Kwanini naunga mkono Urusi kuchukua hatua za kijeshi Ukraine?

Kwanini naunga mkono Urusi kuchukua hatua za kijeshi Ukraine?

Kama hoja ni nato au marekani kwa "makosa" yake huko syria au iraq au libya , au kama shida ni nato au marekani kwa wanayotaka kuyafanya na ukraine, basi uamuzi sahihi kwa putin na nyie mnaomuunga mkono ilikuwa ni kuwavamia hao nato na marekani kuua watu wao na kuharibu nchi zao, sio ukraine, kwanini chuki zenu kwa nato na marekani mnazipeleka kwa wanyonge ukraine, kila sababu mnazotoa mnahusisha matendo ya marekani , kamvamie sasa huyo marekani ili apate haki yake. Hamma hoja team putin ubabe wa ki hitler huo
Inaonekana hufahamu mambo mengi katika mzozo huu.
Hujui vizuri siasa za USA na Russia.
Ungekua unajua Cuban missile crisis usingesema hayo unayosema.
 
Picha ya kwanza juu ni kiongozi wa Jamhuri ya Watu wa Donetsk bwana Denis Pushilin, Na picha ya chini ni kiongozi wa Jamhuri ya Watu wa Luhansk bwana Leonid Pasechnik, Jamhuri hizo ni majimbo yaliyojitenga toka alance ya dunia na inapumua vizuri sasa.

Na Yericko Nyerere
View attachment 2136291View attachment 2136292
hao watu wanaishi kule mashariki, km nia ya urusi ilikuwa ni kuwalinda andepeleka majeshi kuwalinda kulekule kwe ,majimbo ambayo urusi imeshayatambua kuwa ni huru na si kuvamia nchi yote, utakua umetumia hisia tu
 
Picha ya kwanza juu ni kiongozi wa Jamhuri ya Watu wa Donetsk bwana Denis Pushilin, Na picha ya chini ni kiongozi wa Jamhuri ya Watu wa Luhansk bwana Leonid Pasechnik, Jamhuri hizo ni majimbo yaliyojitenga toka Ukraine.

Naomba nianze utangulize wa makala yangu kwakusema, Dunia ili iwe salama inatakiwa kuwa na wakubwa wawili au zaidi (balance of power), sio mmoja tu anaamua yeye kwaajili ya dunia na hapingwi, Mbele ya Urusi sasa hatutaona vita vya holela vya Marekani na washirika wake.

Sababu ya kwanza ya kuunga mkono Urusi ni kwamba ni hatua muhimu ya kukomesha mauaji ya miaka karibu kumi sasa yanayofanywa na Ukraine dhidi ya Wananchi wa Majimbo ya Luhansk na Donetsk. Kwa msiojua Mtangulizi wa Rais Zelensk wa Ukraine, bwana Petro Poroshenko tangu ashike madaraka 2014 aliendesha mauaji ya wapinzani wengi katika majimbo ya DPR na LPR yaliyotaka kujitenga hadi alipoondoka tu vita havikumalizika.

Alipoingia Zelensk nae akafuata nyayo za mtangulizi wakw, akaigeuza Ukraine kuwa jehanamu kwa aliowaita waasi, aliendesha mauaji makubwa sana hasahasa 2021 dhidi ya raia kule katika miji ya Donbass katika kile alichokiita kudhibiti waasi wanaotaka kujitenga. Dunia hii ilikaa kimya, Urusi ikawa ndio pango la kupokea wakimbizi zaidi la laki tatu,

Kiongozi Jimbo la Donetsk Bwana Denis Pushilin amenusurika mauaji zaidi ya marakumi hadi alipoomba ulinzi wa kimataifa kutoka Moscow, na mwisho akaongoza mapambano na kufanikiwa kujitangazia Uhuru.

Vile vile kiongozi wa jimbo la Luhansk bwana Leonid Pasechnik nae ilimlazimu kutafuta hifadhi ya kisiasa Moscow kwa lengo la kunusuru maisha yake dhidi ya Rais wa Ukraine bwana Zelensk aliyeapa kufuta uasi katika majimbo hayo, Aliongoza mapambano kwa ushirika wa Kiongozi wa jimbo la Donetsk bwana Pushilin na hatimaye wiki jana wamefanikiwa kumshinda Zelensk na Kujitangazia Uhuru.Urusi imeyatambua majimbo hayo kama nchi huru, Belarus na nchi nyingine tano yayari zimetambua. Ukraine imepinga uhuru huo ikaapa kuendesha vita nzito zaidi dhidi ya waliojitenga, Hatua hiyo ikawalazimu viongozi wa mapinduzi waombe msaada wa kijeshi kutoka Urusi. Na wameupata. Oparesheni ya Urusi ndio mwarobaini wa kukomesha mauaji ya miaka zaidi ya kumi sasa, kinyume na hapo miji itaendelea kuvuja damu kila kukicha.

Sababu ya pili ya kuunga mkono Urusi ni kitendo cha Marekani kutaka kujenga ngome ya kijeshi Ukraine, na katika kutimiza hilo Marekani kwakutumia washirika wake wa Nato wakamshawishi avunje Mkataba wa Minsk wa 2015 pamoja na mambo mengine, ulisema Ukanda wa Kaskazini Magharibi mwa Urusi (Ukraine) uliokuwa Umoja wa Kisoviet ya zamani Hautaruhusiwa kujiunga na Umoj wa Ulaya. Katika kibri cha Zelensk akaomba kujiunga NATO. Moscow akajibu kwa moto.

Sababu ya tatu ya kuunga mkono Urusi ni kitendo cha Marekani kupitia shirika lake la kijasusi la CIA kuvuruga dili la Urusi la kujenga bomba la awamu ya pili la gesi maarufu kama NORD STREAM II, ambalo lingelisha gesi Ulaya yote kwa 90% tofauti na sasa mbapo Ulaya inategemea gesi ya Urusi kwa 40% tu, Marekani ameitumia Ukraine kukwamisha mradi huu na baadhi ya nchi za Nato. Kitendo hiki ilikuwa ni uchokozi wa kiuchumi na kijasusi, Jibu la Urusi limeanzia kwa Ukraine kwanza.

Mtazamo wangu vita hivi ni kati ya Urusi na Marekani, na vitaisha kwa nchi hizi mbili kukaa chini na kukubaliana terms and conditions kama mihimili miwili mikuu duniani. Na sio vinginvyo, Ukraine kwa sasa ni uwanja wa biashara ya Silaha ya ulaya na Marekani.

Baada ya vita hii Urusi ataheshimiwa na kuogopwa sana, na vikwazo hivi amini ni geresha tu, havitachukua miezi 18 vitaondolewa, Rejea vikwazo vya 1990 alivyowekewa Urusi alipoivami Afghanustan vilimwathiri nani na viliishia wapi zaidi ya Afghanistan kusambaratishwa? Haya vikwazo vya Urusi vya 2008 alipoivamia Georgia viliishia wapi na vilimwathiri nani zaidi ya Georgia kuwa eneo muhimu la Urusi hadi leo? Vikwazo vya Urusi vya juzi tu baada ya kuivamia Cremia vimefiki wapi?.

Kikwazo ambacho kilikuwa tishio kwa uchumi wa Urusi alichowekewa na EU ni hiki cha kuzuia huduma ya kibenki ya SWIFT, Lakini ndani ya saa 24 tu, Rais wa Urusi Vlamir Putin ametangaza hatua za dharula kukabili vikwazo vya kiuchumi, na haraka Urusi na China wamekubaliana kutumia huduma ya kibenki ya China ya Cross-Border Interbank Payment System, or CIPS. Kwa tafrisi hiyo nikuwa kikwazo cha uchumi hakitaiathiri Urusi moj kwa moja.

Ukweli ni kuwa Nchi nyingi duniani haziwezi kuendesha chumi zao, katika nyanja nyingi kama za kijeshi na mengineyo bila Urusi. Dunia inaihitaji Urusi kuliko Urusi inavyo ihitaji dunia yenyewe. Japo wanategemeana. Mataifa ya Umoja wa Ulaya (EU) yapo 27, ukijumlisha na Marekani jumla ni nchi 28 tu, haya mataifa sio yote yanaipinga Urusi, Dunia ina nchi 195 + Donetsk na Luhansk, ni 197, Sasa jiulize nchi 164+ ziko upande upi?. Bado mtu anasema Urusi imetengwa na dunia? Basi huyo mtu haijui dunia sawasawa.

Ni wazi kwamba, Dunia leo iko mapande matatu, kuna Urusi, Kuna Uchina na kuna Marekani... Kwenye nchi 28 Uchina hayuko huko, zingatia kuna nchi za kati zenye uchuki mkubwa ambazo ni India hayuko na Ukraine, huko Brazil hayuko huko na Ukraine... Na hawa wanamuunga mkono Mrusi.... Dunia sasa inastawi na hii ndio balance ya dunia na inapumua vizuri sasa.

Na Yericko Nyerere
View attachment 2136291View attachment 2136292
Yericko hili bandiko lako umeonekana una bias Sana hivyo wasomaji wengi wamekupuuza Sana. Kuanzia leo mavitabu na matakataka yako sitoyasoma tena umeonekana na ushabiki una mawazo ambayo hayabalance poor you
 
Hivi ikitokea mikoa wa Mwanza na Kagera zikatangaza uasi dhidi ya serikali ya jamhuri ya Tanzania vipi Rais atakaekuwepo ataacha hiyo Hali iendelee?vipi hatachukua hatua za kijeshi ili kulinda Taifa lake na kuleta umoja wa kitaifa? Je huoni kwamba asipochukua hatua za kijeshi ni kama atachochea mikoa mingine kujitenga?
Kwa maana hiyo je kosa la Zelenski liko wapi Mana alikua anazima uasi ili kulete umoja wa Taifa lake?
Pia tambua Ukurain ni Taifa huru hivo kujiunga NATO sio kosa

Mwisho acha kudanganya watu vikwazo vya kiuchumi lazima vitaua uchumi wa Urusi ni swala la muda tu.
Kwa hii thread Leo umepuyanga.
I second u[emoji106]
 
Rubbish, huwa nakuunga mkono mambo mengi lakini sikuungi kwa ujinga huu wa kuua watu wasio na hatia, kama mrusi ana nguvu kwanini asiende kuvamia Marekani?
Marekani anapoua mbona kelele si nyingi?...Iraq, Libya, Syria, Afghanistan, Vietnam, etc? Hujiulizi kwa nini? Siungi mkono mauaji ya raia. Lakini hii vita imetafutwa na NATO na hasa Marekani.
 
Watanzania wengi wanapenda ushabiki, hawapendi kusoma. Hawajui hata makubaliano kati ya urusi na marekani ambayo pia yalimlazimisha mrusi kuondoa silaha zake cuba.
Putin anatakiwa kuwalinda urusi tena alitakiwa kumpa ukraine kipigo cha maana ili nato na un wafikirie mara mbilimbili wanachotaka kuwafanyia urusi.
Hatukusikia chochote irak, libya. Syria . Yemen, ethiopia na kwingineko ambako raia wasio na hatia wanauawa. Ila sasa tunaona mpaka uefa na fifa wamekuja juu.
Kama kweli wewe ni mfuatiliaji wa habari za kimataifa lazima uwe umesikia mijadala mingi tu iliyofanyika na inayoendelea kuhusu uongo na uovu uliofanywa na marekani na washirika wake huko Iraq, Afghanistan, Libya, n.k. ripoti zimetolewa na taasisi rasmi za US, UK, NGOs na wengine kuhusu ghilba zilizofanyika kuanzisha vita ya Iraq. Tony Blair na George Bush wametajwa kama war criminals.

Malalamiko kuhusu Saudi Arabia na Iran kwenye vita ya Yemen yanasikika kila mara. Vita za Syria na Ethiopia zinazungumzwa. Hakuna ujinga unaopita hapa duniani, watu wote wakakaa kimya. Wapo watakaoliamsha. Uzuri wa Marekani na Ulaya viongozi wao wanakosolewa hadharani tena kwenye media za kimataifa. Mambo yao yanachambuliwa hadharani. Hata uongo wa CIA au jeshi kama pale walipoua familia kwa drone kule Afghanistan CNN walichunguza na kuripoti kimataifa na baadaye Pentagon na State Department wakakiri kosa na kuahidi kulipa kifuta machozi.

Huko Urusi hakuna mwenye jeuri ya kumuhoji Putin kitu. Na anayemkosoa ajiandae kupakazwa au kulishwa polonium na watu wasiojulikana. Hao Warusi anaodai kuwalinda hashauriani nao chochote kwa sababu anajua hakuna ukweli zaidi ya yeye kutaka kuimarisha utawala wake mrefu wa kidikteta huko Urusi. Hayuko tayari kuona demokrasia ikistawi jirani yake halafu wananchi wake wakaanza kumhoji na kukimbia nchi.
 
Rubbish, huwa nakuunga mkono mambo mengi lakini sikuungi kwa ujinga huu wa kuua watu wasio na hatia, kama mrusi ana nguvu kwanini asiende kuvamia Marekani?
Halafu eti unaweka stand by nuclear weapons kuweza kutumika FOR WHAT!!!!!???? Rubbish,hivi huyo Putin anaakili sawa sawa hajatosheka tu alivyoimega Ukraine na kuunda vikundi vya waasi??
 
Picha ya kwanza juu ni kiongozi wa Jamhuri ya Watu wa Donetsk bwana Denis Pushilin, Na picha ya chini ni kiongozi wa Jamhuri ya Watu wa Luhansk bwana Leonid Pasechnik, Jamhuri hizo ni majimbo yaliyojitenga toka Ukraine.

Naomba nianze utangulize wa makala yangu kwakusema, Dunia ili iwe salama inatakiwa kuwa na wakubwa wawili au zaidi (balance of power), sio mmoja tu anaamua yeye kwaajili ya dunia na hapingwi, Mbele ya Urusi sasa hatutaona vita vya holela vya Marekani na washirika wake.

Sababu ya kwanza ya kuunga mkono Urusi ni kwamba ni hatua muhimu ya kukomesha mauaji ya miaka karibu kumi sasa yanayofanywa na Ukraine dhidi ya Wananchi wa Majimbo ya Luhansk na Donetsk. Kwa msiojua Mtangulizi wa Rais Zelensk wa Ukraine, bwana Petro Poroshenko tangu ashike madaraka 2014 aliendesha mauaji ya wapinzani wengi katika majimbo ya DPR na LPR yaliyotaka kujitenga hadi alipoondoka tu vita havikumalizika.

Alipoingia Zelensk nae akafuata nyayo za mtangulizi wakw, akaigeuza Ukraine kuwa jehanamu kwa aliowaita waasi, aliendesha mauaji makubwa sana hasahasa 2021 dhidi ya raia kule katika miji ya Donbass katika kile alichokiita kudhibiti waasi wanaotaka kujitenga. Dunia hii ilikaa kimya, Urusi ikawa ndio pango la kupokea wakimbizi zaidi la laki tatu,

Kiongozi Jimbo la Donetsk Bwana Denis Pushilin amenusurika mauaji zaidi ya marakumi hadi alipoomba ulinzi wa kimataifa kutoka Moscow, na mwisho akaongoza mapambano na kufanikiwa kujitangazia Uhuru.

Vile vile kiongozi wa jimbo la Luhansk bwana Leonid Pasechnik nae ilimlazimu kutafuta hifadhi ya kisiasa Moscow kwa lengo la kunusuru maisha yake dhidi ya Rais wa Ukraine bwana Zelensk aliyeapa kufuta uasi katika majimbo hayo, Aliongoza mapambano kwa ushirika wa Kiongozi wa jimbo la Donetsk bwana Pushilin na hatimaye wiki jana wamefanikiwa kumshinda Zelensk na Kujitangazia Uhuru.Urusi imeyatambua majimbo hayo kama nchi huru, Belarus na nchi nyingine tano yayari zimetambua. Ukraine imepinga uhuru huo ikaapa kuendesha vita nzito zaidi dhidi ya waliojitenga, Hatua hiyo ikawalazimu viongozi wa mapinduzi waombe msaada wa kijeshi kutoka Urusi. Na wameupata. Oparesheni ya Urusi ndio mwarobaini wa kukomesha mauaji ya miaka zaidi ya kumi sasa, kinyume na hapo miji itaendelea kuvuja damu kila kukicha.

Sababu ya pili ya kuunga mkono Urusi ni kitendo cha Marekani kutaka kujenga ngome ya kijeshi Ukraine, na katika kutimiza hilo Marekani kwakutumia washirika wake wa Nato wakamshawishi avunje Mkataba wa Minsk wa 2015 pamoja na mambo mengine, ulisema Ukanda wa Kaskazini Magharibi mwa Urusi (Ukraine) uliokuwa Umoja wa Kisoviet ya zamani Hautaruhusiwa kujiunga na Umoj wa Ulaya. Katika kibri cha Zelensk akaomba kujiunga NATO. Moscow akajibu kwa moto.

Sababu ya tatu ya kuunga mkono Urusi ni kitendo cha Marekani kupitia shirika lake la kijasusi la CIA kuvuruga dili la Urusi la kujenga bomba la awamu ya pili la gesi maarufu kama NORD STREAM II, ambalo lingelisha gesi Ulaya yote kwa 90% tofauti na sasa mbapo Ulaya inategemea gesi ya Urusi kwa 40% tu, Marekani ameitumia Ukraine kukwamisha mradi huu na baadhi ya nchi za Nato. Kitendo hiki ilikuwa ni uchokozi wa kiuchumi na kijasusi, Jibu la Urusi limeanzia kwa Ukraine kwanza.

Mtazamo wangu vita hivi ni kati ya Urusi na Marekani, na vitaisha kwa nchi hizi mbili kukaa chini na kukubaliana terms and conditions kama mihimili miwili mikuu duniani. Na sio vinginvyo, Ukraine kwa sasa ni uwanja wa biashara ya Silaha ya ulaya na Marekani.

Baada ya vita hii Urusi ataheshimiwa na kuogopwa sana, na vikwazo hivi amini ni geresha tu, havitachukua miezi 18 vitaondolewa, Rejea vikwazo vya 1990 alivyowekewa Urusi alipoivami Afghanustan vilimwathiri nani na viliishia wapi zaidi ya Afghanistan kusambaratishwa? Haya vikwazo vya Urusi vya 2008 alipoivamia Georgia viliishia wapi na vilimwathiri nani zaidi ya Georgia kuwa eneo muhimu la Urusi hadi leo? Vikwazo vya Urusi vya juzi tu baada ya kuivamia Cremia vimefiki wapi?.

Kikwazo ambacho kilikuwa tishio kwa uchumi wa Urusi alichowekewa na EU ni hiki cha kuzuia huduma ya kibenki ya SWIFT, Lakini ndani ya saa 24 tu, Rais wa Urusi Vlamir Putin ametangaza hatua za dharula kukabili vikwazo vya kiuchumi, na haraka Urusi na China wamekubaliana kutumia huduma ya kibenki ya China ya Cross-Border Interbank Payment System, or CIPS. Kwa tafrisi hiyo nikuwa kikwazo cha uchumi hakitaiathiri Urusi moj kwa moja.

Ukweli ni kuwa Nchi nyingi duniani haziwezi kuendesha chumi zao, katika nyanja nyingi kama za kijeshi na mengineyo bila Urusi. Dunia inaihitaji Urusi kuliko Urusi inavyo ihitaji dunia yenyewe. Japo wanategemeana. Mataifa ya Umoja wa Ulaya (EU) yapo 27, ukijumlisha na Marekani jumla ni nchi 28 tu, haya mataifa sio yote yanaipinga Urusi, Dunia ina nchi 195 + Donetsk na Luhansk, ni 197, Sasa jiulize nchi 164+ ziko upande upi?. Bado mtu anasema Urusi imetengwa na dunia? Basi huyo mtu haijui dunia sawasawa.

Ni wazi kwamba, Dunia leo iko mapande matatu, kuna Urusi, Kuna Uchina na kuna Marekani... Kwenye nchi 28 Uchina hayuko huko, zingatia kuna nchi za kati zenye uchuki mkubwa ambazo ni India hayuko na Ukraine, huko Brazil hayuko huko na Ukraine... Na hawa wanamuunga mkono Mrusi.... Dunia sasa inastawi na hii ndio balance ya dunia na inapumua vizuri sasa.

Na Yericko Nyerere
View attachment 2136291View attachment 2136292
Umechambua vizuri sana Yericko. Ongeza na hoja ya Muhoozi Kainerugaba, si ya kupuuzwa.
Ubabe wa NATO na Marekani nao ni wa kihalifu. Nakumbuka ukatili na uhalifu walioufanya Libya na kwingeneko duniani. They have no moral stance and/or authority!
 
Kama kweli wewe ni mfuatiliaji wa habari za kimataifa lazima uwe umesikia mijadala mingi tu iliyofanyika na inayoendelea kuhusu uongo na uovu uliofanywa na marekani na washirika wake huko Iraq, Afghanistan, Libya, n.k. ripoti zimetolewa na taasisi rasmi za US, UK, NGOs na wengine kuhusu ghilba zilizofanyika kuanzisha vita ya Iraq. Tony Blair na George Bush wametajwa kama war criminals.

Malalamiko kuhusu Saudi Arabia na Iran kwenye vita ya Yemen yanasikika kila mara. Vita za Syria na Ethiopia zinazungumzwa. Hakuna ujinga unaopita hapa duniani, watu wote wakakaa kimya. Wapo watakaoliamsha. Uzuri wa Marekani na Ulaya viongozi wao wanakosolewa hadharani tena kwenye media za kimataifa. Mambo yao yanachambuliwa hadharani. Hata uongo wa CIA au jeshi kama pale walipoua familia kwa drone kule Afghanistan CNN walichunguza na kuripoti kimataifa na baadaye Pentagon na State Department wakakiri kosa na kuahidi kulipa kifuta machozi.

Huko Urusi hakuna mwenye jeuri ya kumuhoji Putin kitu. Na anayemkosoa ajiandae kupakazwa au kulishwa polonium na watu wasiojulikana. Hao Warusi anaodai kuwalinda hashauriani nao chochote kwa sababu anajua hakuna ukweli zaidi ya yeye kutaka kuimarisha utawala wake mrefu wa kidikteta huko Urusi. Hayuko tayari kuona demokrasia ikistawi jirani yake halafu wananchi wake wakaanza kumhoji na kukimbia nchi.
Marekani hataki mrusi aweke silaha cuba lakini anataka kumzunguka mrusi akiweka silaha nchi jirani na urusi, hii vita imetengenezwa na nato
 
Kama hoja ni nato au marekani kwa "makosa" yake huko syria au iraq au libya , au kama shida ni nato au marekani kwa wanayotaka kuyafanya na ukraine, basi uamuzi sahihi kwa putin na nyie mnaomuunga mkono ilikuwa ni kuwavamia hao nato na marekani kuua watu wao na kuharibu nchi zao, sio ukraine, kwanini chuki zenu kwa nato na marekani mnazipeleka kwa wanyonge ukraine, kila sababu mnazotoa mnahusisha matendo ya marekani , kamvamie sasa huyo marekani ili apate haki yake. Hamma hoja team putin ubabe wa ki hitler huo
Unazungumziaje matendo ya Marekani mnaemuita mama wa demokrasia kuvamia Syria, Iraq,Libya...?
 
Ni wazi kwamba, Dunia leo iko mapande matatu, kuna Urusi, Kuna Uchina na kuna Marekani... Kwenye nchi 28 Uchina hayuko huko, zingatia kuna nchi za kati zenye uchuki mkubwa ambazo ni India hayuko na Ukraine, huko Brazil hayuko huko na Ukraine... Na hawa wanamuunga mkono Mrusi.... Dunia sasa inastawi na hii ndio balance ya dunia na inapumua vizuri sasa.
Kwanini sisi hatuhesabiki
 
Back
Top Bottom