Kwanini Mungu anaitwa Mungu na hakuitwa jina lingine? Kama Shetani ni mharibifu kwanini aliachwa hai?

Katika mambo ambavyo hutakiwi kuhoji saaana nai mambo ya Imani vinginevyo utaishia kukufiru!!! Ni kazi ngumu sana kumsoma Mungu na ninadhani haiwezekan!! Na Mungu si mwanadam na hafanani na chochote na tumeambiwa tusimfananishe na chochote, japo Tena hapo hapo tunaambiwa tumeumbwa Kwa mfano wake lakin mimi mtazamo wangu ni kwamba hakuna amjuaye Mungu hata Kwa udogo wa chembe ya haradali!!! Hata biblia Bado kunamikanganyiko Mingi sana na inawachanganya watu ndo maana kunaibuka madhehebu mengi sana!! Sisi mbele za Mungu kazi yetu ni ndogo tu!!! kutambua uwepo wake na kumuishi tukitambua tu kuwa yeye ndiye aliyetufanya tuishi!!! Haya ya kumtafkari saaana na kujiuliza mengi juu yake hatutoboi popote na tutakwama sio mbali!!! Tuishie kumshukiru na kumtukuza tu!!!! Mengine tuachane nayo Kwa sababu tunayafikiria kibinadam na uwezo wetu ni kiduchu sana juu yake na tutaishia kugongana na kumkufuru tu!!!
hilo ni suala la maana katika lugha husika,ukirudi katika uhalisia wa kuitwa hivyo na tukawa na tafsiri hiyo moja,yaani MUNGU mbaye ni GOD,ambaye ni SEBA nk,ningesemabasi kwanini LIITWA SEBA na sio ELIA,ndio hoja yangu
 
Acha uwoga wewe, kukufuru ndo Nini, ehe wamekudanganya ukichunguza ukweli unaenda kuchomwa, Mungu mjua yote na mpenda wote hawezi zidiwa akili na binadamu, wanaokuambia Mungu hachunguzwi ndo ambao wamezitengeneza dini. Acha uwoga, Kama unaogopa moto Kama mtoto wa la 5 anavyoogopa kuchapwa sawa.
 
Sasa huyo Mungu muweza wa yote alipaswa kuzima hyo sehemu kwenye ufahamu wetu, ile sehemi ambayo ubongo utataka kumchunguza yeye angeislip tu... Just a simple code.

Muumbaji hawezi shindwa kuedit mfumo wake.

God is a vanity project my dear
 
Kwanza jiulize kwanini unamuogopa ili Hali huna uhakika kama yupo.
 
Lakini pia anamajina mengine wenzako wanamuita. Kuna wanamuita
Allah
Jehova
God
Crishna

Sasa wewe na lugha yako ndio mnamuita mungu
 
hayo yote ni Majina Ya Demons, Ukweli pekee wa Huu ulimwengu Anao Zouloula(Mzaliwa wa Pili) tu Hao wengne wote hawana wanalolijua.

Ukipenda kamsikilize Youtube
 
Mungu ni cheo mkuu ila ana majina yake. Kila jamii ina Mungu wake ila na hata wewe ikiwa kile kitu kinachokufanya ukihangaikie sana au kuwa bize nacho hicho ndio Mungu kwako. Ila kama unamzungumzia huyu Mwamba mwenyewe Mzee wa siku. Ana majina yake.
 
Jina "Mungu" limetumiwa kwa muda mrefu kuelezea nguvu ya juu na mwenye uwezo wa kuumba na kutawala ulimwengu. Jina hilo linatokana na lugha mbalimbali, kama vile Kiebrania (Elohim na Yahweh), Kigiriki (Theos), na Kilatini (Deus). Kwa hiyo, jina hilo limetumiwa kwa sababu ya jukumu kuu la nguvu ya juu, ambalo ni kuumba na kutawala ulimwengu.

Kuhusu swali lako kuhusu shetani, kuna mengi yanayojadiliwa kuhusu mada hiyo katika imani mbalimbali za kidini. Kwa mfano, katika Ukristo, inaaminiwa kwamba shetani ni malaika mwasi ambaye alitaka kuwa kama Mungu na aliungana na wengine kumpinga Mungu. Inaaminiwa pia kwamba shetani ana uwezo wa kuwadanganya watu na kuwafanya wakose kufuata mafundisho ya Mungu.

Kuhusu kwa nini Mungu hakummaliza shetani huko nyuma, hii inaweza kuelezewa kwa njia mbalimbali. Kwa mfano, baadhi ya imani za kidini zinaamini kwamba Mungu ana mpango wake na kuna sababu kwa nini shetani bado yupo duniani. Inaaminiwa pia kwamba Mungu anatupa uhuru wa kuchagua na kwamba shetani anatumia uhuru huo vibaya kwa kuwadanganya watu. Hii ina maana kwamba kumuangamiza shetani kwa nguvu kungevunja uhuru huo.

Kwa ujumla, swali hili ni la kina na linafikiriwa kwa njia mbalimbali kulingana na imani za kidini na mitazamo ya kifalsafa.
 
Vipi kama angeitwa jina lingine si ungehoji tena kuhusu jina hilo au unabisha?

Liache liwe kama unavyoona na kulisikia
 
Mungu yupo nje ya time dimension.

So kifupi haeleweki na hatokaa aeleweke.

Ukitakaa uwe kichaa endelea kutaka kumwelewa.
mimi huwa nashangaa mitume na manabii wanavyojidai kuongea live na Mungu, siwaelewagi kabisa, ni wezi wa mchana
 
Mungu mwenyewe ni roho
Jamaa amekuuliza, kwani Mungu hawezi kuiua hiyo roho?
Unajibu, "Mungu mwenyewe ni roho"

Hujajibu swali bro, binadamu anaweza kumuua binadamu mwenzie, kwa hiyo nategemea uje ujibu kwamba huyo roho aitwaye Mungu anaweza kumuua roho aitwaye shetani.

Baada ya hapo tutakuuliza kwa nini sasa hamuui huyo roho shetani?
 

Msiogope waangamizao mwili wasiweze kuiagamiza roho, Bali mwogopeni awezaye kuiangamiza roho pamoja na mwili.

Ni maneno ya MUNGU mwenyewe.

Sasa kwanini useme roho haiwezi kufa ikizaliwa wakti Yupo awezaye kuiangamiza?
 
Haeleweki? Afu habari za Kuwa nje ya time dimension ni mafundisho labda..

Au jamani haeleweki tu kwasababu hayupo maana huu utata bhan...
Wewe mtu humwoni kimwili, hajulikani alianzaje kuwepo, hajulikani aliishi wapi kabla hajaiumba hiyo MBINGU anayoiishi sasa, mara sijui hana MWANZO wala MWISHO.

Sasa kiumbe wa hivo utaniambiaje anaeleweka ?


Mungu angekuwa ndani ya time dimension basi chanzo chake kingejulikana na mwisho wake pia
 
Unauhakika kuwa hayuko ndani ya time dimension ama tu unamtoa kumpeleka mbali ili asihojiwe?

Umejuaje yuko nje ya dimension ya muda na unadai kuwa haeleweki ndugu. Umemuelewaje kuwa yuko nje ya Muda watati umedeclare haeleweki?
You can't see a contradiction here mr.

Huyo Mungu ni nadharia tu na ni mawazo ya watu tu, kila mmoja hujaribu kumuelezea ajuavyo yeye.

Ukitaka kujua hilo, ni jinsi mnavyomuelezea sasa ni tofauti kabsa na zamani alivoelezewa. Zamani hao mitume (kama mnavodai kwa mujibu wenu watu wa imani) wenu hawakumuelezea Mungu kuhusu kuwa nje ya time dimension,
Mungu kaanza kuelezewa kuwa nje ya time dimension baada ya kujengeka kwa nadharia ya space_time katika mfululizo wa mabadiliko na uvumbuzi katika sayansi.

Sayansi ni threat kwa dini coz imeviproof wrong hvo vtabu vyenu vya mafundisho visivyo na update. Vitabu vilivyopitwa na wakati, vitabu vyenye idea kuwa dunia ni tambarare, vitabu vyenye idea kuwa jua linazunguka dunia and etcetera.

Sayansi imewaletea mwamko wa kuwa na wanazuoni (wa kidini) ili kuleta maelezo mapya ya nyongeza ili kuvitetea vitabu hivyo, ingawaje wanadai kitabu cha Mungu kinajitosheleza.
Sasa kama kinajitosheleza why nkisoma kwa ufahamu naona kuna makosa lakini naambiwa nisisome kama gazeti ili sasa yaingizwe mafundisho mapya yaliyoelezewa na wanazuoni ili kuepusha aibu iliyomo kwenye vitabu vyao vinavodaiwa kujitosheleza.

Sasa na ndio maana
wafia dini huhisi kama sayansi iko kushindana na wao, wengine hadi wameigroup kwenye upande wa adui yao (shetani). Na wengine hudai kuwa hata ni mpango wa shetani(sayansi).

Kwasababu sayansi ni threat kwa dini hivyo baadhi wa wana dini wenye kujaribu kuskia hoja za kisayansi na kuzijadili hutumia hii theory ya space_time ili kumtoa Mungu wao mtegoni.
Lakini nnaamini kabisa kuwa Mungu aliyejieleza kwenye vitabu vyenu (vitabu vitakatifu kwa mujibu wenu) hakusema yuko nje ya time dimension.
Na nnaamini pia si kila mwana dini ataelezea kama wewe kuwa Mungu yuko nje ya time dimension. Ni kwamba utanyumbulika tu kulingana na mijadala ili uwe against.

Ukisoma kwa ufahamu hvo vitabu utaelewa kabisa mtunzi wa fadihi zile alimaanisha mbinguni ni hapo juu ya mawingu tu.
Nashangaa sana kuwa Mungu alisemwa yuko mbinguni kwenye mawingu hapo lakini baada ya Sayans kufika ametolewa nje ya dimension ya Muda.

Sasa huyo mungu mbona hataki kuface watu wake anaowapenda?
Au ni kwasababu tu hayupo?

Huoni kuwa ni mwanzo wa kujenga mawazo hasi juu ya uwepo wake. Binafsi Sioni sababu ya kuamini kitu chenye kubadilika badilika namna hii.
Nakunali kujifunza vitu vipya vyenye uhalisia.

Hope sayansi itatoka nje ya muda pia sijui mtasema yuko wapi sasa.

Ni afadhali Huyo Mungu mnavyozidi kumficha huko nje ya Muda, nje ya ulimwengu na kokote mnakompeleka.
Ila right kama kweli angekuwepo ilikuwa ni rahisi Kumuangamiza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…