Kwanini flyover Ubungo haimalizi tatizo la foleni?

Kwanini flyover Ubungo haimalizi tatizo la foleni?

maroon7

JF-Expert Member
Joined
Nov 3, 2010
Posts
11,311
Reaction score
15,640
Naipongeza Serikali yetu kwa juhudi kubwa za kutuletea maendeleo ikiwemo kuboresha miundombinu yetu. Leo daraja la juu pia limefunguliwa kwa magari yanayotokea mwenge kuelekea Riverside lakini kinachonishangaza ni kwanini foleni bado ni kubwa sana kwa magari yanayotokea Kimara?

Huenda hawajamaliza upanuzi wa barabara ila ni wazi kwa ramani hii wameamua tu kupunguza tatizo la foleni badala ya kulimaliza pamoja na kutumia billions za kutosha.

Nachojiuliza walishindwa vp kuongezea bilioni zingine wakajenga kitu cha kuishi miaka yote kitakachomaliza tatizo? Na hii hali inajirudia pale mbezi mwisho licha ya mapesa mengi yanayotumika ila hakuna dalili za kumaliza tatizo la foleni sana sana ni kama foleni ya Ubungo wanaihamishia Mbezi Mwisho.

Tuna watu wanaofikiri sawasawa? Hawatembei nchi nyingine? Wakitembea huko hawajifunzi wenzetu wanafanyaje?
 
Naipongeza Serikali yetu kwa juhudi kubwa za kutuletea maendeleo ikiwemo kuboresha miundombinu yetu. Leo daraja la juu pia limefunguliwa kwa magari yanayotokea mwenge kuelekea Riverside lakini kinachonishangaza ni kwanini foleni bado ni kubwa sana kwa magari yanayotokea Kimara?

Huenda hawajamaliza upanuzi wa barabara ila ni wazi kwa ramani hii wameamua tu kupunguza tatizo la foleni badala ya kulimaliza pamoja na kutumia billions za kutosha.

Nachojiuliza walishindwa vp kuongezea bilioni zingine wakajenga kitu cha kuishi miaka yote kitakachomaliza tatizo? Na hii hali inajirudia pale mbezi mwisho licha ya mapesa mengi yanayotumika ila hakuna dalili za kumaliza tatizo la foleni sana sana ni kama foleni ya Ubungo wanaihamishia Mbezi Mwisho.

Tuna watu wanaofikiri sawasawa? Hawatembei nchi nyingine? Wakitembea huko hawajifunzi wenzetu wanafanyaje?
Hauna kapicha kakukoleza story
 
foleni itahamia shekilango baada ya kuvuka flyover ukiwa unaelekea city center.
...mark my word.
Akili ya ccm planners ni fupi hazivuki urefu wa pua zao. Wao wamejenga flyover ubungo few meter toka hapo kuna junctions Shekilango, njia panda ya chuo, sinza na riverside. Walichofanya ni kuhamisha foleni. Sijui kama hata waliona hili
 
Akili ya ccm planners ni fupi hazivuki urefu wa pua zao. Wao wamejenga flyover ubungo few meter toka hapo kuna junctions Shekilango, njia panda ya chuo, sinza na riverside. Walichofanya ni kuhamisha foleni. Sijui kama hata waliona hili

mkuu embu usiye ccm shauri nini wangefanya kwa akili za kawaida kabisa.

makutano ya ubungo au tazara kuna barabara kuu mbili zinakutana pale,kuweka kivuko pale ni kuondoa ukinzani baina ya hizo barabara mbili.

foreni shekirango ni ya makutabo ya barabara nyingine sio hizo tajwa kubwa hapo juu,je tujenge kivuko kingine????

kwahiyo hapa lengo lilikuwa kuondoa foreni ya njiapanda ile,kama bado kuna foreni eneo hilo ndio unaweza sema walikosea,vinginevyo lawama hizi hazina msingi ni muendelezo tu wa ujuaji usio na maana.
 
Naipongeza Serikali yetu kwa juhudi kubwa za kutuletea maendeleo ikiwemo kuboresha miundombinu yetu. Leo daraja la juu pia limefunguliwa kwa magari yanayotokea mwenge kuelekea Riverside lakini kinachonishangaza ni kwanini foleni bado ni kubwa sana kwa magari yanayotokea Kimara?

Huenda hawajamaliza upanuzi wa barabara ila ni wazi kwa ramani hii wameamua tu kupunguza tatizo la foleni badala ya kulimaliza pamoja na kutumia billions za kutosha.

Nachojiuliza walishindwa vp kuongezea bilioni zingine wakajenga kitu cha kuishi miaka yote kitakachomaliza tatizo? Na hii hali inajirudia pale mbezi mwisho licha ya mapesa mengi yanayotumika ila hakuna dalili za kumaliza tatizo la foleni sana sana ni kama foleni ya Ubungo wanaihamishia Mbezi Mwisho.

Tuna watu wanaofikiri sawasawa? Hawatembei nchi nyingine? Wakitembea huko hawajifunzi wenzetu wanafanyaje?
Ujenzi bado haujakamilika
 
mkuu embu usiye ccm shauri nini wangefanya kwa akili za kawaida kabisa.

makutano ya ubungo au tazara kuna barabara kuu mbili zinakutana pale,kuweka kivuko pale ni kuondoa ukinzani baina ya hizo barabara mbili.

foreni shekirango ni ya makutabo ya barabara nyingine sio hizo tajwa kubwa hapo juu,je tujenge kivuko kingine????

kwahiyo hapa lengo lilikuwa kuondoa foreni ya njiapanda ile,kama bado kuna foreni eneo hilo ndio unaweza sema walikosea,vinginevyo lawama hizi hazina msingi ni muendelezo tu wa ujuaji usio na maana.
Foleni haitaondoka mkuu. Itahamia kwenye hizo juction nyingine. Kumbuka barabara ya Morogoro imejengwa mara 5 ndani ya miaka 25 na mara zote inajengwa kuondoa foleni lakini foleni haiondoki. Planners wetu wajifikirie upya. Wanapoplan mradi mkubwa kama huu wafikiri miaka 50 au 100 ijayo siyo 5
 
Ushauri kwa CCM wajiuzulu na wa kubali kushtakiwa na adhabu iwe kunyongwa, hadi kufa. Wakifanya hivyo watakumbukwa milele

sasa kama lengo ni hili tusijengee hoja kwenye vitu vya wazi tutaonekana wendawazimu na tutakosa kuungwa mkono.

kuna matakataka mengi tu ccm wamefanya.
 
Foleni haitaondoka mkuu. Itahamia kwenye hizo juction nyingine. Kumbuka barabara ya Morogoro imejengwa mara 5 ndani ya miaka 25 na mara zote inajengwa kuondoa foleni lakini foleni haiondoki. Planners wetu wajifikirie upya. Wanapoplan mradi mkubwa kama huu wafikiri miaka 50 au 100 ijayo siyo 5

ndio sababu nikakwambia sema serikali unataka ifanye nini??
au ndio unataka mpaka uwe rais ndio utekeleze???
 
Ihamie mara ngapi? Jion yenyewe ukishavuka ubungo ukifika kibo tu folen imeanza hiyo ni mpaka kimara mwisho.
Kuna sehemu katika njia ya kimara mwisho mpk magomeni zina foleni kubwa zinazosababishwa na wavuka kwa miguu mfano manzese (kituo cha mwendokasi) na Korogwe (Kituo cha Mwendokasi). Zile sehemu zitafutiwe ufumbuzi zinaleta kero sana. Kimara Mwisho Daraja la Juu limesaidia otherwise pangekuwa worse kabisa. Pia pale Shekilango asubuhi wakati mabasi ya mikoani yanatoka kunakuwaga na usumbufu. Tunashukuru kwa flyover ila inabidi tuendelee kuumiza vichwa kusolve matatizo ya foleni. Sehemu ya km 18 Posta to Kimara unatumia masaa mawili not fair hata kiuchumi
 
ndio sababu nikakwambia sema serikali unataka ifanye nini??
au ndio unataka mpaka uwe rais ndio utekeleze???
Redesign magari ya kutoka Kimara kwenda CBD yawe na option ya kwenda kushukia mbele ya juction ya Mabibo, ya mwenge yakashukie mbele ya juction ya sinza na ya kwenda buguruni ya yashukie mbele ya external. Hao wanadesign hizo barabara waende hata nchi za watu wakaone wenzao wanavyodesign. Hata hapo Kenya tu waende. Ubungo walitakiwa wajenge interchange siyo flyover ili lanes za pembeni ziende mbali kwenye maeneo nayoyataja bila kukutana tena juction za karibu
 
Redesign magari ya kutoka Kimara kwenda CBD yawe na option ya kwenda kushukia mbele ya juction ya Mabibo, ya mwenge yakashukie mbele ya juction ya sinza na ya kwenda buguruni ya yashukie mbele ya external. Hao wanadesign hizo barabara waende hata nchi za watu wakaone wenzao wanavyodesign. Hata hapo Kenya tu waende. Ubungo walitakiwa wajenge interchange siyo flyover ili lanes za pembeni ziende mbali kwenye maeneo nayoyataja bila kukutana tena juction za karibu

ndio sababu nikasema ushauri ili tujue nawewe umejaza kitu gani kichwani,haaya tumeona.

nikafikiri labda unasema kila makutano yangewekewa daraja ili kuzitatua lawama zako,lakini laa umepita mule mule unaposema wameharibu ccm,unafikiri nini kinafuata kwa makutano mengine ya mbele,mfano buguruni kuna mataa ya dampo kuelekea tabata.yataumana magari tena.
mabibo mbele kuna makutano ya magomeni,nayo yana traffic sio ya kawaida.

halafu kuitaja kenya kwenye swala la foreni bro hujafika kenya,hawa sijui wanakosea kupanga,sijui magari ni mengi,sijui labda wana mji mdogo sijui.wana foreni mbaya kuliko hizo unazozijua wewe,achana na mabarabara ya mviringo unayoyaona nje ya jiji lao hukoo porini.
 
Foleni za Tanzania haziletwi na wingi wa magari bali uzembe wa madereva, kwa hali ya kawaida wala hakuna magari ya kuhitaji flyover Dar, kama Serikali ingedhibiti uzembe tu wa daladala, malori, bodaboda tatizo lingeisha mara moja.

Siku zote penye kituo cha daladala ndiyo kuna foleni, ...
 
Back
Top Bottom