Kwanini Mwalimu Nyerere aliwafukuza Waisrael akawaacha Wapalestina?

Kwanini Mwalimu Nyerere aliwafukuza Waisrael akawaacha Wapalestina?

Akiwa Rais wa Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere aliwafukuza nchini wanadiplomasia wa Israel na kuwaacha wanadiplomasia wa Palestina.

Ni kwa nini Mwalimu aliwafukuza waisrael na kuwaacha wapalestina??

johnthebaptist wewe si ulikuwepo zama zile pale Twiga hotel mtaa wa Samora Jijini Dar es salaam? Hebu tuelezee.
Nyerere alisitisha uhusiano na Israel katika kutekeleza sera zake za kupinga ukandamizaji na uonevu wa binadamu wa aina yoyote ambao ungetokea mahali popote bila kujali rangi na itikadi.

Kwa mtazamo na msimamo wake huo ndiyo uliomfanya aiunge mkono Palestina kwa hali na mali kwa gharama ya kuvunja uhusiano na Israel,nchi ambayo kiuchumi ilikuwa na mwelekeo wa kuwa mshirika makini na muhimu kwa Tanzania.

Kama ambavyo alivyoifanya Tanzania kutumia rasilimali zake kusaidia kwa hali na mali nchi za Zimbabwe, Namibia ,Msumbiji,Angola na Afrika ya kusini katika harakati zao za kudai uhuru na haki,..ndivyo Nyerere alivyoiunga mkono Palestina.

Lakini kwa mshangao wake Nyerere, ilikuwa ni Palestina hiyo hiyo iliyomuunga mkono Idd Amin wakati wa vita ya Kagera mwaka 1978.
Ikumbukwe Palestina na Libya ni nchi zilizoiunga mkono Uganda kwa kutoa silaha na wapiganaji ardhini.
Tanzania iliungwa mkono na Algeria kwa nguvu zote kwa kupewa shehena ya silaha nyingi hadi vita ilipoisha.

Kwa kupitia funzo hilo,nafikiri Tanzania ni vizuri kuendelea na sera yetu ya kutofungamana na upande wowote.
Hii sera maana yake ni ..siyo lazima rafiki yako awe rafiki yangu,au adui yako lazima awe adui yangu pia,..ugomvi wenu siyo lazima unihusu...,na ugomvi wangu na mtu siyo lazima wengine wahusike
 
Akiwa Rais wa Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere aliwafukuza nchini wanadiplomasia wa Israel na kuwaacha wanadiplomasia wa Palestina.

Ni kwa nini Mwalimu aliwafukuza waisrael na kuwaacha wapalestina??

johnthebaptist wewe si ulikuwepo zama zile pale Twiga hotel mtaa wa Samora Jijini Dar es salaam? Hebu tuelezee.
Waisrael wa leo sio wale wa kale. Hawa wa leo inatakiwa wafukuzwe popote wanapoonekana
 
Israel ilikuwa inakalia maeneo ya Misri (Sinai) baada ya ile vita ya siku sita.

Misri alikuwa mwanachama wa umaja wa nchi huru za Afrika. It was that simple. Nchi nyingi za Afrika zilisitisha uhusiano wa kidiplomasia na Israel.

Wapelestina walikuja kutugeuka wakati wa vita ya Kagera kwa kupigana upande wa Nduli.
 
Sema Nyerere angekuwa na ushirikiano wa kidiplomasia na Israeli, tungekuwa mbali sana na wangetusaidia kwenye vita vya Kagera maana Amin aliwateka Wayahudi kabla ya operation Entebbe.

Kiufupi kuwaunga mkono Palestine, Nyerere akizingua sana. Ndo maana tuko hivi mpaka Leo.
 
Nyerere alikuwa.mpenda vita zisizomhusu
Alikuwa mpenda kununua ugomvi iwe wa palestina,iwe wa nchi za kusini mwa Afrika,iwe Uganda,Jimbo.la Biafra Nigeria, iwe wapiganaji waasi wa Polisario wa Sahara wataka kujitenga na Morocco nk yeye kupigana tu na kuunga mkono mavita tu

Nyerere alikuwa Mura mpenda vita.

Ndio maana tumechelewa kuendelea
 
Sema Nyerere angekuwa na ushirikiano wa kidiplomasia na Israeli, tungekuwa mbali sana na wangetusaidia kwenye vita vya Kagera maana Amin aliwateka Wayahudi kabla ya operation Entebbe.

Kiufupi kuwaunga mkono Palestine, Nyerere akizingua sana. Ndo maana tuko hivi mpaka Leo.

Kama ni uwezo why asingekuwa na uhusiano na South Africa ya makaburu?? Si na wao wangetusaidia sana pia?
 
Sema Nyerere angekuwa na ushirikiano wa kidiplomasia na Israeli, tungekuwa mbali sana na wangetusaidia kwenye vita vya Kagera maana Amin aliwateka Wayahudi kabla ya operation Entebbe.

Kiufupi kuwaunga mkono Palestine, Nyerere akizingua sana. Ndo maana tuko hivi mpaka Leo.
Tuko hivi mpaka leo kutokana na thinking kama yako..., Yaani unawaza kusaidiwa na sio kujisaidia au na wewe kusaidia.....

Mtu anapotetea hafanyi hivyo ili apate, anasaidia kutokana na kwamba kuna injustice sehemu fulani; wewe kwa logic yako hata masikini na wasiolipa kodi na wazee wote ungeweza kuwafunga au kuwaua after all huenda at that time mchango wao sio mkubwa.....
 
Lakini kwa mshangao wake Nyerere, ilikuwa ni Palestina hiyo hiyo iliyomuunga mkono Idd Amin wakati wa vita ya Kagera mwaka 1978.
Ikumbukwe Palestina na Libya ni nchi zilizoiunga mkono Uganda kwa kutoa silaha na wapiganaji ardhini.
Tanzania iliungwa mkono na Algeria kwa nguvu zote kwa kupewa shehena ya silaha nyingi hadi vita ilipoisha.
Kwa mtazamo huu Palestina hawaaminiki, ila nimkama Arafat aliwahi kuja Tanzania sijui ilikuwa kipindi gani na alifuata nini
 
Tuko hivi mpaka leo kutokana na thinking kama yako..., Yaani unawaza kusaidiwa na sio kujisaidia au na wewe kusaidia.....

Mtu anapotetea hafanyi hivyo ili apate anasaidia kutokana na kwamba kuna injustice sehemu fulani; wewe kwa logic yako hata masikini na wasiolipa kodi na wazee wote ungeweza kuwafunga au kuwaua after all huenda at that time mchango wao sio mkubwa.....
Sasa unajisaidiaje bila connection?
Connection inaleta transfer of technologies, una wataalam au magenius wa kubuni teknolojia yako mwenyewe? Kwa kizazi cha wabongo kinachowaza ngono muda wote?
 
Kwa kupitia funzo hilo,nafikiri Tanzania ni vizuri kuendelea na sera yetu ya kutofungamana na upande wowote.
Hii sera maana yake ni ..siyo lazima rafiki yako awe rafiki yangu,au adui yako lazima awe adui yangu pia,..ugomvi wenu siyo lazima unihusu...,na ugomvi wangu na mtu siyo lazima wengine wahusike
Umeandika vizuri sana na imeeleweka mno 👍
 
Nyerere alikuwa.mpenda vita zisizomhusu
Alikuwa mpenda kununua ugomvi iwe wa palestrina,iwe wa nchi za kusini mwa Afrika,iwe Uganda,Jimbo.la Biafra Nigeria, iwe wapiganaji waasi wa Polisario wa Sahara wataka kujitebga na Morocco nk yeye kupigana tu na kuunga mkono mavita tu

Nyerere alikuwa Mura mpenda vita.

Ndio maana tumechelewa kuendelea
Aisee..., na huku alifanya hivyo kwanini..., sio kwamba alikuwa hapendi injustices huko nje na humu ndani alikuwa anavision ya a free United Africa ?

Mpinge kwa yote ila atleast alikuwa consistent na alikuwa na vision na principles...., sio leo watu flip-floppers na wanabadilika kila kukicha na wala huwezi kujua wanasimamia nini....
 
Sasa unajisaidiaje bila connection?
Connection inaleta transfer of technologies, una wataalam au magenius wa kubuni teknolojia yako mwenyewe? Kwa kizazi cha wabongo kinachowaza ngono muda wote?
Bora anayewaza ngono anawaza..., kuliko anayedhani hawezi na anasubiri kusaidiwa hence wala hajishughulishi kufanya chochote....

Unaonglea teknolojia hujui kwamba wazee wetu walikuwa wanafua vyuma, wanatengeneza pottery wana nyumba aina zao kutokana na mazingira hadi wengine waliweza kutengeneza nguo kwa magome ya miti (hence they are thinkers and creative) by the way hata usipokuwa innovative katika dunia ya leo unaweza ukawa una-copy na kupaste (Western wamefanya hivyo kwa muda mrefu - teknolojia zote sio kwamba zimeanzia kwao)
 
Back
Top Bottom