1000 digits
JF-Expert Member
- Oct 16, 2012
- 7,201
- 9,529
Hii ni ndefu kwa hiyo kwa wale ambao kusoma para zaidi ya moja ni mtihani wala wasianze kuisoma.
Kuna wanachama na wafuasi wa CHADEMA pamoja na wapinzani wengine wa chama tawala ambao wanaamini kwa dhati kuwa ni wakati muafaka wa kubadilisha approach ya kuleta mabadiliko kwa sababu inayotumika sasa hivi kwa kiasi kikubwa haijafanikiwa.
Wanaamini hii ni kwa sababu Mbowe hawezi kumudu tactics ambazo ni aggresive na confrontational za wakati huo. Na chachu ya tactics hizo itatokana nje ya taratibu za kawaida kama tulivyoona vijana wa nchi jirani walivyotumia tik tok n.k.
Mambo haya yote hayaendani na hulka ya Mbowe ambayo kwa kiasi fulani ni ya traditional politics. Hawa walihitaji kiongozi ambae hana uvumilivu kama wao. Kiongozi ambae yuko tayari kwenda "mano a mano" na serikali bila kujali consequences.
Kwa mtazamo wao Lissu ndio kiongozi anaewafaa. Kwa sababu walimwona Mbowe kama kizingiti kwao wakatumia tactics za kumuaibisha na kumbeza ili aone hahitaji hizo fedheha ajitoe. Bahati mbaya kwao walikuwa hawajamsoma Mbowe vizuri. Hawakujua tactics hizo ndio zitamfanya aone chama chake kinataka kuwa hijacked kihuni.
Kitu vingine ambacho hawakuzingatia ni kuwa watanzania wengi hawapendi confrontation na hivyo kuna uwezekano mdogo wa wao kujitokeza kwa wingi kujiunga nao. Kingine ni kuwa tactic kama hizi hazileti matokeo ya kudumu na mara nyingi zinakuwa hijacked na wana siasa na kufa kifo cha kimya kimya. Tumeona Kenya. Tumeona Malawi. Hata Tunisia na Misri.
Ubaya mwingine ni kuwa ni vigumu ku control ili vurugu zisitawale. Picha za vijana wakiwa wana warushia mawe hazina tija.
Amandla...
Hivi unaamini kwamba Mbowe ndiye aliyeletaaridhiano yaliyopo au yaliyokuwepo Tanzania ?
Maridhiano ya Mbowe yamesaidia nini kama mwaka mmoja tu baadae Uchaguzi unageuka kuwa vita na wanaouawa ni Wanyonge wasiopesawa Rushwa za Bandari .
Wahenga walikua sio wajinga waliposema amani haiji ila kwa ncha ya Upanga.
Wewe kwa akili yako ndogo kama ya Mbowe unadhani kuna siku Tanzania itakua na katiba mpya ya kupewa mezani na Tume huru itakayowakosesha mamia ya wabunge na madiwani wa CCM nafasi kwenye karatasi za kura halali ?
Kama Mbowe hawezi kuachia chama chake ambacho kinategemea Ruzuku na hamasa ya wanachama pekee itakuaje kwa CCM kuachia nchi ya Tanganyika yenye Rasilimali nyingi kuliko zote Afrika mashariki na kusini kwa Afrika ?Yaani Mbowe anganganie KITI kisicho na benki kuu wala jeshi wala kusaini mamikataba ya madini ,ardhi n.k. iwe Serikali ya CCM ikubali kuachia hata mbunge mmoja aondokane na ulaji mkubwa na utajiri unaopatikana Fasta ndani ya serikali na bunge.?
Kwanza jiulize ni mbunge yupi au diwani yupi wa CCM aliyeko tayari kuachia nafasi yake kwa wapinzani?
Jibu ni hakuna na hatakuwepo milele,iwe ni kwa maridhiano au mawizihao?
Sasa siasa kama hizo unaridhiana nini kama sio ghiliba za Rushwa anazofanya Mbowe .?
Maridhiano yaliyoleta matokeo changa yalikua ni yale ya Maalim Seif na Serikali mpaka wakagawana nafsi ndani ya serikali . Hayakuja kwa kuendekeza Rushwa bali ni uadilifu unaopewa nuru na Mungu ili kuinua watu na kupigania taifa lao.
Kwenye hii Chadema ya Rushwa na Mbowe kamwe haitapata kibali mbele za Mungu na watu hawawezi hata kuandamana maana Hakuna roho ya haki inayotoka kwa Mungu ndani yao.
PAKIWA NA HAKI BILA RUSHWA KWA WANASIASA MUNGU ANAINUA WATU WENYE UWEZO WA KUANDAMANA NA HATA KUWATOA WAOVU MADARAKANI . Mbowe amepoteza kibali kwa Mungu hawezi kamwe kuwavuta WATU labda atumie fedha na yeye anafikiria wananchi wanamkubali kama enzi za Dr. Slaa alikua anatangulia mbele na mke wake wanapigwa mpaka anavunjwa mkono na watu wanasonga mbele . Ni kwa sababu ya Haki ya kiMungu iliyokua ndani yake. Sasa leo hii hata Samia kwa mfano na serikali yake tulivaliwa na Rwanda au Malawi tutapigwa kwa sababu watawala wanaua uzalendo . Itabidi Jeshi lipambane peke yao bila kusaidiana na wananchi kwa kujitolea kama enzi ya vita ya Uganda