Kwanini namuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan?

Kwanini namuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan?

Kwa upande wangu sijawahi kumkubali hata mara moja kwa sababu sioni aliko faulu hata sehemu moja, Kila sehemu ana jipapatua bila mafanikio,huko kwenye uchumi ndio kafeli zaidi Kila siku uchumi unazidi kuanguka...
Huoni alipo faulu? Sikushangai lakini. Inategemea sana na upeo wako wa mambo ulivyo!!
 
again ni haki yako na hao wengine kujiondoa ufahamu.

Nimesema Watanzania hawajaridhika na mkataba, hivyo, haina maana hawaungi mkono uwekezaji huo wa Bandar...
Acha kutoa takwimu za jumla. Hivyo ndo unavyozidi kujionesha ulivyo mjinga. Sema wewe sio Watanzania maana mimi pia ni Mtanzania na nimeridhika nao
 
Kwani Bukoba kuna shida gani?
Sina shida na bukoba, Nina shida na KUONGOZWA Kwa kutumia Dira na maono ya mtu mmoja.

Aweza amka na kuhamishia fursa zote huko na mkapiga makofi kama ambavyo saiz kule visiwani kandarasi zinapishana tu mkiangalia na kupiga makofi.

Tunahitaji MAONO ya nchi na Dira ya Taifa Kwa miaka mingi ijayo.

KATIBA mpya ni sasa.
 
Sina shida na bukoba, Nina shida na KUONGOZWA Kwa kutumia Dira na maono ya mtu mmoja.

Aweza amka na kuhamishia fursa zote huko na mkapiga makofi kama ambavyo saiz kule visiwani kandarasi zinapishana tu mkiangalia na kupiga makof...
Maono ya nchi hayawekwi kwenye Katiba. Kuna mfumo maalumu wa kuweka vitu kama hivyo na kuvifuatilia. Ndo mana Tume ya Mipango imerudi.
 
Good umeongea vzuri sana miongoni mwa point niliyoipenda ni kuwa watanzania wengi awapendi challenge ukimchallange tu kidogo basi shida anakuona kama adui vile na ndio kinachotokea asaivi watu wakimchallenge mh rais wangu wa jamhuri ya watu wa Tanzania dr Samia kidogo tu ohoooo wanamtukana rais, ohhh wanaleta udini, ooooh wanaleta ujinsia , ooooh wanaleta uzanzibari.

Hicho kitu kweli ndugu ndicho kinachotufanya tuendelee na umaskini yaani chama changu Cha ccm akipendi kabisa ushindani ukiwaletea ushindani basi wataleta figisu kwenye kitu unachokilingia, kama mfanya biashara hiyo biashara aitadumu, kama wewe wakili basi hiyo leseni jiandae kunyanga'anywa.

Kama mwanamziki Sanaa zako zitafungiwa na wanaweza kufika mbali zaidi ya ata kukupora roho yako Wana ccm wenzangu tubadilike tunajenga Tanzania Moja why tugombanie fito angali ya kuwa tunafanya kitu kwa masilai yetu sote?
 
Maono ya nchi hayawekwi kwenye Katiba. Kuna mfumo maalumu wa kuweka vitu kama hivyo na kuvifuatilia. Ndo mana Tume ya Mipango imerudi.
Maisha Bora Kwa Kila mtanzania Yako wapi Kwa Tume ya mipango ya 004 enzi ya KIKWETE?

Katiba mpya itatukoa kwenye mark time,

Nchi inazeeka mjue, Ina 60+ yrs now!!!!
 
Kumekuwa na maneno maneno humu kuwa mimi na wenzangu tunaomuunga mkono Rais Samia basi kama sio Waislamu basi ni Wazanzibar na kama hauko kote huko basi wewe ni chawa wake...
Kwa hiyo mangii, unaweza kutuambia huyu mama anafuata sera gani ya uchumi?

Maana mimi naona uchumi wetu unaenda ki Laissez-faire
 
Acha kutoa takwimu za jumla. Hivyo ndo unavyozidi kujionesha ulivyo mjinga. Sema wewe sio Watanzania maana mimi pia ni Mtanzania na nimeridhika nao
sasa tunapimana ujinga?
Sasa unalazimisha. Endelea.

Ulishawahi kutelekezwa utotoni? Unajibu kama vile wazazi wako walikuwa wakali kuliko wazazi wa marafiki zako. Unakasirika na kujisikia umedhalilishwa kirahisi hivyo? Pole basi.
 
Sasa wewe tufanye ni msomi. Niambie nchi imeuzwaje?

Usikimbie!
Imeuzwa kupitia mkataba wa 25.10.2022 mkataba ambao uliridhiwa na Bunge 10.06.2023. Ndani ya mkataba huo mwarabu anapewa haki za kipekee za kumiliki njia kuu za uzalishaji mali hususani bandari, maeneo ya biashara na ardhi.

Mkataba huo unampa mamlaka ya kuendelea, kujenga, kuendesha na kuendeleza bandari zote za Tanganyika, shughuli za kuratibu mizigo (logistics centers ambazo sasa zinafanywa na clearing and forward agents), special economic zones (hata mlima Kilimanjaro unaingia hapa, mbuga za wa nyama na madini zinaingaia hapa), trade center kama Kariakoo, Mwanza, Arusha unduma, strategic infrastructure kama SGR, Barabara na madaraja, trade corridors kama maeneo ya Hororiri, Sirari, Tunduma)!

Lakini pia amepewa haki za kumiliki ardhi aitakayo na serikali italazimika kuwapa ardhi hiyo hata kama INA watu basi serikali itapaswa kuwafukuza watu hao ili mwarabu akae. Na akiimiliki ardhi akaanza kujichimbia madini yaliyoko ardhini hatupaswi kumuuliza).

Hayo yote amekabidhi kuanzia tarehe tajwa hadi mwisho wa dunia.
Lakini katika hayo yote mgao wa Tanzania hauwekwi wazi.
Hebu sasa na wewe tuambie, kwa nini unashikilia hoja kuwa nchi haijauzwa?
 
Imeuzwa kupitia mkataba wa 25.10.2022 mkataba ambao uliridhiwa na Bunge 10.06.2023. Ndani ya mkataba huo mwarabu anapewa haki za kipekee za kumiliki njia kuu za uzalishaji mali hususani bandari, maeneo ya biashara na ardhi.
...
Nikadhani unataja vifungu na kuviweka hapa.

Kumbe unapiga siasa
 
Mwisho napenda kumaliza kwa kusema uongozi na maendeleo ya kweli ni matokeo ya kutumia akili vizuri. Sio rasilimali wala sio utajiri ulio nao kama Taifa.
Kwenye suala la bandari kwa mkataba kama ule unaweza kusema akili yako au ya waliofanya vile zimetumika akili vizuri kwa manufaa ya wote au manufaa yao/yenu na ya wenzao/wenzenu wachache?
Unajitoa akili kwa kudhani wanaoipinga mkataba ule hawataki uwekezaji. Watu wanapinga vipengele vya mkataba.
Mkataba hauna ukomo, hauoneshi nchi yetu itafaidika vipi.
Mkataba unazuia mwekazaji asipate ushindani wa kibiashara, hii si sawa na enzi za ujamaa mashirika ya umma yalijengewa kinga (au tuite monopoly) yasiwe na mshindani. Kama unamuondolea ushindani kisha unaweka kipengele cha kutovunja mkataba unawezaje kumuondoa kama akifanya nje ya matarajio au chini ya kiwango cha sasa?

Hapo utasema kuna akili imetumika? Au tumeondokaje kwenye ile monopoly ya zamani?
Hayo ni machache tu ya ovyo kwenye ule mkataba.
HATUKATAI UWEKEZAJI BALI TUNAKATAA VIPENGELE VIBAYA VYA MKATABA WA UWEKEZAJI, USIJITOE UFAHAMU KAMA HUJASIKIA WANAOPINGA WANAPINGA NINI. TANGAZENI TENDA UPYA NA KWA UWAZI UONE KAMA KUTAKUWA NA KELELE HIZI.
 
Kwenye suala la bandari kwa mkataba kama ule unaweza kusema akili yako au ya waliofanya vile zimetumika akili vizuri kwa manufaa ya wote au manufaa yao/yenu na ya wenzao/wenzenu wachache?
Unajitoa akili kwa kudhani wanaoipinga mkataba ule hawataki uwekezaji. Watu wanapinga vipengele vya mkataba.
Mkataba hauna ukomo, hauoneshi nchi yetu itafaidika vipi.
Mkataba unazuia mwekazaji asipate ushindani wa kibiashara, hii si sawa na enzi za ujamaa mashirika ya umma yalijengewa kinga (au tuite monopoly) yasiwe na mshindani. Kama unamuondolea ushindani kisha unaweka kipengele cha kutovunja mkataba unawezaje kumuondoa kama akifanya nje ya matarajio au chini ya kiwango cha sasa?

Hapo utasema kuna akili imetumika? Au tumeondokaje kwenye ile monopoly ya zamani?
Hayo ni machache tu ya ovyo kwenye ule mkataba.
HATUKATAI UWEKEZAJI BALI TUNAKATAA VIPENGELE VIBAYA VYA MKATABA WA UWEKEZAJI, USIJITOE UFAHAMU KAMA HUJASIKIA WANAOPINGA WANAPINGA NINI. TANGAZENI TENDA UPYA NA KWA UWAZI UONE KAMA KUTAKUWA NA KELELE HIZI.
Mkataba una shida gani?
 
Back
Top Bottom