Kwanini Barabara mpya kwa Jiji la Dar es Salaam zinajengwa kwa njia 4?

Kwanini Barabara mpya kwa Jiji la Dar es Salaam zinajengwa kwa njia 4?

Cha kusikitisha hata njia muhimu sana ya kuelekea International Airport, reception ya Taifa inajengwa njia 4, tena finyu likitangulua roli huwezi kuliovertake!!! Hakuna vituo vya daladala, inasikitisha sana, viongozi wetu wana matatizo makubwa sana.ukiangalia njia kuelea Airport nafasi kubwa bado ipo pembeni!!! yakutosha kabisa,

Sitashangaa baadaye itabomolewa tena kuitanua.
 
Wanafanya hivyo mikaka michache ijayo wapige tena.

Kwani world bank si watu kama watu wengine? Unafikiri hakuna wapigaji mule?
Nakubaliana na wewe kabisa dada yangu.

Kutakuwa na upigaji mkubwa sana kuanzia kwa hao wataalam wa World Bank hadi kwa watu wetu. Ndo mana pale jangwani palipojengwa kituo cha Mwendokasi miaka michache tu iliyopita leo kimetolewa alafu linatengwa daraja

Maana kusema kweli haiingii akilini kabisa.
 
Cha kusikitisha hata njia muhimu sana ya kuelekea International Airport, reception ya Taifa inajengwa njia 4, tena finyu likitangulua roli huwezi kuliovertake!!! Hakuna vituo vya daladala, inasikitisha sana, viongozi wetu wana matatizo makubwa sana.ukiangalia njia kuelea Airport nafasi kubwa bado ipo pembeni!!! yakutosha kabisa,

Sitashangaa baadaye itabomolewa tena kuitanua.
Nimepita juzi ndo hadi nimetaka kutoa machozi. Kwa namna ile njia ilivyo na nafasi pembeni alafu unaona watu wanajenga njia 4 unakubali kabisa acha wazungu watuite manyani
 
Kipimo cha uwezo wa mwanadamu kama anafikiri sawasawa ni namna anavyofanya mambo yake kulingana na wakati husika.

Dar es Salaam ndo Jiji Kuu la Biashara la Tanzania. Sio hivyo tu, ndo Jiji lenye watu wengi zaidi Tanzania na kadri siku zinavyozidi kwenda idadi ya watu inazidi kuongezeka.

Kwa binadamu ansyefikiri sawasawa, sikutegemea kama katika karne hii ya 21 tena mwaka 2023 kwenye Jiji hili barabara kuu zingeendelea kujengwa kwa njia 4.

Nipo Dar es Salaam na nimesikitishwa sana maana imejengwa barabara mpya kabisa kutoka mbagala hadi posta ila bado imejengwa kwa njia 4( mbili kwenda na mbili kurudi na katikati mwendokasi). Nimetembea pia njia ya kutoka Posta hadi Uwanja wa ndege nimeona ujenzi unaendelea na hali ni hiyo hiyo.

Swali langu kwenu Viongozi wa Tanzania. Je uwezo wenu wa kufikiri ndo umeishia hapo?

Kwa namna Jiji hili lilivyo na linavyotakiwa kuwa yaaani kama Jiji bora na la mfano Afrika Mashariki na Kati, nilitegemea barabara hizi kujengwa kwa Njia 6 hadi 8 pamoja na mwendokasi.

Kiufupi barabara zote kubwa za Dar zinazoingia Posta kuelekea Kibaha, Pugu, Mbagala, Bunju na inayotoka Morroco hadi Keko bila kusahau ya Mwenge- Ubungo hadi Bandarini zinatakiwa kuwa za njia 3 mpaka 4 kila upande na njia ya mwendokasi/ treni ya umeme katikati.

Ifike wakati nchi hii watu tufikiri kama tunaishi katika dunia wanayoishi wenzetu warabu na nchi za ulaya. Inasikitisha sana kuwa na mipango ya mwaka 1950/ 60 katika karne hii ya 21.

Naomba Viongozi wa Tanzania mbadilike kwa kweli.
Labda afufuke magufuli ndiyo zijengwe hizo 6 to 8
 
Hakuna na bajeti ni uvivu wa kufikiri. Miradi hii inajengwa kwa fedha za mikopo sasa kwa nini tusikope fedha za kutosha na tukafanya jambo kwa kumaliza kabisa? Unaweza kuta baada ya miaka 4-5 unasikia wanaongeza ukubwa tena wa barabara ile ile waliyojenga.
Kuondoa msongamano au foleni ya magari ni kitu kinachohitaji combination ya vitu vingi. Unaweza kuweka hata barabara nane au kumi na ukazidisha tatizo badala ya kuongeza. Kujenga barabara nne kukiambatana na hatua nyingine kunaweza kuleta ufanisi zaidi badala ya kung'ang'ania tu kwenye barabara.
 
Kuondoa msongamano au foleni ya magari ni kitu kinachohitaji combination ya vitu vingi. Unaweza kuweka hata barabara nane au kumi na ukazidisha tatizo badala ya kuongeza. Kujenga barabara nne kukiambatana na hatua nyingine kunaweza kuleta ufanisi zaidi badala ya kung'ang'ania tu kwenye barabara.
Upo sahihi kabisa. Ila suala la kujenga barabara kuu pana haliepukiki katika dhana ya kuondoa foleni kwenye miji mikubwa pamoja na kurahisisha shughuli za maendeleo
 
"imejengwa barabara mpya kabisa kutoka mbagala hadi posta ila bado imejengwa kwa njia 4( mbili kwenda na mbili kurudi na katikati mwendokasi)."

2 kwenda+2 kurudi+mwendo kasi =6.

Kwanini upate 4? Kwani mwendo kasi siyo barabara?

Bado kuna treni ya Mwakyembe

Hata Kivukoni-Kibaha ni njia 6 hadi 8.

Mbagala Posta ni njia 6.

Njia ya kwenda Pugu ni 6.
 
"imejengwa barabara mpya kabisa kutoka mbagala hadi posta ila bado imejengwa kwa njia 4( mbili kwenda na mbili kurudi na katikati mwendokasi)."

2 kwenda+2 kurudi+mwendo kasi =6.

Kwanini upate 4? Kwani mwendo kasi siyo barabara?

Bado kuna treni ya Mwakyembe

Hata Kivukoni-Kibaha ni njia 6 hadi 8.

Mbagala Posta ni njia 6.

Njia ya kwenda Pugu ni 6.
Rudi shule
 
Kipimo cha uwezo wa mwanadamu kama anafikiri sawasawa ni namna anavyofanya mambo yake kulingana na wakati husika.

Dar es Salaam ndo Jiji Kuu la Biashara la Tanzania. Sio hivyo tu, ndo Jiji lenye watu wengi zaidi Tanzania na kadri siku zinavyozidi kwenda idadi ya watu inazidi kuongezeka.

Kwa binadamu ansyefikiri sawasawa, sikutegemea kama katika karne hii ya 21 tena mwaka 2023 kwenye Jiji hili barabara kuu zingeendelea kujengwa kwa njia 4.

Nipo Dar es Salaam na nimesikitishwa sana maana imejengwa barabara mpya kabisa kutoka mbagala hadi posta ila bado imejengwa kwa njia 4( mbili kwenda na mbili kurudi na katikati mwendokasi). Nimetembea pia njia ya kutoka Posta hadi Uwanja wa ndege nimeona ujenzi unaendelea na hali ni hiyo hiyo.

Swali langu kwenu Viongozi wa Tanzania. Je uwezo wenu wa kufikiri ndo umeishia hapo?

Kwa namna Jiji hili lilivyo na linavyotakiwa kuwa yaaani kama Jiji bora na la mfano Afrika Mashariki na Kati, nilitegemea barabara hizi kujengwa kwa Njia 6 hadi 8 pamoja na mwendokasi.

Kiufupi barabara zote kubwa za Dar zinazoingia Posta kuelekea Kibaha, Pugu, Mbagala, Bunju na inayotoka Morroco hadi Keko bila kusahau ya Mwenge- Ubungo hadi Bandarini zinatakiwa kuwa za njia 3 mpaka 4 kila upande na njia ya mwendokasi/ treni ya umeme katikati.

Ifike wakati nchi hii watu tufikiri kama tunaishi katika dunia wanayoishi wenzetu warabu na nchi za ulaya. Inasikitisha sana kuwa na mipango ya mwaka 1950/ 60 katika karne hii ya 21.

Naomba Viongozi wa Tanzania mbadilike kwa kweli.
Ndio shida ya kuwapa uongozi wa nchi makada na wapiga debe wa chama.
 
Haya uliyoyasema ndo yanaunga mkono hoja yangu kuwa jiji hili ni vizuri kuwa na miondombinu sahihi mfano hizo barabara za njia 6 hadi 8.

Kwa kurahisisha shughuli kwenda vizuri na uchumi kwenda sawia hakuna budi kujenga barabara kubwa zaidi kwa njia kuu ili kurahisisha shughuli za uchumi ambapo mapato yataongezeka zaidi na kwenda kuhudumia sehemu nyinginezo.

sasa kwa dargiza uwe na barabara 8 za kwenda wapi na ktkea wapi? dargiza asubuhi watu wote wanaenda posta/kariakoo jioni wanarudi sasa ulitaka barabara 10 kuingia posta?
 
Nakubaliana na wewe kabisa dada yangu.

Kutakuwa na upigaji mkubwa sana kuanzia kwa hao wataalam wa World Bank hadi kwa watu wetu. Ndo mana pale jangwani palipojengwa kituo cha Mwendokasi miaka michache tu iliyopita leo kimetolewa alafu linatengwa daraja

Maana kusema kweli haiingii akilini kabisa.
Huko world bank ndiyo kuna upigaji mkubwa kuliko kokote.
 
sasa kwa dargiza uwe na barabara 8 za kwenda wapi na ktkea wapi? dargiza asubuhi watu wote wanaenda posta/kariakoo jioni wanarudi sasa ulitaka barabara 10 kuingia posta?
Tafuta exposure ndugu
 
Ndio shida ya kuwapa uongozi wa nchi makada na wapiga debe wa chama.
Kusema kweli wanaturudisha nyuma sana. Wanafanya watu weusi tudharauliwe sana kwa kuwa tunaonekana kama thinking capacity zetu zina mushkeli
 
Tafuta exposure ndugu

haujajibu swali langu, barabara za njia 10 dargiza kwenda wapi na kutokea wapi? hiyo miji mingine ya nje wameplan vizuri na miji ina centers nyingi sasa dar kila mtu asubuhi ankwenda posta jioni anarudi, ofisi zote ziko posta hizo njia nane zitapitia wapi na kutoka na kuelekea wapi? nenda hata nairobi tu hapo utaona mji una center mbalimbali angalau, sasa dargiza wote wanafurika posta watapaki wapi hayo magari?
 
haujajibu swali langu, barabara za njia 10 dargiza kwenda wapi na kutokea wapi? hiyo miji mingine ya nje wameplan vizuri na miji ina centers nyingi sasa dar kila mtu asubuhi ankwenda posta jioni anarudi, ofisi zote ziko posta hizo njia nane zitapitia wapi na kutoka na kuelekea wapi? nenda hata nairobi tu hapo utaona mji una center mbalimbali angalau, sasa dargiza wote wanafurika posta watapaki wapi hayo magari?
Barabara ya kwenda bandarini kutokea Ubungo kupita Buguruni na Tazara haina foleni?

Kwenda Kimara from Ubungo hakuna foleni?

Kwenda ubungo from Mwenge hakuna foleni?

Hizo nazo zinaenda Posta?

Unaishi Dar kweli au unahadithiwa kuhusu Dar?
 
Njia nane Kwa eneo lipi bongo mkuu,Hilo la nne lenyewe wamepata Kwa jasho,watu kuvunjiwa makazi na kipigo juu.Dar imejaa,dar inafukuta imefurika watu wengi wasio na ajira na wengi ni wale watuma Kwa namba hii,Nashauri Dar ipunguzwe wengine wapelekwe kulima bush
 
Njia nane Kwa eneo lipi bongo mkuu,Hilo la nne lenyewe wamepata Kwa jasho,watu kuvunjiwa makazi na kipigo juu.Dar imejaa,dar inafukuta imefurika watu wengi wasio na ajira na wengi ni wale watuma Kwa namba hii,Nashauri Dar ipunguzwe wengine wapelekwe kulima bush
Kama njia ya Shekilango- Bamaga imewezekana kutoa njia 4 unashindwaje kuweka njia 6-8 barabara ya mbagala- Posta? Au Bunju- Posta? au Mwenge - Ubungo- Kurasini? au Posta- Pugu?
 
Back
Top Bottom