Kwanini CCM wamechukizwa na kitendo cha Lissu na Samia kukutana?

Kwanini CCM wamechukizwa na kitendo cha Lissu na Samia kukutana?

Labda hawakubaliani na hoja zilizoshiba za Mh. Tundu Lissu kwa mama. Watake wastake, kafiba mpya ni lazima, tume huru ya uchaguzi ni lazima na 2025 tunakwenda na Mh. Tundu Lissu.

You know, chochote kinachotishia maslahi ya chawa ni sumu. Hata hivyo, kwasababu Chief Hangaya ni mnafiki numero uno, chawa wake hawana kihivyo sababu ya kuchukia. Amini usiamini, ukiondoa issue ya Tume ya Uchaguzi, hakuna issue nyingine itakayofanyiwa kazi kati ya sasa na 2025!
 
Haya majinga huwa yanajionaga kama nchi hii niyakwao yenyewe.Ndo maana yanafikiria kuonea nakufanya siasa za chuki na kisasi.Kwa akili zao yanafikiri raisi ni wakwao tu.sasa inapotokea kiongozi wao kafanya tofauti roho zao za kutu zinawauma.ila ni ujinga tu unaowasumbua.Hayana jipya.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Kwa yeyote yule ambae amekasirika na kitendo cha Samia ni bora kwanza angelijiuliza ni kwa sababu gani Rais amekwenda huko ubelgiji? Kwani rais alfika ubelgiji kufanya shoping, matibabu au mapumziko? Jawabu ni rahisi sana, amekwenda kikazi na kila mmoja anajua lengo kuu ni kutafuta/kuomba mikopo ya miradi mbali mbali ambayo daima huwa chini ya mwamvuli wa "kudumisha mahusiano ya nchi mbili hizi". Sasa kwenda kuomba misaada katika nchi ambayo inaamini kabisa kuwa Tanzania haihishimu uhuru wa vyama vingi, nchi ambayo imefanya kila hali kuhakikisha wanamtoa nchini kiongozi wa upinzani kwa sababu wanaamini kuwa serikali haitamtendea haki, unadhani jambo la kwanza watakalo lijadili kabla ya kukubali kutoa aina yeyote ile ya misaada na mikopo? Jawabu ni kuwa "uhuru wa vyama vya upinzani", bila ya shaka serikali ilisisitiza kuwa inaheshimu hilo, na wakaambiwa "prove it" kwa kukutana na kiongozi wa upinzani. Na kama wanavyosema watu "almuhitaji khanith" Samia mkono wake ulipindwa aidha alikuwa arudi patupu au aonane na Lisu na apewe misaada.

Serikali ya Tanzania itajaribu kuipaka hii issue rangi watakazo, waseme lissu ndie aliomba kukutana na Samia na mengineyo, lakini la ukweli ni kuwa Samia kukutana na Lissu ni masharti alopewa na serikali ya ubelgiji kabla ya kukubaliana kurudisha uhusiano mzuri baina ya nchi mbili hizi.
 
Wote wameumia sana,Mh Rais Samia anatakiwa kutambua kuwa maadui wake wapo ndani ya chama chake.
Rais anatambua sana kuhusu maadui wako wapi, alishasema hivi majuzi tu kwamba mtu mzima mmoja mwenye busara zakae alipomtembelea kumpongeza alipochukua kiti cha uongozi wa nchi, alimuambia kuwa watakaokukwamisha ni wavaa kijani wenzako.
Kwa hiyo yupo vizuri kuwaepuka kumpotosha na kumkwamisha kayika uongozi wake.
 
Back
Top Bottom