Kwamba Mzee Warioba, Butiku, Shivji, Bagonza, Pengo, Kitima wamelipwa kukataa Mkataba wa DP World?

Kwamba Mzee Warioba, Butiku, Shivji, Bagonza, Pengo, Kitima wamelipwa kukataa Mkataba wa DP World?

Hao wezi waliokuwa wananufaika na Bandari wana nguvu sana; kama wameweza kumwonga na kumshawishi hadi Waziri Mkuu mstaafu Jaji Warioba , Mzee Butiku ambao ni wazee wa CCM nani tena watashindwa kumwonga?

Kwa taarifa zilizotoka hivi karibuni zinaonyesha wanaopinga mkataba huu ni wezi waliokuwa wananufaika na Bandari na kwamba wanatumia nguvu kubwa kuwahonga wananchi kupinga nia nzuri ya serikali.

Nini mtizamo wako kuhusu version mpya ya utetezi iliyoanzishwa na serikali? Hao wanaohonga ni wakina nani? Niwatanzania wenzetu? Kwanini serikali inashindwa kuwashtaki Kisutu? Je, wakishindwa kuwapeleka Kisutu watawezana na huyu bwana mwenye mkataba wakwenda kuishtakiwa Uingereza au South Afrika?

Kila siku tunatiwa hatiani huko ulimwenguni je tunapokwenda kumwabudu binadamu aitwaye DP World tutamdhibiti vipi asihonge?
Unajuwa sio kila anayepinga au kuunga mkono kalipwa hapana sio kweli ila ziko sababu, na nataka kuongelea hawa wazee maana huku nje tumegawanyika sana. Kuna watu walikuwa kwenye mfumo muda mrefu na wanadhani hawapewi heshima wanayostahili wao au kuna chuki dhidi ya CCM ndani ya mioyo yao mfano tu Warioba muda mrefu amekuwa kitu kinamsumbua kajaribu watoto zake wapenyeze kisiasa kapata ugumu halafu akiona watoto wa wenzake wanapata lazima inamuuma nafsi yake pia inamshusha kwa family yake. Ila huyu huyu siku mtoto wake akibebwa tu utasikia kauli tofauti wote wanajali family zao na matumbo tu sio taifa.

Hawa hawa wanaokataa bandari wakati JPM anawapiga spana wazungu kwenye migodi walitoka hadharani na hasa Lissu kumponda JPM huyu anakurupuka ataleta shida na wawekezaji alisimama na wazungu 100% mpaka ndege inashikwa SA wakaanza kumkebei JPM, leo wamekuwa watetezi. CCM kosa walilofanya wao wangeanza na kuikataa DP tu wapinzania wangekuja CCM majambazi hawataki uwekezaji wangefanya wamewasikia wangepata wanachotaka na kukubali. Kuna watu kama watoto tu lazima ucheze na akili zao jifanye hutaki tu watapinga kumbe ndio unakotaka.
 
Hakuna mkataba wowote wa uendeshaji bandari uliosainiwa, ndiyo kwanza makampuni yanashindanishwa na TPA, vijana wanajilia mihela tu huko kila wanapochelewesha.
Wewe ni nani mpaka uongee maneno haya tofauti na speaker wa Bunge la JMT aliyepitisha huu mkataba na kwa maneno yake mwenyewe Speaker Dr. Tulia alisema Bunge limeupitisha MKATABA?
 
Hivi Usalama wa Taifa kazi yao huwa ni Nini haswa kwenye masuala sensitive kama haya mamikataba ya kipuuzi wananyamaza kimya tu. Ukiangalia Bandari ndio mlango wa kiusalama na wapo kimya tu, mnalinda kitu gani?!?
Samahani kwa kusema haya.


Ni mpumbavu tu anaeongelea mkataba wakati hakuna mkataba.
 
Duh!

Makampuni gani "yanashindanishwa"?
Wewe huyo huyo umekwishaandika mara kadhaa humu, kwamba DP World, tayari anafunga vifaa bandarini, sasa tuelewe lipi?

Kama "Makubaliano", ambayo hutaki kuyaita jina la "Mkataba", ni mabovu, huo "Mkataba" wenyewe unaotokana na makubaliano mabovu utakuwaje?

Hata fikra tu za kufikiri hili kirahisi hivi hamuwezi?

Inaonekana sasa, kila mnaloleta kuwahadaa watu, mnazidi kuonyesha ubovu wa jambo lote mnalotaka kuwasukumia waTanzania.

Hawakutegemea jambo hili kutoeleweka.
 
Pengo
Kitima
Bagonza ..
Hawahitaji kuhongwa ...wao Wana uadui wa kiimani na waarabu....

Shivji haihitaji kuhongwa,Shivji ni Communist ndo maana wala hasemi mkataba urekebishwe ..anasema serikali ifanye kazi hiyo...haelewi dunia ya sasa hata serikali za Uingereza na Ujerumani zimebinafsisha bandari...
Shivji kabaki Karne ya 20...ya kina Nyerere na Mao Zedong...na Lenin ..

Warioba na Butiku wanahitaji anything wawe relevant....hawa ni wazee wa Karne ya 20... Hardliners conservative...wafuasi wa Nyerere....
Hawa wote wanaongea wanayo yaamini huku Karamagi akiwalainisha na kuwapa nguvu financially
Ofcourse nakubaliana na wewe mkuu. Mitazamo ya kijamaa na ubinafsishaji ni paka na panya
 
Pengo
Kitima
Bagonza ..
Hawahitaji kuhongwa ...wao Wana uadui wa kiimani na waarabu....

Shivji haihitaji kuhongwa,Shivji ni Communist ndo maana wala hasemi mkataba urekebishwe ..anasema serikali ifanye kazi hiyo...haelewi dunia ya sasa hata serikali za Uingereza na Ujerumani zimebinafsisha bandari...
Shivji kabaki Karne ya 20...ya kina Nyerere na Mao Zedong...na Lenin ..

Warioba na Butiku wanahitaji anything wawe relevant....hawa ni wazee wa Karne ya 20... Hardliners conservative...wafuasi wa Nyerere....
Hawa wote wanaongea wanayo yaamini huku Karamagi akiwalainisha na kuwapa nguvu financially
Unasema kinyume!! Uwezekano mkubwa ni kuwa wale wanaolazimisha mkataba hata kwa gharama ya kubadilisha sheria zetu ili zikubaliane na mkataba wa bandari, hao ndio tuwatilie mashaka kuwa wamekula kitu kidogo!! Ndiyo kwa mwarabu ni kitu kidogo lakini kwa hawa wabongo wenzetu wanaona wamepokea kitu kikubwa!!
 
Na hao waTanzania wengine wanaosoma nyaraka ya "Makubaliano" na kuielewa kwa uovu uliomo humo ndani unawaweka fungu gani?

Sawa, tukubali akina Pengo na wenzake, umesema "hawahitaji kuhongwa...wao wana uadui wa kiimani na waarabu"; na wewe je?
Huhitaji kuhongwa kwa vile una urafiki na waarabu; kwa kushinda kutwa ukitetea kila kitu ambacho wengine wanaona kina kasoro?
Kitu wanachoshindwa kujua ni kuwa nani nyuma ya DP .
Je uwekezaji wa mafuta Emirates ulifanywa kwa mtaji wa nani?. Walstreet na who controls it?.
Je wamaamini wapo nje ya mtego wa akina Yared Abihud .
Je the superpower kawaruhusu DP worls wawe na monopoly ya transportation hub in the world wasiwe na maslahi?.
Why this is not proxy war between huha na wasap men?.
Our thinking ipo chini sana.anyway nimevamia thread yako tu as a great thinker.
 
Pengo
Kitima
Bagonza ..
Hawahitaji kuhongwa ...wao Wana uadui wa kiimani na waarabu....

Shivji haihitaji kuhongwa,Shivji ni Communist ndo maana wala hasemi mkataba urekebishwe ..anasema serikali ifanye kazi hiyo...haelewi dunia ya sasa hata serikali za Uingereza na Ujerumani zimebinafsisha bandari...
Shivji kabaki Karne ya 20...ya kina Nyerere na Mao Zedong...na Lenin ..

Warioba na Butiku wanahitaji anything wawe relevant....hawa ni wazee wa Karne ya 20... Hardliners conservative...wafuasi wa Nyerere....
Hawa wote wanaongea wanayo yaamini huku Karamagi akiwalainisha na kuwapa nguvu financially
The boss ...

Unazingua HV unajionaga una akili kubwa kuliko watanzania wengine wanao gomea huu mkataba

Una akili Kweli wew
 
Hata kama hawajalipwa ,hao ni Wajamaa minded people ambao hawanaga Msaada wowote Wala hawajui uchumi zaidi ya kuongozaa Kwa hisia na propaganda..

Sasa hao wazee Wana nini Cha kuonesha Kwa miaka Yao yote ya utumishi ikiwa hadi.leo hii madawati na vyoo viliwashinda?

Wakae Kwa kutumia wafundishwe Uchumi wa kuwafanyia Wananchi matajiri,hao ni aina ya watu wanaotaka wenzao wazisi kuwa maskini Ili wao waendee kuwatawal.
Nawew the cost ....

Acha upumbafu
 
Wewe hz hbr umetoa wapi mnk kwa ushabiki wa kijinga uko vzr
Unaonesha huso,i magazeti wala husikilizi taarifa za habari.

Wewe unaingia mitandao ya udaku, nayo pia nadhani huisomi vizuri. Ungekuwa unaisoma basi hata kuandika kwako kusingekuwa hivyo kama unaandikiana sms na mwenzako.

Pole sana kijana, nakuhisi ni kama kondoo unaechungwa na mchungaji aliyepotea.
 
Back
Top Bottom