Pre GE2025 Kwanini kelele kwa Lissu na sio kwa Wenje?

Pre GE2025 Kwanini kelele kwa Lissu na sio kwa Wenje?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Hahaha hakuna asiyetaka agombee, wafuasi wa Lisu ndio wanataka penalt ya bure na hawataki golikipa golini.

Tunajisahau kama chama cha demokrasia, halafu tunataka kukiuka kanuni zetu wenyewe. Hakuna anayemfananisha na Nyerere. Nyerere yupi maana siku hizi wako wengi, kama yule anayeitwa baba wa taifa hana mfano wa kuigwa.

Alipewa nchi na wingereza, hakugombea, na alijipa uwenyekiti wa chama na urais hakuchaguliwa mpaka anaondoka.

Mbowe anachaguliwa kila uchaguzi unapofika, akiwa ni mgombea naye anastahili kuwa na base yake na anatakiwa afanye kampeni.

Lakini wafuasi wa Lisu hawataki mtu mwingine yeyote agombee na Lisu. Wanataka Lisu ashindanishwe na Lisu tu, nasiyo mtu mwingine yeyote, hapo mnakuwa hama tofauti na CCM, ambaye Mwenyekiti wake anapitishwa tu akiisha kuwa Rais.

Sisi tunaolilia haki kila siku tutataka Lisu wetu apitishwe bila kupingwa. Huyo Lisu ndiye mwenye haki pekee ndani ya Chadema, demokrasia mnaitupa wapi na kwanini?

Mnamlemaza mgombea wenu, na mnasahau misingi mnayoipigania kila siku.

Hivi wanaolalamika ni wafuasi wa Lissu au Mbowe. Maana tangu Lissu achakue fomu kelele zimekuwa nyingi dhidi yake. Si ulimsikia yule mwenyekiti wa CHADEMA Mbeya.
 
Gentleman,
kwanza kabisa Lisu has no numbers to beat Mbowe whether the elections will be conducted this year or next year.

Lisu has no such muscles.

Lakini ile muhimu zaidi,
Lisu anajadiliwa sana kwasababu ya ile tamaa na uchu wa madaraka ako nayo.

Lisu anajadiliwa sana kwasababu ile makelele na mdomo ako nayo.


Lisu anajadiliwa sana kwasababu ya ile political blindness ako nayo, hana mpango kabisa wa kuwin the support of members who can vote for him.

Can you at least say,
katika kanda 10, lisu anaweza kupata support ya kanda zaidi ya moja kweli?

kua muungwana tu 🐒

Naomba nikuulize swali. Kati ya Mbowe na Lissu nani ana uchu wa madaraka.
 
Hivi wanaolalamika ni wafuasi wa Lissu au Mbowe. Maana tangu Lissu achakue fomu kelele zimekuwa nyingi dhidi yake. Si ulimsikia yule mwenyekiti wa CHADEMA Mbeya.
Wengi wa Lisu wanataka apite bila kupingwa, yule wa Mbeya wanamuona ni MJINGA kwasababu anataka Mbowe agombee.

Campaign ni haki ya kila mgombea, lazima ujenge ushawishi ili kupigiwa kura, na wote wana wafuasi.
 
Nadhani machawa wa Mbowe ndio wameanza haya malalamiko zamani Sana kabla hata Lissu hajatangaza kugombea uenyekiti. Kuna kipindi Lema alisema wazi kwamba Lissu alishatangaza hatagombea uenyekiti hivyo aheshimu Hadi yake.
Tunapotaka Demokrasia, tuikubali ikija na kwetu. Tusivunje haki za wengine ili kumlinda mpendwa wetu.
 
Wengi wa Lisu wanataka apite bila kupingwa, yule wa Mbeya wanamuona ni MJINGA kwasababu anataka Mbowe agombee.

Campaign ni haki ya kila mgombea, lazima ujenge ushawishi ili kupigiwa kura, na wote wana wafuasi.

Kuna kitu unakisahau. Mimi napinga Mbowe kugombea kwasababu alishatangaza kwamba angestaafu mwaka 2023, hivyo kumfanya makamu wake kuingia ulingoni kugombea nafasi hiyo. Hivyo tunapinga yeye kugombea Tena maana alishatangaza kustaafu.
 
Naomba nikuulize swali. Kati ya Mbowe na Lissu nani ana uchu wa madaraka.
Ni lisu,
kwasasababu wewe ni mtu wa aina gani asubuhi utangaze kugombea umakamu mwenyekiti, tena kwa mbwembwe sana ukiapa kamwe huwezi kuthubutu kugombea nafasi anayogombea Mbowe kwasababu mmetoka mbali na mnaheshimiana sana,

halafu jioni,
unakana maneno yako unaamua kutangaza kugombea uenyekiti kamili. Dah, hiki ni kiwango cha juu sana cha uchu na tamaa ya madaraka gentleman 🐒
 
Tunapotaka Demokrasia, tuikubali ikija na kwetu. Tusivunje haki za wengine ili kumlinda mpendwa wetu.

Hatuvunji Demokrasia mkuu. Tunachotaka ni Lissu atendewe haki ndani ya chama dhidi ya influence ya mwenyekiti Mbowe.
 
Ni lisu,
kwasasababu wewe ni mtu wa aina gani asubuhi utangaze kugombea umakamu mwenyekiti, tena kwa mbwembwe sana ukiapa kamwe huwezi kuthubutu kugombea nafasi anayogombea Mbowe kwasababu mmetoka mbali na mnaheshimiana sana,

halafu jioni,
unakana maneno yako unaamua kutangaza kugombea uenyekiti kamili. Dah, hiki ni kiwango cha juu sana cha uchu na tamaa ya madaraka gentleman 🐒

Kwa hivyo Lissu kugombea uenyekiti ni uroho wa madaraka. Lakini Mbowe kuka kwenye uenyekiti miaka 22 sio uroho wa madaraka. Kuwa mkweli kabisa. Mroho ni yule asiyetaka kutoka kwenye kitu baada ya kukaa kwa muda mrefu.
 
Nilichogundua chadema ina tabia zile zile za unafiki wa CCM. Yaani madhaifu ya wazi wanaogopa kusema ili kulinda vyeo vyao ndani ya chama. Ila siku Mbowe aking'atuka utasikia wakimsema na kumlaumu..... tabia zile zile za CCM.

Kwa staili hii tunadaije demokrasia kama sisi wenyewe hatuiheshimu. Usishangae wakaibuka watu wakasema fomu iwe moja tu au Lissu avuliwe uanachama.

Mbowe bado ana ushawishi hata asipokua mwenyekiti na licha ya kwamba namsupport Lissu ila I'm sure Mbowe ana wajumbe wengi zaidi sababu hakuna mwanasiasa yupo chadema bila influence ya Mbowe.

Kwahiyo angeacha tu demokrasia ichukue mkondo wake I believe anaweza kushinda ingawa kunaweza tokea suprise akaangushwa na inaweza leta damage kwa reputation yake na hata akishinda itaonekana ametumia incumbency kubakia madarakani so either way its a lose-lose situation.

Busara ni kwamba apishe ili awaachie Lissu, Heche, Mnyika etc wagombee uenyekiti kwa open primaries kabisa na hatimaye apatikane mwenyekiti mmoja wa kutuvusha 2025.

In a worst case scenario, Mbowe akigombea na kushinda basi Lissu ateuliwe ukatibu mkuu maana Mnyika amepwaya sana bora arudi kwenye kurugenzi ya Mawasiliano aliyokua anaimudu vizuri zaidi na ambayo Mrema ameprove kuwa failure.
Mbowe ikiwa atagombea kama nilivyodokezwa kuwa itaita press yake soon, itakuwa ni aibu kubwa sana Kwa kushinda kutambuw alama za nyakati.

Ingefaa apumzike wakati Bado anaheshima kubwa.

Vinginevyo cdm itapoteza heshima na itapasuka hakuna namba.
Mwisho...Ufike wakati tuukubali uiweli
 
Mi sidhani kama hiyo ndiyo tatizo, na sidhani kama Mbowe kamzuia mtu kugombea hiyo nafasi, mi naona wengi wanamtaka Lisu, na wanataka awe mwenyekiti wa chadema, lakini hao hao hawataki demokrasia.

Ile nafasi inagombewa, na mgombea siyo Lisu pekee, wapo wengine wanania ya kugombea pia. Na mwenyekiti aliyepo, asiporwe haki yake ya kugombea eti tu kwa sababu amekuwa mwenyekiti kwa muda mrefu.

Kila siku tunapinga utaratibu wa kupita bila kupingwa, tunataka uchaguzi na kura ndiyo iamue mshindi, lakini kuna watu tayari wanamuaona Lisu ndiye mshindi hata kabla ya uchaguzi, demokrasia mmeiacha wapi?

Kumpigia kampeni mgombea siyo tatizo, lakini kuna wanaoenda mbali na kusema eti Mbowe akigombea huko ni kung'ang'ania madaraka!?

Yani nafasi ya demokrasia haitakiwi anapokuwa ni Lisu, na ni lazima ashinde Lisu, kwanini?

Mbowe haachii kiti, Mbowe ashindanishwe na Lisu ili kuleta usawa na haki ndani ya CHADEMA. Kama mnataka aachie, kwanini tunawapinga CCM wanaosema WATANZANIA WALIISHA AMUA S.S.HASSAN MITANO TENA?

Je tukubali Tanzania ni ya CCM peke yao, kaiiba kura ni sawa, wakijitangaza washindi hata waliposhindwa ni sawa?

Tunataka demokrasia lakini hatuitaki inapokuja kwa mgombea wetu wenyewe?

Yani tunapotaka vyetu ,tuko tayari kuminya haki za wengine, ni sawa?

Lisu is known, sijui fear of unknown inatoka wapi?

Lisu ni makamu mwenyekiti chadema, anayoyalalamikia anashindwaje kuya address ndani ya chama?

Watu tunataka sympathy kwa mgombea wetu, huo ni udhaifu ninao uona mimi kitaifa, utahurumiwa ndani ya CHADEMA, Ok Mbowe hata gombea utashinda, ikifika general election tutaomba SS.Hassan amwachie T.Lisu kwa sababu CCM imekuwa madarakani muda mrefu?

Au tutawaambia wananchi CCM wanaogopa T.Lisu asitawale kwasababu they have fear of unknown?

Agombee, aache kuomba huruma ya wananchi na wanachama wa chadema.
Mkuu umena vizuuuuuri 👏👏👏👍🤝
 
Mbowe ikiwa atagombea kama nilivyodokezwa kuwa itaita press yake soon, itakuwa ni aibu kubwa sana Kwa kushinda kutambuw alama za nyakati.

Ingefaa apumzike wakati Bado anaheshima kubwa.

Vinginevyo cdm itapoteza heshima na itapasuka hakuna namba.
Mwisho...Ufike wakati tuukubali uiweli
Mkuu yatakuwa yale yale ya CUF, UDP, NCCR na TLP.
 
Habari wanajamii.

Tangu Lissu atangaze Nia ya kugombea uenyekiti kumetokea kelele za kila aina. Mara ni kirusi ndani ya CHADEMA, mara anafadhiliwa na Msigwa, mara anampango wa kuhamia CCM nk. Kila mtu anasema la kwake.

Nikawaza, Kwanini kelele zimekuwa nyingi kwa Lissu baada ya tangazo lake la kugombea uenyekiti tofauti na Wenje alipotangaza kugombea umakamu mwenyekiti wa CHADEMA.

Kumbuka ya kwamba Wenje alitangaza kuitaka nafasi aliokuwa nayo Lissu. Lakini hakuna aliyemshukia Wenje kwamba ni msaliti au kirusi ndani ya CHADEMA Kwa kutaka nafasi ya anayoshilia Lissu.

Hii sintofahamu inaonesha labda watu walidharau tangazo la Wenje au walimwona ni dhaifu kupambana na Lissu kwenye umakamu Mwenyekiti. Hivyo wakampuuzia. Ila kwa Lissu wamepiga mayowe labda kwa sababu Lissu ana ushawishi ndani ya CHADEMA na anaweza kushinda nafasi hivyo au Lissu anawanachama wengi wanaomuunga mkono kiasi kwamba akifanyiwa figisu anaweza kuhama na kundi kubwa Kama kipindi kile Cha akina Zitto Kabwe na wenzake akina Prof Mkumbo.

Muda utasema na kutoa majibu.
Sasa wewe unatuletea kelele za uvccm ili tufanyeje?
 
Nilichogundua chadema ina tabia zile zile za unafiki wa CCM. Yaani madhaifu ya wazi wanaogopa kusema ili kulinda vyeo vyao ndani ya chama. Ila siku Mbowe aking'atuka utasikia wakimsema na kumlaumu..... tabia zile zile za CCM.

Kwa staili hii tunadaije demokrasia kama sisi wenyewe hatuiheshimu. Usishangae wakaibuka watu wakasema fomu iwe moja tu au Lissu avuliwe uanachama.

Mbowe bado ana ushawishi hata asipokua mwenyekiti na licha ya kwamba namsupport Lissu ila I'm sure Mbowe ana wajumbe wengi zaidi sababu hakuna mwanasiasa yupo chadema bila influence ya Mbowe.

Kwahiyo angeacha tu demokrasia ichukue mkondo wake I believe anaweza kushinda ingawa kunaweza tokea suprise akaangushwa na inaweza leta damage kwa reputation yake na hata akishinda itaonekana ametumia incumbency kubakia madarakani so either way its a lose-lose situation.

Busara ni kwamba apishe ili awaachie Lissu, Heche, Mnyika etc wagombee uenyekiti kwa open primaries kabisa na hatimaye apatikane mwenyekiti mmoja wa kutuvusha 2025.

In a worst case scenario, Mbowe akigombea na kushinda basi Lissu ateuliwe ukatibu mkuu maana Mnyika amepwaya sana bora arudi kwenye kurugenzi ya Mawasiliano aliyokua anaimudu vizuri zaidi na ambayo Mrema ameprove kuwa failure.
Mkuu, unasahau wana ccm na cdm ni watanzania.
Wanasimba na wanayanga ni watanzania.

Hizo ni tabia na asili yao. Hivyo usitarajie sana utofauti.
 
Habari wanajamii.

Tangu Lissu atangaze Nia ya kugombea uenyekiti kumetokea kelele za kila aina. Mara ni kirusi ndani ya CHADEMA, mara anafadhiliwa na Msigwa, mara anampango wa kuhamia CCM nk. Kila mtu anasema la kwake.

Nikawaza, Kwanini kelele zimekuwa nyingi kwa Lissu baada ya tangazo lake la kugombea uenyekiti tofauti na Wenje alipotangaza kugombea umakamu mwenyekiti wa CHADEMA.

Kumbuka ya kwamba Wenje alitangaza kuitaka nafasi aliokuwa nayo Lissu. Lakini hakuna aliyemshukia Wenje kwamba ni msaliti au kirusi ndani ya CHADEMA Kwa kutaka nafasi ya anayoshilia Lissu.

Hii sintofahamu inaonesha labda watu walidharau tangazo la Wenje au walimwona ni dhaifu kupambana na Lissu kwenye umakamu Mwenyekiti. Hivyo wakampuuzia. Ila kwa Lissu wamepiga mayowe labda kwa sababu Lissu ana ushawishi ndani ya CHADEMA na anaweza kushinda nafasi hivyo au Lissu anawanachama wengi wanaomuunga mkono kiasi kwamba akifanyiwa figisu anaweza kuhama na kundi kubwa Kama kipindi kile Cha akina Zitto Kabwe na wenzake akina Prof Mkumbo.

Muda utasema na kutoa majibu.
Mti wenye matunda.......
 
CCM ilishakufa, sema inashikiliwa na Dola.
Usemi wa wajinga huu,mtaendelea kutawaliwa na ccm hadi kiama ,mnakuwa chawa wa wajinga waliofeli elimu ya sekondari(Lema,Sugu,Wenje na Mzee Mbowe) ,mnatagemea hawa wajinga hawajui hata maane ya neno mkakati ndio wachukur nchi?
 
Back
Top Bottom