Kwanini flyover Ubungo haimalizi tatizo la foleni?

Sasa hapo ushasogeza kipande kirefu tu...iyo ya VETA itashughulikiwa kumbuka zikijengwa zote watasema wanafunzi hawana madawati
Hapo sasa hata ubungo foleni kwa jinsi ilivyopungua ni kama haipo kabisa ukilinganisha na zamani na ujenzi bado haujaisha...
 
Ndio umefikiria hapo?!so tunahamishia tatizo kwingine ..vipi na huko kukiwa na foleni tunasogeza tena mbele au sio?
Tukiwa na maeneo yanayojitosheleza kwa huduma zote, iwe ni masoko, shule, ofisi, basi jamii haitalazimika kusafiri umbali mrefu kuzifuata hizo huduma. Kama watu kwa sasa wanapanga nyumba zao nje ya jiji, na shughuli za kuingiza kipato pia zianzishwe/zijengwe hukohuko waliko.
 
Ma ccm akili hayana kabisaaa no creativity at all
 
Hata umasikini hauwezi kwisha,, viongozi ni wale wale
 
Hata umasikini hauwezi kwisha,, viongozi ni wale wale
Viongozi wanabadilika kila Muhula!
Huo usiobadilika ni uongozi gani!?

Na ni wapi walibadilisha viongozi na umasikini ukaisha!? Umasikini ni self initiative kwa sehemu kubwa.. kama hauna hiyo hata ungezaliwa Mauritius bado ungekuwa masikini

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Chukulia tazara mkuu, acha kuumiza kichwa. Kama wewe sio wa mkoani na unatumia barabara ya mandela na nyerere sasa na uliwahi tumia kablabya flyover je kuna foleni kwa kuwepo flyover pale tazara?
Tazara foleni imepungua sana ,ila shida iko kipande cha kutoka temeke kwenda buguruni(gari za chini)...ila kuwepo kwa flyover kumepunguza foleni
 
Hiyo ni tabia ya kulalamika tu ambayo imajaa vichwani mwa baadhi ya watanzania wengi kiasi kuwa linalofanywa na serikali lazima waone kuwa ni baya. Huko ulikookota hizo definition hukupasoma vizuri iwapo unadhani kuwa flyover na daraja ni vitu viwili tofauti. Zote ni structure zinazpita juu ya kitu kingine, zinaweza kuwa zinapita juu ya barabara nyingine, juu mto, au juu ya reli. Halafu unapodhani kuwa flyover lazima ipunguze foleni ni wazi kuwa huenda hujasafiri nje ya nchi kuona hali halisi zikoje. Chicago pale kuna flyover nyingi sana lakini wakati wa rush hour foleni huwa na kali sana. Ukiwa China ambako ndiyo wameenedelea na maflyover karibu kila sehemu lakini nao kuna sehemu nyingi huwa zinagubikwa na foleni sana; India nayo ina flyover nyingi sana lakini folnei haziishi.



Njia kuwa convenient haina maana ya kutokuwapo na foleni, ila inasaidia kupunguza foleni. Huwezi kulinganisha foleni iliyokuwa Ubungo zamani na foleni iliyopo leo. Na kuwepo kwa foleni haukubatilishi ukweli kuwa hiyo ni flyover.
 
Hahahaha kwa hiyo bodaboda wasingezagaa ingekuwa flyover?

Mkuu wewe ni taahira ila bado hujajijua tu, halafu wala ile sio flyover ni interchange (daraja la mapishano)

😃😃 Sasa mkuu iv unajua ukiongea na taahira na ww ni taahira pia ?
Sijui nani sasa atakuwa kiwango kimezidi cha utaahira 😄😄😄😄 mbona ata baba jesca amekuwa aki ziita fly over
 
Hahahaha yani Jf wajuaji wengi wao ni mainginia wa kila jambo.....hahahahs
 
Flyover moja au mbili haziwezi kumaliza foleni.
Lazima kuwa na study ya network ya barabara zote.
Kwa sasa hivi tunahamisha matatizo tu..
Utapita haraka Ubungo na kwenda kurundikana External au Mwenge.

Morogoro rd foleni iko pale pamoja na uwepo wa Mwendokasi. Midalala mibovu ndiyo imeongezeka na haina vituo maalum. Popote wanasimama tu.
 
Kuna tofauti ya Traffic Jam na Traffic Congestion
Ni ngumu kuzuia foleni sehemu yoyote pale iwe ya magari,ya watu lakini unaweza kuzuia mlundikano
Unaweza kuielewa bank ikiw na foleni ya watu kupata huduma lakini huwezi kuielewa kukiwa na mlundikano wa watu
Junction za ubungo na Tazara zilikuw na mlundikano wa magari hivyo kuwa ni kero kwa watumiaji wa barabara,
Madara ya juu yamejengwa kupunguza mlundikano,lakini foleni haizuiliki inapungua tu
 
Ok kumbe mheshimiwa leo kakosea kusema tatizo la foleni limeisha
 
Wakandarasi wetu changamoto sana hebu imagine kimara korogwe daladala hazina kituo zinashushia barabarani zinaongeza foleni kiboya kabisa, wameshindwa hata kuchepusha kimtindo washushie abiria pembeni? Mwenge ndio usiseme maana ukiwa umetokea sam nujoma kuingia bagamoyo road kuelekea itv mnakaa foleni mpaka mnakoma. Taa zinawaka sekunde 15 yanapita magari matatu zinazima. Akikaa traffic police ndo balaa zaidi
 
Kwani ufipa mnahangaika na maendeleo ya vitu nyinyi ulizeni kuhusu watu achaneni na vitu

Wakati mambo yanaanza mlipinga mkasema Bibi wa huko kijijini hali lami Sasa mnashauri lini😀😀
 
Unachosema ni kweli ila tuliaminishwa foleni itaisha ndio maana tunahoji mkuu. Si unaona hata ramani ya kwanza ilivyokua?

 
una uelewa wowote wa uhandisi?
hata mwendo kasi mlifungulia ma thread oo basi zitashusha vipi abiria wakati vituo vinasomeka kulia,kumbe mlikariri tu mabasii yatakuja na milango upande wa kushoto
subiri mradi ukamilike ndipo ulete tathmini yako
Kutolea mfano wa mwendokasi hapo umefeli maana walikiri kabisa kulikua na makosa ndio maana wakatoboa milango upande wa pili. Besides haihitaji elimu ya uhandisi kung'amua tatizo linaloonekana. Au ndio nyie wahandisi mmejenga barabara ya kimara bila vituo vya daladala mmesababisha jam inatucost daily
 
[emoji848]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…