Kwangu mimi Rais Magufuli amefanya jambo la haraka kumuondoa Naibu Waziri wa Madini, hakuna uhusiano wowote kati ya kuzungumza na kufanya kazi

Kwangu mimi Rais Magufuli amefanya jambo la haraka kumuondoa Naibu Waziri wa Madini, hakuna uhusiano wowote kati ya kuzungumza na kufanya kazi

Francis Ndulane alikuwa Mhasibu Mkuu wa Tanroads Mkoa Lindi, Magufuli alipo ingia Madarakani kama Rais akamteua kuwa Mkurugenzi wa Mji Ifakara.

Mwaka huu akagombea ubunge, kwenye kura za maoni ndani ya chama akashika nafasi ya tatu kwa kupata kura 21 nyuma ya Ahmed Raphael Bongi aliyekuwa amshindi wa kwanza kwa kura 155 ambaye alikuwa ni Mhasibu mkuu wa Mkoa wa Lindi.

Ila kamati kuu ya CCM ikarudisha jina aliyeshika nafasi ya tatu Francis Ndulane kuwa mgombea jimbo la Kilwa kusini.

Rais Magufuli mwenyewe ameunda Baraza lake baada ya kupita takriban wiki 3 baada ya uchaguzi kupita ,hivi bila shaka alijidhihirisha kuwa ni mtendaji mzuri.

Kilichompata ndugu yetu kinaweza kumpata mtu yeyote katika mazingira yoyote mathalani ni jambo furaha hivo mhusika alikuwa yuko temper.

Mh. Francis Kumba Ndulane. Mbunge wa Kilwa kaskazini - CCM aliyekuwa ameteuliwa kuwa Naibu Waziri Nishati, kwa bahati mbaya ameondolewa katika nafasi hiyo kwa kile kinachodaiwa kushindwa kuapa. Mh Ndulane anaonekana katika video akisoma kiapo kwa kusitasita kama anakigugumizi (stama).

Kilichompata Mh. Ndulane kisaikolojia kinaitwa ' Occasional Anxiety'. Kiufupi ni hali ya wasiwasi isiyotarajiwa inayomkuta mtu kufuatia jambo fulani kumpata au kulazimika kulifanya.

Jambo hilo laweza kuwa geni kabisa au kutokana na uzito wake likawa na mvuto mkubwa kijamii. Mazingira haya hutufanya baadhi yetu kuingiwa na wasiwasi hatimaye kushindwa kulifanya kwa ufanisi unaotarajiwa.

Katika mazingira ya uanafunzi, baadhi wanapokuwa katika vyumba vya mitihani ya taifa hukumbwa na hali hii. Hukuta hata mwanafunzi anashindwa kushika kalamu na kujikuta vidole vikitoa jasho huku mkono ukitetemeka,saa zingine hutokea wakati wa ku-present kitu ,niliwahi kusoma na msichana yani alipoingia panel alizimia kabisa.

Baadhi yetu tumeshuhudia katika mazingira ya vyuo vikuu, wanachuo wenzetu wakishindwa kusimama mbele ya wanafunzi wenzao na kuzungumza. Ipo mifano mingi.

Hali hii huwa haina kusema umesoma shahada (degree) ngapi. Ni tendo kisaikolojia. Katika matukio kama ya kuhutubia, kuapishwa nk.ndio maana ili kupunguza uwezekano wa kutukia kitu kama hicho, watu hulazimika kufanya kitu kinaitwa ' rehearsal' kabla ya tukio husika.

Tusimshambulie mh. Francis Ndulane kama mtu wa ajabu kwakuwa kilichomtokea, kimewatokea wengi na kitawapata wengi.

Tusimfedheshe. Tumfariji, hasa ukizingatia kapoteza fursa adhimu ambayo wengine huitafuta kwa udi na uvumba,wengine hutoa hadi kafara.

Hapo washauri wa Mh.Rais wanatakiwa kumshaauri vizuri haikupaswa hatua ya kumwondoa iwe kwa haraka vile. Lile ni jambo la kawaida sana.

Hakuna uhusiano kati ya utekelezaji majukumu kwa ufasaha na uwezo wa kuzungumza na ikizingatiwa kwa Ndulane nafasi kubwa kama ile nadhani ni ngeni na ni mara ya kwanza kwake kuteuliwa kuwa naibu waziri , lkn wkt mwingine feelings na namna mtu anavyolichukulia jambo kwa uzito mkubwa huweza kumfanya yeyote akakutwa na hali ile hali...ukichukulia ule ukali wa Magufuli wa kuwatukana mawaziri wapumbavu ndo basi kabisa Ndulane alitaka afanye haraka amalize.

Hata leo Biden alikuwa anaapisha baadhi ya watendaji kuna mama alikuwa anakosea hadi lugha lakini hamkumuondoa.

Tujifunze kuvumiliana.
Thats why there is always a room for the second chance.
Najua washauri wa Rais watamshauri ampatie jamaa nafasi ya pili..Majaliwa na Makamu wa Rais kasi kwenu.
Haijalishi alikuwa nani wala ni nani mimi naona sawa tu hata wangeondolewa wote maana wao ni kuongea tu maagizo toka juu na kurusha mikono juu mbele ya kamera za luninga lakini matatizo ya wananchi hawatatui kabisa huyu hata kusoma tu kiapo kilichotayarishwa na watu wengine hawezi. Maagizo toka juu atafikishaje kwa wananchi ili wapongeze na kusifia juhudi na mafanikio ya Awamu? Waende wote tubaki na Rais wetu mpendwa na matatizo yetu miaka 5 ijayo!
 
Basically Rais hakuwa na options nyingi na hii ya kutengua ni sahihi tu.

Kile kitendo cha kujiumauma mbele ya camera hakikuwa sawa na wala Rais hawezi kulaumiwa kwa aliyoyafanya. Imagine scenario angesamehewa na akaja kushindwa tena..
Yule mwana mama mbona alikuwa anakoseakosea ila hakuna hata Onyo basi ndio kwanza alimsifia.
 
Ilitakiwa katiba ibadilishwe wapendekezwe na rais ila wapigwe drills bungeni au na kamati maalumu wakivuka vihunzi ndio rais awateue rasm na kula kiapo.
Hapana tufuate Rasimu ya Waryoba yenye maoni ya wananchi yanayotaka Mawaziri wasiwe Wabunge ili kumpa Rais Uwanja mpana wa kuteua Mawaziri bora kutoka kuwa Jamii ya Watanzania milioni 60 waliopo na kuthibitishwa na Bunge. Kulazimisha Rais kuteua Mawaziri 46 toka Wabunge 250 tu matokeo yake ndo hayo wateuliwa wanashindwa hata kuapa na kutenguliwa hadharani na wanaopenyeza ndo wanakuwa mizigo kwa wananchi wakiendeleza umasikini usiyoisha. Aende tu Wabunge hata wakina Kibajaji na Msukuma wa kujaza hiyo nafasi wapo wengi wa Chama chake kuwahi kutokea tangu Uchaguzi wa 1995. Shida iko wapi?
 
Kuna ushirikina unahusika. Huwezi jua yamaa kusogelea tu pale zike irizi za meko zikaanza kumchapa fimbo..maana yake asingeweza kufanya naye kazi.
 
Hapana tufuate Rasimu ya Waryoba yenye maoni ya wananchi yanayotaka Mawaziri wasiwe Wabunge ili kumpa Rais Uwanja mpana wa kuteua Mawaziri bora kutoka kuwa Jamii ya Watanzania milioni 60 waliopo na kuthibitishwa na Bunge. Kulazimisha Rais kuteua Mawaziri 46 toka Wabunge 250 tu matokeo yake ndo hayo wateuliwa wanashindwa hata kuapa na kutenguliwa hadharani na wanaopenyeza ndo wanakuwa mizigo kwa wananchi wakiendeleza umasikini usiyoisha. Aende tu Wabunge hata wakina Kibajaji na Msukuma wa kujaza hiyo nafasi wapo wengi wa Chama chake kuwahi kutokea tangu Uchaguzi wa 1995. Shida iko wapi?

Rasimu ya Warioba Haina tena nafasi. Ajiandae kumjibu Nyerere kwanini alitaka kuuvunja muungano huko sote tutakokwenda
 
Hiyo hali hutokea Watu wengi hata Jacob Zuma akishindwa kusoma na kutamka " in the begining" kuna Mkurugenzi alitamka " mimi ni Mkuruzenzi mpya x2" , Barack Obama nae alishindwa kuapa vizuri hata Magufuli mwenyewe alishindwa kutamka neno " Entrepreneur" hili Rais kateleza ajifunze kutokana na hili kosa!
 
Hawezi kuongea kivipi? Huyu ambaye ameshika nyadhifa byingi kabla hata ya kugombea ubunge bila shaka alikutwa na maswahibu ya kisaikolojia yaliyomfanya atekewe na kushindwa kuzungumza. Rais angetafakari kumpa nafasi nyingine.
Haiwezekani akawa kiongozi mzuri kwa ngazi ya uwaziri kama akipata mshtuko kidogo tu anakengeuka kwa muda mrefu vile.....yaani alipewa muda mrefu kurudia kuapa bado akashindwa...hafai
 
Hiyo hali hutokea Watu wengi hata Jacob Zuma akishindwa kusoma na kutamka " in the begining" kuna Mkurugenzi alitamka " mimi ni Mkuruzenzi mpya x2" , Barack Obama nae alishindwa kuapa vizuri hata Magufuli mwenyewe alishindwa kutamka neno " Entrepreneur" hili Rais kateleza ajifunze kutokana na hili kosa!
kuchapia ni tofauti na kushindwa kabisa
 
Back
Top Bottom