Kwaheri CDF Jenerali Mabeyo

Kwaheri CDF Jenerali Mabeyo

Ni waziri mkuu gani huyo ambaye kuanzia anapata hiko cheo hadi anakiacha asiwahi kutembelea wizara hata moja

Na hata ikitokea hiyo siyo hoja sababu nchi yetu inamtambua waziri mkuu kama mkuu wa wizara zote

CDF anatambulika kama chief of defense forces (majeshi ya ulinzi) siyo na security forces (majeshi ya usalama)
Ok mkuu hapa ni kama vile nimekuelewa kiasi chake.
 
Sasa kwanini hafanyi ziara hata siku moja uhamiaji, polisi au magereza?
Je ulishawahi kujiuliza hicho nilichokueleza? Kuna wabunge, wakuu wa Wilaya hawajawahi kufanya ziara kwenye kata za majimbo/Wilaya zao. Hii haimaanishi hizo kata haziko chini yake.
 
Video za wanajeshi kupiga raia zipo na haziongopi. Mabeyo hasafishiki
Ndio maana nilikuuliza jeshi linapoona kuna kundi, chama au mgombea fulani anataka kuhatarisha usalama wa nchi limuache? Mbona hatukuona Tanga, Mbeya, Kigoma, Dar, Kilimanjaro, Kagera na sehem nyingine watu wakipigwa na jeshi? Burundi, Kongo, na maeneo mengine ya vita mambo yalianza kimya kimya kama Zanzibar huku vyombo vya ulinzi na usalama viki relax. Mwisho wa siku jeshi likaja kushtukia nchi ishaingia vitani na matokeo yake kuwadhibiti wapiganaji ikawa shida. Kwahiyo jeshi letu kamwe haliwezi kupuuzia vurugu ambazo baadae zinaweza kuja kuleta vita.
 
Hapana hakumsaidia mkuu, bali alifanya kazi yake iliyomuweka pale kwa mujibu wa sheria. Kutii mamlaka ya raisi, kuilinda na kuisimamia katiba ni moja ya majukumu yake kama mkuu wa jeshi, hata ingetokea wakati wa Mwamunyange pia angefanya hivyo.
Usiongee kirahi rahisi namna hiyo!! CDF angeamua tofauti mambo yangekuwa tofauti
 
Ulishawahi kujiuliza ni kwa nini kwenye sherehe za kitaifa mfano sherehe za uhuru Rais ambaye pia ni amiri Jeshi mkuu wa Majeshi ya ulinzi na usalama huingia uwanjani kwenye gari la wazi akiwa ameambatana na CDF, hukagua gwaride la Majeshi ya ulinzi na usalama akiwa na CDF na hata anapoketi jukwaani pembeni yake anakaa CDF? Afu jiulize pia kwanini siyo IGP, mkuu wa magereza,nk?
Hizo sherehe ni za kijeshi na JW ndyo jeshi mama ndyo maana unaona kuna parade za jeshi jwtz wanatoa viongozi wa parade
 
Usiongee kirahi rahisi namna hiyo!! CDF angeamua tofauti mambo yangekuwa tofauti
Na hapakuwa na sababu ya yeye kuamua tofauti. Kwa vile anafahamu kuwa jeshi letu limekuwa likiendeshwa au kuongozwa kwa mujibu wa sheria na katiba ya nchi.
 
Je ulishawahi kujiuliza hicho nilichokueleza? Kuna wabunge, wakuu wa Wilaya hawajawahi kufanya ziara kwenye kata za majimbo/Wilaya zao. Hii haimaanishi hizo kata haziko chini yake.
Acha upuuzi miaka yote hawafanyi au hawajahi kufanya hata kwenye kata moja?
 
Huyu naye nyota yake bado iko juu.

Kwani yule mtangulizi wake (the man I like) hakuwa mweledi ?
 
Nani asiyekuwa na tamaa ya fedha acha kusingizia Wachaga.
Kweli mkuu hakuna binadam hata mmoja asiekuwa na tamaa ya pesa. Sema ndo hivyo, siku zote mti wenye matuda mazuri lazima upigwe mawe.
 
Huyu alimsaidia maza kuwa Rais vinginevyo bila huyu jamaa asingekuwa, Mwamunyange ni Mwenyekiti wijui wa bodi ya nini nimesahau
Hahaha.. Japo inawezekana kiongozi aliweka mchango wake ktk utawala huu kwa mujibu wa katiba, lkn naamini maamuzi hayakuwa ya kwake peke yake. Kwa vile lile lilikuwa jambo linalohusu ulinzi wa katiba yetu isinajisiwe (kama unavyosema kwamb ilitaka kufanyika ndivyo sivyo) basi ni wazi kuwa kulikuwa na majeneral, na viongozi wengine wakubwa wa jeshi waliochangia kufanya hali iwe sawa. Kumbuka hata mw Nyerere ilishindikana kumpindua kwa sababu katika uongozi wa juu kuna wale waliotaka kufanya mapinduzi na kuna wale waliokataa kufanyika mapinduzi. So usifikiri jambo nyeti la namna hiyo linachukuliwa uamuzi na mtu mmoja tu eti kwa sababu ni kiongozi, no kwa mfumo wa jeshi la Tanzania lililoshibishwa damu ya uzalendo kwa nchi yao, kwa raisi wao na kwa katiba yao, kamwe haiwezekani. Ni lazima uwashirikishe na wengine afu wao wakubali au wakatae. Ukifanya jambo ambalo haliendani na viapo vyao kivyako vyako na ukashtukiwa, huenda wale ma general unaowaongoza wakakugeuzia kibao na kuweka mtu wao wenyew anaowafaa. Hii ni Tanzania yenye jeshi na wanajeshi makini ndugu yang, kamwe usiifananishe na Myanmar au Sudan.
 
Hahaha.. Japo inawezekana kiongozi aliweka mchango wake ktk utawala huu kwa mujibu wa katiba, lkn naamini maamuzi hayakuwa ya kwake peke yake. Kwa vile lile lilikuwa jambo linalohusu ulinzi wa katiba yetu isinajisiwe (kama unavyosema kwamb ilitaka kufanyika ndivyo sivyo) basi ni wazi kuwa kulikuwa na majeneral, na viongozi wengine wakubwa wa jeshi waliochangia kufanya hali iwe sawa. Kumbuka hata mw Nyerere ilishindikana kumpindua kwa sababu katika uongozi wa juu kuna wale waliotaka kufanya mapinduzi na kuna wale waliokataa kufanyika mapinduzi. So usifikiri jambo nyeti la namna hiyo linachukuliwa uamuzi na mtu mmoja tu eti kwa sababu ni kiongozi, no kwa mfumo wa jeshi la Tanzania lililoshibishwa damu ya uzalendo kwa nchi yao, kwa raisi wao na kwa katiba yao, kamwe haiwezekani. Ni lazima uwashirikishe na wengine afu wao wakubali au wakatae. Ukifanya jambo ambalo haliendani na viapo vyao kivyako vyako na ukashtukiwa, huenda wale ma general unaowaongoza wakakugeuzia kibao na kuweka mtu wao wenyew anaowafaa. Hii ni Tanzania yenye jeshi na wanajeshi makini ndugu yang, kamwe usiifananishe na Myanmar au Sudan.
Ana mchango wake mkubwa sn kwenye hilo mkuu
 
Back
Top Bottom