Kwanini Mo 'hatamuweza'Manara

Kwanini Mo 'hatamuweza'Manara

Wewe unaumia nini kwa utapeli wa Mo pale Simba?
Mafanikio ya muda mfupi yasiwafumbe macho, mlumbuke pia hela sio kitu pekee kinacholeta mafanikio kwenye team, kuna hitajika vitu vingine pia.Kuna tena huko Duniani zia hela ila mpaka leo Zina miaka mingi bila makombe.

Kwa hilo la Manara,kila shabiki wa Simba Sc anaejitambua atakuwa amepata picha ya kinachoendelea pale.
 
Bila huyo tapeli Simba ingekua hapo ilipo?
Shida sio Simba ulipo, shida ni kutaka kujifanya Simba Sc kama kampuni lake.

Kwahiyo kumbe hatutakiwi kujadili kinachoendelea simba kwasababu ya nafasi iliyopo? Vipi siku ikishuka hapo ilipo? Au unadhani pesa pekee ndio imefanya Simba Sc iwe hapo? Kama unafikiria hivyo juilize kwanini AZAM FC hawako hapo.
 
Shida sio Simba ulipo, shida ni kutaka kujifanya Simba Sc kama kampuni lake.

Kwahiyo kumbe hatutakiwi kujadili kinachoendelea simba kwasababu ya nafasi iliyopo? Vipi siku ikishuka hapo ilipo? Au unadhani pesa pekee ndio imefanya Simba Sc iwe hapo? Kama unafikiria hivyo juilize kwanini AZAM FC hawako hapo.
Sawa, MO siku mbili hizi anatangaza kuachana na Simba, huyo Albino hawe yeye Sasa mfadhili wa Simba yeye na ukoo wake, si mnasema MO anajinufaisha yeye club hainufaiki,Sasa anaondoka hili Simba hifanye vizuri zaidi
 
Tukiachana pia na ulichokizungumza, Kisheria Haji amemmpiga bao MO.

1. Kutumikishwa kinyume na Sheria za Uajiri kwa miaka sita bila mkataba.

2. MO kumdukua Manara bila ya idhini yake. Hili ni kosa kubwa sana.

MO yupo pale kimaslahi huku akilia kuipambania Simba kwa jasho na damu. Upuuzi tu.
Utopolo mumepata kichaka cha kujifariji baada ya kuukosa ubingwa kwa miaka minne hii na inaelekea mtaendelea kuteseka kwani msimu ujao tunabeba makombe yote kama kawaida yetu.
 
Utopolo ni wahanga wakubwa wa uwekezaji wa Mo Simba. Msimu ujao tunabeba makombe yote kama kawaida yetu,endelezeni majungu tu na usajili wenu wa hao wacheza ndombolo mliowaokota kwa bei che. Simba Nguvu Moja
Bilashaka wewe siyo mdau wa mpira .Wanaojua mpira wanajua kwamba si rahisi kihivyo.Muda utasema hata zile mechi ambazo Simba anacheza na Yanga mlikuwa mnasema lazima mtashinda tena kwa goli nyingi kilichokuwa kinawakuta unakifahamu mpaka mnapoteana na kulaumiana subiri mechi ya Tarehe 25/9 ,mkipigwa kipigo Cha mbwa mwizi huo mvurugano wake utakuwa zaidi ya huo wa Sasa wa vigoli kimoja kimoja mpaka Hindi janja alitishia kujiudhuru na kuacha timu.Tusubiri muda utasema
 
Kuna mambo nayafikiria, yananifanya nisiamini kuwa Manara amekosea ktk hili sakata.

Je ile tume sijui shirikisho la ushindani wa kimasoko/hisa lilikosea kuhoji uwekezaji wa Mo? Walikosea kuuliza Mo amekuwaje Mwenyekiti wa Simba? Yote yale waliyozungumza walikosea?

Tuachane na ile tume, vipi kuhusu Kigwangala? Aliwahi kuhoji mengi mno kuhusu uwekezaji wa Mo Simba.

Twende mbele turudi nyuma, tuweke shahada zetu na stashahada zetu mifukoni, tujadili hili. Simba imeperfom vyema michuano ya kimataifa na ndani pia. Ni kweli Simba imeendeshwa kwa hasara?

Yanga ambayo haina makombe, haijacheza michuano ya nje n.k imeweza tengeneza faida, sembuse Simba ambayo inapeak sana muda huu kuliko timu yoyote East Afrika?

Wakuu embu tuwekeni ushabiki pembeni na tuwe wawazi na wakweli ktk hili.
Hayo mingine yanaweza kuwa sawa lakini la kigwa linajulikana wazi alinyimwa mkopo wa bodaboda
 
Mimi ni mmoja wa watu ninaokubali kabisa kuwa Manara alikuwa 'very unprofessional' mara nyingi sana..
Na hata hiyo nafasi nimewahi Shauri Sana atolewe ..yeye na Jerry Muro niliwahi shauri watolewe wote huko nyuma..

Naweza sema Mimi sio mshabiki wa Manara ..lakini baada ya hili sakata
Nimegundua kitu kwa watu aina ya Manara...
Pascal Mayalla huwa anasema watu aina ya Manara 'wana hidden power'..

Hiki ndo nimekiona kwa Manara na naamini Mo hataweza kabisa kumzima Manara ..
Ukimtazama Manara anapoongea na historia yake yote utagundua kitu kimoja..
'passion'
Huoni 'Proffesionalism'..
Huoni 'ethics'
Huoni 'unafiki wala woga'
Manara siku zote amekuwa Manara
Anaishi kwa sheria zake ..lakini most important ana enjoy ushabiki wake..

Wanaosema nafasi ile inahitaji mtu more Proffesional wako sahihi lakin wanasahu kitu kimoja Tu..je mangapi hatuyafanyi ki Proffesional?
Wananchi watazoea hiyo Proffesionalism inayozungumzwa?
Utamaduni wetu na timu zetu za Kariakoo
Unaruhusu 'Proffesionalism' hiyo?

Au tunasahau na mashabiki wetu na mpira wetu watu kama Manara ndo haswaa wanazalishwa na kupendwa zaidi..?Pengo la Manara likijitokeza tutawapa nini mashabiki?
Manara alikuwa shabiki mkuu wa Simba zaidi kuliko mfanyakazi wa Simba..
Alikuwa maarufu kuliko yeyote Simba..
Hakupata hiyo kazi kwa kuomba
Aliombwa ...
Why watu wamtarajie aje a behave kama muajiriwa mwingine?..
Bado atabaki shabiki mkuu wa Simba kuliko Mo..hata kama hana title official hapo Simba...
Watu wenye passion na wako genuine bila kujali risks za kuwa open na genuine na wanayo ongea mara zote hushinda vita..
Manara ukimsikiliza anapoongea utaona
Anaongea kama mshabiki na sio kama muajiriwa..hajali lolote mradi anausikiliza moyo wake..Mo hatamuweza Manara..
Kwani mo anapvana na manara?
 
MO ni Mpole na Mnyenyekevu hapendi kujikweza wala kugombana na watu.

Manara yupo juu sana, mtoto wa Mjini Daresalama, Mtaa wa Kariakoo. Mjanja wa Mjini.

MO ana Moyo Imara sana la sivyo angeshajitoa kudhamini Simba.
Kila kukicha anakutana na Kejeri, dhihaka, matusi, kashfa humu mtandaoni.

Kisa Kaidhamini Simba, tena kwa kupewa Baraka zote na Wanachama wa Simba na Serikali.
Na mafanikio yanaonekana kwa timu za Simba Wanaume na Simba Wanawake.

Wadhamini wa timu nyingine hawaguswi kabisa. Wao ni Waheshimiwa.

Wakati tutaongea.
 
MO yupo vizuri kwenye biashara. Ni mtu ambaye anaweza kutumia mbinu yeyote ile ili apate faida kibiashara.
Tatizo lake kubwa ni kupenda umaarufu. Anapenda mno umaarufu na kuwa stejini, yaani anatamani angekuwa muimbaji maarufu, mchungaji/shehe maarufu au mwanasiasa maarufu.
Nadra sana kupata vyote.
Ni mimi sana huyu Mudy
 
Hakuna wa kumjibu, alianza kabla ya Derby akajibiwa tuko busy na maandalizi ya mechi..

Akapost huko kwenye mitandao baada ya mechi tu jumatatu ataitisha press, labda alitishia akijua ataitwa, akapotezea. Majuzi baada ya Mo kuweka mzigo kapost tena akisifia kitendo cha mzigo kuwekwa, bado akapotezewa...
Umenichekesha 🤣🤣🤣 watz ni wazee wa tupo pamoja, sasa usiombe upate janga.
 
Back
Top Bottom