Kwanini mbwa hugongwa sana na magari barabarani?

Kwanini mbwa hugongwa sana na magari barabarani?

Juzi nimesafiri kutoka mkoa wa Dar es Salaam kwenda mkoa wa Shinyanga. Kijiografia, ni umbali mrefu, ambapo magari ya abiria hutumia si chini ya masaa 16 kufika mwisho wa safari.

Sasa kuna jambo moja nimeliona katika safari hii ndilo nataka wajuvi wa mambo ya wanyama watueleze, kwani ni jambo la kufikirisha kidogo!

Mnyama mbwa, ni miongoni mwa wanyama wanaotumiwa na binadamu katika shughuli mbalimbali za kijamii, kama ulinzi, kunusa, nk. Lakini pia, mnyama huyu anaweza kufundishwa michezo mbalimbali na akamudu kuicheza sawia.

Kwa muktadha huo, inaonyesha kuwa, mbwa ana akili pengine kuliko wanyama wengine, na ndiyo maana ni rahisi kwake kufundishika, tofauti na wanyama wengineo (most).

Sasa juzi katika safari yangu hiyo, nimeshuhudia si chini ya mbwa 6, mahala tofauti tofauti, wamegongwa na magari. Hapo ndio najiuliza, inakuwaje mnyama mwenye akili kuliko wengine; kama mbuzi, punda, paka, kuku, nguruwe, kondoo, ng'ombe, nk, anagongwa na magari wakati hawa wenye akili kidogo hawagongwi?!

Wakati tunajibu swali hili, majibu yetu tuhusianishe na ubongo wa mbwa, na sio factor nyingine kama uwingi wao, kukosa matunzo, kichaa cha mbwa, nk; kwani hizi ni hoja nyepesi. Mbwa wanaoongelewa hapa ni wakamilifu kwa mitazamo yote.

Mtu anaweza kuona nimeuliza jambo la kijinga, lakini wataalamu wa wanyama najuwa watakuja na sababu za msingi kuhusiana na jambo hili! Au wenzangu hamjawahi kijiuliza kwanini mbwa anagongwa kirahisi sana na magari kuliko wanyama wengine?
Moja ya sababu ya kugongwa kwa mbwa ni la kibaiolojia zaidi tena wanaogongwa ni mbwa dume ipo hivi,mbwa jike anapokua katika heat period kwa binadamu wanawake tunasema wanapokua ovulation( yani siku tayari ya kupata mimba) mbwa majike uwa wanatoa harufu kama ishara yakuwa tayari kwa hilo tendo hivyo kutokana na uwezo wa mbwa kunusa mbwa dume anaweza akaisikia hiyo harufu toka mbali na inapelekea kuanza kutafuta mwelekeo wa hiyo harufu akitumia hisia zaidi na msukumo wa homoni bila kutumia akili katika matendo yake hivyo kutokujali uwepo wa barabara au magari ilimradi lengo lake litimie kwenye mwelekeo wa harufu kwenda kutimiza haja yake hapo ndipo huwa wanapogongwa!
 
Kuvuka barabara kunahitaji calculation zenye uhalisia za haraka sana na ambazo zinahitaji realtime respond.

Unapovuka barabara kwanza unakuwa umeshacalculate mwendokasi wako wa chini na wa juu unaoweza kukuvusha bila kugusana na object inayocross.
Pili calculation za haraka huwa zinafanyika kuhusu umbali wa gari inayopita na mwendokasi wake halisi kisha kuwianisha na mwendokasi wako wa juu na chini kisha kutoa jibu la haraka kwamba uvuke kwa mwendokasi gani ili usigongwe na gari.
Hesabu zote hizi zinafanyika ndani ya sekunde 1 na kukupa uamuzi wa kuvuka.

Sasa tatizo la mbwa kwanza hizo hesabu hapigi zote, anavuka tu kwa spidi.
Pili vyombo vinavyotembea kwa kuzunguka matairi, mbwa ana-detect kama kimesima, kikikaribia kumgonga ndio anashituka na anakwepa kwa kujiokoa.
Kuthibitisha hilo, mbwa anakuelewa vizuri ukiwa unamsogelea na baiskeli huku unazungusha pedeli kuliko ukiwa unamsogelea bila kuzungusha. Anakuona kama umesimama tu.

Nimejibiwa hapa na mtu mmoja.
 
mbwa wanagongwa sana kwa sababu moja tu
Kwa kawaida mbwa jike anapokua anajiskia kupandwa huwa anatoa harufu flani
Ambayo mbwa dume
Anapoiskia harufu hiyo anataka lazima afike kwa jike hilo akale mzigo

Sasa inapokea harufu hiyo inatokea upande wa pili wa barabara hapo ndio ajali inapomkuta
Maana ile harufu inakua imeshamvuruga kiasi ambacho anakosa umakini wa kuhahakisha usalama wake anachojali wakati huo ni kuwahi eneo la tukio tu.
 
Kigezo kimojawapo cha mnyama yeyote (akiwemo binadamu) kufundishika ni lazima awe na akili. Mnyama atashikaje mafunzo kama hana akili?
Ni kweli mbwa anafundishika hilo halijustify kwamba anaweza kuwa na akili maeneo yote, kuna wanafunzi wanaanza shule hawajawahi kushika nafasi ya tatu yeye ni MOJA hilo haliwapi guarantee kwamba wao ni bora kuliko yule wa tatu mwishoni
Tunayaona hata kwenye maisha halisi, halafu umejifunga kwenye factor za ubongo Ila kuna mtu amekuelekeza kuhusu vision hata mm KWA kiasi fulani nimemuelewa

Ungeruhusu mjadala uwe flexible KWA factor tofauti kama mfano wa mbwa koko kwahiyo wanatanga tanga hivyo risk yao ni kubwa pia


Umeweka mada KWA angle MOJA ilihali hata wewe hujui kama wale mbwa ni wazima au laah!! Maana uliwakuta chini wamekufa na ukushuhudia na huna historia ya mbwa hao
 
Mbwa labda umkanyage na tyre ndiyo unaweza kumuua lakini ukimbamiza tu anapona.
 
Ni kweli mbwa anafundishika hilo halijustify kwamba anaweza kuwa na akili maeneo yote, kuna wanafunzi wanaanza shule hawajawahi kushika nafasi ya tatu yeye ni MOJA hilo haliwapi guarantee kwamba wao ni bora kuliko yule wa tatu mwishoni
Tunayaona hata kwenye maisha halisi, halafu umejifunga kwenye factor za ubongo Ila kuna mtu amekuelekeza kuhusu vision hata mm KWA kiasi fulani nimemuelewa

Ungeruhusu mjadala uwe flexible KWA factor tofauti kama mfano wa mbwa koko kwahiyo wanatanga tanga hivyo risk yao ni kubwa pia


Umeweka mada KWA angle MOJA ilihali hata wewe hujui kama wale mbwa ni wazima au laah!! Maana uliwakuta chini wamekufa na ukushuhudia na huna historia ya mbwa hao
Nimeiguide hiyo topic kwa makusudi ili wataalamu watuchambulie jinsi mfumo wa ufahamu wa mbwa ulivyo. Hujawahi kukutana na mbwa anaona gari linakuja halafu yeye anacross barabara. Anafika katikati ya barabara, huku anaona gari imekaribia, anageuza kurudi alikotoka. Wakati anababaika hivyo ndipo gari humkuta na kumgonga. Hapo ndipo ninapohoji, tafsiri ya ubongo wake ikoje? Mbona wanyama wengine hawafanyi hivyo? Hiyo ndio sababu ililiyonifanya nilimit hili swali kwenye ubongo! Unaweza kuwauliza madereva juu ya hili ninalosema, au kama madereva mko humu, je, ninachosema ni uwongo?
 
Nimeiguide hiyo topic kwa makusudi ili wataalamu watuchambulie jinsi mfumo wa ufahamu wa mbwa ulivyo. Hujawahi kukutana na mbwa anaona gari linakuja halafu yeye anacross barabara. Anafika katikati ya barabara, huku anaona gari imekaribia, anageuza kurudi alikotoka. Wakati anababaika hivyo ndipo gari humkuta na kumgonga. Hapo ndipo ninapohoji, tafsiri ya ubongo wake ikoje? Mbona wanyama wengine hawafanyi hivyo? Hiyo ndio sababu ililiyonifanya nilimit hili swali kwenye ubongo! Unaweza kuwauliza madereva juu ya hili ninalosema, au kama madereva mko humu, je, ninachosema ni uwongo?
Sawa mkuu mekuelewa
 
Macho yake yapo mbele hayapo pembeni mbuzi na ng'ombe si rahis kugongwa ndo maana hadi buguruni mbuzi wamavuka barababra kuzidi watu
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Interesting topic! Kwa mtazamo wangu, ni mchanganyiko wa sababu zinazofanya mbwa wengi kuwa wahanga wa ajali za gari. Kikubwa nadhani ni upekepeke wa hao wanyama, mbwa huwa wakati mwingine ni wajuaji sana.

Kuna mbwa wa jirani, Mama Kadada ambae jina lake alikuwa anaitwa Tom. Dog Tom ilikuwa lazima aende sambasamba na kila gari inayopita karibia na nyumbani. Anga za usiku, Tom ndio alikuwa mwenyekiti wa vikao. Pale jirani walikuwa wanakuja Mbwa kama hamsini kumfuata huyu mbwa wa Mama Kadada.

Niliporudi kutoka masomoni, nikaambiwa Tom alifariki kwa kugongwa na gari. Tabia za mbwa ni tofauti na paka. Paka ni kama vile wanajua kuepuka ajali kuliko mbwa.
Eti mwenyekiti wa vikao. Lol
 
Moja ya sababu ya kugongwa kwa mbwa ni la kibaiolojia zaidi tena wanaogongwa ni mbwa dume ipo hivi,mbwa jike anapokua katika heat period kwa binadamu wanawake tunasema wanapokua ovulation( yani siku tayari ya kupata mimba) mbwa majike uwa wanatoa harufu kama ishara yakuwa tayari kwa hilo tendo hivyo kutokana na uwezo wa mbwa kunusa mbwa dume anaweza akaisikia hiyo harufu toka mbali na inapelekea kuanza kutafuta mwelekeo wa hiyo harufu akitumia hisia zaidi na msukumo wa homoni bila kutumia akili katika matendo yake hivyo kutokujali uwepo wa barabara au magari ilimradi lengo lake litimie kwenye mwelekeo wa harufu kwenda kutimiza haja yake hapo ndipo huwa wanapogongwa!
Hii mpya mbna, khaaaah
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Tatizo hapo ndugu yangu, ni dogo tu, umeshindwa kutofauti nyakati, Neno, Wakigongwa, na wamegongwa unaweza kuona kama neno moja, ila linatofautisha nyakati, nadhani umenielewa.
safi sana
 
Nimekuambia hivi, juzi nimesafiri kutoka Dar es Salaam mpaka Shinyanga, nimeshuhudia mbwa 6:wamegongwa, lakini sijashuhudia mtu hata mmoja amegongwa (simaanishi kuwa nataka mtu agongwe), hivyo unaweza kuona uwiano huo. Kama utataka kutafuta uhalisia wake, basi unaweza kukuta akigongwa mtu mmoja, basi watagongwa mbwa 1000 (uwiano). Hivyo, kugongwa watu hakuondoi ukweli kuwa mbwa wanagongwa kwa kiwango kikubwa sana, pengine kuliko wanyama wengine wote. Kwahiyo hoja yangu ina mashiko
kuna mtu alijaribu kukutetea hapo kwenye bold akidhani hukumaanisha hvyo
 
Back
Top Bottom