Kwanini dhehebu la SDA huwa wanalishambiulia zaidi Kanisa Katoliki na siyo madhehebu mengine?

Kwanini dhehebu la SDA huwa wanalishambiulia zaidi Kanisa Katoliki na siyo madhehebu mengine?

Utakapojua siku ya Saba ya juma ipi hautabishana sana.maandiko yanasema ht baada ya uumbaji Mungu alipumzika yaani siku ya Saba (JUMAMOSI),hata siku ya kwanza ya juma (JUMAPILI) Yesu alifufuka yaani JUMAPILI.
Siku ya saba alipumzika. Je Siku ya nane akaendelea na kazi gani?
 
HISTORIA YA KANISA IV: MARTIN LUTHER NA VISABABISHI VYA MATENGENEZO YA KANISA - 1.
Sababu zilizopelekea Matengenezo ya Kanisa (the Reformation) zilikuwa ni nyingi na zilianza hata kabla Martin Luther hajazaliwa. Nitakuwa nikieleza moja baada ya nyingine. Leo nitagusia mgogoro wa kiuongozi uliodumu kwa miaka 39.
Mgogoro huo wa uongozi ulilipasua Kanisa hadi kuwa na Mapapa 3 kwa wakati mmoja. Papa Urban VI alichaguliwa mwaka 1378 kuwa Askofu Mkuu wa Roma na hivyo kuwa Papa. Miezi michache baada ya kuchaguliwa kwake aliwaweka kando Nyumba ya Makadinali (College of Cardinals). Baada ya kuona kuwa wamepuuzwa na kuwekwa kando, Makadinali wa Ufaransa na wengine waliondoka Roma na wakatangaza kuwa uchaguzi wa Papa Urban VI ulikuwa batili (kwa maneno mengine walibatilisha uchaguzi)!Baada ya hapo Makadinali wale walimchagua Kadinali Robert wa Geneva kuwa papa na kujulikana kama Papa Clement VII. Papa Urban IV aligoma kuondoka Roma (ofisini) hivyo Papa Clement VII pamoja na Makadinali wake walihamia Avignon, Ufaransa na hivyo Kanisa la Roman Katoliki lilikuwa na Mapapa wawili kwa wakati mmoja kila mmoja akijiona kuwa ndiye Papa kwa kuwa kila mmoja alikuwa na idadi ya Makadinali waliokuwa wakimuunga mkono.
Mtaguso Mkuu wa Pisa uliofanyika mwaka 1409 uliazimia kumaliza tatizo kwa kuwafukuza Mapapa wote wawili na badala yake akachaguliwa Papa Alexander V. Mapapa wale wawili kila mmoja alikataa kujiuzulu na hivyo kukawa na Mapapa watatu!
Mtaguso Mkuu wa Constance uliitishwa mwaka 1414-1418 ulihudhuriwa na Makadinali, Maaskofu Wakuu, Maaskofu, Wakuu wa Vyuo nk. Mfalme wa Dola ya Kirumi alimshawishi Papa mmojawapo ili aitishe Mtaguso Mkuu. Yule Papa alifanya hivyo akijua kuwa yeye angepona. Matokeo yake alichaguliwa Papa mwingine kabisa baada ya wote watatu kutolewa. Papa mpya aliitwa Martin V. Mara tu baada ya kuchaguliwa Papa Martin V alijitangaza kuwa juu ya Mtaguso Mkuu wa Kanisa! Katika kipindi chote hicho, Mapapa walikuwa katika magomvi ya madaraka hivyo mambo ya kiroho yaliachwa kando na kulikuwa na mmomonyoko mkubwa wa maadili miongoni mwa Mapadre na watawa hasa ikizingatiwa kuwa Mapapa wenyewe walikuwa wamekosa uadilifu. Katika kipindi hiki ndipo Padre Profesa John Huss alianza kuhubiri uamsho (matengenezo). Cha kusikitisha ni kwamba Mtaguso wa Constance ndio uliomhukumu kifo. Wafuasi wake waliendelea na uamsho (matengenezo) na hatimaye walianzisha Kanisa la Moravian.
Martin Luther alikuja miaka 100 baadaye.

Mwanakondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula - Mkuu wa Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania.
Kumbe Moravian ina umri mkubwa kuizidi Lutheran!
 
Mwisho hizo amri zote waisrael walipewa kutokana na agano ambalo Mungu alilifanya pamoja nao. Sasa soma Yeremia 31:31,32.... Inaonyesha Mungu anaanzisha agano jipya. Je unadhani hilo la zaman linalohalalisha hizo amri ambazo mnajitutumua kuzifuata bad liko hai? Je hilo agano jipya unalijua ni lipi? Na msingi wa agano jipya ni nani? Then malizia Soma wagalatia 4:8-11 na wakolosai 2:16,17

Nimeamua nikupe hili andiko moja tu ili tumalize mjadala mana nyie ni wabishi sana
Na jipya likishaanza kazi, kuukuu hukaa pembezoni.

Wakristo wanaishi katika Agano Jipya, Agano lililo bora zaidi ambalo Mdhamini wake ni Yesu Kristo.
 
Nikuambie kitu kimoja Tu ambacho ni muhimu.
Madhehebu hufasiri biblia wanavyotaka wao, biblia imekataza na unatakiwa ufahamu kwamba Neno la Mungu ni Neno la kinabii.

Sasa biblia imepiga marufuku kufasiri kama mtu anavyotaka
2 Petro 1:20-21
Mkijua neno hili kwanza, ya kwamba hakuna unabii katika maandiko upatao kufasiriwa kama apendavyo mtu fulani tu.
Maana unabii haukuletwa po pote kwa mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na Roho Mtakatifu.

Hivyo Neno la Mungu harifasiliwi kama mtu anavyota Bali Tu lazima uongozwe na Roho mtakatifu. Na Roho mtakatifu hamuongozi mtu ambaye hafuati neno lake,

Mfano Leo hii huwezi kuniambia hasa hawa wachungaji wa kimadhehebu wana Roho mtakatifu wakati huo wameruhusu haki Sawa kanisani
Twende kwa andiko maana daima nitatetea Neno la Mungu naomba Mungu anisaidie kwa hilo.

1 Wakorintho 14:34
Wanawake na wanyamaze katika kanisa, maana hawana ruhusa kunena bali watii, kama vile inenavyo torati nayo.

Haina haja ya kufasiri ni kwamba mwanamke ni marufuku kuhubiri kanisani.
Sasa je unaweza kuniambia huyu anaongozwa na Roho mtakatifu wakati ameshindwa kulifuata neno la Roho mtakatifu?

NAludia tena ndugu nakupenda mno kutoka moyoni, usijiunge na kanisa toka kwenye hiyo mifumo uludi kwenye Neno, ulitetee Neno,uliishi Neno ili uwe salama ndugu yangu[emoji120] na lazima upate ubatizo Harisi hiyo ni kweli.

ukiacha ama kuongeza neno kwenye biblia. Maana yake huifuati bible
Naona umekazana kutoa hoja hiyo ya kukataza wanawake kuhubiri kanisani.Sasa hebu soma hii kisha uniambie hapa wanaambiwa wakristo gani."Bali kila mwanamke asalipp,au ANAPOHUTUBU bila kufunika kichwa,yuaaibisha kichwa chale;kwa maana ni sawa na yule aliyenyolewa.(1 wkorintho 11:5)".
*Sasa hapo ni yule yule Paulo akiwaambia makanisa.Hebu nipe elimu kidogo hapo.
 
Kuna sehem nimesema Yesu alitunga sheria? Acha kukurupuka. Yesu alikazia hilo kuwa msingi wa sheria zote. Amri saba za torati zinaingia hapo tumia akili kufikri sitak kuandika sana. Pili hujajib swali lang... Sabato manyoshika ni ile ya Mungu kumaliza kazi, ile ya waisrael kufanya kazi siku sita na kupumzika au zinginezo? Mind you sabato zilikua nyingi tu. Mwisho ujibu kwann mnangangania tu hii ya kufanya kaz siku sita na saba kutofanya?
Kabla Musa hajapanda mlimani Sinai kuandikiwa amri na MUNGU,sabato ilikuwa inatunzwa.Ukisoma (kutoka 16:1,),utaona walifika katika bara ya Sinai tarehe 15 ya mwezi wa 2 tangu watoke misri.Na aya ya 23 wanaambiwa waendelee na taratibu ya kuitunza sabato.Ukisoma (Kutoka 19:1-3) utaona waisrael walifika katika mlima Sinai mnamo mwezi wa tatu baada ya kutoka misri,Ndipo Musa akapanda mlima Sinai kuandikiwa amri na MUNGU.Hii ni kuonesha amri za MUNGU ikiwemo amri ya nne ya kutunza sabato zilikuwa zikitunzwa hata kabla ya waisraeli kuwepo duniani.Kipindi hiko haizikuwa zimeandikwa,ila walizisikia zikitamkwa na MUNGU.SOMA MWANZO 26:5 inasema:"Kwa sababu Ibrahim alisikia sauti yangu akayahifadhi maagizo yangu,na AMRI ZANGU,NA HUKUMU ZANGU NA SHERIA ZANGU."Kwo hakuna sabato ya wayahudi bwa shee.Nikikuambia utoe aya inayosema sabato ni ya wayahudi hutatoa hadi Yesu anarudi.Sabato ni ya BWANA MUNGU(Kutoka 20:10).Ile ile ya uumbaji.
 
Nashukuru Kwa kuungana na Mimi kuwa Yesu hakuwahi kuwa na sheria wala hakuleta SHERIA.

Unaweza nitajia hao watunzi hata mmoja ambaye anaziita hizo sheria za Kristo?
Kisha unitajie na hizo sheria ambazo zinaitwa za Kristo.
Utashitakiwa Mtibeli.Unatoaje nondo namna hii?Sasa swali kama hili kwa nini umwambie atoe kwenye Biblia?Ungemwambia atoe kwenye vitabu vya historia ya watakatifu wa kikatoliki bwa shee
 
Naona umekazana kutoa hoja hiyo ya kukataza wanawake kuhubiri kanisani.Sasa hebu soma hii kisha uniambie hapa wanaambiwa wakristo gani."Bali kila mwanamke asalipp,au ANAPOHUTUBU bila kufunika kichwa,yuaaibisha kichwa chale;kwa maana ni sawa na yule aliyenyolewa.(1 wkorintho 11:5)".
*Sasa hapo ni yule yule Paulo akiwaambia makanisa.Hebu nipe elimu kidogo hapo.
Mkuu biblia haijawahi kujipinga kwenye hicho kifungu twende sawa sasa. Hapo fasiri ya Kiswahili imekosea kidogo hutaweza kunielewa 1corinthians 11:5 but any woman who prays or prophesies with her head unveiled........ Hapo unaona prophesies ama kutoa unabii na tunajua kuna manabii wa kike kama Miriam,Anna na wengine. Lakini si kufundisha kanisani biblia inakataza Jambo hilo mwanamke kufundisha pia inakataza kua na cheo kanisani, hapo Paulo anaongea juu ya mwanamke kusali ama kutoa unabii. Shikilia hilo. Kaka kamwe Paulo hawezi akasema Jambo hili hapa na Jambo jingine pinganishi kule haiwezekani. Bible inasema ndio yenu iwe ndio na sio iwe sio hilo NI Neno la Mungu. Naomba namba yako mkuu kuna mengi ya kuzungumza
 
Nimekaa na kutafakari sana Kwa nini wasabatho wanalipiga vita sana kanisa katoliki na hiyo vita siyo kwa makanisa mengine?

Wajuzi mnijuze!

View attachment 2757316
Kwa kuwa lina wafuasi 1.2 Bilion duniani kote na ndiyo Kanisa Takatifu la Mitume lililoanzishwa na Yesu Kristo mwenyewe (Mathayo 16:1) "Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda"

Achana na vikundi vya ki-itikadi (cult) kama SDA vilivyoanzishwa na mwanamke mtabiri nyota mwaka 1844.

Watu walitaka wasafiri kwenda Ufaransa kuhubiri injili bila kuwa na passport wala tiketi, hao ndiyo washindane na RC?
 
Unazunguka Lakini unaludi palepale ya kwamba askofu imempasa, ukipata mstari wowote ule ambao askofu sio lazima kuoa nitaandika Bango linalosema MIMI NI MPINGA KRISTO. Usisahau askofu imempasa kuoa huo ni wajibu sio hiyari kinyume cha hapo Hana sifa ya kuongoza kondoo wa Yesu Kristo huyo ana sifa ya kuongoza, kundi la Wana wa upotevu.

Usisahau pia haya.
Mwanamke kua na mamlaka kanisani ni kinyume na maandiko, kubatiza kwa kunyunyizia ni kinyume na maandiko.

Ndugu yangu sio kwamba nakuvuta uje ninaposali hapana, Mimi Ninachotimiza ni kimoja tu kukushuhudia Neno la Kristo tu ni hivyo tu. Biblia haiwezi hapa ikasema askofu aoe na sehemu nyingine ikasema tofauti, ama pale isimluhusu mwanamke kua na mamlaka kanisani halafu pale ikasema vile. Kamwe haiwezi kua hivyo.

wewe Amini kwamba biblia imesema imempasa askofu aoe na hakuna sehemu Inayopinga Jambo hilo, Amini hivyo hilo ni kweli Amini Tu ndugu yangu. Yesu aliwaambia msipoamini mtakufa katika dhambi yenu. Hakuna hata sehemu moja aliposema MSIPOELEWA no ni kuamini Tu Amini Tu ndugu.


natamani kuongea na wewe kwa simu ndugu. Ubarikiwe

Yesu hakuoa msio tambua hili ndio mtabaki kuleta mihemko,RC iko strong kwa sababu hii ya maaskofu wake kuwa watawa,makanisa mengi ambayo maaskofu wameoa na familia taaaisi zao zimejaa migogoro ya kila aina kwasababu mwanaume aliyeoa ni mwanaume dhaifu hawezi simamia taaisis vyema kwa sababu lazima ataweka mbele maslahi ya familia yake.

Wakatoliki sio wajinga wanajitambua na wanajua nini wanafanya,bila ukatoliki ukristo usingekuwepo duniani.
 
Ndugu wakolinto wa Kwanza Sura ya 7:32-34 hapo hakuna askofu na usipalazimishe pawe. Maana maelezo yako unalazimisha, Neno linasema askofu imempasa awe na mke mmoja Tu. Hilo ndivyo ilivyo si vinginevyo hakuna nyongeza ya hiyo. Askofu ni wajibu kuoa. Unapokuja kwa Paulo usifosi iwe kwake kwa maana yeye alikua na huduma nzito mno ya kupeleka ujumbe kwa wamataifa Paulo yeye ana huduma ya tofauti na amepata hiyo neema, ni sawasawa na Musa Mungu anawaambia waislael kwamba msijitengenezee vinyago Lakini anaambiwa Musa tengeneza nyoka Wa Shaba, hivyo neema hiyo, hiyo kwa Musa ndivyo ilivyo kwa Paulo .

Neno la Mungu linasema askofu imempasa awe na mke mmoja

Unajikanyaga sana,hujui kila mtumishi kabeba maono makubwa kwa kazi ya Mungu au wewe unaweka mpaka katika utumishi?
 
Unajua kazi ya Paulo ni kua nuru ya mataifa unajua kua Paulo yeye alikua
NI mjumbe kwa wamataifa na ndio maana alikua na mamlaka ya kumfokea petro. Amka usingizini huyo papa mnaedai haoi alafu mnakuja kusema kua petro ni papa wa Kwanza wakati huo huyohuyo petro ameoa. Amka usingizini. Mimi sipo kwa Ajili ya kubishana Ila Angalia Neno la Mungu nakuonesha mlipodondoka, ndugu kama hutojali nikupe no ya simu ili tuone je mpo nje ya bible kwa Neno hilo tu ama nengi?

hebu wazia mwaka 1500s Martin Luther aliandika makosa ya catholic 95 ambayo yanahitaji masahihisho na aliwaambia kua kama mnataka niache kutangaza hivi basi nionyeshe I KOSA langu kwenye biblia, na nionyesheni kwamba kwa mujibu wa andiko gani mnafanya haya.

ikikupendeza nipe no ya simu tuongee tena huku kila mtu akiwa ameshika biblia ili uone je kipi NI kipi.. TOKA HUKO NDUGU WW NI NDUGU, MIMI NI NGUMU KWASABABU KILA KITU NAKUONESHA KWA NENO, NA NIMEKAA ROMAN CATHOLIC MIAKA MINGI, NIKAFUNDISHA HADI MASWALA PRIMARY, SECONDARY, CHUO KOTE NILIKUA KIONGOZI WA ROMAN CATHOLIC LAKINI WAMEANGUKA KWA MAKOSA MENGI MNO

Hongera kwa kuliacha kanisa na kufuata illuisions,uzuri ni kwamba kanisa katoliki haliyumbishwi lina misingi imara ya kujisimamia milele zote.
 
sio wasabatho wanawapinga wakatoliki hata waislamu hawawapendi wakatoliki tena afadhali ya sabatho

Waislamu wanaliogopa kanisa katoliki kama ukoma mana walileta ujinga ujinga crusade war ili wanyoosha,hadi leo papa anaingia msikitini na viatu,thubutu shehe au muumini wa kawaida kuingia msikinitni na viatu kama hawajakupopoa[emoji28]
 
Yesu hakuoa msio tambua hili ndio mtabaki kuleta mihemko,RC iko strong kwa sababu hii ya maaskofu wake kuwa watawa,makanisa mengi ambayo maaskofu wameoa na familia taaaisi zao zimejaa migogoro ya kila aina kwasababu mwanaume aliyeoa ni mwanaume dhaifu hawezi simamia taaisis vyema kwa sababu lazima ataweka mbele maslahi ya familia yake.

Wakatoliki sio wajinga wanajitambua na wanajua nini wanafanya,bila ukatoliki ukristo usingekuwepo duniani.
Usijibariki, twende kwenye neno usimfananishe Yesu na askofu ama papa, huyo papa mnayedai ni petro alioa, kila kitu nenda Neno la Mungu.

Unaposema askofu akioa hahudumii majukumu yake ipasavyo, Una maana kwamba Roho mtakatifu alikosea kusema "askofu imempasa awe na mke mmoja" si ndio maana yako.

ndugu yangu tetea Neno la Mungu na sio kuleta mbambamba hapa nimekuwekea kifungu ambapo Roho mtakatifu ndani ya Paulo anasema askofu imempasa kuoa
 
Naomba niwaulize wa sababto ambao mnasema Yesu hakutengua torati ya musa bali alikuja kuikamilisha,je ukiondoa suala la amri 10 za Mungu,ni vitu gani vingine mliovichukua agano la kale na vitu gani mlioviacha agano la kale na kwanini?
 
Hongera kwa kuliacha kanisa na kufuata illuisions,uzuri ni kwamba kanisa katoliki haliyumbishwi lina misingi imara ya kujisimamia milele zote.
Lina misingi imara ipi ndugu, misingi imara ya kanisa ni Neno la Mungu, je unakumbuka mnamo 1500s Martin Luther aliorodhesha makosa 95 ya kuyafanyia masahihisho kwa sababu yamepingana na Neno la Mungu, unalijua hilo. Na je kama wameliacha Neno linakuaje na misingi imara ama je ni Bora liwe na misingi imara ya kibinadamu au Neno la Mungu.

Kanisa katoliki lilikua na misingi imara kabla ya mwaka 325 baada ya mwaka huo Tu na kuanza vikao vya kujadili Neno la Mungu liwe wanavyotaka lilianguka. Sasa biblia inasema kanisa likianguka hakuna tena neema ya kusimama

Waebrania 6:5-6
na kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu za zamani zijazo,
wakaanguka baada ya hayo, haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu; kwa kuwa wamsulibisha Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zao, na kumfedhehi kwa dhahiri.
 
Utashitakiwa Mtibeli.Unatoaje nondo namna hii?Sasa swali kama hili kwa nini umwambie atoe kwenye Biblia?Ungemwambia atoe kwenye vitabu vya historia ya watakatifu wa kikatoliki bwa shee

Unajua kuna Watu wanashindwa kutofautisha mambo
 
Usijibariki, twende kwenye neno usimfananishe Yesu na askofu ama papa, huyo papa mnayedai ni petro alioa, kila kitu nenda Neno la Mungu.

Unaposema askofu akioa hahudumii majukumu yake ipasavyo, Una maana kwamba Roho mtakatifu alikosea kusema "askofu imempasa awe na mke mmoja" si ndio maana yako.

ndugu yangu tetea Neno la Mungu na sio kuleta mbambamba hapa nimekuwekea kifungu ambapo Roho mtakatifu ndani ya Paulo anasema askofu imempasa kuoa

Usijichanganye Mtume Paulo alikua natoa maoni yake katika masuala mengi sana,hili la kuoa ama kutokuoa ni ushauri tu,ila kama unataka utende vyema kazi ya kristo ni vyema usioe kabisa ila kama utawaka tamaa basi ao ila ndoa ya mke mmoja tu.

Kwakuliona hilo kanisa la RC lenye mfungamano na kristo na mitume wake likaona ni vyema maaskofu wake wasioe ili wawe imara katika kutenda utume wa injili kama kristo mwenyewe.

Narudia tena RC ndio taaisis ya kidini imara kuliko zote ulimwenguni moja ya sababu kuu ni sera ya utawa,siku ukiona kanisa limeondoa sera hii ndio anguko la kanisa hili na kwa hili sahau kama itakuja tokea mana RC nia kanisa linalojitambua.
 
Usijichanganye Mtume Paulo alikua natoa maoni yake katika masuala mengi sana,hili la kuoa ama kutokuoa ni ushauri tu,ila kama unataka utende vyema kazi ya kristo ni vyema usioe kabisa ila kama utawaka tamaa basi ao ila ndoa ya mke mmoja tu.

Kwakuliona hilo kanisa la RC lenye mfungamano na kristo na mitume wake likaona ni vyema maaskofu wake wasioe ili wawe imara katika kutenda utume wa injili kama kristo mwenyewe.

Narudia tena RC ndio taaisis ya kidini imara kuliko zote ulimwenguni moja ya sababu kuu ni sera ya utawa,siku ukiona kanisa limeondoa sera hii ndio anguko la kanisa hili na kwa hili sahau kama itakuja tokea mana RC nia kanisa linalojitambua.
Mkuu Mimi nataka andiko sitaki maneno yako tupu, kumbuka Neno la Mungu linasema Neno la Mungu liwe kweli na mtu Tu iwe uongo nayo Neno la Mungu ni kweli, njoo na andiko.

Kumbuka Paulo baada ya kuandika hayo amesema hivi katika
1 Timotheo 3:15
Lakini nikikawia, upate kujua jinsi iwapasavyo watu kuenenda katika nyumba ya Mungu, iliyo kanisa la Mungu aliye hai, nguzo na msingi wa kweli.

kwamba hivyo ndivyo iwapasavyo watu kuenenda katika nyumba ya Mungu yaani kanisa, unaona hili ni Neno la Mungu sio ushauri ndio maana amesema askofu imempasa na pia anasema hivyo ndivyo iwapasavyo watu kuenenda shikilia iwapasavyo maana ni wajibu ni lazima na sio wakipenda wafanyaj hivyo hapana. Hivyo ndivyo iwapasavyo watu kuenenda katika nyumba ya Mungu. Shikilia hilo haliwezi kubadilika hata kidogo na hii ni injili kumbuka.

NAOMBA andiko maana kwa andiko utakua salama Lakini kwa maneno kutoka katika kanuni mlizojitungia kutoka katika mitaguso hiyo itakupeleka kuzimu. Maana imeandikwa mnaliharifu Neno la Mungu kwa mapokeo ya wanadamu
 
Back
Top Bottom