Kwanini Matajiri wa siku hizi hawawezi kuishi na watu wengi majumbani mwao kuliko wale wa enzi za zamani?

Kwanini Matajiri wa siku hizi hawawezi kuishi na watu wengi majumbani mwao kuliko wale wa enzi za zamani?

marehemu Baba aliwalea ndugu kibao, lakini hao aliowalea hakuna hata mmoja anaonyesha fadhila kiduchu tu ya hata kunijulia hali mimi mwakilishi wa Baba.

kwasababu hii ya waliolelewa kukosa fadhila, ndiyo maana matajiri wa siku hizi hawataki kukaa na ndugu.
Yani wa kujulie hali kwani wewe ndo uliwalea, nyie ndo mnajifanyaga miungu watu, na waliolelewa kwenu wasifanikiwe zaidi yenu, roho mbaya tu
 
Mzee wangu hakuwai tajiri ila tumeishi na ndugu zake karibia wote pamoja na bibi na babu nyakati tofauti walikuja wakiwa wanaumwa ,ila hao ndugu mzee alistaafu miaka kibao nyuma hkuna hata mmoja anakuja kumsalimia na sisi watoto tushaondoka hana mtu.

Hata mawasiliano hawana kabisa ila vijana wawili walisoma form one mpaka four wakiwa kwake maana shule enzi izo za secondary vijijini hamna basi wanakuja town kukaa likizo wako kwao..na yupo mmoja ni mtu mkubwa serikalini ila hata kumsalimia mzee wapi.
 
Miaka ya nyuma, hata urudi katika vitabu vitakatifu, watu matajiri waliishi na watu wengi nyumbani na wote walinyooshwa na kutii sheria za nyumbani.

Mfano Nabii Ibrahim alikuwa Bilionea aliyeishi na mamia ya watu kwenye familia yake. Alikuwa hadi anajeshi la watu 300 ambao ni sehemu ya familia yake.

Wazee wetu matajiri wa zamani walikuwa na wake wengi pamoja na watoto kibao. mji ulikuwa na ndugu lukuki hadi wale walioomba jujiunga na undugu. Bado wote walinyooshwa kwa mkono wa chuma, unaweza usisikie hata mtoto anamimba bila kuolewa.

Siku hizi tatizo ni nini?

Unakuta mtu tajiri, hajiamini, anaishi na vitoto vyake viwili na housegirl/Boy na mkewe. Hataki kusikia shangazi, mjomba wala kuarika watu kwake.

Karibuni kwa maoni.
JE uwezo wa wanaume wenye pesa mingi kutiisha familia zao umeshuka?

Je, utajiri wa hofu?

Je, ndugu na marafiki wa zama hizi usnitch na umbea umezidi kiasi kwamba huwezi kuwanyoosha?

Unadhani kwanini
Ni
Wezi
Wambea
Wana wivu
Wanaroga
Halafu wanakula sana
 
Miaka ya nyuma, hata urudi katika vitabu vitakatifu, watu matajiri waliishi na watu wengi nyumbani na wote walinyooshwa na kutii sheria za nyumbani.

Mfano Nabii Ibrahim alikuwa Bilionea aliyeishi na mamia ya watu kwenye familia yake. Alikuwa hadi anajeshi la watu 300 ambao ni sehemu ya familia yake.

Wazee wetu matajiri wa zamani walikuwa na wake wengi pamoja na watoto kibao. mji ulikuwa na ndugu lukuki hadi wale walioomba jujiunga na undugu. Bado wote walinyooshwa kwa mkono wa chuma, unaweza usisikie hata mtoto anamimba bila kuolewa.

Siku hizi tatizo ni nini?

Unakuta mtu tajiri, hajiamini, anaishi na vitoto vyake viwili na housegirl/Boy na mkewe. Hataki kusikia shangazi, mjomba wala kuarika watu kwake.

Karibuni kwa maoni.
JE uwezo wa wanaume wenye pesa mingi kutiisha familia zao umeshuka?

Je, utajiri wa hofu?

Je, ndugu na marafiki wa zama hizi usnitch na umbea umezidi kiasi kwamba huwezi kuwanyoosha?

Unadhani kwanini
zama zimebadilika kutoka kuishi kiujamaa na sasa tunaishi kwenye ulimwengu wa ubepari, kwenye ulimwengu wa ubepari kanuni ni kila mtu afe na tai yake shingoni ukijifanya una huruma ya kuwajaza ndugu zako maskini nyumbani kwako hao hao maskini wanakuangamiza.. kuna mzee mmoja niliwahi kutana naye Tanzania 2018 alianiambia Mtu maskini ni rahisi sana kukumkubali shetani na kuishi naye.. sikumuelewa ila baada ya kupigwa matukio kadhaa nilimuelewaaa, maskini wengi wana roho mbaya sana japo sio wote..
 
Sasa mtu mmoja akajiuliza mnataka watu muwe maskini wa kutupa Mungu asiinue wakuu?! [emoji848]

Wenzetu wachaga tu kwa wastani ndio hawanaga mambo ya uchawi na ushirikina.

Na ndio maana walau wanaendelea.

Lakini the rest ni shida.
 
Wachaga kama majira haya ya siku kuu za mwisho wa Mwaka ni shangwe na furaha kwa jamii nzima kuona mtoto wa fulani kaja na Gari lake,

Kaja na mtoto ,

Kaja na mke au mumewe.

Mtoto wa mwenzie akifaulu mtihani ni fahari ya jamii nzima.

Lakini the rest kuna shida .

Ni kinyume chake.

Wakiona mtu Mungu anamuinua wanatafuta kumshusha chini au kumuangamiza kabisa.

Ndio maana Mungu akaruhusu kwa hasira na kuagiza “ asiachwe Mwanamke Mchawi kuishi” maana yake auliwe.

Mungu mpaka akaandika hivyo usizani uchawi ni jambo la masihara.
 
Kwa niaba yangu binafsi na kwa niaba ya matajiri wenzangu naomba nikupe sababu zifuatazo;
1. Ilishatabiriwa kwamba kadiri siku zinavyoelekea mwishoni upendo wa wengi utapoa (soma Mathayo 24). Na huu upendo ni kwa pande zote. Maskini hana upendo na tajiri hana upendo.
2. Mabadiliko ya mfumo wa maisha wa binadamu. Kadiri maarifa yanavyoongezeka ndo mambo mengi yanavyobadilika ikiwemo LIFESTYLES... Kama zamani tulikuwa tunaishi wengi nyumba moja basi kwa sasa hali ilivyobadilika haiwezekani.
3. Ubepari pia unachangia kwa kiasi kikubwa mambo kuwa hivi. Wenyewe mabeberu wanakuambia NO FREE LUNCH IN AMERICA. Yaani huruma hakuna. Sasa nasi tulipogeukia siasa za mabeberu tumejikuta tunaiga hadi mfumo wao wa maisha usio na huruma hata chembe.
4. Kutokana na upendo wa wengi kupoa pia usalama umepungua sana. Siku hizi adui yako ni mtu wa karibu. Wahanga wa matukio ni sisi matajiri. Wakati wa mvua matajiri wengi hukesha macho kwa kuhofia majambazi ambao hupenda kuvamia mvua ikinyesha.
5. Roho mbaya. Hakuna namna ili uweze kudumu na utajiri lazima uwe na roho mbaya. Muda wote tajiri anawaza kupunguza matumizi ili kuongeza faida. Sasa kubeba kijiji kizima nyumbani kwake inakuwa ni hasara. Hata ikitokea tumechukua ndugu kukaa nae tunachukua yule ambaye angalau mwenye manufaa. Mfano wachaga wao huchukua ndugu anaoweza kuwaweka dukani au kwenye biashara yake nyingine ili kufidia gharama. Hata kwenye mapenzi matajiri wengi mabahili sana kwa mademu kuliko maskini.
 
Binafsi isingekuwa hayo mambo ya uchawi na ushirikina wala nisingejali sababu Mungu ni Pendo na ametuagiza kuwa wakarimu kwa wageni.

Ni Baraka sana kuwapenda ndugu Na kuwakarimu wageni maana kwa kufanya hivyo wengine huweza kuwakaribisha
Malaika wa Mungu ndani ya Nyumba na familia zao.
Na akiingia Malaika basi ni baraka kuzidi sana Na ustawi full package.


Na huwa ni fahari kuwatendea ndugu mema na watu wengine pasipo kutaka kujionesha.

Lakini linapokuja swala la uchawi na ushirikina ndipo huwa nachoka kabisa !
 
zama zimebadilika kutoka kuishi kiujamaa na sasa tunaishi kwenye ulimwengu wa ubepari, kwenye ulimwengu wa ubepari kanuni ni kila mtu afe na tai yake shingoni ukijifanya una huruma ya kuwajaza ndugu zako maskini nyumbani kwako hao hao maskini wanakuangamiza.. kuna mzee mmoja niliwahi kutana naye Tanzania 2018 alianiambia Mtu maskini ni rahisi sana kukumkubali shetani na kuishi naye.. sikumuelewa ila baada ya kupigwa matukio kadhaa nilimuelewaaa, maskini wengi wana roho mbaya sana japo sio wote..
Jibu sahihi ndo hili... CAPITALISM!
 
Mambo ni mengi kwa kweli. Imagine ndugu anasaidiwa, lakini huyo huyo ndio chanzo cha matatizo kwa anatoa msaada. Binafsi nimeshuhudia hili, lakini pia wapo ndugu wengine waliamua kujitenga kabisa na mambo ya ukoo sikuwahi kujua sababu. Kwa umri wangu mdogo tiyari namimi naona hatihati ya kujiweka pembeni ipo. Unaweza ukajinyima ili usaidie na ndugu wengine lakini bado ukaonekana mbaya.
 
Umagharibi unatuumiza, tunafata maisha ya magharibi, tunageza kila Jambo.

Hatimae siku hizi hatuna mapenzi, mtu anaishi miaka dahari hajuk jirani yake anaishi vipi, ni kwenye gari, akirudi ndaani.
Nyumbani ni yeye na watoto zake wawili, mbwa na wafanyakazi.

Hilo moja, pili(nazungumzia mpaka masikini) Maisha yamebadilika, mahitaji siku hizi si nguvu ni pesa inahiitjika, zamani unaishi na mtoto wa mjomba, sijui nani na nani, ila una shamba kubwaa nguvu ya kulima((nguvu kazi ipo) una ng'ombe kadhaa. Asubuhi mnakamua lita kadhaa ndani mipunga kibao na mahindi, nyuma kisamvu, matembele, maboga maisha yanasogea. Ila siku hizi kimbembe, ugali tabu, huna hela hujala, mjini una chumba na sebule tu.
Umbea umezidi siku hizi

Ndio maana raia wameamua kuishi kivyaovyao.
 
Back
Top Bottom