Kwanini historia ya Zanzibar ya kweli haisomeshwi?

Kwanini historia ya Zanzibar ya kweli haisomeshwi?

Kuna tofauti kati Waarabu na Uislam, Na Kuna viashiria vya baadhi ya wachangiaji wana waadhibu Waislam Kwa makosa ya waarabu, si Sawa . Waarabu wapo mpaka walokole kama si Othodox au Roma.
 
Mkuu Gavana, kwanza pole kwa madhila ya yale Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, kwa hayo unayoyasema, kila binadamu mwenye utu, yatamgusa, hata nilipokisikia kisa cha Hamudi iliyemuua Karume, nikaelewa.

Hili la ubaguzi Zanzibar lipo, tena sio tuu ni ubaguzi wa kutubagua Wabara, hata nyinyi wenyewe kwa wenyewe mnabaguana, Luna Wanzanzibari na Wazanzibara. Ndani ya Wazanzibari pia mnabaguana kuna Waunguja na Wapemba. Kwa vile Pemba haikushiriki yale Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, Wanamapinduzi kindakindaki waliwahi kujiapisha " Zanzibar imepatikana kwa Mapinduzi, Pemba haikushiriki Mapinduzi, hivyo Mpemba kamwe hawezi kupewa urais Zanzibar kwenye karatasi ".

Baada ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, Wamatumbi ndio waliruhusiwa kujitwalia vibinti vya Kiarabu, na ilikuwa ni marufuku kukataa.

Mpaka leo, mpaka kesho, baadhi ya Waarabu wanajisikia wao ni bora zaidi, na baadhi ya Wamatumbi wanajisikia wanyonge.

P


Ninakuambia tena Ubaguzi uko kwenu bara . Au nasema uongo ???

Huku kwetu ubaguzi unapandikizwa na nyinyi Watanganyika ili kuhalalisha uvamizi wenu.

Kwanza huku tunajuana na wa kuja anajulikana. Kuoana watu makabila tofauti hiyo ipo tokea kabla ya mapinduzi .

Karume Sr. asingalimwoa huyo bibi Fatma kama unavyosema wewe.

Babu yangu alimwoa msichana wa kiarabu mweupe kuliko karatasi.Wala hakubaguliwa na mtu yeyote.

Unguja na pemba ni utani wa kijadi ambao nyinyi mnaugeuza kupandikiza ubaguzi.

Mimi nimeoa Pemba wala sikuambiwa kuwa wewe ni muunguja wala sijawahi kubaguliwa na Mpemba yeyote na nimeishi pemba miaka mingi na nimesoma Pemba primary na secondary

Uzanzibari na uzanzibara upo hivi sasa kwa watu kama nyinyi kuja kupandikizwa na kupewa id za uZanzibar ili muipigie kura CCM

Hiyo ipo kwani hata mimi nikija Kwenu nikapewa id ya uongo ya kuwa nimezaliwa huko ili niipigie kura CCM hamtonikubali maisha
 
Mkuu Gavana, kwanza pole kwa madhila ya yale Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, kwa hayo unayoyasema, kila binadamu mwenye utu, yatamgusa, hata nilipokisikia kisa cha Hamudi iliyemuua Karume, nikaelewa.

Hili la ubaguzi Zanzibar lipo, tena sio tuu ni ubaguzi wa kutubagua Wabara, hata nyinyi wenyewe kwa wenyewe mnabaguana, Luna Wanzanzibari na Wazanzibara. Ndani ya Wazanzibari pia mnabaguana kuna Waunguja na Wapemba. Kwa vile Pemba haikushiriki yale Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, Wanamapinduzi kindakindaki waliwahi kujiapisha " Zanzibar imepatikana kwa Mapinduzi, Pemba haikushiriki Mapinduzi, hivyo Mpemba kamwe hawezi kupewa urais Zanzibar kwenye karatasi ".

Baada ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, Wamatumbi ndio waliruhusiwa kujitwalia vibinti vya Kiarabu, na ilikuwa ni marufuku kukataa.

Mpaka leo, mpaka kesho, baadhi ya Waarabu wanajisikia wao ni bora zaidi, na baadhi ya Wamatumbi wanajisikia wanyonge.

P

Ubaguzi Zanzibar unaendeshwa na CCM chama chenu mkuu. Bila ya CCM Zanzibar ni shwari.

Opera Snapshot_2019-04-23_165551_www.jamiiforums.com.png
 
Kuna tofauti kati Waarabu na Uislam, Na Kuna viashiria vya baadhi ya wachangiaji wana waadhibu Waislam Kwa makosa ya waarabu, si Sawa . Waarabu wapo mpaka walokole kama si Othodox au Roma.
Wakristo na Waislamu ni watoto wa baba mmoja Nabii Abraham, (Ibrahim). Waislamu ni uzao wa mwanae wa kwanza Ismael (Ismaili) aliyezaa na mtumwa mjakazi wa Kimisri, Hajir (Hagai). Wakristo ni uzao wa mwanae wa pili Isaac (Isiaka).

Hata Yesu Kristo Kiislamu ndiye Nabii Issa Bin Maryam, japo alizaliwa Bethlehem ya Uyahudi, lakini alikulia Misri na kurejea Israel akiwa na umri wa miaka 30, akahubiri kwa miaka 3 tuu, akasulubiwa, akafa msalabani na kuzikwa, siku ya tatu, akafufuka na kupaa mbinguni.

Hivyo Wakristu na Waislamu, sisi ni ndugu.

P
 
"Pascal Mayalla, post: 33648454, member: 17813"]Hii hoja ya kumleta Okello na kusema Okello sii lolote sii chochote ni tuu kuhalalisha ile hoja yake ya zile ngano za Kipumbwi ili kuonyeshea waliompindua Sultan, sio Wanzanzibari bali ni Wanzanzibara.
Ndivyo alivyoanza katika ngano ya Sykes kwa kumfanya Nyerere si lolote si chochote na kuzua yale ya bandiko#39 kuhusu ujio wa Nyerere Dar.

Miaka 10 iliyopita aliweka picha za Nyerere akiwa na Kaptula yake kama Mwl katika jitihada za kumfanya si lolote si chochote. Tunazo kumbu kumbu hapa JF

Kwa Okello, picha aliyoweka haina maelezo, ni jitihada tu za kumfanya si lolote si chochote

Kuhusu ngano za Kipumbwi, bandiko hili limeibua mengine.

Mzee kafanya kitu tunaita ''self inflicted wound'' katika bandiko#125 alipodai kwamba Abdallah K Hanga ndiye kiongozi wa Mapinduzi.

Kwa mantiki hiyo ni Hanga aliye organize Kipumbwi. Nyerere kasamehewa
Zanzibar kuna ubaguzi sana wa matabaka, tabaka la juu walikuwa Wazungu, Europeans, wakafuatia Indians, Arabs, Washirazi na machotara, tabaka la mwisho ni Wamatumbi, ndio wanaitwa Africans, sasa katika ujumla wake, wanahesabu wenye halali ya kuwa Wanzanzibari halisi ni Wahindi, Waarabu na Machotara, ambao kwao hao ndio Wazanzibari wale Africans wanawaita Wanzanzibara.
Ndiyo maana katika picha ya Okello isiyo na tarehe, mahali na majina ya washiriki ametumia neno ''Wazanzibar Khalisi''
Kwamba ana challenge watu waonyeshe ''Wazanzibar khalisi'' kwa maana uliyoeleza hapo juu
Sasa ili kuyadogosha Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, hatua ya kwanza ni kumdogosha kiongozi wa Mapinduzi yale Okello kuwa sii lolote sii chochote.

Kisha kuweka picha ya Wajumbe wa Baraza la kwanza la Mapinduzi, ndio waliopindua ili kuonyeshea sio Wanzanzibari, bali ni watu wakuja wakishirikiana na Wanzanzibara.

Lengo ni juhudi za kuya discredit Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ili wayaite mauaji ya kimbari yaliyofanywa na Wanzanzibara kuwateketeza Wazanzibari.
Hapa anapata wakati mgumu sana.

Kusema Mapinduzi ni haramu ataudhi jamii ile inayoamini katika mapinduzi daima.

Kusema ni halali, ataudhi Wazanzibar anaoita ''khalisi''

Hayo yanamweka njia panda kwasababu kuna kitu ''common' kwa makundi 2 na yeye

Mshtuko mkubwa kwangu ni pale anaposema Sultan hana damu mikononi.

Yaani soko la binadamu walotengwa na familia zao, wanaokwenda kuhasiwa na kuteswa liwe chini ya usimamizi wa Sultan halafu mikono iwe safi! I mean duh! ngumu sana hii

Ndiyo! tunasema kuhasiwa kwasababu hakuna mabaki ya Waafrika middle east(Uarabuni)

Hata hoja ya TransAtlantic ni mufisili kwasababu, biashara hiyo imetokea tena ikiongozwa na Wamishenari wakiombea watumwa katika ''Door of no return''

Tofauti na Waarabu, Wazungu wanakiri unyama huo na leo kuna mjadala wa ''reparations''

2008 John McCain na Obama waliulizwa tukio baya la kiroho lililofanywa na Wamarekani

Wote walizungumzia mambo nje ya jambo moja, Utumwa.

Siku iliyofuata iliandikwa wazi kwamba hawakujibu sawa sawa, tukio baya la kiroho ni biashara ya utumwa.

Kasome maandiko na habari za Watumwa katika maktaba zao
Mabaki ya Watumwa yapo hadi leo, si Uarabuni.

Utumwa ni unyama tu uwe umefanywa na yoyote yule, tunachoshindwa kuelewa baadhi yetu ni jinsi watu wanavyotafuta uhalali wa biashara ya utumwa Zanzibar !!!
 
Ndivyo alivyoanza katika ngano ya Sykes kwa kumfanya Nyerere si lolote si chochote na kuzua yale ya bandiko#39 kuhusu ujio wa Nyerere Dar.

Miaka 10 iliyopita aliweka picha za Nyerere akiwa na Kaptula yake kama Mwl katika jitihada za kumfanya si lolote si chochote. Tunazo kumbu kumbu hapa JF

Kwa Okello, picha aliyoweka haina maelezo, ni jitihada tu za kumfanya si lolote si chochote

Kuhusu ngano za Kipumbwi, bandiko hili limeibua mengine.

Mzee kafanya kitu tunaita ''self inflicted wound'' katika bandiko#125 alipodai kwamba Abdallah K Hanga ndiye kiongozi wa Mapinduzi.

Kwa mantiki hiyo ni Hanga aliye organize Kipumbwi. Nyerere kasamehewa
Ndiyo maana katika picha ya Okello isiyo na tarehe, mahali na majina ya washiriki ametumia neno ''Wazanzibar Khalisi''
Kwamba ana challenge watu waonyeshe ''Wazanzibar khalisi'' kwa maana uliyoeleza hapo juu
Hapa anapata wakati mgumu sana.

Kusema Mapinduzi ni haramu ataudhi jamii ile inayoamini katika mapinduzi daima.

Kusema ni halali, ataudhi Wazanzibar anaoita ''khalisi''

Hayo yanamweka njia panda kwasababu kuna kitu ''common' kwa makundi 2 na yeye

Mshtuko mkubwa kwangu ni pale anaposema Sultan hana damu mikononi.

Yaani soko la binadamu walotengwa na familia zao, wanaokwenda kuhasiwa na kuteswa liwe chini ya usimamizi wa Sultan halafu mikono iwe safi! I mean duh! ngumu sana hii

Ndiyo! tunasema kuhasiwa kwasababu hakuna mabaki ya Waafrika middle east(Uarabuni)

Hata hoja ya TransAtlantic ni mufisili kwasababu, biashara hiyo imetokea tena ikiongozwa na Wamishenari wakiombea watumwa katika ''Door of no return''

Tofauti na Waarabu, Wazungu wanakiri unyama huo na leo kuna mjadala wa ''reparations''

2008 John McCain na Obama waliulizwa tukio baya la kiroho lililofanywa na Wamarekani

Wote walizungumzia mambo nje ya jambo moja, Utumwa.

Siku iliyofuata iliandikwa wazi kwamba hawakujibu sawa sawa, tukio baya la kiroho ni biashara ya utumwa.

Kasome maandiko na habari za Watumwa katika maktaba zao
Mabaki ya Watumwa yapo hadi leo, si Uarabuni.

Utumwa ni unyama tu uwe umefanywa na yoyote yule, tunachoshindwa kuelewa baadhi yetu ni jinsi watu wanavyotafuta uhalali wa biashara ya utumwa Zanzibar !!!
Nguruvi 3,
Laiti ningelikuwa na ujinga wa kiasi cha kutojua mchango wa Mwalimu Nyerere katika TANU na uhuru wa Tanganyika ningelikiua kitabu cha Abdul Sykes mapema sana kwani hakuna watu wangenichukulia mimi kama mtafiti na mwandishi makini.

Mwalimu nimemwandika kama anavyostahili kuandikwa licha ya kuwa kilichofanya kitabu changu kipate umaarufu na kupendwa ni kule kueleza historia yake kama ilivyostahili.

Mimi sikuanza historia ya TANU na Mwalimu Nyerere 1954.

Nimeanza historia ya TANU kwa kuzieleza siasa za mji wa Dar es Salaam kama zilivyokuwa mwanzo wa karne ya 20 yaani 1920s kwa kueleza ushawishi wa akina Sykes, Plantan na Dossa katika kila jambo muhimu la mji huu.

Kleist Sykes na wanae Abdul na Ally, Thomas Plantan walikuwa viongozi wa African Association na Mashado Plantan alikuwa na gazeti lake yeye mwenyewe akiwa mhariri na ndilo lilikuwa sauti ya Waafrika wa Tanganyika.

Gazeti hili likiitwa ''Zuhra'' na nakala zake zipo Maktaba ya Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, East Africana.

Mashado Plantan ni mmoja wa wanachama wa African Association ambae alihudhuria ufunguzi wa ofisi ya chama hicho mwaka wa wa 1933 na anaonekana kwenye picha pamoja na Kleist Sykes.

Gazeti hili ndilo lililowajulisha Waafrika wa Tanganyika jina la Julius Nyerere kama kiongozi wa TAA mwaka wa 1953 baada ya uchaguzi ambao Abdul Sykes na Julius Nyerere waligombea nafasi ya urais na Nyerere akashinda.

Kipande hiki mwanzo wa kitabu kiliwavutia wasomaji wengi na khasa kwa kuwaeleza kuwa haya niandikayo yanatoka katika Nyaraka za Sykes.

Wasomaji walichukua hili kama Abdul Sykes mwenyewe sasa anazungumza kutoka kaburini na anaeleza historia yake na vipi aliunda TANU kijilti alichokipokea kutoka kwa baba yake pale alipofariki mwaka wa 1949.

Huku si kumdogosha Mwalimu wala si ''ngano.''

Hii ilikuwa historia ambayo hakuna aliyekuwa anaijua labda watu wachache wenyeji wa mji wa Dar es Salaam.

Wengine kama wewe ndugu yangu mlipata mshtuko mlipoingia sasa katika historia yenyewe vipi Mwalimu kakutana na Abdul, nini uhusiano wa Abdul Sykes, Hamza Mwapachu, Julius Nyerere na Sheikh Hassan bin Ameir aliyekuwa Mufti wa Tanganyika.

Sheikh Hassan bin Ameir, Abdul Sykes na Hamza Mwapachu walikuwa wajumbe wa TAA Political Subcommittee toka mwaka wa 1950 wakati Nyerere hajafika Dar es Salaam na kamati hii ilikuwa inashughulika na mambo yote ya siasa ndani ya TAA.

Pamoja na hii kamati kwa pembeni alikuwapo Earle Seaton kama mshauri wa kamati hiyo katika mambo ya nchi zilizokuwa chini ya udhamini wa Umoja wa Mataifa.

Kwa mara ya kwanza wengi ndiyo walikuwa wanasikia kuwa ndani ya TANU kulikuwa na sheikh tena Mufti wa Tanganyika aliyekuwa na sauti kubwa ndani ya TANU na harakati za kudai uhuru na pia kusikia jina la Earle Seaton.

Kila aliyenisoma alinipa hongera na baadhi ya rafiki zake Abdul Sykes walikuwa hai na walinipongeza kwani historia hii ndiyo historia yao.

Picha ya Mwalimu kuvaa kaptula kwangu mimi si kitu cha kunishangaza.

Baba yangu anafanyakazi Exchange kama ilivyokuwa inaitwa kampuni ya simu 1950s kijana wa miaka ya katikati 20 nikimuona kwa macho yangu anavaa kaptula na stockings anakwenda kazini.

Abdul Sykes uniform yake ya Market Master Kariakoo Market ilikuwa shati jeupe kaptula ya khaki nyeupe na stockings.

Tumewaona wazee wetu katika mavazi haya nyumbani kwetu kwani haya yalikuwa mavazi ya wasomi wa nyakati hizo.

Vipi nimshangae mwalimu wa shule kuvaa kaptula ilhali walimu wengi walikuwa wakivaa kaptula kazini?

Unasema nimeweka picha ya Nyerere kavaa kaptula ili kumdhalilisha na una ushahidi.

Tafadhali na haraka sana weka hiyo picha na ushahidi kuwa imewekwa kwa ajili ya kumdhalilisha Nyerere.

Hayo mengine nimeyanyamazia kwa kuwa hayana maana kwangu.
 
Sishinikizwi kama wewe
Nguruvi3,
Ahsante sana niwie radhi hakika nakuunga mkono huna sababu ya kuniitika.

Muhimu ni huku mimi kueleza jinsi historia niliyoandika mimi ilivyotofautiana na historia rasmi iliyozoeleka.

Mmesoma historia na matukio hamkupatapo kusoma popote.

Hapa ndipo panapowatatizeni.

Akili inataabika kuamini kuwa haya usomayo ni kweli na yale uliofundishwa shule hayakuwa yamekamilika.

Lakini ikiwa utaiuliza akili yako kwa nini iwe hivi, haitakuwa tabu kupata jibu.
 
Muhimu ni huku mimi kueleza jinsi historia niliyoandika mimi ilivyotofautiana na historia rasmi iliyozoeleka.Mmesoma historia na matukio hamkupatapo kusoma popote.

Hapa ndipo panapowatatizeni.

Akili inataabika kuamini kuwa haya usomayo ni kweli na yale uliofundishwa shule hayakuwa yamekamilika.Lakini ikiwa utaiuliza akili yako kwa nini iwe hivi, haitakuwa tabu kupata jibu.
Mohamed, wapo wanaokuambia kuwa historia yako ina tatiza watu.
Pengine wanafanya hivyo kukupendeza!

Binafsi nikueleze sitatiziki na historia yoyote , nina tatizika na facts.

Swali ninalojiuliza baada ya kutuliza akili yangu ni moja, hivi kuna motive gani ya kubadilisha historia au kuzua au kupotosha?

Mfano, kwanini mtu anajua Nyerere alifika Dar mwaka 1948, lakini anakataa hata pale penye ushahidi. Nini motive ya mtu huyo! Hivi ndivyo vina tatiza wengi

Tena vina tatiza kwasababu kama ukweli mdogo kama huu unakataliwa, ukweli usiohitaji hata dakika ya fikra, yale wasiyoyajua watu yana ukweli kiasi gani? Hili lina disturb sana
 
Mohamed, wapo wanaokuambia kuwa historia yako ina tatiza watu.
Pengine wanafanya hivyo kukupendeza!

Binafsi nikueleze sitatiziki na historia yoyote , nina tatizika na facts.

Swali ninalojiuliza baada ya kutuliza akili yangu ni moja, hivi kuna motive gani ya kubadilisha historia au kuzua au kupotosha?

Mfano, kwanini mtu anajua Nyerere alifika Dar mwaka 1948, lakini anakataa hata pale penye ushahidi. Nini motive ya mtu huyo! Hivi ndivyo vina tatiza wengi

Tena vina tatiza kwasababu kama ukweli mdogo kama huu unakataliwa, ukweli usiohitaji hata dakika ya fikra, yale wasiyoyajua watu yana ukweli kiasi gani? Hili lina disturb sana
Nguruvi 3,
Nimepata kuulizwa kwa nini nadhani historia ya TANU pale chama chenyewe kilipoamua iandikwe na Abdul Sykes na Dr. Wilbard Klerruu wakaanza hiyo kazi iliingia katika matatizo na Abdul Sykes akajitoa?

Nimepata kuulizwa pia kwa nini Chuo Cha CCM Kivukoni ilipoamua mwaka wa 1981 kuandika historia ya TANU "notes" za Hassan Upeka za mahojiano aliyofanya na Abdul Sykes kuhusu historia ya TANU zilikataliwa kupokelewa?

Nimepata vilevile kuulizwa kwa nini jarida la Africa Events lilipochapa makala "In Praise of Ancestors,"mwaka wa 1988 makala yakimtaja Abdul Sykes katika historia ya kuasisi TANU toleo hili liliondolewa kwenye mzunguko?

Hayo ni baadhi ya maswali ambayo nimepata kuulizwa katika miaka 21toka kitabu cha maisha ya Abdul Sykes kitoke mwaka wa 1998.

Yapo maswali mengine nimejiuliza mwenyewe.

Kipi kimepelekewa Abdul na Ally Sykes kutunukiwa Medali ya Mwenge wa Uhuru baada ya miaka 50?

Kwa nini medali hii hawakupewa wazalendo wengine pia waliokuwa bega kwa bega na hawa ndugu wawili kama Hamza Mwapachu, Steven Mhando, Dr. Vedasto Kyaruzi, Sheikh Hassan bin Ameir, Zuberi Mtemvu kuwataja wachache?

Natatazika na maswali bado yapo mengi tu.

Kwa nini kitabu cha Abdul Sykes kimependwa kiasi hiki na kusababisha uchukuliwe uamuzi wa kuandika historià ya Mwalimu Nyerere na kuandika upya historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika?

Kipi kilichopungua hadi sasa inaandikwa historia mpya ya TANU na uhuru wa Tanganyika?

1575605867268.png
 
"Mohamed Said, post: 33689460, member: 12431"]
Nimepata kuulizwa kwa nini nadhani historia ya TANU pale chama chenyewe ilipoamua iandikwe na Abdul Sykes na Dr. Wilbard Klerruu wakaanza hiyo kazi iliingia katika matatizo na Abdul Sykes akajitoa?
Tangu mkutano wa Arnatouglo hadi 1961, Abdul alikuwa na ushiriki gani wa siasa za Tanzania? Kwanini alotoweka katika uongozi baada ya muda huo
Nimepata kuulizwa pia kwa nini Chuo Cha CCM Kivukoni ilipoamua mwaka wa 1981 kuandika historia ya TANU "notes" za Hassan Upeka za mahojiano aliyofanya na Abdul Sykes kuhusu historia ya TANU zilikataliwa kupokelewa?
Hassan Upeka kajaliwa Umri? Kwa maana nzuri tu ya kuelewa
Nimepata vilevile kuulizwa kwa nini jarida la Africa Events lilipochapa makala "In Praise of Ancestors,"mwaka wa 1988 makala yakimtaja Abdul Sykes katika historia ya kuasisi TANU toleo hili liliondolewa kwenye mzunguko?
Unakumbuka Africa Now? Unamkumbuka mtu anayeitwa Abdulrahman Babu?
Kipi kimepelekewa Abdul na Ally Sykes kutunukiwa Medali ya Mwenge wa Uhuru baada ya miaka 50?
Kwa nini medali hii hawakupewa wazalendo wengine pia waliokuwa bega kwa bega na hawa ndugu wawili kama Hamza Mwapachu, Steven Mhando, Dr. Vedasto Kyaruzi, Sheikh Hassan bin Ameir, Zuberi Mtemvu kuwataja wachache?
Unakumbuka muda wakati alipotunukiwa kulikuwa na hali gani ya kisiasa? Nani alikuwa madarakani?
Kwa nini kitabu cha Abdul Sykes kimependwa kiasi hiki na kusababisha uchukuliwe uamuzi wa kuandika historià ya Mwalimu Nyerere na kuandika upya historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika?
Ni kitabu chako na una uhuru wa kukieleza unavyoweza. Ni maoni yako ambayo si lazima ya sahihi au makosa, tunayaheshimu

Hebu tuanzie hapa maana yapo mengi mazuri ya kujadili

 
Tangu mkutano wa Arnatouglo hadi 1961, Abdul alikuwa na ushiriki gani wa siasa za Tanzania? Kwanini alotoweka katika uongozi baada ya muda huo
Hassan Upeka kajaliwa Umri? Kwa maana nzuri tu ya kuelewaUnakumbuka Africa Now? Unamkumbuka mtu anayeitwa Abdulrahman Babu? Unakumbuka muda wakati alipotunukiwa kulikuwa na hali gani ya kisiasa? Nani alikuwa madarakani?
Ni kitabu chako na una uhuru wa kukieleza unavyoweza. Ni maoni yako ambayo si lazima ya sahihi au makosa, tunayaheshimu

Hebu tuanzie hapa maana yapo mengi mazuri ya kujadili

Nguruvi 3,
Umekosea kuliuliza swali la ushiriki wa Abdul.

Abdul hakuwa mtu wa kupanda jukwaani.

Lakini Abdul nimeambiwa alikuwa katika mikutano ya TANU ile ya mwanzo kabisa pale Mnazi Mmoja akionekana nyuma kabisa akichukua hotuba Nyerere akizungumza katika hati mkato (short hand) verbatim yaani neno kwa neno.

Katika mambo yanayonisikitisha hadi leo ni kule kutopewa idhini ya kusoma shajara za Abdul Sykes ambazo nimeziona kwa jicho langu.

Bila shaka kuna mengi kaandika katika zile "interesting times."

Abdul hakuwa na nafasi yoyote katika chama kuanzia 1954 baada ya kuundwa kwa TANU.

Juu ya hili mikutano yote ya kupanga mikakati ya kusukuma mambo ilikuwa ikifanyika nyumbani kwake na "retreats," zote.

Nadhani unakifahamu kisa cha kudhaniwa Nyerere kalishwa sumu nyumbani kwa Abdul Sykes.

Hii ilikuwa nyumbani kwa Abdul katika moja ya hizi "retreats."

Sasa jiulize kwa nini mikutano na hizi "retreats," zifanyike kwa Abdul ilhali viongozi wa TANU wapo?

Kipi kilifanya TANU imtwishe Abdul mzigo huu?

Ndiyo maana nyaraka za TANU za wakati ule wanazo akina Sykes na ndiyo hizi nilizotumia kuandika historia ya TANU.

Abdul hakutoweka.

Mfuko wake ulikuwa wazi kwa TANU siku zote na wengi katika viongozi wa TANU wa wakati ule wanaijua ile ofisi yake ndogo iliyokuwa nyumbani kwake Mtaa wa Stanley na Sikukuu.

Mwalimu Nyerere kaitumia sana ofisi hii katika siku za mwanzo za TANU.

Amesema mwenye kusema tena huyu ni Mzungu akiitwa Staley.

Huyu alikuwa Engineer Dar es Salaam Municipal Council, "Nikienda kula chakula cha mchana kwa Abdul na tukifika kwake nakuta watu wengi wakimsubiri nje na kila aliyetoka ndani ya ofisi ile alikuwa na tabasamu usoni."

Ni viongozi mfano wa Abdul ndiyo waliifanya TANU ipendeze na Nyerere kama rafiki wa Abdul na yeye apendwe.

Abdulrahman Babu tumefahamiana London nilijulishwa kwake na Ahmed Rajab aliyekuwa mhariri wa Africa Analysis.

Ahmed akiandika na Africa Now gazeti la Peter Enahoro.

Siku hizo mimi nikiandika na Africa Events mhariri wake marehemu Mohamed Mlamali Adam.

Hassan Upeka kaingia TANU 1956 baada ya kumaliza Tabora School na moja kwa moja akatiwa kwenye ukachero.

Upeka mie ni kaka yangu na vilevile ni mzawa wa Dar es Salaam kama mie.

Anaijua historia ya TANU vizuri kabisa.

Yeye na Ditopile ndiyo walioanzisha Maktaba ya CCM Dodoma na ndiyo walioniwezesha mimi kuingia katika maktaba ile na kufanya utafiti.

Hayo mengine sina majibu naomba unisaidie kunifahamisha.

Sisi hawa ni baba zetu na ndiyo maana tunakuelezeni nyinyi historia hii kwani hamuijui na wala hamlaumiwi kwani hamkuwepo sasa mtajuaje si lazima tukufahamisheni?

Leo kuna bango nyumbani kwa Mzee Mwinjuma Mwinyikambi linatangaza kuwa TANU iliasisiwa ndani ya nyumba ile.

Ati TANU iliasisiwa nyumbani kwa Mzee Mwinjuma Mwinyikambi Mwananyamala ilhali Nyerere kapokelewa na Abdul Sykes na mipango ya kuunda TANU mara ya kwanza masikioni kwake kaisikia nyumbani kwa Abdul Kariakoo.

Mzee Mwinjuma ni babu yangu na mkewe Bi. Fatuma ni bibi yangu.

Mzee Mwinjuma akishakausha nazi zake anazipeleka Kariakoo sokoni na pale Market Master ni Abdul Sykes na Collector wa soko Sharif Abdallah Attas na ni kupitia kwa Abdul ndiyo Nyerere akamjua Mzee Mwinjuma na wazee wengine wa Dar es Salaam.

Shariff Attas akimjua vyema Mwalimu Nyerere na ni burdani ya pekee kumsikiliza akikumbuka siku zile wakiunda TANU.

Nyerere hakumjua Mzee Mwinjuma kwa kuwa aliundanae TANU.
 
"Mohamed Said, post: 33690121, member: 12431"]Abdul hakuwa mtu wa kupanda jukwaani.Lakini Abdul nimeambiwa alikuwa katika mikutano ya TANU ile ya mwanzo kabisa pale Mnazi Mmoja akionekana nyuma kabisa akichukua hotuba Nyerere akizungumza katika hati mkato (short hand) verbatim yaani neno kwa neno.
Na bila shaka kwa rejea ya bandiko#191 aya ya kwanza, utakuwa umeambiwa pia kuwa Abdul Sykes na Wilbard Kleruu walipata matatizo walipotaka kuandika historia ya TANU
Katika mambo yanayonisikitisha hadi leo ni kule kutopewa idhini ya kusoma shajara za Abdul Sykes ambazo nimeziona kwa jicho langu.
Hukuziona nyaraka na bado unatueleza historia
Abdul hakuwa na nafasi yoyote katika chama kuanzia 1954 baada ya kuundwa kwa TANU.
Na alitaka kuandika historia ya TANU.
Ndiyo maana nyaraka za TANU za wakati ule wanazo akina Sykes na ndiyo hizi nilizotumia kuandika historia ya TANU.
Na unasikitika kutoona nyaraka za Abdul! lakini umetumia nyaraka kuandika historia
Abdul hakutoweka.
Umesema hakuwa na nafasi ndani ya chama. Kutoweka si kimaumbile bali katika siasa za nchi.
Ni viongozi mfano wa Abdul ndiyo waliifanya TANU ipendeze na Nyerere kama rafiki wa Abdul na yeye apendwe.
Well, bila nafasi ndani ya TANU, aliweza kutenda. Kwamba bila Abdul, Nyerere angekuwa na wakati mgumu saana. Kwamba Nyerere alisafiria nyota ya Abdul
Abdulrahman Babu tumefahamiana London nilijulishwa kwake na Ahmed Rajab aliyekuwa mhariri wa Africa Analysis.Ahmed akiandika na Africa Now gazeti la Peter Enahoro.
Siku hizo mimi nikiandika na Africa Events mhariri wake marehemu Mohamed Mlamali Adam.
Nimesoma magazeti ya Africa Events na Africa Now. Nimemleta Abdulrahman Babu kwasababu alikuwa na makala zake kuhusu maendeleo ya Africa, na picha yake katika makala ilikuwa na 'sweta'' kama nitakuwa na kumbu kumbu sawa.

Magazeti hayo mwanzo nilidhani ni ya Nigeria kwasababu yalikuwa na habari nyingi za akina Murtala Mohamed, Obasanjo, Alhaji Othmani Shehu Shagari n.k.
Ni sehemu nzuri sana ya kupata ''coup de tat' zilizokuwa zinafanyika Nigeria

Hata hivyo, magazeti hayo yalikuwa yanasema sana Ujamaa wa Nyerere.
Moja ya habari nilizosoma zilihusu ujenzi wa Uwanja wa ndege wa Termina 2
Kwamba, walisema Mwl hakuwa a haja ya kujenga uwanja mkubwa akiwa hana ndege
Pesa hizo zingetumika kuendeleza mabonde ya mpunga ingalikuwa bora zaidi

Makala hizo ziliendelea kuudhi viongozi wakati huo wa chama kushika hatamu.
ndipo yalipopigwa marufuku, wengine tuliyasoma kwa kupitia ''wazee' waliokuwa na access na sehemu nyingine kama Nairobi

Hoja yangu hapa ni rahisi, magazeti hayakupigwa marufuku kwasababu ya makala zako
Kama ilitokea basi ilikuwa ni katika ujumla ule ule wa kupiga marufuku
Hivyo basi unaposema makala zako ndizo chanzo, si kweli, ni kupotosha na kutafuta ''credit''
Hassan Upeka kaingia TANU 1956 baada ya kumaliza Tabora School na moja kwa moja akatiwa kwenye ukachero.
Nimekuuliza kama ana umri kwa maana ya kama bado tupo naye. Katika bandiko 191 umesema naye alizuiliwa kuandika historia.
Hakuna mahali umeweka ushahidi wa maneno yake au nyaraka za kuthibitisha hilo.
Tunaweza kukubaliana nawe kwani huenda umeambiwa
Ati TANU iliasisiwa nyumbani kwa Mzee Mwinjuma Mwinyikambi Mwananyamala ilhali Nyerere kapokelewa na Abdul Sykes na mipango ya kuunda TANU mara ya kwanza masikioni kwake kaisikia nyumbani kwa Abdul Kariakoo.
Kudogosha ndiko huku.
Mwalimu alikuja Dar kikazi. Kabla ya hapo (1948) alikuja kisiasa. Hapa ni katika jitihada za kuonyesha mwenye TANU ni Abdul. Sina kumbu kumbu nzuri, hivi mkutano wa Anatoglo ulifanyika lini?
Mzee Mwinjuma akishakausha nazi zake anazipeleka Kariakoo sokoni na pale Market Master ni Abdul Sykes na Collector wa soko Sharif Abdallah Attas na ni kupitia kwa Abdul ndiyo Nyerere akamjua Mzee Mwinjuma na wazee wengine wa Dar es Salaam.

Shariff Attas akimjua vyema Mwalimu Nyerere na ni burdani ya pekee kumsikiliza akikumbuka siku zile wakiunda TANU.

Nyerere hakumjua Mzee Mwinjuma kwa kuwa aliundanae TANU
.
Nimepotea njia
 
Na bila shaka kwa rejea ya bandiko#191 aya ya kwanza, utakuwa umeambiwa pia kuwa Abdul Sykes na Wilbard Kleruu walipata matatizo walipotaka kuandika historia ya TANUHukuziona nyaraka na bado unatueleza historia
Na alitaka kuandika historia ya TANU.Na unasikitika kutoona nyaraka za Abdul! lakini umetumia nyaraka kuandika historia
Umesema hakuwa na nafasi ndani ya chama. Kutoweka si kimaumbile bali katika siasa za nchi. Well, bila nafasi ndani ya TANU, aliweza kutenda. Kwamba bila Abdul, Nyerere angekuwa na wakati mgumu saana. Kwamba Nyerere alisafiria nyota ya Abdul Nimesoma magazeti ya Africa Events na Africa Now. Nimemleta Abdulrahman Babu kwasababu alikuwa na makala zake kuhusu maendeleo ya Africa, na picha yake katika makala ilikuwa na 'sweta'' kama nitakuwa na kumbu kumbu sawa.

Magazeti hayo mwanzo nilidhani ni ya Nigeria kwasababu yalikuwa na habari nyingi za akina Murtala Mohamed, Obasanjo, Alhaji Othmani Shehu Shagari n.k.
Ni sehemu nzuri sana ya kupata ''coup de tat' zilizokuwa zinafanyika Nigeria

Hata hivyo, magazeti hayo yalikuwa yanasema sana Ujamaa wa Nyerere.
Moja ya habari nilizosoma zilihusu ujenzi wa Uwanja wa ndege wa Termina 2
Kwamba, walisema Mwl hakuwa a haja ya kujenga uwanja mkubwa akiwa hana ndege
Pesa hizo zingetumika kuendeleza mabonde ya mpunga ingalikuwa bora zaidi

Makala hizo ziliendelea kuudhi viongozi wakati huo wa chama kushika hatamu.
ndipo yalipopigwa marufuku, wengine tuliyasoma kwa kupitia ''wazee' waliokuwa na access na sehemu nyingine kama Nairobi

Hoja yangu hapa ni rahisi, magazeti hayakupigwa marufuku kwasababu ya makala zako
Kama ilitokea basi ilikuwa ni katika ujumla ule ule wa kupiga marufuku
Hivyo basi unaposema makala zako ndizo chanzo, si kweli, ni kupotosha na kutafuta ''credit''
Nimekuuliza kama ana umri kwa maana ya kama bado tupo naye. Katika bandiko 191 umesema naye alizuiliwa kuandika historia.
Hakuna mahali umeweka ushahidi wa maneno yake au nyaraka za kuthibitisha hilo.
Tunaweza kukubaliana nawe kwani huenda umeambiwa Kudogosha ndiko huku.
Mwalimu alikuja Dar kikazi. Kabla ya hapo (1948) alikuja kisiasa. Hapa ni katika jitihada za kuonyesha mwenye TANU ni Abdul. Sina kumbu kumbu nzuri, hivi mkutano wa Anatoglo ulifanyika lini? Nimepotea njia
Nguruvi3,
Mimi sina tatizo na vipi unaichukulia historia ya TANU.

Kila siku nakuambia unaweza ukaikataa na wala si tabu kwangu.

Chuo Cha CCM Kivukoni wameandika historia hii na wala Abdul hakutajwa popote ila kwenye orodha ya watu 17 walioasisi TANU.

Hakuna aliyepelekwa polisi.
Maisha yameendelea kama kawaida.
 
Nguruvi3,
Mimi sina tatizo na vipi unaichukulia historia ya TANU.

Kila siku nakuambia unaweza ukaikataa na wala si tabu kwangu.

Chuo Cha CCM Kivukoni wameandika historia hii na wala Abdul hakutajwa popote ila kwenye orodha ya watu 17 walioasisi TANU.

Hakuna aliyepelekwa polisi.
Maisha yameendelea kama kawaida.

The James Bond Years.

Rais Mwinyi miaka hii akiandamwa na Pastoral Letters kutoka Tanzania Episcopal Conference (TEC)na mashambulizi kutoka kwa Reverend Mtikila.

Gazeti la serikali na gazeti la chama chake mwenyewe yanamshambulia Mwenyekiti na Rais wake.

Mwinyi akawa hana wa kumtetea na akajikuta katika hali ngumu sana.

Mhariri wa Africa Events alikuwa marehemu Ahmed Saleh Yahya.

Tukinywa chai na sambusa hoteli moja katikati ya mji Dar es Salaam aliponialika akaniambia, ''Mohamed hebu msaidie mzee wetu.''

Toka awali nilipopata mwaliko nilijua si bure kuna jambo.

Kuna zigo la misumari ya ncha kali nataka kubebeshwa

Waamerika wana msemo, "There is no free lunch in America."

Nami naamini tunaweza kuwa na msemo wetu,"Hakuna chai na sambusa za bure Dar es Salaam."

Nikampa makala na yeye akaipamba makala yangu na cover hiyo hapo chini.

Nilicheka hadi machozi yakanimwagika.

Rais Mwinyi kamgeuza "caricuture."

Mwinyi meli yake imepigwa ''torpedo,'' na inawaka moto na inapigwa na dhoruba kali.

Inaelekea atazama na chombo.

Mambo yanakwenda ki-James Bond napigiwa simu nakutana na mtu ananikabidhi bahasha.

Special Correspondent huyo.

Rafiki zangu wananishinikiza niandike kitabu wanasema ati nina mengi sana.

Sijui.

1575749939206.png


---​
 
Bwana Mohammed Saidi. Kisiwa cha Zanzibar kina historia ndefu, waandishi wengi wameandika historia ya kisiwa hichi, hata hivyo kuna mambo mengi watoto wetu hawayajuwi kwa vile hayasomeshwi au kupewa nafasi katika vyombo vyetu vya habari.

Watoto wetu husomeshwa habari za Mapinduzi, jambo ambalo limewafanya watoto na vijana wetu wakuwe na kasumba ya kutokujuwa vizuri historia ya nchi yetu. Siasa imechangia sana kupotosha historia ya Visiwa hivi.

Wanasiasa wameitumia historia ya Visiwa hivi kwa manufaa yao na kuzidisha chuki, na kutoelewana miongoni mwa raia wa kisiwa hichi. Uwafrika, Uwarabu, Utumwa ndio nyenzo na Turufu za watanganyika na zaidi wakristo kwa maslahi ya siasa. Pamoja na kuchakaa kwa nyenzo hizo bado viongozi wa naendelea nazo.

Wao ukiyaanika matendo walioututendea kuanzia 1964 hadi sasa huwa wanashindwa kuvumilia. Gazeti la DIRA la Marehemu Nabwa walilipiga marufuku kwa sababu eti lilikua likitia chuki nchini.

Mengi tukiyapanga na kuyaeleza tuliotendewa Wazanzibari na ndugu zetu wa Tanganyika utastaajabu. Wametuuwa bila ya sababu na wauwaji hao wametokea huko Tanganyika. Wametuchoma katika matanuri ya mbata bila ya sababu. Wametupiga risasi msikitini tukiwa tuna swali. Wamechukuwa watoto zetu wanawari na kuwaowa kwa nguvu bila ya ridhaa za wazee.

Wamewabaka nakuwaingilia kwa nguvu wazazi mbele ya mabinti zao huko pemba, wamekamata watu na kuwapeleka kwenye chemba za mateso (kwa Mandera) kisha kuwauwa. Mashekhe zetu wamewakamata na kuwapeleka ndani ya magereza ya Tanganyika hadi leo na wakawatendea unyama usioweza kuelezeka.

Wamerudia tena mauaji kwa mara ya tatu hapa Zanzibar Machafuko ya June ya miaka ya Ukoloni wameuwa watu 61 wengi wao ni Waarabu kama si wote. Wamerudia tena 1964,na wakanogewa tenan 2001.

Wametufanyia unyama watanganyika,unyama usioweza kuelezea. Je, wataweza kuiandika hustoria ya kweli ya nchi hii?.
 
Wanasiasa wameitumia historia ya Visiwa hivi kwa manufaa yao na kuzidisha chuki, na kutoelewana miongoni mwa raia wa kisiwa hichi. Uwafrika, Uwarabu, Utumwa ndio nyenzo na Turufu za watanganyika na zaidi wakristo kwa maslahi ya siasa. Pamoja na kuchakaa kwa nyenzo hizo bado viongozi wa naendelea nazo.

Wao ukiyaanika matendo walioututendea kuanzia 1964 hadi sasa huwa wanashindwa kuvumilia. Gazeti la DIRA la Marehemu Nabwa walilipiga marufuku kwa sababu eti lilikua likitia chuki nchini.
Wakisema wao haya ,ni sawia,hawatii chuki nchini,lakini wakisemwa wao wayatendayo hivi kila uchao ni kosa la jinai na unaweza kuozea jela.
1575899025572.png
1463833148482.jpg
 
Leo tarehe 12 January ni Sikukuu ya Mapinduzi ya Zanzibar, nachukua nafasi hii kuwatakia nyote heri na fanaka za Mapinduzi na kukutakieni maadhimisho mema ya sherehe ya kumbukumbu ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar kwa watakao shereheka kwa wale wenye kumbukumbu njema, na kwa vile Mapinduzi Matukufu yale pia yaliandamana na umwagaji damu, natoa pole kwa wenye kumbukumbu chungu.
P
 
Back
Top Bottom