Kwanini Matajiri wa siku hizi hawawezi kuishi na watu wengi majumbani mwao kuliko wale wa enzi za zamani?

Tafuta hela uondokane na hayo makasiriko
 
Hebu bill lugano aje atuambie vp yy anaishi na nan
 
Ndumba mzee hao bandugu wanaharibu sana.
 
Dunia imebadilika sana na inaenda kwa kasi
Kukiwa na ndugu wengi hata wachache ni yaleyale tu wote wamekuwa hawana maadili na heshima kama zamani
Mtoto anakuja kukaa kwa mda mfupi au mrefu lakini vituko unaona mara arudi manane ya usiku na ukimkaripia anakunja uso na kumwambia mama yake ooh uncle ananinyanyasa

Watoto na Mali ni Fitna hili tumefundisha kwenye vitabu

Kaa mbali nao kama kuwasaidia wasaidie walipo ila usiwalee zaidi ya yatima

Siku hizi hata uliemzaa anakulia time kama una mali anataka utangulie kuzimu
 
Marehemu Baba aliwalea ndugu kibao, lakini hao aliowalea hakuna hata mmoja anaonyesha fadhila kiduchu tu ya hata kunijulia hali mimi mwakilishi wa Baba.

Kwasababu hii ya waliolelewa kukosa fadhila, ndiyo maana matajiri wa siku hizi hawataki kukaa na ndugu.
 
Sababu wamegundua uadui huanziaga kwa ndugu wa nyumbani mwa mtu.

Ukianza kupata neema ya kipato basi ujue unaingia kwenye short list ya target ya kurogwa na ndugu.

Yaani hawana maana hata kidogo.

Yaani watakuroga pande zote za Dunia kila mtu anakupiga kivyake.

Baba Mungu Jehova na awalipe maana visasi na hukumu kasema viko mikononi mwake yeye mwenyewe.
 
Kweli nimeaamini ya kuwa Dunia haina haki wakati mwingine.

Unaweza kuwa na moyo wa kupenda sana ndugu lakini ukawa mtu wa kupigwa vita na uadui mkubwa bila wewe mwenyewe kujua mpaka Mungu aamue kukufunulia kwa kadiri ya rehema zake!
 
Matajiri wa sa hii ni wachoyo kheeeeee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…