lakini kati ya hawa wawili, ni uamuzi wa Mwinyi, anayetarajiwa kuzikwa huko Zanzibar Jumamosi, Machi 2, ndiyo ambao umebaki kwenye kumbukumbu za Watanzania walio wengi.

Hii inatokana na uamuzi wa makusudi aliouchukua Mwinyi, aliyeaga dunia akiwa na umri wa miaka 98, wa kumuandikia barua Julius Nyerere, aliyekuwa rais wakati huo, hapo Januari 22, 1977, akimuomba kiongozi huyo aruhusu kusudio lake la kujiuzulu kufuatia kashfa hiyo iliyokuwa inahusisha maafisa wa vyombo vya ulinzi na usalama.
 
Back
Top Bottom