Kwako Rais Magufuli sasa pasipo na kupepesa maneno: Kwa unavyoshughulika na Corona sasa - NO!

Kwako Rais Magufuli sasa pasipo na kupepesa maneno: Kwa unavyoshughulika na Corona sasa - NO!

Nitakuwa nauvuruga mjadala maana nimegundua kumbe mjadala umekaa kisiasa siasa zetu za Tanzania kwamba lazima uwe muungaji mkono au mpingaji wa serikali.

Mkuu kwani unadhani wala unatupa pressure. Tumekuelewa.

Kwani hata darasani wanafunzi wote ni lazima waelewe somo?

Ni hivyo hivyo hata humu jamvini IQ zote zipo.

Jimwage mkuu uko vizuri.
 
Nitakuwa nauvuruga mjadala maana nimegundua kumbe mjadala umekaa kisiasa siasa zetu za Tanzania kwamba lazima uwe muungaji mkono au mpingaji wa serikali.
Angalia maandiko yako yako vema... nilikunukuu ili utambue wapi kuna tatizo. Hili janga halihitaji siasa ni la wote ni mapambano ya pamoja si mapambio wala mapambo... ni hiyari yetu na jukumu letu kuchukua hatua stahiki la sivyo...
 
Ni wazi kuwa wenye ujasiri wa kuandika nyuzi kama hizi kwa maslahi ya taifa ndani ya vitisho vilivyopo si wengi, hivyo tafadhalini msiwe sehemu ya kuwanyamazisha.

Wanasema nani mwenye kumfunga paka kengele? Ni muhimu sasa bila ya kupoteza muda zaidi wala kumung'unya maneno, tumfunge paka huyu kengele vinginevyo twafa tukijiona.

Wenye ujasiri wamejitahidi kuweka jitihada binafsi kuwahami wananchi.

Heko baba askofu Niwemugizi. Pongezi anazoendelea kuzipata baba askofu huyu ni wazi kuwa hatua za namna hii ndizo zilizokuwa zikihitajika kwa muda sasa.

Mh. Rais tafadhali tuachane na mambo ya uchumi na siasa. Ugonjwa huu utamaliza watu kwa uzembe wenu.

Gharama za kuwaweka watu manyumbani salama wasife kwa njaa (peke yake) tu ni ndogo mno na zitazidi kupanda kadri siku zinavyopita.

Kwa jinsi ambavyo umekuwa ukishughulikia suala hili tangia mwanzoni wewe kama mtendaji mkuu imetugharimu kweli kweli. Hatukuweza kuuzuia ugonjwa
huu kuingia nchini, na wala hatukumwona hata mmoja katika safu zako aliyewajibishwa au kuwajibika.

Umekuwa ukilishughulikia suala hili kuuzuia ugonjwa huu kusambaa na bado ugonjwa unasambaa. Hatujamwona hata mmoja katika safu yenu aliyewajibishwa au hata kuwajibika.

Kwa mwendelezo huu ni wazi kuwa hatunayo nia ya dhati (seriousness) wala hatuchukulii umuhimu wowote mafanikio
au kushindwa katika vita hivi nyeti ambavyo hakuna taifa hata moja duniani lenye watu makini waliojaribu kuidunisha.

Kwa sababu ugonjwa huu unaenda kutuathiri kimaisha moja kwa moja (sisi na wapendwa wetu), kwa vile wawakilishi wetu labda hawakufikishii maoni yetu vilivyo, na kwamba eti wewe huyaoni haya, tunaomba kutumia maneno yako wewe mwenyewe:

"Kwa jinsi ambavyo umekuwa ukiendesha vita vya ugonjwa huu, tafadhali sasa NO!

Tunakupenda sana mheshimiwa. Lakini mheshimiwa kwenye hili la Corona, big No!

Kwa nini angalau Dar na Zanzibar haziko locked down? Mh. rais, Big No! Tumevumilia kweli kweli hadi tumelazimika kukupa ukweli huu. Mkuu big No!"

Cha kufanya kinafahamika. Kenya Rwanda na Uganda walio kama sisi wamefanya nini na sasa wanaudhibiti juu ya ugonjwa huu na karibu wanaanza kurejea kwenye shughuli zao za kawaida?

Please, Big NO!
Ati inadai Mh. Rais tafadhali tuachane na mambo ya uchumi na siasa. Ugonjwa huu utamaliza watu kwa uzembe wenu, mimi nakwambia hivi, ugonjwa huo utawamaliza watu wengi kwa uzembe, mzaha, sunyojali, na ujeuri wao. Serikali imetoa na insendelea kusisitiza matumizi ya kinga dhidi ya maambukizi, lakini wapi. Ni Sikio la kufa halisikii dawa.
 
Ni wazi kuwa wenye ujasiri wa kuandika nyuzi kama hizi kwa maslahi ya taifa ndani ya vitisho vilivyopo si wengi, hivyo tafadhalini msiwe sehemu ya kuwanyamazisha.

Wanasema nani mwenye kumfunga paka kengele? Ni muhimu sasa bila ya kupoteza muda zaidi wala kumung'unya maneno, tumfunge paka huyu kengele vinginevyo twafa tukijiona.

Wenye ujasiri wamejitahidi kuweka jitihada binafsi kuwahami wananchi.

Heko baba askofu Niwemugizi. Pongezi anazoendelea kuzipata baba askofu huyu ni wazi kuwa hatua za namna hii ndizo zilizokuwa zikihitajika kwa muda sasa.

Mh. Rais tafadhali tuachane na mambo ya uchumi na siasa. Ugonjwa huu utamaliza watu kwa uzembe wenu.

Gharama za kuwaweka watu manyumbani salama wasife kwa njaa (peke yake) tu ni ndogo mno na zitazidi kupanda kadri siku zinavyopita.

Kwa jinsi ambavyo umekuwa ukishughulikia suala hili tangia mwanzoni wewe kama mtendaji mkuu imetugharimu kweli kweli. Hatukuweza kuuzuia ugonjwa
huu kuingia nchini, na wala hatukumwona hata mmoja katika safu zako aliyewajibishwa au kuwajibika.

Umekuwa ukilishughulikia suala hili kuuzuia ugonjwa huu kusambaa na bado ugonjwa unasambaa. Hatujamwona hata mmoja katika safu yenu aliyewajibishwa au hata kuwajibika.

Kwa mwendelezo huu ni wazi kuwa hatunayo nia ya dhati (seriousness) wala hatuchukulii umuhimu wowote mafanikio
au kushindwa katika vita hivi nyeti ambavyo hakuna taifa hata moja duniani lenye watu makini waliojaribu kuidunisha.

Kwa sababu ugonjwa huu unaenda kutuathiri kimaisha moja kwa moja (sisi na wapendwa wetu), kwa vile wawakilishi wetu labda hawakufikishii maoni yetu vilivyo, na kwamba eti wewe huyaoni haya, tunaomba kutumia maneno yako wewe mwenyewe:

"Kwa jinsi ambavyo umekuwa ukiendesha vita vya ugonjwa huu, tafadhali sasa NO!

Tunakupenda sana mheshimiwa. Lakini mheshimiwa kwenye hili la Corona, big No!

Kwa nini angalau Dar na Zanzibar haziko locked down? Mh. rais, Big No! Tumevumilia kweli kweli hadi tumelazimika kukupa ukweli huu. Mkuu big No!"

Cha kufanya kinafahamika. Kenya Rwanda na Uganda walio kama sisi wamefanya nini na sasa wanaudhibiti juu ya ugonjwa huu na karibu wanaanza kurejea kwenye shughuli zao za kawaida?

Please, Big NO!
Kufungia watu ndani HAPANA. Raising wetu yuko kwenye njia sahihi. Huwezi kuelewa leo. Na hakuna namna us kukuelewesha. Fuatilia aesema nini na etoa with gani. Huwezi kuufuata wito wake kaa kimya. Ukiona vipi jiweke gerezani mwenyewe. Kama una misuli ya imani ingia vitani.
 
Hivi kufunga mipaka ya nchi kuzuia uhonjwa usiingie Ni siasa? Mkuu utakuwa Na tatizo kichwani.Tunawalaumu wanasiasa kwa kutochukua maamuzi thabiti.
Sasa mkuu na mie kusema kwamba corona ni janga duniani ndiyo kwamba nionekane natetea serikali na kwamba nalipwa? navyojua hayo maneno ya kwamba kuna watu humu sijui wanalipwa kwa kutetea serikali ni maneno yapo kwenye mabishano ya kisiasa sasa nashangaa mtu ananiambia nalipwa kwa kutetea serikali kwahiyo kumbe jamaa anachofanya ni kuishambulia serikali na ndio maana anaona mie naikingia kifua serikali.
 
Hivi kwa nini usiji lockdown wewe na familia yako na ukoo wako ikiwezekana ili muwe salama? Kuendelea kusubiria amri ni ujinga kama ujinga huu ulioandika . HUU UGONJWA NI UPEPO TU , KILA TAIFA UTAVUMA NA KUATHIRI NA KUPOTEA KWA NAMNA YAKE . NA TANZANIA NAMNA TETU NI HII HII YA KUMTEGEMEA NA MUNGU . HATULINGANISHWI NA NCHI YOYOTE HATA IWE KUBWA KIASI GANI .

JICHIMBIE HANDAKI KAKAE HUMO WEWE FAMILIA UKOO NA MARAFIKI NA JAMAA ZAKO .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Km unataka lockdown kaa Ndani Wewe na familia

Hivi vitumishi vyenye uhakika wa mwisho wa mwezi kero kweli

Kumbuka kuna watu lazima watoke Ndio wale

Sent using Jamii Forums mobile app
Upe ubongo nafasi ya kufanya kazi hii kabla ya mdomo, hamna aliyesema kuwa tunajitosheleza majumbani, na wala hakuna nchi yenye watu woote wana mishahara. Kinachozungumzwa hapa ni serikali kuwawezesha watu kukaa ndani. Ni vyema na nafuu yakifanyika mapema kuliko tutakapokuwa na waathirika milioni 4
 
Wamarekani wanaandamana toka juzi kupinga lockdown, watanzania wanalilia lockdown, hii dunia ina maajabu mengi sana.

Pengine watu waangalie takwimu za mataifa ya afrika kwa kulinganisha maambukizi dhidi ya wanaokufa.

Kuna uwezekano takwimu za vifo vya malaria zingekuwa nazo zinatolewa kama hizi za corona, tungeacha kutiana hofu za corona.

Fuata maelekezo chukua hatua hapo ulipo
 
Upe ubongo nafasi ya kufanya kazi hii kabla ya mdomo, hamna aliyesema kuwa tunajitosheleza majumbani, na wala hakuna nchi yenye watu woote wana mishahara. Kinachozungumzwa hapa ni serikali kuwawezesha watu kukaa ndani. Ni vyema na nafuu yakifanyika mapema kuliko tutakapokuwa na waathirika milioni 4
Kaa ndani na familia yako period
 
Kwa sababu hujasoma lolote huna ulichoelewa. Huna ulichojadili. Huna hoja. Huna lolote.

Hakuna povu lolote kwenye bandiko langu bali povu (au pumba) unaloliongelea unalo wewe na lipo kwenye bandiko lako.

Msitutishe. Hii nchi ni yetu sote. Ikibidi paka tutamfunga kengele. Hatuwezi kusubiria kufa tukiona ati kuwa tuondoke. Ondokeni nyinyi.
Kaaa ndani na familia yako. Kama wewe umejitosheleza kimaisha usilazimishe watu wengine wafe njaa. Kama unaona nje kuna ugonjwa kiherehere cha nini kwenda kuzurura. Tuliza kwato zako ndani angalia katuni na wanao, msaidie mkeo kufua khanga.
 
Mkuu kwani unadhani wala unatupa pressure. Tumekuelewa.

Kwani hata darasani wanafunzi wote ni lazima waelewe somo?

Ni hivyo hivyo hata humu jamvini IQ zote zipo.

Jimwage mkuu uko vizuri.
Najua kwa humu ni rahisi kunielewa maana humu ni lazima uwe mpingaji au muungaji mkono tu.
 
Mnapenda kuamrishwa kama Ng'ombe. Kwani wewe na familia yako mkikaa ndani si tayari lockdown tosha. Athari za ugonjwa huu mnazijua saaa why msubiri kila kitu hadi rais aseme? Mmepewa elimu ya huuu ugonjwa basi tumieni elimu hiyo kujilinda. Na kama mnaona lockdown ni suruhisho basi kaeni ndani na familia zenu. Mmekariri lockdown kama suluhisho la maambukizi.

Lockdown tensions grow as people seek to resume work or play

Coronavirus: US faced with protests amid pressure to reopen
Fikirisha kidogo akili yako mkuu. Issue sio mtu na familia yake, ugonjwa unaoambukiza hauishi kwa mtu mmoja kutibiwa na mwingine kuachwa au huyu kujikinga mwingine abaki kuwa carrier. Mimi nikiwa salama jirani yangu ana maambukizi, hapo hatujatokomeza ugonjwa bali tunaufuga, sasa sijui kwa nini ujitoe akili kwa jambo dogo hili ujifanye huoni umuhimu wa serikali kuingilia kwenye hili.

Kama una taahira kiasi cha kuamini hivi, mbona huishauri serikali iachane na vita ya madawa ya kulevya kwamba atakayetumia shauri yake? Acha siasa kwenye hili
 
Sawa kabisa na mie nikamaliza kwa kusema hakuna nchi yenye huo ugonjwa ambayo haikufanya uzembe kila nchi imefanya uzembe na ndiyo maana corona imeingia katika hizo nchi,kama unavyosema kuwa Tanzania ingefuata ushauri basi corona isingeingia kwa maana nyengine corona imekuwa janga duniani kwa sasa sababu dunia ilifanya uzembe.

Kwahiyo mie mkuu nilichokuwa naeleza ni kwamba corona ni janga duniani ila wewe hoja yako ni kwamba ni uzembe tu ndio unaofanya nchi kukumbwa na corona.

Dah kazi kweli kweli. Aliimba bwana mmoja "tuko tofauti". Mwisho wa kumnukuu.

Ila ambaye:

1. Hakuzuia ndege tokea kulikokuwa na waathirika wa ugonjwa huu,
2. Hakuwaweka quarantine wageni wote wakiwamo wale wa kutokea China kwa angalau siku 14 kabla ya kuwaruhusu kuingia nchini,
3. Hakufunga mipaka
4. Nk nk,

Hakufanya hadi ugonjwa wa hatari kama huu ukaingia nchini.

Endeleeni kumfariji.

Ila waathirika sisi hatuna maneno mazuri kwake kwa balaa alilotuletea na analoendelea kulilea likiendelea kusambaa kizembe uzembe namna hii.
 
Kwa sababu hujasoma lolote huna ulichoelewa. Huna ulichojadili. Huna hoja. Huna lolote.

Hakuna povu lolote kwenye bandiko langu bali povu (au pumba) unaloliongelea unalo wewe na lipo kwenye bandiko lako.

Msitutishe. Hii nchi ni yetu sote. Ikibidi paka tutamfunga kengele. Hatuwezi kusubiria kufa tukiona ati kuwa tuondoke. Ondokeni nyinyi.
Aunt punguza hasira,endelea kumuunga mkono mwana Ufipa mwenzio Askofu Niwemugizi maana alichokiamua Jimboni Lulenge ilikuwa ni katika kupingana na Rais Magufuli ktk kuliombea Taifa, ni hivyo tu.
 
Fikirisha kidogo akili yako mkuu. Issue sio mtu na familia yake, ugonjwa unaoambukiza hauishi kwa mtu mmoja kutibiwa na mwingine kuachwa au huyu kujikinga mwingine abaki kuwa carrier. Mimi nikiwa salama jirani yangu ana maambukizi, hapo hatujatokomeza ugonjwa bali tunaufuga, sasa sijui kwa nini ujitoe akili kwa jambo dogo hili ujifanye huoni umuhimu wa serikali kuingilia kwenye hili.

Kama una taahira kiasi cha kuamini hivi, mbona huishauri serikali iachane na vita ya madawa ya kulevya kwamba atakayetumia shauri yake? Acha siasa kwenye hili
Kaa ndani na familia yako period. Huyo jirani unayesema hakuna distance ya 2metres? Acha ujuaji
 
Km unataka lockdown kaa Ndani Wewe na familia

Hivi vitumishi vyenye uhakika wa mwisho wa mwezi kero kweli

Kumbuka kuna watu lazima watoke Ndio wale

Sent using Jamii Forums mobile app
Ningejua lupo ningekuleta barakoi yenye maambukizi,wenzako wote wanacomment seriously wewe tu.
Watu tuna ndugu wazazi na watoto wanye familia wewe unataka nijiunge mimi tu itasaidia nini kama wewe unapoteza maisha kizembe
 
Back
Top Bottom