Fundi Mchundo
Platinum Member
- Nov 9, 2007
- 10,448
- 8,705
- Thread starter
- #41
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Sanduku la kura litaamuaKwa hiyo uelevu wako ni kuona kwamba Mbowe ndiye mwenye haki miliki ya kuwa mwenyekiti wa cdm
Kwanini Kuna juhudi kubwa ya kumzuia na kumponda Lissu juu ya kugombea UMWENYEKITI??Hii ni ndefu kwa hiyo kwa wale ambao kusoma para zaidi ya moja ni mtihani wala wasianze kuisoma.
Kuna wanachama na wafuasi wa CHADEMA pamoja na wapinzani wengine wa chama tawala ambao wanaamini kwa dhati kuwa ni wakati muafaka wa kubadilisha approach ya kuleta mabadiliko kwa sababu inayotumika sasa hivi kwa kiasi kikubwa haijafanikiwa.
Wanaamini hii ni kwa sababu Mbowe hawezi kumudu tactics ambazo ni aggresive na confrontational za wakati huo. Na chachu ya tactics hizo itatokana nje ya taratibu za kawaida kama tulivyoona vijana wa nchi jirani walivyotumia tik tok n.k.
Mambo haya yote hayaendani na hulka ya Mbowe ambayo kwa kiasi fulani ni ya traditional politics. Hawa walihitaji kiongozi ambae hana uvumilivu kama wao. Kiongozi ambae yuko tayari kwenda "mano a mano" na serikali bila kujali consequences.
Kwa mtazamo wao Lissu ndio kiongozi anaewafaa. Kwa sababu walimwona Mbowe kama kizingiti kwao wakatumia tactics za kumuaibisha na kumbeza ili aone hahitaji hizo fedheha ajitoe. Bahati mbaya kwao walikuwa hawajamsoma Mbowe vizuri. Hawakujua tactics hizo ndio zitamfanya aone chama chake kinataka kuwa hijacked kihuni.
Kitu vingine ambacho hawakuzingatia ni kuwa watanzania wengi hawapendi confrontation na hivyo kuna uwezekano mdogo wa wao kujitokeza kwa wingi kujiunga nao. Kingine ni kuwa tactic kama hizi hazileti matokeo ya kudumu na mara nyingi zinakuwa hijacked na wana siasa na kufa kifo cha kimya kimya. Tumeona Kenya. Tumeona Malawi. Hata Tunisia na Misri.
Ubaya mwingine ni kuwa ni vigumu ku control ili vurugu zisitawale. Picha za vijana wakiwa wana warushia mawe hazina tija.
Amandla...
Hilo sio swali langu.Kwanini Kuna juhudi kubwa ya kumzuia na kumponda Lissu juu ya kugombea UMWENYEKITI??
umepata jibu, leta Uzi mwingine 🤔🤔🤔
Sanduku la kura litaamua
Miaka kumi ya mwisho ya Mbowe kwenye chaguzi za local 2014/2024, Chadema imepata uwakilishi chini ya 1%... Uchaguzi Mkuu 2020 Chadema ilipata mbunge mmoja wa kuchaguliwa. Kwa vipimo vyote kwa namna siasa za CCM zilivyobailika ni ukweli kuwa Mbowe hawezi kutuvushaWith all due respect, I don't agree with you. Hivi ni nani dhaifu kuliko Mbowe ambae walitegemea atamrithi wakati Makamu wake ni Lissu! Hakuna mtu alie mzuia Lissu kugombea lakini pamekuwa na shinikizo la ajabu la kumtaka Mbowe ajitoe hata kabla hajatangaza nia ya kugombea. Aidha, haushangai kuona CCM wakimsupport Mbowe waziwazi na kwa sauti kubwa. Unadhani hawajui kwa kufanya hivyo wanawaaminisha watu kama wewe kuwa Mbowe ni kibaraka wao na hivyo kuwafanya mumgeuke? Lissu angetangaza kugombea Uenyekiti bila kuwaachia surrogates wake wamchafue Mbowe wote tungefurahia kuwa Chadema inaonyesha maturity kwa kuwa na viongozi wao wawili wa juu kabisa na ambao wana mvuto mkubwa katika chama wanagombea kwa kuheshimiana bila kuchafuana. Aige mfano wa Mbowe ambae hawakuchelea kumtaka kiongozi aliyemkashifu Lissu aombe radhi. Na akaomba radhi.
Lakini haiwezekani kuwa watu wanaodai kuheshimu demokrasia wanafanya kila juhudi ili mtu wao asishandane na mtu atakayempa ushindani. Hivi mtu wao akishinda, atafanya nini katika uhaguzi ujao abapo hatakuwa na mpinzani mwenye stature ya Mbowe. Kama kweli ana nia nzuri na chama chake, Lissu anatakiwa aupoze moto na awahakikishie wafuasi wake kuwa hata kama atashindwa Chadema kitabakia salama. Kama hawezi kusema hivyo basi ni heri aseme wazi kuwa hatabaki katika Chadema ya Mwenyekiti Mbowe.
Amandla...
Wasimangaji wakubwa ni wale wanaomuunga mkono LissuTUNDU LISSU ASISIMANGWE KWA KUWA ANAGOMBEA UENYEKITI.
ANA HAKI YA KIKATIBA (YA CHADEMA NA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA) KAMA ILIVYO KWA MWANACHAMA YEYOTE WA CHADEMA.
Ni kosa kumzuia asigombee. Huo utakuwa utamaduni wa CCM na Fomu moja. Ni afya kwa chama kuwa na 'incumbent vs Challenger'' . Hiyo ingelikuwa demokrasia ya hali ya juu.Hakuna mtu alie mzuia Lissu kugombea lakini pamekuwa na shinikizo la ajabu la kumtaka Mbowe ajitoe hata kabla hajatangaza nia ya kugombea.
CCM hawampendi TAL kwasababu hizi. Mbowe ni 'moderate'' TAL ni extremist.Aidha, haushangai kuona CCM wakimsupport Mbowe waziwazi na kwa sauti kubwa.
Ukweli ni kwamba walioanza ni ''Chawa' wa Mbowe! Trick hizi wamezitumia katika nyakati tofuati, bahati mbaya nyakati ni tofuati. Ukifuatilia kwa makini tatizo lilikuwa kumlinda M/kitiLissu angetangaza kugombea Uenyekiti bila kuwaachia surrogates wake wamchafue Mbowe wote tungefurahia kuwa Chadema inaonyesha maturity kwa kuwa na viongozi wao wawili wa juu kabisa na ambao wana mvuto mkubwa katika chama wanagombea kwa kuheshimiana bila kuchafuana.
Hapana! ile ilikuwa mbaya sana ! hata Vijana wa Mbowe waliona ni mbaya! Ilimlazimu MboweAige mfano wa Mbowe ambae hawakuchelea kumtaka kiongozi aliyemkashifu Lissu aombe radhi. Na akaomba radhi.
Nashangaa sana, Chama cha Demokrasia lazima kionyeshe kwa vitendo.Lakini haiwezekani kuwa watu wanaodai kuheshimu demokrasia wanafanya kila juhudi ili mtu wao asishandane na mtu atakayempa ushindani.
Mimi sikubaliani kuwa CCM wanamuogopa TAL kuliko Mbowe. TAL ni mtu wa kwenye majukwaa na anachukua misimamo ambayo inawasaidia sana CCM. Kwa mfano kugoma kuingia kwenye majadiliano ya maridhiano while itawafurahisha watu wake lakini kwa wengine ( hasa mataifa ya nje) ataonekana unreasonable. Mbowe amekubali kuingia kwenye majadiliano hayo na yamefanikisha kuachiwa wanachama waliokuwa ndani, viongozi wenzake muhimu ( akiwemo Lissu kuweza kurudi kuongeza nguvu katika mapambano yao) kuruhusiwa mikutano ya hadhara na kufungua njia ya wao kupokea ruzuku. CCM walikuwa hawana jinsi bali kukubali haya ili wasionekane kuwa wao ndio unreasonable. Baada ya kufanikisha haya, Mbowe ameweza kujitoa kwenye hayo majadiliano bila kuonekana kuwa yeye ni mkorofi na unreasonable. Wangesusa kama alivyotaka Lissu yote haya yasingepatikana na mbaya zaidi wanachama zaidi ya mia wangeendelea kusota rumande au jela.CCM hawampendi TAL kwasababu hizi. Mbowe ni 'moderate'' TAL ni extremist. CCM wangependa mtu wanayeweza kucheza cheza naye mezani kama ''Maridhiano' uyalivyopoteza muda wa kudai Katiba.
CCM wanamhofia sana TAL
Sio kweli. Juhudi za kumchafua Mbowe zilianza mapema tu. Alianza Msigwa kwa kutangaza vita ya wazi wazi against Mbowe. Lissu akawa anachochea moto kwa kuzungumzia in public kuhusu uozo ulioko CDM. Wengine tukaanza kujiuliza kuwa inakuaje Makamu Mwenyekiti anaona mahali pekee pa kucriticize chama chake ni in public. He overplayed his hand alipoleta hadithi yake ya kutunga kuhusu Wenje na Abdul na viongozi wengine ( wink wink) waliopokea mshiko kutoka Abdul.Ukweli ni kwamba walioanza ni ''Chawa' wa Mbowe! Trick hizi wamezitumia katika nyakati tofuati, bahati mbaya nyakati ni tofuati. Ukifuatilia kwa makini tatizo lilikuwa kumlinda M/kiti
Natamani yasingetokea ili uwe mfano wa demokrasia nchini.
Jaribio la kumuua TAL lilifanyika kwasababu hakukuwepo na namna ya kumdhibiti.Mimi sikubaliani kuwa CCM wanamuogopa TAL kuliko Mbowe.
Wakati Mbowe (FAM) amekamatwa kutokana na vugu vugu la kudai Katiba.TAL ni mtu wa kwenye majukwaa na anachukua misimamo ambayo inawasaidia sana CCM. Kwa mfano kugoma kuingia kwenye majadiliano ya maridhiano ataonekana unreasonable. Mbowe amekubali kuingia kwenye majadiliano hayo na yamefanikisha kuachiwa wanachama waliokuwa ndani, viongozi wenzake muhimu ( akiwemo Lissu kuweza kurudi kuongeza nguvu katika mapambano yao) kuruhusiwa mikutano ya hadhara na kufungua njia ya wao kupokea ruzuku.
CCM walikuwa hawana jinsi bali kukubali haya ili wasionekane kuwa wao ndio unreasonable. Baada ya kufanikisha haya, Mbowe ameweza kujitoa kwenye hayo majadiliano bila kuonekana kuwa yeye ni mkorofi na unreasonable. Wangesusa kama alivyotaka Lissu yote haya yasingepatikana na mbaya zaidi wanachama zaidi ya mia wangeendelea kusota rumande au jela.
Mbowe amekubali kuingia kwenye uchaguzi akijua thika kuwa watendaji wa CCM watafanya walioyazoea. Sasa akigoma kuingia katika uchaguzi mkubwa ujao ataeleweka. Asingeingia CCM wangeweza kudai kuwa uchaguzi ungekuwa wa haki ila ni uoga wa CDM. Sasa hivi wameshindwa hata kushangilia ushindi wao wa kishindo.
CCM wamekiri kuwa walianza mazungumzo na Msigwa mapema tu. Mbowe alipopata fununu hakusita kumshughulikia kama alivyowashughulikia wakina Sumaye, Mashinji na Nyalambu. CCM wanajua hadanganyiki kirahisi na nyuma ya zile tabasamu ni mtu ruthless linapokuja masuala ya chama chake. Ndio maana strategists wanafanya kila mbinu kuhakikisha Lissu anashinda ikiwa ni pamoja na kumsifia sana Mbowe ili watu waamini amenunuliwa na wasimpigie kura. Mbowe ni hatari zaidi mara 100 kwa CCM kuliko Lissu.
Amandla...
Awali ya yote, nakushukuru kwa response iliyokuwa measured na civil. Kitu ambacho ni adimu sana siku hizi.Jaribio la kumuua TAL lilifanyika kwasababu hakukuwepo na namna ya kumdhibiti.
Akiwa Bungeni aliongea katika misingi ya sheria, hawakuweza kumfukuza
Akiwa nje ya Bunge aliongea katika misingi ya sheria, kesi zilizofunguliwa zilishindikana kumwadhibu
CCM wanampenda FAM kwasababu wana uwezo wa ku buy time naye.
Mathalan, suala la COVID-19 halikupaswa kufika lilipofika.
Handling yake ilikuwa poor katika hali ile ile ya FAM kuwa moderate. COVID wanamaliza Bunge!
Suala la Maridhiano, ilikuwa ku buy time wakati wanatafuta muda. Walipounda kamati ya Mkandala maridhiano yakafa kwasababu tayari walikuwa na position
Wakati Mbowe (FAM) amekamatwa kutokana na vugu vugu la kudai Katiba.
Pressure ilikuwa kubwa Nchini. Mkutano wa Mwanza alikokamatwa FAM ulikuwa wa Katiba.
FAM akiwa Magereza kwa miezi 8 Wanachama wa CDM na hapa credit kwa Vijana walikuwa mikoani wakieleza umuhimu wa Katiba. FAM akipelekwa Mahakamani wafuasi walijazana Kisutu si kutaka aachiwe bali kudai Katiba Mpya. Nyimbo na ujasiri wa kuwakabili FFU haukuzungumzia Mbowe, ilikuwa Katiba Mpya.
Pressure ilimtisha CCM na Serikali, kwamba, baada ya miezi 8 FAM akiwa ndani moto wa Katiba unawaka nje.
Ilikuwa dhahiri kumfunga FAM kungechochea Katiba. Mbinu iliyotumika ni '' Keep your fiend close and your enemies closer''. Maridhiano yakaasisiwa
Maridhiano ni reconciliation! swali, CDM waligombana na nani?
Huwezi kuwa Victim ukaomba reconciliation.
Kutokana na pressure ya Wanachama FAM alikuwa katika position ya ''strength'' ndio maana alipoachiwa Magereza aliitwa Ikulu kumvunja nguvu kwa kumweleza '' tulia tuongee''. FAM akaingia '' Kingi''
Je maridhiano ni kitu kibaya? Jibu ni hapana, ingawa definition ni awkward tukubaliane tu kwamba ''CDM na CCM walikoseana'' na walihitaji maridhiano.
Watu wanakwenda kwenye maridhiano katika' position of strength wakiwa na bargaining chip .
Katiba mpya ndiyo 'chip' yenyewe. Mbowe kuachiwa, Wafungwa na ruzuku ni haki. Kudai katiba ndilo tatizo
Kosa alilofanya FAM na kumfanya awe weak kuanzia hapo ni hili la kutoka Magereza na kwenda Ikulu wakati Wanachama wake wanamsubiri mahakamani.
Kwenda Ikulu wakati hajakutana na Viongozi wenzake waliokuwa nje na wanaojua hali ya kisiasa.
In essence FAM alionekana very weak mbele ya wenzake na leo tunajua walimpinga!
Hili la kumpinga kwa kura ni matokeo ya weakness aliyoonyesha.
Maridhiano aliyoasisi victim Mbowe yaliua hoja ya Katiba na CCM wakawa na muda wa kutengeneza kamati ya Mkandala. Kamati ya Mkandala ilipopata political legitimacy, maridhiano yakafa , FAM akapoteza kila kitu.
CCM wanataka mtu kama FAM kwasababu for almost 15 years kuanzia zama za JK, wanacheza naye mezani.
Kulikuwa na taarifa za uhakika COVID-19 wameitwa Bungeni kwa njia za ulaghai.Tuanze na suala la Covid-19. What were the options? Mass mobilization? Kwa watu ambao wakisikia tu kesho wanajeshi wanafanya usafi hawatoki nje? Mimi personally naamini Mbowe alitaka kuwa lenient kwa wakina Halima. Lakini wenzake walipomtilia ngumu, aliwakubalia na mpaka sasa hivi hajabadilisha msimamo. Hiyo sio sign ya dictator kama Lissu anavyotaka kum portray.
Ndicho kipindi pekee kilichoonyesha CDM ilikuwa ni taasisi.Mbowe amekaa ndani muda mrefu na kwa kweli juhudi za wakina Martin na wakina mama wa Bawacha zilisaidia sana kuweka presha kwa serikali.
Mbowe amekiri kulikuwa na mazungumzo kati ya viongozi wa kiroho na Serikali kabla ya kuachiwa.Ni wazi alijua nini kinaendelea.Ametoka, ameitwa na Rais ulitaka afanye nini? A sulk na kwenda nyumbani au aende kumsikiliza halafu arudi kuwa brief wenzake kuhusu mazungumzo yake. Alipoenda bila shaka hakujua anaitiwa nini. Labda aliitwa kuombwa radhi kwa yaliyompata n.k.
Kunaweza kuwa na Wajumbe hata 100 kwa mfano, lakini kila chama au taasis ina ''stalwart''.Alipotoka kwenye huo wito, aliieleza Kamati Kuu kuhusu yaliyosibu. According to Lissu ni yeye, Msigwa, Heche, Lema, Wenje na mwingine ndio walikuwa vehemently against hicho kitu. Mimi sijui ukubwa wa Kamati Kuu lakini nadhani ina wajumbe zaidi ya 12 hivyo hawakuwa majority.
Point yangu kubwa si kwamba TAL ana panacea ya matatizo, ni kwamba back lash na opposition ya M/Kiti anayopitia ni matokeo ya uongozi wake uliolega lega.Kupatikana kwa ruzuku kulitoa relief. Lissu anasema Mbowe alilipwa hela zote alizokuwa anaidai CDM halafu ana hint kuna mikopo ya kiujanja janja iliendelea ambayo haikupata baraka za KK. Anafanya hivi bila kusema hayo madeni alilipwa lini.
Mtu yeyote anaesema kuwa CCM ingebadilisha njia na kurudisha haki ambazo ziliondoa kwa sababu Lissu na watu wa Club house wanafoka anaishi dunia nyingine. Na hizo serikali za nje ni risk averse. Hauwezi kuwaambia kuwa CCM hawaelewi lugha nyingine bila kuonyesha kuwa angalau umejaribu lugha nyingine hasa kwa sababu kuna Mwenyekiti Mpya.
Amandla...
Upo kaka? 🤣Ni kosa kumzuia asigombee. Huo utakuwa utamaduni wa CCM na Fomu moja. Ni afya kwa chama kuwa na 'incumbent vs Challenger'' . Hiyo ingelikuwa demokrasia ya hali ya juu.
CCM hawampendi TAL kwasababu hizi. Mbowe ni 'moderate'' TAL ni extremist.
CCM wangependa mtu wanayeweza kucheza cheza naye mezani kama ''Maridhiano' yalivyopoteza muda wa kudai Katiba. CCM wanamhofia sana TAL kwa misimamo mikali isiyoyumba
Ukweli ni kwamba walioanza ni ''Chawa' wa Mbowe! Trick hizi wamezitumia katika nyakati tofuati, bahati mbaya nyakati ni tofuati. Ukifuatilia kwa makini tatizo lilikuwa kumlinda M/kiti
Natamani yasingetokea ili uwe mfano wa demokrasia nchini.
Hapana! ile ilikuwa mbaya sana ! hata Vijana wa Mbowe waliona ni mbaya! Ilimlazimu Mbowe
Nashangaa sana, Chama cha Demokrasia lazima kionyeshe kwa vitendo.
Kuwa na Wagombea katika ballot box kwa njia za kistaarabu ni maturity na inajenga confidence.
Hii ni missed opportunity kwa Chadema! so sad
JokaKuu
Mkuu FundiTuanze na suala la Covid-19. What were the options? Mass mobilization? Kwa watu ambao wakisikia tu kesho wanajeshi wanafanya usafi hawatoki nje? Mimi personally naamini Mbowe alitaka kuwa lenient kwa wakina Halima. Lakini wenzake walipomtilia ngumu, aliwakubalia na mpaka sasa hivi hajabadilisha msimamo. Hiyo sio sign ya dictator kama Lissu anavyotaka kum portray.
Mwenyekiti wa kudumu wa chama cha siasa, jibu nikwamba anahubiri demokrasia lakini yeye hataki mabadiliko wa nyazifa ya uwenyekiti, yaani ujinga ni kufunya jambo lile lile kwa mbinu zile zile, halafu unategemea matokeo chanyaHii ni ndefu kwa hiyo kwa wale ambao kusoma para zaidi ya moja ni mtihani wala wasianze kuisoma.
Kuna wanachama na wafuasi wa CHADEMA pamoja na wapinzani wengine wa chama tawala ambao wanaamini kwa dhati kuwa ni wakati muafaka wa kubadilisha approach ya kuleta mabadiliko kwa sababu inayotumika sasa hivi kwa kiasi kikubwa haijafanikiwa.
Wanaamini hii ni kwa sababu Mbowe hawezi kumudu tactics ambazo ni aggresive na confrontational za wakati huo. Na chachu ya tactics hizo itatokana nje ya taratibu za kawaida kama tulivyoona vijana wa nchi jirani walivyotumia tik tok n.k.
Mambo haya yote hayaendani na hulka ya Mbowe ambayo kwa kiasi fulani ni ya traditional politics. Hawa walihitaji kiongozi ambae hana uvumilivu kama wao. Kiongozi ambae yuko tayari kwenda "mano a mano" na serikali bila kujali consequences.
Kwa mtazamo wao Lissu ndio kiongozi anaewafaa. Kwa sababu walimwona Mbowe kama kizingiti kwao wakatumia tactics za kumuaibisha na kumbeza ili aone hahitaji hizo fedheha ajitoe. Bahati mbaya kwao walikuwa hawajamsoma Mbowe vizuri. Hawakujua tactics hizo ndio zitamfanya aone chama chake kinataka kuwa hijacked kihuni.
Kitu vingine ambacho hawakuzingatia ni kuwa watanzania wengi hawapendi confrontation na hivyo kuna uwezekano mdogo wa wao kujitokeza kwa wingi kujiunga nao. Kingine ni kuwa tactic kama hizi hazileti matokeo ya kudumu na mara nyingi zinakuwa hijacked na wana siasa na kufa kifo cha kimya kimya. Tumeona Kenya. Tumeona Malawi. Hata Tunisia na Misri.
Ubaya mwingine ni kuwa ni vigumu ku control ili vurugu zisitawale. Picha za vijana wakiwa wana warushia mawe hazina tija.
Amandla...
Mkuu Nguruvi3,Mkuu Fundi
Hapa kuna hoja naomba nizirejee. Kuhusu COVID-19 nimeshaeleza options alizokuwa nazo Mwenyekiti, hata hivyo nikukumbushe, Mbowe aliulizwa kuhusu suala hilo akiwa katika Maridhiano, alijibu ;
'' Suala linashughulikiwa na serikali. Ni suala lililopo katika taasisi linahitaji tuwape muda wa kulishughulikia kitaasisi'' Huyu ni Mbowe anakuwa msemaji wa Serikali ya CCM! Kwanini unadhani CCM haitampenda!
Kuhusu Mass mobilization, halikuwa suala la maandamano kwa nature yake kwavile ni la sheria.
Kama unakumbuka Mahakama ilianza kwa ubabaishaji, baada ya public pressure Mahakama haikuwa na namna ikalimaliza ! Kilichotakiwa ni pressure kwa Speaker aliyetumia Mahakama kama kichaka.
Pressure haikuwepo! Tukaona COVID-19 wakichangia pesa za charity za Mwenyekiti!
Hoja ya watu kisikia maandamano hawatoki!
Kuna sehemu mbili, kwanza ni Watanzania tunaowaulaumu kila siku kwa kutojali mambo yanayogusa maisha yao.
Pili, kuna ukweli kwamba M/Kiti Mbowe akiwa Ikulu aliacha watu wake juani Mahakamani Kisutu.
Nani amwamini tena? Madhara ya kupoteza public trust ndiyo hayo
Na Mwisho, Mbowe akiwa Mwanza alisema '' Jiandaeni na Uchaguzi wa Serikali za mitaa Mwakani. Muda ni mfupi wa kuandika Katiba mpya. Tutaendelea kudai minimal reforms katika Tume ya uchaguzi''
Mwenyekiti wa CDM anakuwa msemaji wa Serikali ya CCM kuhusu Katiba, kwanini CCM wasimpende!
Hayo yote hayaondoi haki ya Mbowe kuwania Uenyekiti. Ni afya kwa CDM kwasababu ni takwa la demokrasia , ni ukomavu wa kisiasa na huenda ikawa template ya vyama vya siasa.
TAL kasema , anataka ukomo wa uongozi ! Mfumo huru na haki wa uchaguzi. Mfumo wa wazi wa fedha
Mwenyekiti anajibu vipi hayo? Kama hana majibu, nini maono yake kwa miaka 5 ijayo ?