Kwanini kitabu cha Enoch kinapingwa vikali na Wanathiolojia?

Kwanini kitabu cha Enoch kinapingwa vikali na Wanathiolojia?

Wapendwa, msidanganyike. Enoki alikuwa na vitabu viwili. Cha kwanza, ni mile kilichohusika na majina ya malaika wote , ukiwa ni pomaja na wale majemadari 72 waliofukuzwa mbinguni. Kitabu hiki, ndicho kinachotumiwa na waganga, na hata wahubiri wa makanisa ya sasa katika kazi ya utoaji wa mapepo. Waganga Hawa, pia hutumia vitabu viwili vya mfalme sulemani alivyoviandika na kuvitumia katika mambo ya uuguzi. Kwa hivyo,kitabu cha Enock cha majina ya malaika, hakina faida yoyote kwa Mtu asiyekuwa na mambo ya uganga.wanaokitumia kitabu hiki, ni wale wanaotaka kutumia watu vipande, na kutibu kwa njia ya uganga. Sasa kama mkristo, unakatazwa kutafuta msaada kutoka kwa watu, viumbe vilivyoko mbinguni,(malaika), ya nini kuhangaika na kitabu chenye majina ya malaika?. Kitabu cha pili cha Enock ni kitabu kinachohabari zote za maisha na kazi aliyoifanya Bw. Yesu. Yaani vitabu vya Injili (Mathayo, Marko, Luka , na Yohana. Maelezo ni Yale yale , tofauti ni kuwa badala ya jina la Yesu imeandikwa "kiongozi wa watu".) Hivyo hakukuwa na sababu yoyote ya kuhangaika na kitabu cha Enock . Anayetaka kusoma kitabu cha pili cha Enock, asome Injili za mathato, Marko, Luka, na Yohana,.Achana na vitabu vya Enock vitakutenga na jina tamu, la Yesu maana wa Mungu Aishiye milele.
Duh dini zina vitu vingi tusivo vijua
 
Ni hv kwa kifupi tu huko nyuma kuna tukio kubwa sana lilitokea na hadi leo athari zake zinatawala maisha yetu.tukio hilo ni interaction kati ya binadamu na viumbe fulani wengine wa Mwenyezi Mungu(huwa tunawaita tu malaika hii inatupa upofu sana)walikuwa 200 wakiongozwa na mkuu wao Azazel waliposhuka ktk kilele cha mlima Hermon na kuigiza maumbile ya kibinadamu.kilichowaleta ni kutamani binadamu.walitaka kukaa nao,wawatawale,wazae nao,waanzishe empire yao tofauti na utaratibu waliopangiwa na Mungu.wakafanya hivyo.ikazaliwa offspring ya ajabu,majitu makubwa yenye nguvu za kutisha na akili za ajabu na roho za ajabu maana nusu binadamu nusu malaika.waliitwa nephilims,leo tunawaita titans(usifikiri hadithi ya kigiriki hii)!kutokana na hiyo offspring kuwa imbalance,ilileta vurugu kubwa duniani,na kama Mungu asingeingilia kati mbegu ya binadamu pure ingetoweka.hao malaika pamoja na hayo matoto yao ndio walifundisha binadamu mambo meengi ambayo leo yana sehemu kubwa ktk sayansi,elimu na tamaduni zetu hasa mashariki ya mbali,India na america.base yao kuu ilikuwa bara la Atlantis lililokuwepo katikati ya america na ulaya.kitendo hiki kilimchukiza Mungu mno akaamua kutuma gharika ya maji na kuteketeza dunia nzima pamoja na bara la Atlantis isipokuwa binadamu mmoja anaitwa Nuhu na watoto wake na baadhi ya wanyama ambao hawakuchafuliwa(nephilims walizaana hata na mijusi,kilichotoka hapo ni balaa).LAKINI kuna laana alitamka Mungu,kwamba roho za viumbe hao hataziangamiza,ataziacha na zitakuwa chanzo cha kila uovu duniani kwa umri wote wa dunia hadi mwisho ili viumbe wake wote wapate darasa how serious was this mistake!roho hizo ndizo zilimuongoza Nimrod kuijenga Babylon na kuanzisha idol worshiping na tamaduni za Atlantis zikaanza kurudi taratibu huku spidi yake ikivurugwa na elimu ya dini ya mitume na manabii wa Mungu.ilibidi utaratibu wa kuinteract na binadamu ili kutimiza lengo lao waufanye kwa siri,taratibu,miaka na miaka,wakiibadili dunia taratibu hadi mazingira yakiruhusu,roho hizi zikiwa ndani ya miili ya kibinadamu,zitaigeuza dunia nzima kuwa kama Atlantis!ndipo hapa vyama vya siri na dini zisizoeleweka vinaposhamiri underground.
Very useful hizi zipo lakini kumbe ni story ya kweli[emoji111] [emoji111]
 
Nilichojifunza katika kitabu cha Enoch ni juu ya origin ya mtu mweupe (kina eleza Mungu aliumba mtu mweusi ila mtu mweupe alitokana na malaika wenye tamaa i.e fallen angels waliokuwa wakiwaingilia kimwili binadamu).?

Mkuu kama ndivyo ulivyoelewa hivi, basi hukukielewa kitabu cha Enoch! Na pengine ni kwa sababu ya lugha!

Enoch alipozaliwa alikuwa ni mtu mwenye muonekano wa tofauti manaa hata ngozi yake ilikuwa inang'aa sana.

Sasa wakati wa enzi hizo, wana wa Mungu (malaika) waliwatamani wanawake wa kibinadamu. Moja wa malaika wao kiongozi alikuwa anaitwa Azazel na wakashuka wakawachumbia wana wa binadamu, wakaingia kwao wakazaa watoto. Hao watoto walikuwa wanaitwa Wanefil.

Hao kina Azazel wakawafundisha wana wa binadamu juu ya mambo mbali mbali ikiwa ni pamoja na kujipamba, kujipodoa na hata kutengeneza vioo vya kujiangalia. Walifanya machukizo mengi sana mbele za Mungu.

Basi hao wanefil wana wa hawa malaika walikuwa ni madubwana na walikuwa wamekuwa mzigo mkubwa mbele za jamii maaana walikula vyakula vyote vikaisha, wanyama, ng'ombe n.k.

Basi binadamu wakamlilia Mungu juu ya hao wanefil maana walikuwa wameilemea nchi. Sasa kwa matokeo hayo Mungu akaagiza kuwa kina Azazel na malika wengine wafungwe kwenye gereza huko kuzimu mpaka siku za mwisho, pia akawatupa hao wanefil huko kuzimu ndio wakawa majini au pepo wabaya unaowasikia sasa hivi.

Enoch ndiye aliyeitwa na Mungu mpaka mbinguni na wakati anaelekea huko mbinguni kuongea na Mungu nadhani alikuwa amefika kwenye mbingu ya tatu ndipo alipokutana na kina Azazel wakawa wanamsihi awaombee msahmaha kwa Mungu kutokana na matendo yao ili waachiliwe...

Basi kufika huko mbinguni, Enoch alipanda mpaka mbingu ya saba kuongea na Mungu juu ya mambo mbali mbali na ndipo Mungu akampa Enoch kazi ya kwenda kuwahukumu hao malaika wakosefu kina Azazel...

Kwa hiyo sio kweli kuwa Wanefil ndio walikuja kuwa watu weusi... Bali ndio walikuja kuwa majini!

Na hao wanefil ni madubwana makubwa kweli kweli. Yani Mnefil mmoja wanaigina kina Le Mutuz Watano hivi!
 
Mkuu kama ndivyo ulivyoelewa hivi, basi hukukielewa kitabu cha Enoch! Na pengine ni kwa sababu ya lugha!
Enoch alipozaliwa alikuwa ni mtu mwenye muonekano wa tofauti manaa hata ngozi yake ilikuwa inang'aa sana.
Sasa wakati wa enzi hizo, wana wa Mungu (malaika) waliwatamani wanawake wa kibinadamu. Moja wa malaika wao kiongozi alikuwa anaitwa Azazel na wakashuka wakawachumbia wana wa binadamu, wakaingia kwao wakazaa watoto. Hao watoto walikuwa wanaitwa Wanefil.
Hao kina Azazel wakawafundisha wana wa binadamu juu ya mambo mbali mbali ikiwa ni pamoja na kujipamba, kujipodoa na hata kutengeneza vioo vya kujiangalia. Walifanya machukizo mengi sana mbele za Mungu.
Basi hao wanefil wana wa hawa malaika walikuwa ni madubwana na walikuwa wamekuwa mzigo mkubwa mbele za jamii maaana walikula vyakula vyote vikaisha, wanyama, ng'ombe n.k.
Basi binadamu wakamlilia Mungu juu ya hao wanefil maana walikuwa wameilemea nchi.
Sasa kwa matokeo hayo Mungu akaagiza kuwa kina Azazel na malika wengine wafungwe kwenye gereza huko kuzimu mpaka siku za mwisho, pia akawatupa hao wanefil huko kuzimu ndio wakawa majini au pepo wabaya unaowasikia sasa hivi.
Enoch ndiye aliyeitwa na Mungu mpaka mbinguni na wakati anaelekea huko mbinguni kuongea na Mungu nadhani alikuwa amefika kwenye mbingu ya tatu ndipo alipokutana na kina Azazel wakawa wanamsihi awaombee msahmaha kwa Mungu kutokana na matendo yao ili waachiliwe...
Basi kufika huko mbinguni, Enoch alipanda mpaka mbingu ya saba kuongea na Mungu juu ya mambo mbali mbali na ndipo Mungu akampa Enoch kazi ya kwenda kuwahukumu hao malaika wakosefu kina Azazel...
Kwa hiyo sio kweli kuwa Wanefil ndio walikuja kuwa watu weusi... Bali ndio walikuja kuwa majini!
Na hao wanefil ni madubwana makubwa kweli kweli. Yani Mnefil mmoja wanaigina kina Le Mutuz Watano hivi!
haya maelezo yananikumbusha muvi fulani ivi nimeisahau jina
 
Hawa Wazungu Ni Devils. Tulifichwa,Tumefichwa,Tunafichwa Na Tutafichwa Vitu Vingi Sana Hasa Katika Dini Ya Ukristo Na Biblia. Sasa Mtu Anaanzaje Kuedit Biblia For Example?
That Simply Means Vile Ambavyo Ni Incosistent Au Against Their Interests Na Beliefs Basi Vitang'olewa Kwa Makusudi.
Iweje aving'oe kwenye Biblia halafu aviache kwenye Google wakati anajua huu ni ulimwengu wa utandawazi? Safari bado ipo.
 
Back
Top Bottom