Kwanini Mzanzibar Shaka Hamdu Shaka ni Mkuu wa Wilaya bara, na Zanzibar hakuna Mtanganyika anayeongoza?

Kwanini Mzanzibar Shaka Hamdu Shaka ni Mkuu wa Wilaya bara, na Zanzibar hakuna Mtanganyika anayeongoza?

Kwani kati ya wabara na wavisiwani nani ambae anafosi muungano?

Siku zote anaefosi mapenzi vyake ndio huteketea.
Kwa akili ya kawaida Samia hawezi kuruhusu muungano uvunjike. Maana ukivunjika hana kazi anarudi kwao Kizimkazi kulea wajukuu.

Wanaoung'ang'ania ni watu wachache wenye manufaa yao.

Kule Zanzibar wana CCM wengi wamewekeza bara au wamepewa fursa Tanganyika kupitia CCM , wana kila sababu kuutaka muungano na kuwapuuza wapemba ambao wapo tu visiwani na hawana maslahi Tanganyika.

Kwa huku bara, kikundi kinachotaka huu muungano ni marafiki wa niliowataja hapo juu. Si kila mwana CCM bara anapenda muungano maana wanufaika ni wachache.
 
Back
Top Bottom