Kwani CHADEMA huo mkutano ni kongamano la injili? Mnajiharibia

Kwani CHADEMA huo mkutano ni kongamano la injili? Mnajiharibia

Unataka vipi suala la mkataba lisihusishwe na dini wakati unaposema hivyo uko pembeni mwa Askofu?
Kwani Askofu anazuiwa na nani kutoa maoni yake? Mafundisho ya dini yanakemea rushwa, na wale wahuni waliosaini wana dini zao na walikula rushwa, hawateeki kamwe.
 
Kwani Askofu anazuiwa na nani kutoa maoni yake? Mafundisho ya dini yanakemea rushwa, na wale wahuni waliosaini wana dini zao na walikula rushwa, hawateeki kamwe.
Askofu anatoaje maoni yake bila kuleta maswali kwamba suala hili ni la udini?

Madeleka kasema hili suala ni la kisheria, habari za imani acheni kanisani, mbona hata sheria nazo hazikubali rushwa? Kwa nini tusikemee rushwa ki secular kwa sheria bila kuhusisha dini?

Huoni kukemea rushwa kidini wakati mmeshasema mambo ya imani acheni kanisani ni contradiction?

Kama mafundisho ya kidini yanakemea rushwa, na wale wana dini zao wamekula rushwa, huoni kwamba mafundisho ya kidini hayasikilizwi, tunatakiwa kujenga legal case na kuwashitaki watu kisheria bila kutegemea dini?
 
KWANI CHADEMA WAMEITA KONGAMANO LA INJILI?

Na Thadei Ole Mushi.

Kosa la Kifuufundi hili Chadema wamelifanya.

1. Sakata la Bandari toka awali lilianza kuhusishwa na imani za Kidini.

2. Mkutano wa Keshokutwa wa Chadema wazungumzaji wanne kati ya 13 ni viongozi wa dini ya Kikristu.

4. Wengine Tisa waliobakia pia ni wa madhehebu ya Kikristu.

5. Katika Sayansi ya Siasa hapa Chadema Wamenesa bila kujua.

6. Inductive na Deductive appoach zote kwa pamoja zinaruhusu watu wa-Draw conclusion kuwa Chadema na Ukristu ni vitu vibavyokwenda Sambamba.

7. Nilitamani wangerekebisha hili Kosa kwa kuwa Chadema tunaitegemea kama Chama Mbadala wa CCM. Siku CCM ikichoka kuendesha nchi Chadema ichukue Nchi.

8. Nafikiri hawa Maaskofu na Mapadre na Wachungaji ni vizuri zaidi wangekuwa wanatolea misimamo yao kwenye mimbari ya kanisa na sio kwenye majukwaa ya Kisiasa.

9. Cardinali pengo aliwahi kutuasa tusichanganye Siasa na Dini ni hatari.

10. Fanyeni Mpango leo na Kesho mchanganye wazungumzaji ili kuleta umoja wa Kitaifa. Huu ni mkutano wa kisiasa sio mkutano wa maombi.

Ukweli lazima usemwe tu chadema na udini ni pete na kidole. Kuanzia leo narudisha kadi ya chadema naenda CCM!
Ole Mushi huwa unakosea sana unapodhani kuwa siku zote wakati wote mawazo yako huwa ni sahihi. Hapa na wewe umekosea sana kwa hili andiko lako. Kwanini utangulie kuiona dini ya mtu kabla ya utu wake? Kuna taarifa umeletewa kuwa kuna watu wa Islam wamenyimwa nafasi ya kutoka mawazo yao katika mkutano huo kwasababu ya dini yao?

Wewe mwenyewe unaonekana unao sana udini kwasababu umeweza hata kuwahesabu washiriki kwa majina au dini zao. Kwanini unadhani palitakiwa kuwepo balance ya dini? Mgema akisifiwa sana......
 
Hatuwezi kuwasubiri mashekhe wamaoshindwa kuyaona makosa ya Samia kwasabb ya uislam wake.

Ukombozi unaanza na mtu mmoja ama kundi moja. Mtu huyo ama kundi yaweza kuwa waislam ama wakristo

Zingatia hoja na madhumuni ya mkusanyiko siyo aina ya watu waliokusanyika
Hii nchi kuna wapumbavu wanaamini kuna dhehebu linaloiendesha.
 
KWANI CHADEMA WAMEITA KONGAMANO LA INJILI?

Na Thadei Ole Mushi.

Kosa la Kifuufundi hili Chadema wamelifanya.

1. Sakata la Bandari toka awali lilianza kuhusishwa na imani za Kidini.

2. Mkutano wa Keshokutwa wa Chadema wazungumzaji wanne kati ya 13 ni viongozi wa dini ya Kikristu.

4. Wengine Tisa waliobakia pia ni wa madhehebu ya Kikristu.

5. Katika Sayansi ya Siasa hapa Chadema Wamenesa bila kujua.

6. Inductive na Deductive appoach zote kwa pamoja zinaruhusu watu wa-Draw conclusion kuwa Chadema na Ukristu ni vitu vibavyokwenda Sambamba.

7. Nilitamani wangerekebisha hili Kosa kwa kuwa Chadema tunaitegemea kama Chama Mbadala wa CCM. Siku CCM ikichoka kuendesha nchi Chadema ichukue Nchi.

8. Nafikiri hawa Maaskofu na Mapadre na Wachungaji ni vizuri zaidi wangekuwa wanatolea misimamo yao kwenye mimbari ya kanisa na sio kwenye majukwaa ya Kisiasa.

9. Cardinali pengo aliwahi kutuasa tusichanganye Siasa na Dini ni hatari.

10. Fanyeni Mpango leo na Kesho mchanganye wazungumzaji ili kuleta umoja wa Kitaifa. Huu ni mkutano wa kisiasa sio mkutano wa maombi.

Ukweli lazima usemwe tu chadema na udini ni pete na kidole. Kuanzia leo narudisha kadi ya chadema naenda CCM!
Taasisi yenye watu makini na wenye kusudi la kushika dollar hawawezi kupuuza angalizo hili nyeti lisiloonekana kirahisi. Italifanyia kazi japo sio Lazima iwe kesho au keshokutwa ili kuleta umoja imara na kuepusha minong'ono
 
Askofu anatoaje maoni yake bila kuleta maswali kwamba suala hili ni la udini?

Madeleka kasema hili suala ni la kisheria, habari za imani acheni kanisani, mbona hata sheria nazo hazikubali rushwa? Kwa nini tusikemee rushwa ki secular kwa sheria bila kuhusisha dini?

Huoni kukemea rushwa kidini wakati mmeshasema mambo ya imani acheni kanisani ni contradiction?

Kama mafundisho ya kidini yanakemea rushwa, na wale wana dini zao wamekula rushwa, huoni kwamba mafundisho ya kidini hayasikilizwi, tunatakiwa kujenga legal case na kuwashitaki watu kisheria bila kutegemea dini?
Hii nchi kwa akili kama yako tutasubori sana. Kwani askofu anatoa maoni kama askofu au kama mwananchi? Kwahiyo kama mtu ni askofu anakosa haki ya kuwa mwananchi? Ccm imefanikiwa sana kwenye hili eneo.....
 
Wakristo wakiamua kumuunga kila kiongozi mkono mkristo hata km anaboronga km waislam wanavyofanya mjue ndio itakuwa mwisho wa TANGANYIKA

Waislam acheni kuweka dini kwenye maslahi ya Taifa kiongozi apimwe kwa uwezo wake sio mnatumia mgongo wa dini kumfichia uhaini
Kwani nyie mnaitakia mema Tanzania? Mnakoelekea hata hamkujui, wenzenu wanapakukimbilia.
Ubelgiji ana bangalow, na mwenzangu mimi utakimbilia wapi?
 
hawana ujanja kabisa, kesi yao ya Mbeya mbona hawaiongelei tena?

Nasikia mawakili uchwara walikula fimbo usiku hawajuwi zinapotokea.
Hakuna kesi pale, jifurahisheni tu. Wala hakuna cha kupoteza muda kuzungumzia kesi ile. Wasiokuwa na muda ndio waende huko mahakamani na kuandika hapa JF.
 
Wajanja tulishajua kitambo kuwa hii ni vita ya Kidini na CHADEMA kwa kuwa uwanzishwaji wake ulikuwa na mrengo huo ili ku counter attack CUF kipindi hicho na waka take advantage. Wewe umeona wapi Ma askofu wachungaji na viongozi wengine wa kikristu wakawa ghafla wameguswa na issue ya Bandari ilihali hatukuwasikia hapo kabla kwenye issue nyingine za ki inchi. Ina maana tangu Uhuru hii ndo jambo kubwa zaidi?
Tatizo siasa sijui mmeanza kufuatilia juzi, nani asiyemjua Askofu Mwamakula?, Na Padri Kitima je, vipi kuhusu Dkt Slaa? Yaani hata kama huna kumbukumbu basi hata google tu uone harakati zao since wayback na changamoto walizopitia kabla ya kuongea Shudu kuwa wameibukia kwenye huu mkataba
 
Back
Top Bottom