Kwanini Canaan alilaaniwa na sio Ham?!

Kwanini Canaan alilaaniwa na sio Ham?!

watakwambia mungu ..hapangiwi...yaani trilion 1.5 aibe jiwe halafu hukumu apew jesca like serious "" Mungu huyu Mungu gani aliyejaa visasi kama mzee wa chatle ..na bado watu wana mnyenyekea tu ..lakini mzee wa chatle alipoleta visasi vyake watu wamepga makelele mpaka basi
Ahahaaha magu akiweka visasi sio sawa lakn Mungu akiweka visasi sawa binadamu kweli wanakatabia kakuvutia upande wao
 
Kuna kitu sijaelewa bado:

Tendo la kuuchungulia uchi wa baba lilitokea kipindi gani?

Nuhu alikishuhudia lini kitendo hicho cha kuchunguliwa uchi wake?

Caanan alizaliwa lini?

Caanan alilaaniwa lini?

Caanan alikufa kipindi kipi?
 
Angalia katika koo ama soma bandiko la laana za kifamilia... Unakuta waliofanya kosa ni wengine kabisa lakini taabu wanaipata mpaka kizazi cha tatu... Connection ya damu
Wakati Caanan akilaaniwa..Baba yake alikua hai bado?..

Kama alikua hai, Kwanini Laana isianze kwake na iendelee kwa kizazi chake?..
 
Mada ni nzuri sana na yenye kufikirisha

Maswali ya kujiuliza ni mengi lakini kubwa ni kwanini kosa afanye Ham na laana apewe Caanan?

Kitu ninachojua hapo kale kulikua na kanuni kwamba kile konachosemwa huwa. Mf Isaca alipombariki Yakobo hali yakua akijua ni Esau wakati sio yeye ile baraka ilimfikia moja kwaoja Yakobo na Esau hakupata jema japo alidhulumiwa .

Kwa hio kufanya kosa ama kutokufanya hakuwezi kuzuia yaliotamkwa juu yao. Nadhan ndivyo yaliomkuta Caanan.

Lakin pia tunana huyo Caanan alikuja kua taifa ambalo Mungu alijipatia Utukufu kwa Israel kuwashinda katika vita. Chukulia pia Misri na kiongozi wake Mungu alivyowaadhibu kwa kosa alilofanya kiongozi wao ambalo Mungu mwenyewe alisema ataufanya moyo wa Farao kua mgumu ili ajipatie utukufu. Unaweza kuunganisha na yalimkuta Caanan labda aliandaliwa ajekua sababu ya mapigano yenye kumpa Mungu Utukufu. Kumbuka pia Mungu huitwa pia Mungu wa majeshi hovyo huandaa vita ili aje ashinde.

Huo ni mtazamo wangu ndani ya Biblia, lakini tukirudi kwenye zile nadharia uwezekano unakua mdogo Ham kulala na mama yake maana kibinadamu huwa ni ngumu mwana kumlala *****. Lakini pia inaweza kua hivyo iwapo mhanga ataingiliwa na roho ya kishetani.
Kama ilivyo kua kwa Nimrod.
Hii ya kula na ***** nakataa ila mara nyingine inaweza kua.


Niseme tuu kwa kweli hii familia ya Nuhu ina mengi ya kujiuliza maana nje ya hii familia uovu wote ulishaondolewa na gharika, lakini tunaona simbali na tukio hilo uovu umerudi tena. Labda tuseme hivi vitabu viwili tulivyo navyo vinavyotufunza juu ya iman tulio nayo visitufunge kifanya marejeo ya vitabu vingine tuone vinasemaje juu ya Mungu.
 
Mada nzuri sana ila kwenye suala la laana kuna mkanganyiko mkubwa nafikir ilikuwa na laana ya pili baada ya ile ya kwanza kula tunda ata huyu Nuhu alikuwa na laaana sasa anawezaje kutoa laana mwenye laana?
Inawezekana kabisa mtu/ mtoto kuchukua laana ya baba au babu zake.

Hilo liko wazi. Mungu anasema katika Amri zake

"Nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukizao" kibiblia kizazi cha 3 na cha 4 ni miaka mia 3 kwa miaka mia 4.

Mifano:-

Daudi pamoja na kuwa alikuwa karibu sana na Mungu na alikuwa Mteule pia, alirithi roho ya uzinzi iliyoanza kumpata bibi yake na kisha mama yake....naye alikuja kuzini na mke wa Uria

Vilivile Ibrahim (Baba wa Imani) aliwahi kusema "UONGO" kule Misri kuwa mkewe ni dada yake ili asije kuuwawa na kisha mkewe kuolewa na mtu mwingine. Wakati huo yeye hauona kuwa ni dhambi na wala Mungu hakumhukumu straight away...

Lakini tunakuja kuona kuwa mtoto wake yaani Isaka naye alikuja kupata shida kwaajili ya uongo wakati wa kumbariki Yakobo badala ya Esau

Baadae tunaona pia Yusuphu alipata shida kutokana na uongo wa ndugu zake kusema kuwa amekufa kumbe haikuwa hivyo.

Samahani kwa kwenda nje ya mada ila nilitaka kujustify jinsi laana inayosababishwa na dhambi inavyoweza kuspread kizazi hata kizazi.
NB:Mods naomba msihamishe mada hii kwenda jukwaa la dini sababu licha ya kuwa nimequote baadhi ya mistari ya vitabu vya dini ila uzi huu ni mtiririko wa mada zilezile nilizoanza humu JF intelligence kuhusu wanefili na wanadamu wa kale so mkihamisha mtaharibu mtiririko wa mijadala yangu kwa wanaofuatilia.... Ntashkuru kwa ushirikiano wenu

Cc JamiiForums Innovator Invisible Reserved
 
Mkuu lawama na laani ni vitu tofauti sana. Waziri hawezi kuua mtu huko Iringa then Magufuli ndo akamatwe Mmmh!! hapana.

Haya maandiko ya Bible me yananivuruga sana Ukisoma Mwanzo 3:17 Mungu anailaani ardhi sababu ya Adamu sasa ardhi ilifanya kosa gani pale Eden?

Yoshua 7:24+ Akani alifanya dhambi ya kuiba aliteketezwa yeye na uko wake mzima hadi ng'ombe, punda, na vitu vyake vyote. sasa wao viumbe wengine walikosa nini wahusike kwenye adhabu ya Akani?

Sikumbuki ni kitabu gani but utanisaidia kama unakijua. kuna mtumishi mmoja wa Elisha Nabii alifanya kosa kumuomba zawani Naamani alieponywa ukoma na Elisha nabii. Huyo mtumishi alipatwa na ukoma yeye na ukoo mzima. sasa wao ndugu zake wengine walifanya kosa gani mpk wahusishwe kwenye adhabu ya huyo mtumishi?

Najiuliza Mungu yukoje? na anatumia kanuni, sheria, utaratibu gani kuadhibu watu vitu ambavyo hata havijahusika kuadhibiwa pasipo kosa?
Ana mapepo pia, kama anaadhbibu kwa jazba.[emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
kama tukiendelea na mada za aina hii bhas yule malaika ambae mkuu anatamani ashuke azime mitandao ya kijamii nina uhakika hatoshuka kwa kuwa hata yeye nahisi anapenda mada hizi!
 
Ahahaaha magu akiweka visasi sio sawa lakn Mungu akiweka visasi sawa binadamu kweli wanakatabia kakuvutia upande wao
umeona "" mkuu ""!?? halafu Mungu huyo huyo ametutaka tuwe tuna samehe 7×70 ""wakati yeye hilo limemshinda"". ..hatari sana hii"" hivi vitabu kwakweli vitazamwe upya...""
 
Hamna laana yeyote kwanini ioo laana Mungu akuigeuza apewe mlevi
haha hahaa hapo sasa ""? Maana katika ulimwengu wa sasa ulevi ni sifa mbaya "" lakini maandiko yanatuambia mlevi ametoa laana kwa mtu ambaye hajalewa na laana hiyo Mungu akaipokea ...hahaaa ....""" INA maana huyo Mungu atakuwa nimjinga kiasi gani "" ?? kiasi kwamba ashindwe kutambuwa kuwa tatizo lipo kwa mlevi " maana kama asingelewa " asinge kaa uchi " na wala HAM asingepata nafasi ya kumchungulia au "" kulala na mama yake kama baadhi ya wachangiaji wasemavyo """,....yaani kweli mtume wa Mungu alishindwa kutambua madhara ya pombe ni yapi " pindi atapo inywa ""!? mtume wa Mungu hana hata elimu/hekima ya kutambua athari za unywaji pombe ""? " ikiwa hata mtoto mdogo leo hii anajua madhara ya unywaji pombe ni yapi "" huyu mtume aliyeshindwa kujua madhara ya unywaji pombe "" ana sababu zipi za kuitwa mtume """?
 
Tukisema: 'mtoto wake Ham' tutamaanisha, mtoto anaye zaliwa na Ham, ambaye ni Canaan. Au mtoto wa Nuhu aitwaye Ham. Tukiendelea, kusema ndugu zake Ham, tutamaanisha watoto wengine wa Nuhu wenye vinasaba na Ham. Kwa mantiki hiyo aliyetenda kosa ni mtoto wa Ham, ambaye ni Canaan na wala siyo Ham, mtoto wa Nuhu. Katika muktadha huo, mwandishi alitaka kujenga uzito wa tukio kwa kusema 'mtoto wake Ham' baada ya kutaja moja kwa moja 'mjukuu wake Nuhu, ambaye ni Canaan, mtoto wa Ham.
 
Inawezekana kabisa mtu/ mtoto kuchukua laana ya baba au babu zake.

Hilo liko wazi. Mungu anasema katika Amri zake

"Nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukizao" kibiblia kizazi cha 3 na cha 4 ni miaka mia 3 kwa miaka mia 4.

Mifano:-

Daudi pamoja na kuwa alikuwa karibu sana na Mungu na alikuwa Mteule pia, alirithi roho ya uzinzi iliyoanza kumpata bibi yake na kisha mama yake....naye alikuja kuzini na mke wa Uria

Vilivile Ibrahim (Baba wa Imani) aliwahi kusema "UONGO" kule Misri kuwa mkewe ni dada yake ili asije kuuwawa na kisha mkewe kuolewa na mtu mwingine. Wakati huo yeye hauona kuwa ni dhambi na wala Mungu hakumhukumu straight away...

Lakini tunakuja kuona kuwa mtoto wake yaani Isaka naye alikuja kupata shida kwaajili ya uongo wakati wa kumbariki Yakobo badala ya Esau

Baadae tunaona pia Yusuphu alipata shida kutokana na uongo wa ndugu zake kusema kuwa amekufa kumbe haikuwa hivyo.

Samahani kwa kwenda nje ya mada ila nilitaka kujustify jinsi laana inayosababishwa na dhambi inavyoweza kuspread kizazi hata kizazi.
Okay nimekuelewa ila unaweza kutusaidia KWANNI MUNGU hufanya hivyo Yaani kutoa adhabu kwa vizazi sio mtu?? Embu tusaidie hapo na swali jingine kwanini ile laana isiende kwa watoto wengine wa Ham kma cush na put ila ielekezwe kwa canaan kma canaan na tunaona mbeleni anakuja kufutwa kizazi chake na wana wa yakobo..... Je kwanini canaan na sio watoto wengine

Cc mitale na midimu
 
Wakati Caanan akilaaniwa..Baba yake alikua hai bado?..

Kama alikua hai, Kwanini Laana isianze kwake na iendelee kwa kizazi chake?..
Hapa pia sielewi sababu wakati wa laan Ham na canaan wote walikuwepo ila laana ilienda kwa CANAAN peke yake ila watoto wengine wote wa HAM hawakuguswa na laana hiyo ndio maana najiuliza kama ni laana ya vizazi kwanini isianzie kwa baba ila inaanza kwa mtoto mmoja tu na sio watoto wengine wote wa baba huyo aliyefanya dhambi
 
Hapa pia sielewi sababu wakati wa laan Ham na canaan wote walikuwepo ila laana ilienda kwa CANAAN peke yake ila watoto wengine wote wa HAM hawakuguswa na laana hiyo ndio maana najiuliza kama ni laana ya vizazi kwanini isianzie kwa baba ila inaanza kwa mtoto mmoja tu na sio watoto wengine wote wa baba huyo aliyefanya dhambi
Pia.

Kama Nuhu alimpenda sana Ham mpaka kufikia kushindwa kumlaani kwa mahaba yake kwake..Akaamua kumlaani mjukuu..

Iweje.
Mungu aikubali kuipitisha hiyo laana iliyobebwa na Mahaba/Chuki ya kibinadamu?
 
Angalia katika koo ama soma bandiko la laana za kifamilia... Unakuta waliofanya kosa ni wengine kabisa lakini taabu wanaipata mpaka kizazi cha tatu... Connection ya damu
Kwahiyo mkuu inawezekana watu wakaenda motoni kwa kosa la mababu zao?
 
Mkuu ambacho nataka kieleweke ni kwamba Nuhu kweli alilewa pamoja na mkewe alafu Ham kuona mama yake yupo kihasara akamuingilia hivyo hapo ndipo ALIFUNUA UCHI WA BABA YAKE hivyo wakifunika UCHI itakuwa kinyume chake labda walienda kumzuia HAM kuendelea kufanya kitendo hicho kwa Mama yao so kwakuzuia WAMEFUNIKA UCHI WA BABA YAO ndio maana wakabarikiwa

Najaribu kufikiri tu ngoja wataalam watakuja nisahihisha
It make sense
 
Back
Top Bottom