Kwanini kusiwe na mshindani wa NHIF? Kiukweli wanachofanya ni dhuluma

Kwanini kusiwe na mshindani wa NHIF? Kiukweli wanachofanya ni dhuluma

Hata wa ndugu wanakataa wanataka watoto uliowazaa wewe mwenyewe, na kama wa ndugu uwe umemuasili, yaani inatia sana uchungu.

Mimi ninakatwa ila hakuna anaefaidika imebidi tu niwe na kadi mbili moja ninayokatwa mimi nyingine kwa kupitia Mr. atleast nipooze machungu
Hili ni tatizo kuna haja ya kuifanyia marekebisho halafu hii tabia ya watu wachache kuamulia watu wengi ni tatizo wachangiaji ndiyo wanaopaswa kusema hiki ndiyo kifanyike siyo wao watoa huduma maana wao lengo ni kupata faida hawawezi kuleta sera au miongozo ya kuwapunguzia mapato ndiyo maana kuna shida hii

Hii bima mwanzo ilikuwa nzuri sana na huduma zilikuwa bora ila baada ya serikali kukwapua fedha zao kufinance activity zake bila kurejesha ndiyo sheria hizi zikaja futa baadhi ya dawa, futa vipimo, punguza umri nk maana hawawezi kulipa bills zinapokuja

Kwa hiyo ni mambo mengi tu yanayopelekea haya
 
Nimetumiwa meseji na Mfuko wa bima ya afya ya taifa NHIF inasema nanukuu " kadi ya mtoto wako .....itakoma kutumika tarehe .... Mwezi wa kumi namoja baada ya kutimiza umri wa miaka 18. Fika ofis ya NHIF au piga 0800110063" mwisho wa kunukuu.

Ninachangia laki moja na elfu ishirini kila mwezi toka kwenye mshahara wangu kwenye mfuko wa NHIF. Nina watoto wa wili wa kike , mmoja 18 years kasoro, wapili 15 years. Hawa ndo Dependants wanufaika wa mfuko ukiniacha mie. Mke wangu ni mchangiaji pia hivyo naye anatumia bima kutokana na michango yake.

Kwa umri wangu ntaendelea kuchangia for 15 years more nikiwa mwajiriwa.

Sasa hapa wizi ninaouona nikwamba pamoja na kuchangia Sh. Laki moja kila mwezi watoto wangu ati wanaondolewa kama beneficiaries eti ametimiza 18 years. Huyo mtoto bado ni Dependants maana yupo shule bado. Siomwajiriwa au anayejitegemea.

Pili value ya mfuko wa bima ya afya inaonekana pale unaposaidia kutibu close Dependants kama watoto ,baba na mama. Sasa kamna waondoa watoto then value ya hicho ninacho changia haipo ndipo ninapohisi kudhurumiwa.

Nauliza wadau. Hivi hakuna mfuko mbadala zaidi ya NHIF? Na kama ipo, je sheria inaruhusu kujitoa kwenye huu mfuko nyonyaji wa NHIF.
Mkuu pole sana sana. Kwa kweli NHIF ni wababaishaji sana ili jambo lako ni kubwa ila langu mimi naamini ni kubwa kuliko.

Nimeanza kazi kampuni fulani hivi, mpaka sasa nina miezi kama 9, makato ya bima kila mwezi ni Tsh.83,000 ya mshahara wangu na mwajiri na yeye anachangia 83,000 jumla yake kwa mwezi na changia 166,000 kama makato ya NHIF, cha kushangza zaidi mpaka sasa sijapata kadi kwa muda wote wa miezi hiyo 9,natunaambiwa NHIF yeye anaanza kukata pale muajiri anapojiunga na kampuni bila kujali unatumia huduma yao au kinyume chake.

Tunajaribu kufuatilia lakini majamaa hawana mpango kabisa,huu mfuko wa NHIF ni kati ya mifuko hovyo kabisa kwenye hii dunia, mifuko haijali wanachama wake hata kidogo,huduma zao ni mbovu sana sana.

Sheria zao kwanza ni zakibabe sana. Huduma kwa wateja nao ni hovyo kuliko kitu chochote kile duniani, wakipigiwa simu hawapokei, ukienda ofisini kwao hawana cha maana wanachosema, mbaya zaidi ukienda unakutana na bonge la foleni.

Halafu leo wanampango wakufanya mfuko lazima kwa watu wote, kama kwasasa mfuko wa bima haijachukua hata asilimia 5 ya watanzania lakini wanashindwa kutoa huduma ya maana kwa wateja wao,je wakifanya kwa wote wote itakuwaje???

Kati ya Taasisi ambazo Mh.Rais TAL akiambishwa tu inabidi avunjevunje harala iwezekanavyo basi hii taasisi,hii taasisi utendaji wake ni kinyaa hata kuendelea kuandika kuhusu wao.

Kwa kweli tusifanye makosa tena oct 28, hii ccm wamekuwa wanababaisha mpaka kwenye jambo la msingi la afya zetu.
 
Mjomba mbona katika ile fomu ya bima kule upande wa pili wa masharti kama mtoto amezidi miaka 18 inatakiwa awe mwanafunzi ndo anaendelea kuhudumiwa au huyo mwanao sio mwanafunzi?
 
Sitaisemea NHIF vibaya as inampa mzee wangu huduma kwa makato yangu, sijawahi kutoa hata mia na napata dawa zote, nasema napata dawa zote bila kutoa senti. Ningekuwa nalipia cash huenda familia ingekuwa inapumulia mirija as tangu 2018 hadi leo mzee ni yeye na muhimbili tu.
 
Mjomba mbona katika ile fomu ya bima kule upande wa pili wa masharti kama mtoto amezidi miaka 18 inatakiwa awe mwanafunzi ndo anaendelea kuhudumiwa au huyo mwanao sio mwanafunzi?
Ni mwanafunzi bos nineonesha kwenye Uzi wangu mkuu
 
Lengo ,mafanikio na matumaini ya nchi ni kila mmoja kuwa na bima ya afya ilii tupate taifa la watu wenye afya na kulijenga kwa kufanya kazi

Suala la kuwatoa wategemezi si sawaaa hata kidogo kwani ni kuongeza tatizo zaidi kwa familia na kutotimiza ndoto ya nchi ya kila MTU kuwa na bima ya afyaa.

Maoni ,kwakuwa watumishi wa umma wanakatwa bima kila mwezi ni vyema wategemezi wao kadri ya sheria wasiondolewe kwenye bima haijarishi wana umri gani.

Wanasheria wa nchii hii sijui wanasomaga nn huko vyuoni ? Hawajawah kuja na kesi mahakaman kupigania masuala kama haya yanayosumbua jamiiii.
 
Hudhulumiwi, isipokuwa hiyo fedha inamsaidia mnufaika mwingine wa NHIF ambaye pengine amelazwa muda mrefu au anaumwa ugonjwa sugu wenye gharama kubwa sana ya matibabu kuliko kiasi chake anachochangia kwa mwezi/mwaka.
Kw hiyo yeye watoto wake wakiugua muda mrefu au magonjwa sugu ni jukumu la nani kuvover hizo garama ilhaki bado anachangia bkma?
 
Hio ni kawaida kwa mifuko yote ya bima hata bima za Private. Kuna umri Fulani dependents wakifikia inabidi wawe na bima zao. Inategemea na bima, zingine zinasema 18years zingine 21years.

Labda ungeenda NHIF na documents zake urequest waextend useme bado ni mwanafunzi labda unaeza kusaidiwa.
Sasa wanamtoa mtoto mwenye 18yrs mwanafunzi na tegemezi... wanamwacha baba mwenye 50yrs anayejitegemea...kigezo walichokiweka ni cha wizi
 
Mkuu kwa mujibu wa sheria, NHIF wapo sahihi, baada ya kufikisha umri wa miaka 18 huyo sheria inamtambua kuwa sio mtoto tena, kwa suala lako nakushauri nenda kwenye ofisi ya NHIF ya mkoa uliopo ukawaeleze kuwa huyo mwanao bado ni mwanafunzi watakuelekeza cha kufanya na ataendelea kutumia bima mpaka atakapo maliza shule.

Kimsingi elimu kuhusu bima bado inahitajika, hakuna bima ya Afya isiyo na masharti kote duniani
Sasa kama wanamtoa mtoto tena tegemezi wanawaacha wazazi amnao ni 45+ yrs kuna logic gani?
 
Hudhulumiwi, isipokuwa hiyo fedha inamsaidia mnufaika mwingine wa NHIF ambaye pengine amelazwa muda mrefu au anaumwa ugonjwa sugu wenye gharama kubwa sana ya matibabu kuliko kiasi chake anachochangia kwa mwezi/mwaka.
Kwa hiyo yeye makato yake ya kila mwezi yatapungua kwa kuwa dependant mmoja kaondokewa??
 
Pole

Ukiwa ni mtumishi wa umma hakuna mfuko mbadala zaidi ya NHIF ambayo ni lazima;

Hata mtoto wako angekuwa na miaka 40 bado angestahili kufaidika na bima yako, ishu sio umri au kujitegemea kwa mnufaika, cha kuzingatia ni slots zinazotolewa kwa mnufaika ndio zizingatiwe. Umepewa nafasi 5 zitumike hizo bila kujali ni kina nani wananufaika na bila kujali hata umri wao;

Hapo bado hujakwenda hospitali na kuambiwa ugonjwa huu haupo katika magonjwa yanayotibiwa kwa NHIF. Yaani unachangia laki na ishirini kwa mwezi, mtoto wako akiumwa unamlipia tena kumtibu na wewe mwenyewe ukienda hospitali kutibiwa bado utatakiwa kujilipia[emoji24][emoji24]

Hizi ndio sheria zinazoitwa kandamizi, zikifuatiwa na sheria ya utumishi wa umma, sheria ya mifuko ya jamii na sheria za kodi, tuna nafasi ya kuzibadilisha, tuitumie vizuri.
Halafu kwa maajabu ya dunia eti nao wanatoa gawio kwa serikali wakati baadhi ya dawa au vipimo unaambiwa haiko covered. Juzi juzi nimetaka miwani ya kusomea aisee nikaambiwa limit ni miwani ya elfu 20, ambayo utadhani ni ya mtoto. Ikabidi niongezee elfu 40 ndiyo nikapata miwani imara na mizuri kwa 60,000. Bure kabisa hili limfuko.
 
Nenda na vitambulisho kuwa anasoma. pili taifa lolote lina kiwango cha umri kuwa ni mtu mzima na watoto kwenye mahesabu wasipoyatumia hayo yatawadondosha.
Si kweli, kila member ana nafasi 6 za kutibiwa kulingana na makato ya kila mwezi. Pia ukumbuke kwamba pamoja na kukatwa for 12 months unaweza kumaliza mwaka mzima wameumwa 2 au 1 au hakuna.
 
Lengo ,mafanikio na matumaini ya nchi ni kila mmoja kuwa na bima ya afya ilii tupate taifa la watu wenye afya na kulijenga kwa kufanya kazi

Suala la kuwatoa wategemezi si sawaaa hata kidogo kwani ni kuongeza tatizo zaidi kwa familia na kutotimiza ndoto ya nchi ya kila MTU kuwa na bima ya afyaa.

Maoni ,kwakuwa watumishi wa umma wanakatwa bima kila mwezi ni vyema wategemezi wao kadri ya sheria wasiondolewe kwenye bima haijarishi wana umri gani.

Wanasheria wa nchii hii sijui wanasomaga nn huko vyuoni ? Hawajawah kuja na kesi mahakaman kupigania masuala kama haya yanayosumbua jamiiii.
Kabisa mkuu maana inavyo onekana lengo la huu mfuko limeshapotea . kwa sasa ni kitengo cha kuibia watumishi kwani hatuna njia mbadala
 
Kulikua na chama Cha walimu kinaitwa CHAKAMWATA kikawa kinawakata walimu asilimia moja ya mshahara badala ya 2 ya kile pendwa, kikawa kinatetea kikokotoo kwa nguvu zote, kikawa kinawapa walimu gawio la asilimia 50 ya michango yake yaani Ile asilimia moja. Wakubwa wakaona hiki kitatuletea vyoko vyoko. Kufumba na kufumbua akaunti zote za chama zikafungiwa. Hakija kaa sawa kikafutiliwa mbali.
Wakubwa kamwe hawataki mnyonge atoke. Japo serekali yetu Ni ya wanyonge ambao ndio wapiga kura.
Kesho kaangalie Ni wangapi wanapiga Kura Masaki.
 
Una hamu ya kufaidika na bima ya afya?

Ni kuomba uugue ugonjwa mkubwa na wa muda mrefu ndio utafaidi vizuri bima yako
Mkuu, Kunufaika na huduma ya bima sio kutamani majanga ila ni kuwa na uhakika kuwa uko covered. Ndio maana tunalipia kabla.
 
Pole sana Kiongozi
Sijasoma michango wa wengine kuona kama umesha shauriwa, Kama bado;
Naomba nikupe muongozo kwani mimi ni moja ya watu walio fuatilia masuala ya Bima ya Afya
Bima ya Taifa NHIF humtambua mtoto kama anaweza kujitegemea pale anapo timiza mika 18 kama hayupo shuleni/chuoni
Kwa watoto wanaosoma Sekondari au Chuo, Bima huendelea hadi watakapo maliza masomo yao, haijalishi miaka.
Cha kufanya; wapelekee uthibitisho unao onesha kuwa mtoto wako yupo shuleni/Chuoni
inaweza kuwa ile formu ya kujiunga shule/chuo au Barua kutoka shuleni/chuoni yenye picha yake inayo onesha anasoma (Mwezi wa kuanza na mwezi tarajiwa wa kumaliza.
Natumaini umesaidika
Pamoja na hayo watakupora Tshs. 50,400/= (utakuwa unalipa kila mwaka hiyo fedha mpaka huyu mwanafunzi amalize masomo halafu wamtoe kabisa kwenye BiMA).
 
Pia unakuta mke anakatwa, mume anakatwa kwa wakati mmoja tena pengine wote wakiwa kwenye taasisi moja, Je huo sio wizi?
Sikuombei but siku ikifika zamu yako kuumwa ugonjwa mkubwa ambao gharama zake ni mara kumi au zaidi ya ulichochangia wewe na mwenza wako ndipo utabaini kumbe bima sio wizi
 
Back
Top Bottom