Kwanini kuweka mifumo imara nchini kunaogopwa?

Kwanini kuweka mifumo imara nchini kunaogopwa?

Kwani mfumo ndio nini, na mfano wa mfumo ni upi ambao ni tofauti na uliopo, kwamba Rais anakuwa na wasaidizi toka juu kabisa Hadi ngazi ya kitongoji??

Kuna kipi kinachokosekana hapo, kuna Bunge, Mahakama na Ile Taasisi ya Uraisi, ni mfumo gani huo mwengine

Maana kila mtu, anaongelea Mfumo, mfumoo, bila kuongoza mjadala wa Hilo Neno mfumo,

Mfumo ndio kitu gani Hilo na linafanaje??

Shida siyo mfumo, shida ni wananchi wenyewe,

Kwanza ni wachezea mfumo, lakini pili, Wapo tayari kutetea waharifu wa mfumo,

Nchi yangu hii, iko tofauti Sana pengine na watu wote wa Dunia hii, ni nchi pekee ambayo, watu wake wanaweza kushirikiana na wahamiaji haramu kuwaficha majumbani mwao na kuwasafitisha Kutokea makwao Kwa kutumia magari Yao, ni nchi pekee ambayo watu wake hawajali pindi Mali na utajiri wa nchi Yao unaposombwa na kina Manji, ni nchi pekee inayo walilia wauza dawa za kulevya wake kuwekeza nchini Kwa madai eti walionewa

Ni nchi pekee ambapo watu wake hukaa kimya mafuta ya serikali yanapoibiwa waziwazi huku wananchi wake hawatoi tarifa hata kama nyumba inayofanya uharifu huo imepakana na Watanzania

Ni nchi pekee ambapo mapolisi wanaweza kusindikiza mwizi wa Tanzanite Kwa ulinzi na vingora kumvusha mipakani na bado asikari huyo akapandishwa cheyo

Nchi yangu ya ajabu hii,

Ikipata Raisi wa kukomesha hayo, ataitwa mnyanyasaji na eti hapendi wawekezaji, ni nchi pekee ambapo wakubwa wake, wanauhuru wa kufanya biashara na wasilipe Kodi eti tu wamekuwa viongozi, unajiuliza, ni kivipi Kodi za wananchi zinatumika kuwalipa?

Nenda US, Trampo alichunguzwa Kwa kampuni yake ilipoonekana kuna kipindi ilitaka kukwepa kulipa kodi, tofauti na kwetu ambapo kiongozi anaweza kuwa imma Muuza ngada ama fam...! Yake na bado Watanzania wakaendelea kupiga makofi na kusifia

Mungu wangu..!
Kila siku tunaambiwa mfumo mfumo hivi ni kitu gani hicho je mfumo haiwahusu binadam Kama Kama binadam anahusiswa ambaye anamadhiafu yake kila kona ni dhahiri kabisa lazima wapo watu makini wa Kusimamia hao watu maana strong people
 
Mifumo imara kama ipi?

Hebu ainisha ni mifumo ipi imekosekana hapa nchini?
Mnaposema magu angekuwepo basi kitu flani kisingetokea au kingetokea hiyo ndio dalili kwamba Tz hakuna mfumo imara. Na mbaya zaidi hata magu hakuwa na akili ya kuunda maana angeunda basi asinge abudiwa na mataga kama wewe.
 
Mnaposema magu angekuwepo basi kitu flani kisingetokea au kingetokea hiyo ndio dalili kwamba Tz hakuna mfumo imara. Na mbaya zaidi hata magu hakuwa na akili ya kuunda maana angeunda basi asinge abudiwa na mataga kama wewe.
Mifumo ipo ila tatizo lipo kwa wasimamizi wa hiyo mifumo ni kwamba wako lege lege!

Ni kama kwenye famili unakuta famili nyingine baba amewalea wanae mpaka raha lakini nyingine baba ni lilevi mitoto inajiendea tu kama mbuzi.
 
Naona kila mmoja anaongelea, mifumo, mifumo. lkn mnaelewa maana ya mifumo? Na mnaelewa ya kuwa mifumo bila ya usimamizi thabiti ni sawa na buree?

Na usimamizi bora bila mifumo ni kazi bure.

Hapa ni mfano wa ujenzi wa nyumba!! Tunataka ramani nzuri na fundi mzuri.

Ukiwa na ramani nzuri unaweza kubadilisha mafundi na bado ukapata nyumba ya ndoto uako.
Hivyo ji vema kuwa na Taasisi Imara na utawala wa kila mmoja kufuata sheria bila kujali nafasi au cheo chake.

Kwa hapa kwetu taasisi zenyewe bado ni dhaifu kisha hazina autonomy, zinaingiliwa mno na wanasiasa.

Kusema hujui mifumo ninini hata wewe umeshaingiliwa namna yako ya kufikiri. Huna independent thinking! Sema mwenyewe hata hujojui ivo utabisha!!
 
Na usimamizi bora bila mifumo ni kazi bure.

Hapa ni mfano wa ujenzi wa nyumba!! Tunataka ramani nzuri na fundi mzuri.

Ukiwa na ramani nzuri unaweza kubadilisha mafundi na bado ukapata nyumba ya ndoto uako.
Hivyo ji vema kuwa na Taasisi Imara na utawala wa kila mmoja kufuata sheria bila kujali nafasi au cheo chake.

Kwa hapa kwetu taasisi zenyewe bado ni dhaifu kisha hazina autonomy, zinaingiliwa mno na wanasiasa.

Kusema hujui mifumo ninini hata wewe umeshaingiliwa namna yako ya kufikiri. Huna independent thinking! Sema mwenyewe hata hujojui ivo utabisha!!
Mkuu, hapa unaweka matamanio ya fikra zako zisizo na chanzo na namna ambavyo mfumo unaundwaje na unaendeshwaje naukoje

Mfano wa mfumo tulionao ni

Tuna, Bunge, Mahakama, Taasisi ya Uraisi Kwa maana ya (Serikali) na kila Aina ya mfumo huu, unatenda tofauti lakini mtazamo wake ni mmoja na kila mmoja akimsimamia na kumshauri mwenzake Kwa lengo la kuwa imara wakati wote,

Huo mfumo wenu mnaotamani uwe ni iukoje,

Kwa sababu ni rahisi kusema huo mfano wako wa ramani ya nyumba, lakini ni kivipi huo mfumo utakufanya upate mtu mwaminifu asiyeweza kuiba material ya vifaa vyako?

Narudi pale pale, ukiweza, tupe huo mfano wa mfumo na unavyoweza kuwa Kwa sababu nyinyi inaonyesha mnaudhoefu mkubwa
 
Kutawala nchi ambayo wananchi wake wengi ni wajinga ni jambo rahisi sana...
 
Mkuu, kelele za mifumo imara mnazoimba, mfano wake ndio huu??

Hovyo Sana!! Yaani mpaka hapa, bado sjaona mwenye kuuelezea huo mfumo imara na maana yake
Kama tafsiri yangu ya MFUMO haikukidhi matarajio yako, uungwana ungetoa nawe tafsiri yako ya MFUMO hasa hasa unachodai "mfumo imara".

Ili kujibu hoja yako, "Mfumo" wa serikali ni ule unaotoa madaraka ya kutosha miongoni mwa Taasisi mbalimbali katika kila ngazi ya utendaji serikalini. Kwa mfano katika Sekta ya Afya, pamoja na kuwepo Wizara inayoshughulikia Sera, kumeundwa Taasisi mbali za Serikali na kila moja imepewa majukumu yake kisheria. Uimara wa "Mfumo" huo ni kiasi cha madaraka yanayomilikiwa na serikali katika shughuli za kila siku.

Kama nilivyoeleza kwenye bandiko langu la awali ufanisi wa Mfumo hutegemea uwajibikaji wa kila mtumishi. Baadhi ya watumishi hawatimizi wajibu wao ipasavyo kwa sababu ya maslahi binafsi. Mifano iko mingi. Km Sekta ya Afya mgonjwa hapati huduma hadi atoe chochote.
 
Na usimamizi bora bila mifumo ni kazi bure.

Hapa ni mfano wa ujenzi wa nyumba!! Tunataka ramani nzuri na fundi mzuri.

Ukiwa na ramani nzuri unaweza kubadilisha mafundi na bado ukapata nyumba ya ndoto uako.
Hivyo ji vema kuwa na Taasisi Imara na utawala wa kila mmoja kufuata sheria bila kujali nafasi au cheo chake.

Kwa hapa kwetu taasisi zenyewe bado ni dhaifu kisha hazina autonomy, zinaingiliwa mno na wanasiasa.

Kusema hujui mifumo ninini hata wewe umeshaingiliwa namna yako ya kufikiri. Huna independent thinking! Sema mwenyewe hata hujojui ivo utabisha!!

Sijaelewa bado your final thoughts, lakini nakubaliana na wewe kuwa na ramani pamoja na fundi ni jambo zuri, lkn kuwa ramani nzuri pamoja na fundi mzuri ni jambo zuri zaidi. Mifumo siyo event, ni process. Siyo kitu ambacho ukiingia tu madarakani unakijenga kama daraja la mfughale. ni social and cultural transformation. mfano sasa tunapambana na ndoa za utotoni, ukeketaji, utii wa sheria bila shuruti, elimu ya kujitegemea, elimu kwa wote... tukiweza kwenye haya mifumo itakuwa rahisi kufanya kazi. lkn huwezi kulazimisha mifumo bila kuwa na cultural and social acceptance. It's like the law, if the law is not compartible to the moral and values of a given society, then that law can be regarded as a bad law.
 
Kazi ya kuweka misingi imara inaanzia kwenye katiba.

Sasa ukitaka kuwakosesha raha CCM wewe watajie neno linaloitwa katiba mpya...hapa ndipo tatizo lilipo.
 
Mwendazke na uzalendo wake wote hakutaka kuweka mifumo kabisa ndo maana kwa sasa kila kitu chake kishapinduliwa.

Mama na yeye haelekei kujenga mifumo bali anafuata nyayo za mwendazake, Je ni kitu gani wanaogopa? Kwanini hawataki kuweka mifumo?

Mama anaweza kuacha legacy ya kuwa Rais pekee aliyetengeneza mifumo ambayo kuja ku temper nayo kutahitaji kazi ngumu sana.

Kwa sasa naona mama kaanza zile misele za mtangulizi wake mara Kariakoo mara sijui anawaomba wasaidizi wake wawe wanahesabu bati na tofali.

Bila mifumo imara tusidanganyane hakuna kitakacho songa mbele.

Mimi naona tuache kuwa taifa la kasuku. Ebu kuwa specific, mfumo upi ambao unaona haupo na unataka uwepo.
 
Akiweka mifumo imara hawezi kuabudiwa, watawala wengie Africa wanataka kuabudiwa
Mifumo imara ktk Taasisi imara haipendwi Afrika kwasababu itawaumbua watawala wetu na kelele zao za kujionyesha ni wachapa kazi kumbe vibaka tu! Wengi ni wababaishaji ambao hawana uwezo wa kusogeza au kusimamia miradi mikubwa ikafanikiwa!
 
Kazi ya kuweka misingi imara inaanzia kwenye katiba.

Sasa ukitaka kuwakosesha raha CCM wewe watajie neno linaloitwa katiba mpya...hapa ndipo tatizo lilipo.

Katiba ni sehemu ndogo sana ya mfumo. Katiba ni sheria kuu ya nchi ambayo inafaa iendane na mila na desturi.
 
Back
Top Bottom