Kwanini Mmiliki wa Samaki Samaki kapewa Kuwekeza Coco Beach sasa ila Kipindi cha Hayati Magufuli hakupewa?

Kwanini Mmiliki wa Samaki Samaki kapewa Kuwekeza Coco Beach sasa ila Kipindi cha Hayati Magufuli hakupewa?

Ngoja nikutumie no yake umuulize
Screenshot_2023-06-19-07-57-44-314_com.whatsapp.jpg
 
Hilo eneo (Coco Beach) Hayati Magufuli alikataa kabisa kupewa Watu (hasa Matajiri) wawekeze hapo akisema kuwa paachwe wazi ili hata Masikini akina GENTAMYCINE tuwe tunakuja Kutembea, Kuogelea na Kupunga Upepo mwanana wa Baharini (wenye Afya) bila tatizo.

Cha Kushangaza na Kusikitisha tayari sehemu ya Eneo la Coco Beach ameshapewa Mwekezaji (Mfanyabiashara) maarufu Mmiliki wa Samaki Samaki na kuanza Kuzungushia kabisa na Mabati Eneo Kubwa tu ambalo huko nyuma lilikuwa likikaliwa na Sisi 'Beach Goers' tuliotukuka huku tukipunguza Mawazo ya Shida zetu za Kimaisha.

Na Wenye Akili tunajua huyu Mfanyabiashara Samaki Samaki nyuma yake kuna akina nani, anafanya Biashara gani nyingine ya Siri isiyotakiwa hivyo kupewa Kwake hilo eneo ni Kututhibitishia kuwa kile alichokikataa Hayati Magufuli sasa kinafanyika na Siku si nyingi Matajiri na Mafisadi watagawana Coco Beach yote na Masikini kuingia hapo kwa Hela au ukijua Kuogelea kama GENTAMYCINE unakuja huku maeneo ya Police Officers Mess unaogelea taratibu na kwa Mikogo huku ukielekea usawa wa Coco Beach na ukifika unatoka Majini unafanya yako na Maisha mengine yanaendelea.

Na nasikia hata Beach nyingine ya Sisi Masikini ya Kawe Beach nayo pia mnataka kuwapa Matajiri na Mmoja ni Rafiki wa Karibu wa Mtoto wa Kiongozi Mmoja Mstaafu ( ambaye Nyumba yake ya sasa inatizamana na Kawe Beach ) ili awekeze na pia muwafukuze Wavuvi walio Jirani nae kwa Kigezo cha kulinda Usalama wake.

Kwakuwa mmeamua taratibu kutunyang'anya Sisi Masikini akina GENTAMYCINE Beach zetu zote za Coco Beach na Kawe Beach tunaomba mtuombee kwa DP World watutafutie Beach mpya ili tuwe tunaenda huko kwani yawezekana hawa ndiyo wakawa na Uchungu wa Maisha Magumu ya Watanzania kuliko hata ilivyo kwa Viongozi Wetu ambao pia ni Watanzania Wenzetu.
sawa,nimekupata
 
alipokuwa wizara ya ardhi lake oil imeongeza vituo vya mafuta vingi sana mijini kapata ardhi nyingi sana. na ardhi nyingi kahodhi huyu akjnamzidi Dp world
Lake oil sasa hivi wamechukuwa mpaka viwanja vya Tazara na Kujenga kiwanda cha sulphur.

Sasa hivi lake oil wamedhamiria kuwauwa kwa Sumu ya sulphur wakazi wa Kiwalani, Minazi mirefu, Temeke sandali na maeneo Jirani na hayo.
 
Mwambie watafanya Siri Mambo yao ila GENTAMYCINE nina Uwezo mkubwa wa kujua Taarifa za Ndani na huwezi Ukanificha nikitaka kujua.

Iambie hiyo Familia ya huyo Fisadi na huyo Mwanae Fisadi Aliyeshindikana kwakuwa anaogopwa na walio Juu kuwa tunajua aliye nyuma ya huyo Samaki Samaki ni Wao na Yeye hapo Wamemtanguliza tu ili Kutuzuga tuliowazidi kwa Akili, Upeo na Maarifa.
Umewazidi AKILI, UPEO na MAARIFA na bado unashindwa kuwazuia katika huo 'ufisadi' wao mnaoupigia kelele kila siku. We kweli POPOMA, hujui tu hata unaongea nini!!

Mwenye akili, upeo na maarifa hana muda wa kusugua kisigino cha mguu kwenye jiwe kisha kukaa barazani kumsengenya na kumzushia mtu day in, day out. Na kama ikimlazimu kumsema mtu kwa mabaya yake, basi hufanya hivyo kwa USHAHIDI usio na shaka na sio zile blah blah za wenye njaa na wivu.

KUUUBWA zaidi we popoma, akili, upeo na maarifa havitangazwi kwa nguvu; vitajionyesha vyenyewe......na ikilazimika kutangazwa basi hutangazwa na mashuhuda (yaani sisi tunaosoma mabandiko yako ndo tutaona hayo maupeo, akili na maarifa na sio wewe kutulazimisha kuona vitu hivyo wakati havipo).

Uwe na Jumatatu njema!
 
Ulidhani Ridhiwani Kikwete aliwekwa wizara ya Ardhi kwa bahati Mbaya?

Ndio maana huyu mtoto huwezi kumuona anakwenda Umra Saudi Arabia anaweza akafia hukohuko kwa roho Mbaya aliyorithi kwa babake.y
Baba mtu roho mbaya,mtoto karithi ,anafanya atakacho ......HV fisadi kama yule ,muuza madawa kweli wa kumpa uwaziri kweli???
Shame Tanzania.
#KataaMuungano,Muungano ni utapeli
#Dai katiba
 
Mbona yule mtoto wa kiongozi nchi nzima ni yake nilienda Gairo nikaonyeshwa huu mlima ni wake umejaa madini,nikaenda Mahenge nikaambiwa huu msitu wote wanakijiji walihamisha ni kupisha hifadhi Siri umejaa madini tupu za chini ni wake anashirikiana na wa yuesi ei,Kila mkoa utasikia ili eneo ni lake,huyu mtu ni tajiri sana ee.
Bado kwenye malori story ni nyingi
Ni uzushi tu.
 
Mkuuu kumbe tukiachana na mambo ya YANGA kumbe upo vizuri upstairs??!
Dr Matola PhD ni very Intelligent ( japo zamani tulikuwa Maadui kweli kweli hapa JamiiForums hata Malaika wa Mbinguni wanajua ) ila likija tu Suala
la Yanga SC yake huwa nadhani ama kuna Bange anavuta au anakunywa Gongo kwani hata kama Jambo likiwa la Kweli Yeye atalikataa tu.

Kwa mfano kuna Uzi wa kuihusu Yanga SC nakuja nao muda si mrefu na Nitamtagi na ukiona haukatai au haukosoi naenda Kukojoa Makusudi pale MP1 Makongo ili MP Afande Victor na Afande Peter wanigombee kama Mpira wa Kona kwa Kunipiga na Kuniadhibu.

Cc: Bujibuji Simba Nyamaume
 
Binadamu tumejaaliwa unafki sana,,,lakini naamini asilimia kubwa tungebahatika kuwa kwenye nafasi aliyokuwa nayo huyo riz,,tungeyafanya haya haya anayo yanafanya tena wengine nafikiri ingekuwa zaidi ya haya!!Ni nafasi yake acha aitumie,,nawe tumia nafasi yako kwa levo na uwezo wako pia ndio asili ya ulimwengu hatuwezi fanana kamwe,,hata mbinguni malaika wanatofautiana uwezo,,hawalingani kama wapo lakini!!
 
Back
Top Bottom