Kwanini Magufuli aliwaogopa sana Nape na January Makamba?

Kwanini Magufuli aliwaogopa sana Nape na January Makamba?

Mkuu,

Unaelewa "logical non sequitur" ni nini?

Unaelewa kwamba mimi kushindwa kuthibitisha hayo uliyoyasema hakuthibitishi Mungu yupo?

Unaelewa kwamba mimi ninaweza kushindwa kuthibitisha hayo yote, kwa sababu Mungu hayupo?

Unaelewa kwamba, katika ulimwengu ambao Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hayupo, watu kushindwa kuthibitisha vitu na kuwa na majibu ya uhakika si kitu cha ajabu, kwa sababu hakuna Mungu wa kuwapa majibu na wao inabidi wachambue mambo na kupata majibu, na hawana uwezo wa kupata majibu yote mara moja.

Kwa hiyo, kushindwa kwangu kuwa na majibu ya maswali, hakuoneshi mgogoro wowote na dhana kwamba Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na mapenzi yote hayupo.

Ila, katika ulimwengu ambao Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote yupo, mtu yeyote anatakiwa kuwa na majibu ya swali lolote na ujinga hautakiwi kuwepo.

Kwa sababu, Mungu huyo mwenye neema kuu hawezi kuruhusu viumbe wake watawaliwe na ujinga.

Na ikitokea kuthibitika kwamba kuna ujinga wowote popote, huo ni uthibitisho kwamba Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hayupo.

Angekuwepo angefuta ujinga wote.

Hoja yako ya kuniuliza maswali ambayo unaona nitashindwa kuyajibu, ambayo wewe unaona inathibitisha Mungu yupo, kiukweli ni hoja inayothibitisha Mungu hayupo.

Unaelewa kwamba umetoa hoja inayozidi kuthibitisha Mungu hayupo?
Mkuu kwema!

Mbona kama leo nimesoma huko juu kidogo umeandika kua "Magufuli hakuamini kama Mungu yupo na alijiona yeye ndio Mungu mtu na alikua na ubaya" je ina maana kwa statement hizi wee ulitaka aamini kua Mungu yupo au lah.

Niimewasilisha
 
Aisee hata mimi nashangaa.
Yaani alikuwa na nguvu ya kunyamazisha Pemba ile....

Amewapa Wazanzibar Hussein Mwinyi ambaye hawakumtaka asilani, japo leo wanafaidi matunda yake kuliko bara.

Nguvu zake ni kama za Nyerere. Angekuwa hai Magufuli leo, Raila angekuwa rais na nchi za Magharibi zisingeingilia uchaguzi wa Kenya. Angewadhibiti kama Nyerere alivyowadhibiti Sultan Jamshid Zenj, Kaburu Shelisheli na Buyoya Burundi akapambana hadi Mandela kawa huru. Achilia akina Obote, Lule na Binaisa aliowapandikiza.

Magufuli alimrudisha Mugabe toka ukimbizini Singapore (Mnangagwa akasingizia eti amelazwa tu).

Magufuli aliiokoa DR Congo kupasuka (it didn't secede) kwa kuiingiza EAC. Nyerere naye aliingiza China kwenye Veto Club ya UN pia aliing'oa Afrika Kusini ya Makaburu toka Jumuiya ya Madola.
 
Aliwasamehe, lakini je wao - Makamba, Nape walikuwa wa kweli?
Nashangaa...

Hivi leo mtu amtukane Samia kama hao walivyomtukana Magufuli atakuwa salama?

Mleta mada anapima nguvu za rais kwenye mzani kama ule wa rula?

Mleta mada akisema akili za hao aliowapamba ni njema basi za Makonda ni gold kabisaaa...
 
Ni kweli hazikuwa za haki, lakini still wapinzani walikuwa wanazidi kuzoa viti. Ingekuwa vinapungua hapo sawa.
Mkuu.

Walizoa viti sawa lkn waliwahi kupata quorum Bungeni?

Wapinzani ni CCM B. This is Africa mind you.
 
Bado ccm walikuwa wengi bungeni na ndio walikuwa na nguvu, na huo ni upande wa wabunge tu ambao ndio walikuwa wanaachia mgombanie ila kwenye urais huko hata upinzani wamsimamishe Kikwete hawatoboi.
Magufuli huyo huyo wasiyemtaka angeenda upinzani bado wangempa nafasi kama walivyofanya kwa Lowasa, Mrema na Maalim. Hawa wote walikuwa Makada wa CCM tangu 1977.
 
Makamba ndiye aliyeingilia mfumo wa tume ya uchaguzi na kupunguza kura za Lowasa ili za jiwe zitoshe.

Nape ndiye aliyepiga kampeni mpk akavunja mkono huko vijijini kabisa ili watu wampigie kura jiwe maana by then ccm ilikuwa imekanwa kabisa na watanzania.

In short ,these two guys are smarter by far than jiwe, hence jiwe was haunted by unspeakable fear for them.
Kazi wafanye state security sifa wapewe Mkm na Np.
 
Kumbe Tundu Lissu ni kiroboto na upigwaji wake risasi hauhusiki Kwa serikali wala mkuu wa serikali aliekuwepo?....oohho nimekupata
Huyo Tundu Lissu mwenyewe hana uhakika mpaka leo nani alitaka kumtoa roho! Unafikiri kutotaka kurudi anauogopa mzimu wa Magufuli? Hapana kuna yule mwenye macho ya makengeza ni mtu hatar na nusu ukiingia kwenye anga zake
 
Wingi wa wabunge wa CCM ulikuwa ukienda ukipungua, fahamu msemo usemao bandubandu humaliza gogo. Nguvu ya wabunge wa CCM haikuwa kwenye hoja huko bungeni, bali kura. Na wananchi walikuwa wanazidi kuamka kwani walikuwa wanaangalia ubora na sio wingi.
Lowasa aliionya Chadema isipoacha siasa za vurugu ikafanya siasa za ustaarabu atarudi CCM.

Sasa kama CCM ya Magufuli ilikuwa mbaya kwanini Lowasa, Sumaye, Kingunge, Zitto Kabwe, Kitila Mkumbo, Marando, Mbatia, Selasini, Mashinji, Katambi, Mgana Msindai, Anthony Komu, Saed Kubenea, David Kafulila, Suzy Masele, Joyce Sokombi, Lazaro Nyalandu name them, walikimbia? Ina maana walikimbia pazuri kwenda pabaya?
 
Magufuli alikuwa na uwezo wa kumfanya yoyote kuwa mbunge refer kwa Katambi, Kimei, Ndalichako, etc ambao hawakua na mizizi CCM lakini akawabeba
Kwani Samia huwezo uo hana? Mbona hakumfanya Furaha mtoto wa dadaake kuwa mbunge Jimbo la Kawe licha yakuongoza kura za maoni?
 
Huyo Tundu Lissu mwenyewe hana uhakika mpaka leo nani alitaka kumtoa roho! Unafikiri kutotaka kurudi anauogopa mzimu wa Magufuli? Hapana kuna yule mwenye macho ya makengeza ni mtu hatar na nusu ukiingia kwenye anga zake
Nani huyo Makengeza?
 
Mkuu.

Walizoa viti sawa lkn waliwahi kupata quorum Bungeni?

Wapinzani ni CCM B. This is Africa mind you.

Hawakuwa mbali na quoram huko bungeni. Unapoona vitimbi, ukatili, uhayawani nk dhidi ya wapinzani wakati wa uchaguzi, basi ujue zama za CCM zilishapita. Unfair election ndio iliyoendelea kuifanya CCM kuwa na wabunge wengi, sio zaidi ya hapo.
 
Lowasa aliionya Chadema isipoacha siasa za vurugu ikafanya siasa za ustaarabu atarudi CCM.

Sasa kama CCM ya Magufuli ilikuwa mbaya kwanini Lowasa, Sumaye, Kingunge, Zitto Kabwe, Kitila Mkumbo, Marando, Mbatia, Selasini, Mashinji, Katambi, Mgana Msindai, Anthony Komu, Saed Kubenea, David Kafulila, Suzy Masele, Joyce Sokombi name them, walikimbia? Ina maana walikimbia pazuri kwenda pabaya?

Lowassa hakuwahi kuwa CDM na wala hatakuwa, kuanzia ujana wake mpaka uzee vyote vimemkutia CCM, iweje awe CDM akiwa mzee tena mgonjwa? Viongozi kadhaa wa Cdm kwa tamaa ya fedha ndio walimpokea Lowassa na kumpa nafasi ya kugombea mtu ambaye hakuwa sahihi.

Hao wote uliowataja walikuwa na DNA ya CCM, wengine ni wezi na wasaka madaraka, baada ya kuona siasa chafu za Magufuli, ilibidi wajisalimishe kulinda mali zao za wizi, ama kufuata vyeo baada ya kufanyiwa vitisho. Lakini hakuna aliyekwenda CCM kwa kufuata itikadi, au ubora wa Magufuli, bali uoga nje ya ulevi wa madaraka wa Magufuli ikabidi wajisalimishe.
 
Viongozi kadhaa wa Cdm kwa tamaa ya fedha ndio walimpokea Lowassa na kumpa nafasi ya kugombea mtu ambaye hakuwa sahihi.
Hili lilikuwa kosa kubwa sana kwa chadema. Na ndiyo chanzo cha kufa kwa morali ya wapigania haki na mabadiliko.

Kabla ya kosa hili ilikuwa yakiitishwa maandamano watu wanajitokeza Sana na serikali inatetemeka.
 
Hili lilikuwa kosa kubwa sana kwa chadema. Na ndiyo chanzo cha kifa kwa morali ya wapigania haki na mabadiliko.

Kabla ya kosa hili ilikuwa yakiitishwa maandamano watu wanajitokeza Sana na serikali inatetemeka.

Kabisa, na Lowassa ndio alipandikiza siasa za kikondoo ndani ya CDM. Cha ajabu Lowassa alikuwa anawaambia CDM wafanye Siasa za kistaarabu, lakini kila siku tunaona vijana wa CCM wakiwafanyia ukatali wapinzani. Na Lowassa alipokuwa CCM alikuwa akishinda ubunge kwa kuagiza vijana wa CCM wawafanyizie wapinzani!
 
Kwanini avujishe kwa Siri?, Kwanini hakudeal nao kimya kimya, akaamua kuwatafutia sababu in public?
Ndio nasema kwamba kama Magufuli angekuwa kama hivyo anavyoelezwa basi asingewaacha wala kuogopa chochote maana walikuwa maadui zake kabisa, sasa wenye kusema Magufuli aliwaogopa ndio nauliza kwani hao jamaa walikuwa na kipi chenye kumuogopesha Dikteta?
 
MAGUFULI NI UTITIRI ALIYEMBEBA TEMBO KWA SPIDI YA CHEETAH.

Kama NECTA wangepewa kusahihisha posts za JF na kutoa matokeo ya wanaostahili kubaki JF nadhani wangebaki watano tu (mimi nikiwemo) na Mello angelazimika kufunga JF maana hasingeweza kutumia rasilimali fedha kuendesha jamvi la watu watano tu.

Watanzania tutafute kuijuwa vizuri historia ya nchi ili tubalance story zetu tunapoandika. Huo ndiyo uandishi unavyotakiwa kuwa.

Kila kukicha propaganda zinashamiri juu ya Ben Saanane, Tundu, Roma Mkatoliki.

Kimsingi, ifahamike kwamba sipingani na yaliyowatokea maana ni dhahir shahir yamewatokea, ila kwa nia gani na kwa mikono ya nani siyo hoja yangu.

Kinachonishangaza ni kuwa hatutendi haki kwa Magufuli kumuhusisha na hao watu.

Ifahamike kwamba Tz haikuanza enzi ya Magufuli 2015, Tz ilikuwepo tangu Tanganyika na matukio yalikuwepo tena mengi kuliko enzi ya Magufuli maana enzi zile dunia ilikuwa kwy vita ya itikadi (nipige nikupige).
Diplomasia ilipoteza uwezo wa kusimamia amani ya dunia, na silaha za maangamizi ya umma ndiyo zikachukuwa nafasi ya diplomasia. Zikaundwa kambi za kujihami za NATO na WARSAW PACT zilizotokana na dhana za Unipolar na Bipolar kwa mtiririko huo.

Ili kutenda haki inabidi unayepost u balance story. Tujuwe binadamu ana hulka kwamba akisikiliza habari moja tuu 24/7/30/365... inamkifu na habari hiyo inapungua thamani, uzito na umuhimu kwenye masikio, ubongo na mtima wa mlaji wa habari hiyo.

Kila kukicha ni Ben Saanane, Tundu, Roma Mkatoliki kama vile hawa pekee ndiyo wamefikwa na madhila hayo kwenye nchi.

Mbona hamumtaji Chacha Wangwe? Mbona hamumtaji Akwilina Akwilini?

Kila siku ni Ben Saanane, Tundu, Roma Mkatoliki.

Ina maana hao wana nguvu za kikatiba na kiitifaki kuliko wafuatao?

1. Rais Sheikh Abeid Karume?

2. Rais Sheikh Aboud Jumbe Mwinyi?

3. Sheikh Thabit Kombo Katibu Mkuu wa ASP?

4. Abdulla Sadala Mjumbe wa Baraza la Mapinduzi?

Namba 3 na 4 walijeruhiwa kwy mauaji (uhaini) ya Rais Karume Kisiwandui 7 Apr 1972.

Ina maana Roma ana nguvu kuliko hao marais?

Hayo mambo Magufuli amezaliwa ameyakuta, ameingia kwenye urais ameyakuta, hajaondoka nayo ameyaacha pia.

Kama hujui kudurusu historia utaandika zombie tu. Binadamu akichoshwa na habari moja tuu hutamani kusikia ya kale ili ajuwe alikotoka, alipo na aendako (anatamani kurejelea ya kale ambayo ni dhahabu).

Hivi kwanini hamshikii bango kwa kuandika juu ya wafuatao au hamjui historia ambayo ina kawaida ya kuweka kumbukumbu?

1. Bibi Titi Mohammed alifia Afrika Kusini.

2. Abdullah Kassim Hanga Waziri Mkuu wa Znz aliyedumu kwa miezi 3 na nusu tu 12 Jan 1964 hadi 27 Apr 1964.

3. Abdulaziz Twaha Znz.

4. Fr. Joseph Anselmo Mwagambwa Znz. Alishambuliwa kwa tindikali.

5. Prof. Abdulrahman Babu. Mkimbizi.

6. Oscar Kambona. Mkimbizi.

7. Kassanga Tumbo. Mkimbizi.

8. Hussein Shekilango Waziri wa Maliasili. Ndege ndogo aliyopanda ilianguka Monduli milimani. Habari za kuvumishwa zinadai ndege ilishambuliwa na majangili. Shekilango aliacha rekodi ya ushupavu kwy wizara hiyo ngumu duniani.

9. Edward Sokoine Waziri Mkuu wa JMT. Msafara wake uliingiliwa na kugharimu uhai wake. Operesheni yake dhidi ya wahujumu uchumi ilimjengea kutopendwa na waovu kama Magufuli alivyokuwa hapendwi na waovu. Nilishuhudia wafanyabiashara wakimwaga ela kwa tipa (binua mchanga) mtoni kwenda ziwani na wavuvi wakaacha kuvua samaki wakawa wanavua ela tu, vijiji vikatapakaa ela. Nyerere ikambidi akabili anguko la uchumi kwa ela kuzagaa kwa kubadili noti kuleta mpya na walioenda na mifuko ya ela kuzibadili benki waliswekwa ndani. Mbona Magufuli tuu ndiyo nongwa eti kanyang'anya watu ela! Kwanza Sokoine hana legacy ya kuonekana kwa macho ukimlinganisha na Magufuli.

10. Lt. Gen. Imran Kombe.

12. Stan Katabalo.

13. Saed Kubenea.

14. Adam Mwaibabile (aliwekwa kizuizini bila kupelekwa Kortini na kupigwa marufuku mkoa wa Ruvuma kwa ripoti zake za uchunguzi dhidi ya wakubwa hadi hapo nguvu za kalamu za umma wa wanahabari zilipomtoa kizuizini na kufikishwa Kortini na kuhukumiwa kihalali kwa kosa la kuhujumu usalama wa taifa kufuatia kujipatia nyaraka za siri zilizoandikwa kumzuia kupewa vibali vya kazi zake. Alikufa 1 Feb 2007 kwa matatizo ya figo).

15. Daudi Mwangosi.

16. Dr. Stephen Ulimboka.

Ijulikane kwamba Saanane, Tundu na Roma siyo mashujaa wa nchi hii hadi wasujudiwe kihivyo.

Mtu kuwa shujaa wa taifa kuna vigezo vinavyozingatia maisha yake chanya na hasi. Umma haujui upande hasi wa Saanane, Tundu na Roma ili uone kama wanatosha kuwa mashujaa.

Tundu mwenyewe hilo analijuwa vizuri ndiyo maana alipambana Bungeni kuondoa jina la Dr. Lawrence Gama kwy orodha ya mashujaa kwy Makumbusho ya taifa Songea.

Abdallah Said Fundikira alikuwa mpinzani lakini kwa nguvu ya katiba, sheria, mila na desturi alitambuliwa kama shujaa wa taifa kwa wadhifa wake wa Chifu wa Unyanyembe. Mfumo huo huo alioishi kuupinga ndiyo huo haukuwa na choyo ya kumtambua kama shujaa wa taifa.

Tundu hili analijuwa, sasa kama alimpinga Dr. Gama kutambuliwa kama shujaa mbona hampiganii Roma Mkatoliki et al watambuliwe kama mashujaa?

Magufuli mwenyewe hakuwa mpigania uhuru, ameingia kwenye orodha ya mashujaa wa taifa kwa nguvu ya katiba iliyompa wadhifa wa kiongozi wa nchi (rais). Sasa Tundu, Saanane na Roma walipigania uhuru?

Kumsemasema Magufuli kila siku ili achukiwe na umma wote ni kumpa umaarufu bila kujuwa. Hiyo ni kumsujudia ambako ni sawa na kumuabudu na ghadhabu ya MUNGU haitawaepuka maana MUNGU ni mwenye wivu.

Hatuwezi kufungua ukurasa mpya tukamwacha Magufuli akapumzika? Hatuna habari zingine za kuandika? Kweli nimeamini Magufuli hafutiki kwa kemikali yoyote duniani. Kama mmenasa kwa Magufuli anayewakera mjuwe watu wenye vinasaba kama vyake wataendelea kuzaliwa hivyo mjiandae kukereka milele yote.

Maswali ya msingi tunayopaswa kujiuliza ni haya:-

1. Mauti ya Magufuli kama yanapaswa kufurahiwa YAMELETA MABADILIKO GANI NAFUU KWENYE NCHI? Watz wote 100% wanafaidika na kifo chake?

2. Uhai wa Magufuli kama unapaswa kufurahiwa ULILETA MABADILIKO GANI NAFUU KWENYE NCHI?

Tusipokuwa makini na kumsemasema Magufuli ipo hatari inatunyemelea ya kumfanya Idol (kama ambavyo Nyerere amefanywa Mtakatifu na Wakatoliki) na watazuka watu watatumia uhuru wa katiba wa kuabudu utakacho kujenga sanamu kubwa ya Magufuli na kwenda kuiabudu kwa kuiomba iwape majibu ya matatizo ambayo serikali imeshindwa kuwapa. Ni hapa ndipo Idol itakuwa na nguvu kuliko kiongozi aliye hai.

Kama Wakatoliki wamempa Nyerere kuwa Mtakatifu iko siku zitazuka dhehebu au dini nyingine nazo zitamsimika Magufuli kuwa Mtakatifu wao (na hapa pia ndipo tutakapopima kauli ile ya Makamba ya wema na wabaya)

Caucasians wenyewe wanatamani wangepata kinasaba chake wangeenda kuchunguza kama kweli alikuwa mwafrika 100%.

Msiba wake kwa kauli ya PM ulifuatiliwa na watu 3.5 bl kati ya watu 7.5 bl wa dunia.

Marais 14 duniani walisitisha kazi kwa muda kufuatilia maziko Kijijini Mlimani Chato kwa njia ya TV.

Viongozi wa nchi na serikali zaidi ya 20 hawakujali Uviko-19 na wakahudhuria maziko. What if kama Uviko-19 isingekuwepo? Tz pangetosha? Siingekuwa kama nyomi la Kombe la Dunia!.

Kwa mara ya kwanza nilishuhudia wapiganaji (maaskari) wakitokwa machozi hadharani Kijijini Mlimani.

Kiongozi wa nchi ni nembo ya nchi, ukimdhihaki umeidhihaki nchi yako na ukiidhihaki nchi yako umejidhihaki mwenyewe (wewe ni mtumwa)

Watz tunatia aibu. Hata kwenye forums za ughaibuni Watz wanatia aibu. Watz wanashindwa kujenga hoja. Hawawezi kutengeneza mahusiano ya maudhui/content, muktadha/context na mantiki/logic. Hawana maarifa ya Critical Thinking/Kufikiri kwa makini na Critical Reasoning/Kujenga hoja kwa umakini. Watz wakipewa changamoto wanaishia kutukana (wanajibu hoja kwa matusi na dhihaka badala ya kujibu kwa point)

Screenshot_20221225-135246.jpg
Screenshot_20221225-150041.jpg
 
Mkuu kwema!

Mbona kama leo nimesoma huko juu kidogo umeandika kua "Magufuli hakuamini kama Mungu yupo na alijiona yeye ndio Mungu mtu na alikua na ubaya" je ina maana kwa statement hizi wee ulitaka aamini kua Mungu yupo au lah.

Niimewasilisha
Hapana, hiyo ni logical non sequitur tu.

Nilikuwa naonesha unafiki wa wanasiasa tu.

Kuamini au kutoamini uwepo wa Mungu peke yake hakuna maana mtu ni mzuri au mbaya. Na hivyo, nikisema mtu fulani aliamini au hakuamini Mungu, maana yake ni hicho ninachokisema tu, haina maana ningependa aamini au asiamini Mungu.

Kwa sababu, unaweza kuwa mtu unayeamini Mungu ukawa muuaji.

Unaweza kuwa mtu unayeamini Mungu ukawa unapenda na kusaidia watu.

Unaweza kuwa mtu usiyeamini Mungu ukawa muuaji.

Unaweza kuwa mtu usiyeamini Mungu ukawa uanapenda na kusaidia watu.
 
Wote waliohusika kumsema Magufuli kwenye zile sauti zilizovuja, wote walipotezwa kisiasa kasoro Nape na Makamba.

Ngeleja japo hakuwa mshiriki mkubwa na kuwa wa kwanza kuomba msamaha lakini alipotezwa kwenye ubunge baada ya Magufuli kumfadhili mshindani wake.

Membe alifukuzwa, Kinana nae akawa suspended kwenye chama(hata hivyo baadae Magufuli alimrudisha licha ya Kinana kutoomba msamaha rasmi).

Lakini Nape na Makamba japo ndio walikuwa viongozi wakuu wa uasi ule, Magufuli aliwaacha wakapita kwenye kura za maoni ndani CCM na majina yao hakuyakata na wakarudi bungeni na sasa ni mawaziri wenye nguvu kwenye Serikali ya Samia.

Sasa nauliza kwa nini Magufuli alikuwa anaogopa kuwaadhibu hawa watu?

Leo hii wafuasi wa Magufuli wanateseka sana wakiona Nape na Makamba wanavyotesa na kuvimba huku wakiwatupia vijembe.
Labda ni wataalamu wa yale magoli ya hand balls ⚽️ 😅🤓
 
Back
Top Bottom