Kwanini Makamba na Byabato wametolewa wote Wizara ya Nishati na wote kupelekwa Wizara ya Mambo ya Nje?

Mambo yangekuwa yanakwenda vizuri asingetolewa pale ili akamilishe alichokianza Ila baada ya mambo kwenda mrama wameamua kumpeleka sehemu ambayo hatoonekana sana kufeli kwake.

Nishati safi ya kupikia ni siasa kama siasa zingine zilizopita mfano kilimo kwanza sijui matokeo makubwa sasa😁acheni kufanya maisha ya watu usanii hiyo gesi bibi yangu uwezo wa kununua na kutumia hana ugawaji wa mitungi ndio unakupa mihemko acheni kucheza na maisha ya watu.
 
Nnasemajee, kazi imefanyika kubwa sana kwa muda wake aliokaa contrary kwa mnavyotaka kutuaminisha.


Ukitaka kuzitafuta takwimu utazipata.
 
Jamani kunamtu anajua kwanini hawa mabwana wameondolewa Nishati na wote wamepelekwa mambo ya Nje?
Ilitakiwa na bodi ya Tanesco ukiweka na maharage ndani nayo iondolewe au ipelekwe mambo ya nje.
 
Wamejenga teamwork nzuri

Ila foreign palitakiwa Naibu Waziri kutoka Zanzibar ila hawa January na Byabato wanatoka mkoa Mmoja!
Byabato mbunge wa Bukoba Kagera na January Bumbuli Tanga,huo Mkoa mmja vipi?

Binafsi nilipendelea Doto Apewe Ardhi na Nishati apandishwe Byabato
 
Ukionekana unatumia bwawa kujiandaa na Urais ndio madhara yake.

Huyo alizidi kukusanya vikundi mbalimbali na kuvipeleka huko kuonesha alivyofanikiwa ,hii na Ile ya kugawa mitungi ya gas Kwa wamama ndio vimemtoa.

Hakuna mtawala mjinga Dunia hii eti awe anakuacha unajijenga tuu kienyeji kienyeji ,Bora kama huna interests za Urais unaweza achwa.Wewe hujiulizi.kwa nini Makamba anashambuliwa zaidi? Ni wasaka Urais wenzie ndio wanafanya hayo.
 
Ilitakiwa na bodi ya Tanesco ukiweka na maharage ndani nayo iondolewe au ipelekwe mambo ya nje.
Kwa nini labda? Maharage ni kichwa na amefanya vyema kuwakomesha wapuuzi hapo Tanesco haondoki Leo Wala kesho
 
Kwa nini labda? Maharage ni kichwa na amefanya vyema kuwakomesha wapuuzi hapo Tanesco haondoki Leo Wala kesho
Maharage ndiye mp....zi mkubwa
1. Kapandisha gharama za kuunganisha umeme kutoka 27k hadi 320k
2. Umeme wa JNHEP ulitakiwa ushushe bei ya umeme hadi Tsh 100 kwa KW, lakini huyo mj....ga mwenzako kasema haushuki.

Hata hivyo nampongeza Maharage kwa 'kuwanyorosha" wale wapuuzi wa kitengo cha huduma kwa wateja na wale wa Emergency. Sasa hivi ukitoa taarifa ya tatizo lako lolote la umeme linatatuliwa muda huo huo.
 
Maharage ndiye mp....zi mkubwa
1. Kapandisha gharama za kuunganisha umeme kutoka 27k hadi 320k
2. Umeme wa JNHEP ulitakiwa ushushe bei ya umeme hadi Tsh 100 kwa KW, lakini huyo mj....ga mwenzako kasema haushuki.
Kama amepandisha gharama inakuaje Tanesco ivunje rekodi ya kulinganisha wateja zaidi ya 500k mwaka Jana? Kwa nini tusingeona wakiunganisgwa wengi kabla ya gharama kupanda? Acha blaa blaa zisizo na msingi.

Mwisho Kwa Sasa Tanesco ni profitable chini ya Maharage Chande Sasa wewe unatakaje labda? Shirika life Kwa sababu wewe unataka bei ya chini?

Umewahi jiuliza Kwa nini bei ya maji ya kwenye chupa Dar ni chini kuliko Mikoani?
 
Usifurahie bei ndogo ya maji ya chupa ya Dar.

Mengi ya hayo maji yanatengenezwa na wahuni huko mitaani.

Hii inapelekea mimaji feki kujaa mitaani, hivyo bei kushuka.

Fuatilia statistics za wagonjwa wa tumbo na kuhara kwenye mahospitali ya Dar ndiyo utajua hujui.
 
Huna hoja na hujui kitu.Rudi darasani ukijua hiyo sababu ndio inafanana na Tanesco
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…