Kwangu mimi Rais Magufuli amefanya jambo la haraka kumuondoa Naibu Waziri wa Madini, hakuna uhusiano wowote kati ya kuzungumza na kufanya kazi

Yeye ndi

Yeye ndiye aliyemchagua na yeye ndiye aliyemuondoa tatizo lipo wapi? Tuvimiliane maana yake una muhali wewe nchi haitaenda kwa kuvumiliana
Tuvumiliane katika ukosefu wa weledi wenye athari kubwa kwa maslahi mapana ya nchi!A big NO,hii sio awamu ya akina Vasco Dagama,hapa kazi tu,kama huwezi kazi,kule!
 
Siamini kama watu wa vetting hawakuwa na taarifa sahihi za huyu jamaa,chamsingi Rais kabla ya kusema pale angechunguza kwanza........
 
Naambiwa jamaa kumbe alipigwa na stroke wakati wa uchaguzi hvo hayuko fit 100%.
Na ameshika nyashifa mbalimbali hadi TFF amekuwa akisafiri na team.
TFF ni chaka Mkuu,ni kuwekana tu.Anyway aliyehusika kumchomekea Rais kihiyo kama huyo naye anastahili kuwajibishwa.Hatuwezi kuendelea hivi.
 
Naambiwa jamaa kumbe alipigwa na stroke wakati wa uchaguzi hvo hayuko fit 100%.
Na ameshika nyashifa mbalimbali hadi TFF amekuwa akisafiri na team.
TFF ni chaka Mkuu,ni kuwekana tu.Anyway aliyehusika kumchomekea Rais kihiyo kama huyo naye anastahili kuwajibishwa.Hatuwezi kuendelea hivi.
 
Hapana .nimeambiwa Ndulane alipata stroke kipindi cha uchaguzi.
Sawa,kama walijua alipata stroke,kwa nini walimchomeka,si wangeacha apone kwanzaa.....!Wana haraka gani?No,waliomchoneka watafutwe, wawajibishwe,hawako makini.Wameliabisha taifa.Si tunaonekana sasa kwamba watanzania wote ni vihiyo,no haikubaliki.Tukio hili lina very far reaching repercussions.
 
ikitokea tukamuchagua Rais siku ya uapisho akashindwa kabisa kuapa je atapisha ama uchaguzi utarudiwa??
 
Suspect no 1 atakuwa Ni KsK
 
Waziri siyo mtendaji bali anashughulika zaidi na sera sasa kama hawezi kuongea then he is unfit for the position.
Acha uboya wewe, mbona Magu mwenyewe hawezi nyoosha sentensi tano za kingereza so naye hafai
 
Brother kuwa muangalifu na taarifa zako.sio kilwa kusini ni kilwa kaskazini!Aligombea kilwa kaskazini
 
Mm nahic jamaa huoni wake ni hafifu inawezekana Yale maandishi alikuwa anashindwa kuyaona vizur
 
Kushindwa kuongea ni kitu tofauti kabisa na kushindwa kusoma mistari michache. Huyu kashindwa kusoma hata baada ya kuachwa ajikusanye

Kama hawezi kucontrol emotions mbele ya camera, bora tu abakie na ubunge wake akakae benchi la nyuma kabisa
Kama ungefuatilia historia yake ya utendaji kazi, wala usingeandika hayo uliyoandika, ila kwakuwa kuna watu kila jiwe alifanyalo lazima mu support, sawa!! Kweli kwa mtizamo wa kibinadamu, hilo lilikuwa na kufanya utengue uteuzi wake?!!
 
ikitokea tukamuchagua Rais siku ya uapisho akashindwa kabisa kuapa je atapisha ama uchaguzi utarudiwa??
Haiwezekani Rais aliyechaguliwa kushindwa kuapa,that is unthinkable mkuu. Hata hivyo swali lako lina nia mbaya:kujaribu kuonyesha kwamba kitendo alichofanya Rais si sahihi,kwa hiyo tuvumiliane.

Nisisitize,maamuzi aliyofanya Rais ni 100% correct.Wengine wanasema alipata stroke huko nyuma,basi atibiwe kwanza apone,hatuwezi kufanya makosa kwenye masuala ya msingi.
 
Kwani wewe unafikiri ukiweza kunyoosha kiingereza basi wewe ni intelligence enough? Mkuu argue construstively!!
Yaani mkuu Watanzania dah!Yaani sijui kwa nini tunashindwa kuelewa kwamba Kingereza ni kama Kigogo,Kinywamwezi,Kizaramo nk.,it's just a language like any other. Walichofanya Waingereza ni kukipaisha Kingereza ili kionekane kwamba it is associated with sophistication and intelligence, hakuna lolote.People need to wake up.
 

Labda amemsaidia mapema. Maana kwa uoga huo, uwaziri wa nini?
Halafu JPM alivyo....kaenda tena nje ya bunge ili waendelee kurogana
 
Kama ungefuatilia historia yake ya utendaji kazi, wala usingeandika hayo uliyoandika, ila kwakuwa kuna watu kila jiwe alifanyalo lazima mu support, sawa!! Kweli kwa mtizamo wa kibinadamu, hilo lilikuwa na kufanya utengue uteuzi wake?!!
Basically Rais hakuwa na options nyingi na hii ya kutengua ni sahihi tu.

Kile kitendo cha kujiumauma mbele ya camera hakikuwa sawa na wala Rais hawezi kulaumiwa kwa aliyoyafanya. Imagine scenario angesamehewa na akaja kushindwa tena..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…