kama sheria, mamlaka, jamii na asasi za kiraia zinakulinda kwanini usiyaone matamu? Kawaulize watoto wa Mengi walivyotokea kwenye tundu la sindano kutapeliwa utajiri wa familia na klyn, uone kama watakua na mtazamo kama wako.
I second you in every post
Nina ka single maza hapa natafuna mdogo mdogo tu wala sina haraka..
Sasa kinachonifurahisha na kunitia huzuni ni kwamba kananiimbia nyimbo za ndoa,, mara kwenda kukalipia mahari na mambo kibao tu..
Sasa Mama yake amekuwa akikauliza eti huyo mwanaume ana pesa? Kanasema ndiyo.
Kwake pazuri? Kanasema ndiyo.
Una uhakika biashara hizo ni za kwake?
Kanasema ndiyo.. Japo huwa wanaongea kikabila chao kitutsi lakini naelewa vizuri tu maana nasikia sana ila kujibu ndio siwezi..
Sasa mimi nabaki na huzuni tu yaani mama mtu haoni shoti aliyo nayo binti yake
Ila anaweka standards kwa mwanae as if she deserves those merits..
Nipo zangu kimya tu binti hajui nachowaza kuhusu future yangu..
Kiukweli niseme wazi tu kama kuna sehemu nitafika kwaajili ya kufunga ndoa basi sitakuwa mimi huyu labda mzimu wangu..
Ndoa ni kasheshe fulani hivi ambayo mwanaume utakuwa unawindwa ukalishwe mwanzo mwisho, uporwe kile ulichonacho iwe kwa maneno matamu kutoka kwa mkeo au kupitia loopholes zilizopo kwenye mkataba wa ndoa.
Nachofanya kwa sasa ni kuzaa na wanawake tofauti tofauti hata kumi.
Baadae nikusanye watoto wangu niwaweke kwenye kambi yao
Na kwenye baadhi ya miradi yangu..
Suala la ndoa libaki kwenye masikio ya wengine..
Mimi kwasasa natumia mfumo wa sogea tuishi ukichoka huu mfumo unaruhusiwa kutafuta Simp atakae funga ndoa na sherehe kubwa juu huku maex zako wakiwa ni robo ya ukumbi.
Sitaki habari za ndoa haijalishi nimekukuta bikra au una mtoto au watoto..
Njoo tuishi kawaida mapenzi yakiisha chagua msela mwingine kutoka kwenye phonebook yako kapendane nae tena maana najua naishi na wewe na wao umewabeba kwenye simu yako..