#COVID19 Kwanini nchi zilizochanja wananchi wake na kuchukua tahadhari zote ndio zinaendelea kuongoza kwa maambukizi na COVD-19

#COVID19 Kwanini nchi zilizochanja wananchi wake na kuchukua tahadhari zote ndio zinaendelea kuongoza kwa maambukizi na COVD-19

Na ile taarifa iliyotolewa juzi katika kituo kimoja cha habari nchini Marekani ya kwamba wanaopoteza maisha kwa Covid 19 ni wale ambao hawakupata chanjo,mtoa uzi huu unalizungumziaje kwa upande wako
Ulitaka waseme otherwise ili watu wasichome chanjo .....?!

Hili unalizungumziaje kwa upande wako?!
 
Lete data ,otherwise unaleta udaku tu.Ukiangalia kwenye update ya "worldmeter/coronavarus update" hicho kitu hakuna mbona.Wewe unaangalia website au report za BUZA naona.Mama kasema chanjo ni hiari kama unaona haikusaidii usichange acha kula covidol yako kalale utupishe sisi tupite.
Una uhakika na hizo source hawatumanipulate na hizo information zao kwa manufaa yao binafsi??
 
Unasimamaje na alie lala...??
Mambo ya corona virus ni magumu kuelewa lakini.
Hayana ugumu wowote, Ni simple logic
Tabia hatarishi zipo kwa asilimia 100, lakini maambukizi Ni asilimia 0.
Kumbuka tangu tumeanza kutishwa na watanzania wenzetu wanaojikweza, huku wakisema sisi watanzania hatuna akili, kana kwamba wao Ni wamarekani.
Wakati wa mazishi ya hayati kwa mfano , Hawa wajikwezao walisema Sana humu kutokana na umati ule na kutozingatia kanuni za watu wale, wakatabiri kwa hesabu zao mbovu kwamba baada ya wiki mbili kutakuwa na msiba mkubwa maana watanzania wengi watakufa kwa corona, Nani anaweza kushuhudia kwamba baada ya maombolezo Yale, Ni waombolezaji wangapi walikufa au hata kuugua corona!!!?
Je watanzania wanavyojaa kwenye nyumba za ibaada, kumbi za starehe, viwanja vya michezo na mausafiri ya umma
Mnasemaje???
Nauliza watu mnaojisingizia kuwa na akili kuliko akili yenyewe!!!
 
Kama kuna watu wanafanya utafiti wa corona na madhara yake..
basi waanzie kwenye mwendo kasi
Halafu ile tume ya corona, ilitumwa kutafiti Hali ya corona Tanzania, Jambo la kushangaza , ripoti yao Haina maelezo yanayoonesha Hali ya corona Tanzania, badala yake wamekuja tu na mapendekezo namna ya kukabiliana na corona , ambayo hawajatuambia ipo kwa kiasi gani....
 
Juzi Rais wa Rwanda katangaza kufunga vyuo na shule kuanzia 01.07.2021
Kenya curfew imekuwa extended for 60 more days
Uganda Ligi kuu imelazimishwa kumalizika coz ya Covid
Burundi, India, Brazil na nyingine mambo ni yaleyale.

Tanzania mbona watu wanadunda tu mtaani bila tahadhali yoyote na hatuone wagonjwa kama ilivyokuwa katika "wimbi" la kwanza?

Hatuoni Kila duka/ kibanda/ofisi kuwa na ndoo zenye maji na zinazotumiwa kikamilifu na kila mtumiaji.
Barakoa wanatumia watu wachache saaana
vitakasa mikono huvioni kama zani vilikuwa ninaning'inia kwenye luksi kama keyholder, mikono ya pochi za wanawake.

Ila matangazo kwa upande ya mataifa mbalimbali yamekomalia saana uwepo wa hii kitu hapa TZ

imagine MAMA juzi kasema TZ kuna wagonjwa 100 tu

100/50,000,000 = 0.0002%

DISCO, kama kawa, mwendokasi kama kawa, njumba za Ibada kama kawa full nyomi .

na kwa kuudhihirishia ulimwengu waje KWA MKAPA 03.07.2021 washangae

CORONA TZ HAMNA. kama mnataka fedha za COVAX fine ila MSITUTISHE!!!!!



KWA HILI NASIMAMA NA DR. JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI
Mshukuru Mungu tunaomba anatujibu na sio kwamba sisi ni wema kuliko hao,unakosea kusimama na mfu, usije ukamfuata.
 
India walikuwa wanatoa takwimu. Naona wewe uko zaidi kwenye ile watu wanafariki mpaka huduma za hospital na mazishi zinaelemewa. Lakini kumbuka bado kunaweza kuwa na idadi kubwa kiasi ya wagonjwa na vifo na usione athari! Nchi kama Tanzania wakifariki wastani wa wagonjwa wawili kwa siku, katika kila mkoa kwa muda labda wa miezi mitatu hutaweza kuona athari kama zile za India lakini bado ni idadi kubwa ya watu. Mambo ya vifo kwenye nchi bila takwimu ni ngumu sana kujua ukubwa wake. Kwa mfano, kwa hali ya kawaida kabla ya korona, Tanzania ungeweza kukaa mwezi mzima bila kusikia mtu unayemjua amefariki, lakini hii haiondoi ukweli kwamba kuna watu wengi wanakufa kila siku.
Tunazungumzia corona kama ugonjwa hatari sana na wenye kuambukiza kwa kasi na usio na dawa, Tanzania ambayo imeacha kuchukua tahadhari za kujikinga na huu ugonjwa kwa kipindi kirefu, hivyo tungetegemea hali ya maambukizi kwa huu ugonjwa kuwa mbaya hivyo tungeona japo huduma za hospitali kuelemewa kutokana na kutofuata njia za kujikinga na maambukizi ya huu ugonjwa, nakumbuka kuliwahi kutokea uvumi wa kwamba Dar hospitali zimezidiwa wagonjwa wa corona, hiyo yote ni kutokana na jinsi tulivyokuwa tuna shughulikia hili suala la corona na ndio hali tunayoendelea nayo hadi sasa.
 
Halafu ile tume ya corona, ilitumwa kutafiti Hali ya corona Tanzania, Jambo la kushangaza , ripoti yao Haina maelezo yanayoonesha Hali ya corona Tanzania, badala yake wamekuja tu na mapendekezo namna ya kukabiliana na corona , ambayo hawajatuambia ipo kwa kiasi gani....
Ni kweli kabisa, mfano humu huwa kuna watu wanadai kwamba madaktari huko mahospitalini ndio wanajua uhalisia wa corona, hivyo nilitaraji kusikia hilo suala kwenye ile ripoti ila ndio kwanza tunaona rais mpaka juzi hapo anaenda kutembelea hospitali huku akiwa hana taarifa zozote kuhusu uwepo wa wagonjwa wa covid kwenye hiyo hospitali.
 
Tunazungumzia corona kama ugonjwa hatari sana na wenye kuambukiza kwa kasi na usio na dawa, Tanzania ambayo imeacha kuchukua tahadhari za kujikinga na huu ugonjwa kwa kipindi kirefu, hivyo tungetegemea hali ya maambukizi kwa huu ugonjwa kuwa mbaya hivyo tungeona japo huduma za hospitali kuelemewa kutokana na kutofuata njia za kujikinga na maambukizi ya huu ugonjwa, nakumbuka kuliwahi kutokea uvumi wa kwamba Dar hospitali zimezidiwa wagonjwa wa corona, hiyo yote ni kutokana na jinsi tulivyokuwa tuna shughulikia hili suala la corona na ndio hali tunayoendelea nayo hadi sasa.
Again. Wewe na watu wengi wenye mlengo wa Magufuli kuna details mnazi-mis. Hii ni kutokana na pengine kutokuelewa kiingereza sawasawa au uvivu wa kusoma makala na maelezo ya kitaalam kuhusu huu ugonjwa. Unaposikia vifo au hospital kuelemewa katika nchi kama USA au Ulaya kwa ujumla, wengi wa victims ni wazee wa miaka 65 na kuendelea. Sasa niambia, Bongo population ya wazee ipo kwa kiasi gani? Wazee wengi wenye miaka hiyo walishatangulia mbele ya haki. Kwa kuangalia demografia ya population ya nchi yetu, wengi ni miaka 35 kwenda chini, na huu umri kwa korona huwezi kuona effects zake kwa ukali. Bado nasisistiza statistics kama zingekuwa zinachukuliwa, Tanzania tumeshapoteza watu wengi tu kwa kulinganisha na umri wa population yetu. Nyie mnapiga bla bla bila na kulinganisha nchi inayoacha mambo yajiendee vs nchi zinazorekodi karibu kila mgonjwa na vifo.
 
Mkuu ni nani yuko responsible kutoa takwimu? Serikali kupitia Wizara ya Afya au watu Kitaa? IMF imetunyima mkopo wa $574 millions ili kupunguza athari za uchumi zilizosababishwa na COVID-19 mpaka hapo Serikali itakapoanza kutoa takwimu za kila siku kuhusu wagonjwa wa Covid nchini.

Utajuaje athari ya bila takwimu?
 
Juzi kasema juu juu tu kwamba kuna wagonjwa zaidi ya 100 nchini bila ya kusema wako mikoa ipi na idadi ya waliokufa na kama Serikali inafuatilia watu wa karibu wa hao wagonjwa zaidi ya 100 ili kujua wako salama au tayari wana maambukizi.

Ni kweli kabisa, mfano humu huwa kuna watu wanadai kwamba madaktari huko mahospitalini ndio wanajua uhalisia wa corona, hivyo nilitaraji kusikia hilo suala kwenye ile ripoti ila ndio kwanza tunaona rais mpaka juzi hapo anaenda kutembelea hospitali huku akiwa hana taarifa zozote kuhusu uwepo wa wagonjwa wa covid kwenye hiyo hospitali.
 
Mkuu ni nani yuko responsible kutoa takwimu? Serikali kupitia Wizara ya Afya au watu Kitaa? IMF imetunyima mkopo wa $574 millions ili kupunguza athari za uchumi zilizosababishwa na COVID-19 mpaka hapo Serikali itakapoanza kutoa takwimu za kila siku kuhusu wagonjwa wa Covid nchini.
Unajua kuna dunia hii wainga hawaishi. Dunia yote kuanzia Uchina, Ujapani, India, Uarabuni, Urusi, Ulaya Magharabi, Mashariki ya Kati na Amerika wote wanazungumza lugha moja. Halafu wanatokea wajinga wachache wenye shahada za sayansi za uchochoroni wanawakosoa. Ujinga ulioje huu. Nilimsikia rais Samia juzi alipoulizwa maswali anasema anadhani mtu akijifukiza wakati virus ''wakiwa bado koooni'' kabla hawajaingia kwenye mapafu wanaweza kufa!!! Hii unaweza kuona kabisa ni sayansi ya vichakani na watu hawajui hata kidogo virus wanavyoambukiza na kusambaa ndani ya mwili. Magufuli hivyo hivyo alikuwa anasema ukijifukiza na mvuke wenye temperature 100 degraa cg eti virus hawa-survive!!!! Unaweza kuona kabisa hawajui jinsi virus wanavyoji-attach kwenye cells za mwili
 
Lete data ,otherwise unaleta udaku tu.Ukiangalia kwenye update ya "worldmeter/coronavarus update" hicho kitu hakuna mbona.Wewe unaangalia website au report za BUZA naona.Mama kasema chanjo ni hiari kama unaona haikusaidii usichange acha kula covidol yako kalale utupishe sisi tupite.
Nadhani jamaa yupo sahihi, kwani kwa maisha yetu haya kama kuku wa kienyeji tungekuwa tumeshakwisha kabisa!!!lakini baada ya hofu kuondolewa maisha yanaenda kama kawaida tu sio kama ugonjwa haupo.Approaches nyingi za meko nilikuwa sikubaliani nazo kabisa lakini kwa hili la COVID19, hapa nampa shikamoo huko alipo!!Na ndio maana hata sasa itakuwa ngumu kwa wananchi kuelewa somo kwani ni mwaka sasa ugonjwa upo, na yeye maisha yanaendelea kama kawaida!!TUSITIANE HOFU.
 
Juzi kasema juu juu tu kwamba kuna wagonjwa zaidi ya 100 nchini bila ya kusema wako mikoa ipi na idadi ya waliokufa na kama Serikali inafuatilia watu wa karibu wa hao wagonjwa zaidi ya 100 ili kujua wako salama au tayari wana maambukizi.
Hizo ni takwimu tu za kuchukulia pesa kutoka IMF, WHO.hakuna lolote na wasiwatie wananchi hofu, chanjo sawa zije na anayetaka achanjwe!!aliyewalinda mwaka mzima ndio atakayeendelea kuwalinda tu, japo tahadhari ni muhimu.
 
Eti dhalimu alikuwa sahihi na bado akakimbilia chato kujificha kwa miezi miwili!!! Na kwa ubishi wake wa kutotaka kuvaa masks mwenyewe aliyaita matambara basi COVID-19 haikufanya ajizi bali kulala naye sambamba leo anaitwa MWENDAZAKE!!!! Hakuna anayekutisha ni maisha yako mwenyewe na MAKABURI umeyaona. Chukua hatua muafaka za kujikinga ubishi wa kijinga KAMWE hautakukinga kumbuka zaidi ya watu 3.5 duniani Covid-19 imesitisha uhai wao.

Nadhani jamaa yupo sahihi, kwani kwa maisha yetu haya kama kuku wa kienyeji tungekuwa tumeshakwisha kabisa!!!lakini baada ya hofu kuondolewa maisha yanaenda kama kawaida tu sio kama ugonjwa haupo.Approaches nyingi za meko nilikuwa sikubaliani nazo kabisa lakini kwa hili la COVID19, hapa nampa shikamoo huko alipo!!Na ndio maana hata sasa itakuwa ngumu kwa wananchi kuelewa somo kwani ni mwaka sasa ugonjwa upo, na yeye maisha yanaendelea kama kawaida!!TUSITIANE HOFU.
 
Eti takwimu za kuchukulia pesa IMF!!! 😂😂😂unadhani IMF ni Wapumbavu kiasi hicho!?


Hizo ni takwimu tu za kuchukulia pesa kutoka IMF, WHO.hakuna lolote na wasiwatie wananchi hofu, chanjo sawa zije na anayetaka achanjwe!!aliyewalinda mwaka mzima ndio atakayeendelea kuwalinda tu, japo tahadhari ni muhimu.
 
Back
Top Bottom